KURASA

Thursday, June 10, 2010

AINA 10 ZA MBWA WENYE AKILI ZAIDI DUNIANI

1 - BORDER COLLIE



2 - POODLE



3 - GERMAN SHEPHERD / ALSATION


4 - GOLDER RETRIEVER


5 - DOBERMAN PINSCHER


6 - SHETLAND SHEEPDOG


7 - LABRADOR RETRIEVER


8 - PAPILLON


9 - ROTTWEILER


10 - AUSTRALIAN CATTLE DOG

Thursday, June 3, 2010

URAFIKI WA MBWA NA KOBE

Huyu mbwa mdogo ajulikanaye kama HOPE huwa anapenda kupanda juu ya mgongo wa kobe huyu ajulikanaye kama CARL, CARL naye bila hiyana huamua kumtembeza tembeza rariki yake

Monday, May 31, 2010

KILIMO CHA PILIPILI MANGA


Utangulizi

Jina la kitalaam ni Piper nigram na kwa kiingereza ni black pepper. Zao hili asili yake ni Mashariki ya Mbali, na linalimwa zaidi katika mkoa wa Tanga na Zanzibar.

Matumizi
Pilipili nyeusi na nyeupe zote hutumika kwa mapishi ya nyama, samaki na kwa mapishi mengine mbalimbali. Nchi za magharibi zina matumizi makubwa ya viungo hivi. Aidha pilipili mtama nyeusi ndiyo huzalishwa zaidi hapa nchini.

Uzalishaji
Hali ya hewa na udongo
Viungo vingi humea katika maeneo yenye joto la wastani kati ya nyuzi joto 24-26 na huzalishwa maeneo ya mwambao. Udongo wenye rutuba na unaopitisha maji na wenye uchachu wa kiasi cha pH 6.5. Mahitaji ya mvua ni mililita 1500-2000 kwa mwaka.




• Uchaguzi wa mbegu
Uchaguzi huzingatia mambo yafuatayo:-
a) Urefu wa pingili na ukubwa wa majani
b) Ufupi wa pingili unaoambatana na majani madogo.
Tofauti iko hadi kwenye umbile la matunda. Majani ya mche mama sehemu kinapokatwa kipando huondolewa wiki mbili kabla ya kukata. Vipando vyenye macho (nodes) 3-4 humika. Macho mawili huzikwa kwenye udongo na kipando kiwekewe kivuli. Inashauriwa kuweka mbolea ya samadi wakati wa kupanda.

• Nafasi ya upandaji
Nafasi ya kupanda ni mita 2-3 kati ya mmea na mmea endapo miche imepandwa na miti inayotakiwa kupogolewa mara kwa mara.

Mahitaji ya mbolea
Matumizi ya mbolea hapa Tanzania si makubwa katika kilimo cha viungo. Ingawa kiasi cha kilo 0.4 cha Urea, kilo 0.3 cha Superphosphate na kilo 0.3 cha Potash ya Muriate kinaweza kutumika kwa miche mikubwa.

• Miti ya kusimikia miche

Miche hupandwa kwa kusimikiwa nguzo ili ikue kwa kujizungusha kwenye miti kama mijenga ua, n.k. Mti huo wa kusimikia nao pia hupaswa kupunguziwa majani ili kupunguza giza. Kila kabla ya msimu miti hiyo hupaswa kupunguziwa matawi (pruning).

Kupogolea miche ya pilipili mtama
Mche ukifikia miezi 18 inapaswa kupogolea kwa kukata sehemu ya juu ya mche ili kufanya matawi mengine yachipue chini ya mche. Inashauriwa mche kuwa na urefu wa mita 3-3.5.

Uvunaji
Maua ya kwanza hutoka baada ya miaka miwili. Matunda hukomaa miezi tisa (9) hadi kumi (10).
Uvunaji ni mizunguko 5 hadi 6 kwa mwaka. Pilipili mtama inaweza kuvunwa kwa misimu miwili. Mavuno ni kati ya tani 0.35-3.75 kwa hekta.

