KURASA

Friday, April 30, 2010

MSEELE - delonix elata

Kutokana na maombi ya ndugu Godleader A Shoo alitaka kujua matumizi ya mti wa mdodoma, mti huu hujulikana kitaalam kama delonix elata na jina la kiswahili ni mseele lakini watu wengi wanauita mdodoma kwa sababu imepandwa sana Dodoma na hii inatokana na kuhimili kwake hali ya ukame



Miti hii inauwezo wa kuhimili joto kali na baridi ya wastani kwa hiyo inaweza kuota ukanda wa pwani hadi ukanda wa akti mikoa ya Dodoma, Singida, Shinyanga n.k

MATUMIZI
1- Wengi huipanda kwa ajili ya mapambo na hii hutokana na mwonekano wake mzuri na pia maua yake yanapochanua hupendeza pia
2- Kwenye miti hii tunapata pia kuni kwa ajili ya kupikia na ndio maana hupandwa sana maeneo makame kwa sababu pia inakuwa haraka kiasi
3-Nguzo za kujengea pia zinapatikana kama mti utaacha ukue, nguzo si kubwa sana lakini kwa nyumba za vijijini zinatosha kabisa, pia nguzo hizi huweza kutoa mbao
4- Dawa za magonjwa mbali mbali kama vile majani yakipondwa husaidia kupunguza uvimbe na pia kupunguza sumu ya wadudu kama nyuki, manyigu, na nge. Pia mizizi yake ikichemshwa na kunywewa husaidia matatizo ya tumbo
5- Majani yake huweza kutumika kama chakula cha mifugo, ukipanda miche hii hakikisha hamna wanyama kama mbuzi na Ng'ombe maana wataila ikiwa midogo

MAUA YA MSEELE

Friday, April 23, 2010

FUNGATE LA MKULIMA

Tukiwa na babu na bibi yangu mzee Msumari nyumbani kwake Makorora Tanga, huyu ni mdogo wa mwisho wa Bibi mzaa Baba na ndiye aliyebakia pekee



Tunapata msosi na my wife wangu tukiwa kijijini kwetu, hapa ni Ugali, kuku wa kienyeji na Mchunga bila kusahau ngogwe na chachandu la mbilimbi halafu tunashushia na mnazi au boha



Kaburi la Marehemu Baba yangu mzee Reginald Bennet huko Muhinduro Tarafa ya Maramba Wilaya ya Mkinga Mkoa wa Tanga




Hili ni kaburi la marehemu Bibi mzaa Baba aitwaye Perpetua Mohamed kijijini kwetu Muhinduro Tarafa ya Maramba Wilaya ya Mkinga Mkoa wa Tanga


Wife akishangaa machungwa, yakiwa madogo hivi tunaita mawashata taa



NB Picha za tukiwa Lushoto na Pangani sitaziweka humu kutokana na maombi ya mke wangu (privacy)