Kuhifadhi
Pilipili mtama inaweza ikawekwa kwenye chombo kisichopitisha hewa na kudumu kwa miaka 20 bila kuharibika.

Mashambulizi ya wadudu na magonjwa
Hapa nchini hakuna matatizo makubwa ya wadudu na magonjwa.

Masoko
Soko la pilipili matama linapatikana ndani ya nchi na nje pia. Bei ya ndani ni kati ya Sh1,000-1,500. Zao hili huuzwa katika nchi za Uganda, Kenya, Uingereza, Ujerumani, Mashariki ya Kati, n.k. Bei ya Nje ni wastani wa dola za kimarekani 1,985 kwa tani.

Thursday, May 27, 2010

BIO -GAS / HEWA VUNDE

Kuni na mkaa vimekuwa vikiongezeka bei kila siku pia vikiwa ni vyanzo vya uharibifu wa mazingira kutokana na ukataji miti, njia mbadala inahitajika katika kutatua tatizo hili kwa wakulima, na kinyesi cha wanyama kinaweza kutumia kuzalisha nishati ijulikanayo kama BIO –GAS

Kinachofanyika ni kukusanya kinyesi cha wanyama hasa ng’ombe wanaofugwa ndani, kikichanganyika na mkojo pamoja na maji yanaelekezwa katika tanki maalum kwa ajili ya kuzalisha nishati hii. Baada ya bacteria kuozesha mchanganyiko huu kwa njia isiyohitaji hewa ya oksijeni (anaerobic fermentation) nishati ya bio gas huzalisha ikiwa na wastani wa hewa ya METHANE 65% na kasha gasi hii huelekezwa kwenye nyumba kwa kutumia mabomba hadi jikoni kwa ajili ya kupikia

Mchanganyiko uliokwisha tumika hutoka nje wenyewe kwa kusukumwa na mchanganyi ko mpya mara uingiapo, kinyeshi kinachotoka nacho pia hutumika kama mbolea kwa ajili ya kustawisha mazao ya mkulima



FAIDA ZA BIO-GAS
1-Huongeza kipato cha mkulima kwa kupunguza muda wa kutafuta kuni na mkaa

2-Husaidia katika utunzaji wa mazingira kwa sababu haichafui hewa na hupunguza ukataji miti hovyo

3-inaweza kutumika kuwashia taa kama itazalishwa ya kutosha

4-mbolea inayobaki hutumika kwa ajili ya kustawisha mazao

5-Afya ya mkulima hulindwa kwa sababu upikaji kwa kutumia bio gas hauna moshi, kina mama jikoni hawaathiriki na moshi kama wakitumia kuni, badala ya kinyesi cha wanyama kuwa kingi na kukosa matumizi na kugeuka uchafu sasa kitatumika kuzalisha nishati hii

Monday, May 17, 2010

ZANZIBAR HAKUNA MBUNG'O

Ni miaka zaidi ya sita (6) tokea mbung’o waache kuonekana katika visiwa vya Zanzibar na tokea kipindi hicho ng’ombe kadhaa wamekuwa wakipimwa damu ili kujua kama wana ugonjwa wa ndigana/nagana unaosambazwa na mbung’o lakini matokeo yamekuwa mazuri yakionyesha kwamba ng’ombe hawana vimelea vya ugonjwa huo hatari kwa mifugo

MBUNG'O WAKIPANDANA


Hii imesababisha uzalishaji wa maziwa kuongezeka mara tatu zaidi, uzalishaji wa nyama marambili zaidi, matumizi ya samadi ya mifugo nayo yameongezeka mara tano zaidi na hii inamaanisha kwamba wafugaji wa ng’ombe kipato chao kimeongezeka zaidi. Je sababu ya haya yote na mbung’o kupotea ni nini?

Kwa kawaida mbung’o jike akishapandwa mara moja hawezi kupandwa tena maisha yake yote, yaani inamaanisha kwamba huwa wana mzao mmoja tu katika maisha yao yote. Sasa kinachofanyika kitaalam ni kwamba mbung’o wanakamatwa wakiwa hai kisha wana tengwa majike na madume, majike yanauwawa na madume yanapelekwa kwenye maabara na kupigwa mionzi ya gamma kutoka katika cobalt 60, baada ya hapo yanakuwa yanapanda majike kama kawaida ila yanapoteza uwezo wa kuwazalisha kwa maana hiyo watapandana bila kuzalishana na pole pole kizazi kinapotea na kufutika kabisa

MTEGO WA KUKAMATIA MBUNG'O



Kwa Zanzibar zoezi lilifanikiwa asilimia 100 kwa sababu mbung’o hawawezi kutoka sehemu nyingine na kuhamia Zanzibar kwa kuwa ni kisiwa, pia wao walizalisha madume mengi kwenye maabara na kuyaachia baada ya kuyaua kizazi, njia hii inajulikana kama sterile male technique

Thursday, May 6, 2010

KUPUNGUZIA MATAWI MITI JAMII YA MICHUNGWA

Bw Elyc ameniambia kwamba nimwelekeze jinsi ya kupunguzia matawi ya miche yake jamii ya michungwa nami namwomba azingatie haya

1- Kipindi kizuri cha kupunguzia matawi miti yako ni kipindi cha jua na wakati huu mimea isiwe na matunda wala maua

2- Matawi yanakatwa sehemu zile zenye magonjwa , zilizokufa, matawi yaliyofungamana au katikati ya mti ili kuufanya utawanyike vizuri

3- Pia punguza matawi yaliyopo kwenye njia pamoja na matawi yanayoelekea kuelemewa kutokana na kuwa na matawi madogo mengi zaidi

4- Tumia zana maalum za kupunguzia matawi kama mikasi na misumeno maalum inayopatikana kwenye maduka ya pembejeo za kilimo, uwe mwanagalifu vifaa hivi visikuumize maana vina ncha kali na tumia vifaa vya kujikinga kama mabuti maalum ya mashambani na glovu za mikononi

5- Milimao inabidi ipunguziwe matawi kila Mwaka au kila baada ya miaka miwili, kila tawi lipunguze kiasi cha robo au theluthi ya juu, kwa kufanya hivi mlimao hautakuwa mkubwa sana na kusababisha usumbufu wakati wa kuvuna

MCHUNGWA AINA YA JAFFER



6- ZINGATIA
(a)Panda miche yako kwa nafasi zinazokubalika kitaalam laa sivyo mime yako ikibanana itakuwa inakimbilia juu, kwa michungwa aina ya jaffer panda mita 8 kwa 8 (8m * 8m) na kwa aina ya Valencia panda (5m * 8m)

(b)kumbuka kupunguzia miche yako jamii ya michungwa kuna maanisha kupunguza mazao kwa sababu mti mkubwa ndio unazaa matunda mengi, usiupunguze matawi mti wako kama huna sababu ya kufanya hivyo

(c)Vifaa vinavyotumika kwa ajili ya kupunguzia matawi viwe na makali ya kutosha kuepusha kupasua na kuchana matawi, unaweza kuomba afisa ugani wa eneo lako ili akuonyeshe kwa vitendo

(d)Kama utachanganya michungwa ya jaffer na Valencia uipande kwa uwiano wa 2:5 yaani katika kila michungwa 7 miwili iwe jaffer na mitano iwe Valencia, hii ni kwa sababu michungwa aina ya jaffer ni mikubwa na inazaa sana na inawahi kuiva lakini haihimili sana ukame, michungwa ya Valencia ina uzazi wa wastani na inahimili ukame kwa hiyo ukiichanganya shambani utapata mavuno ya mwanzo kwenye jaffer na mavuno ya kati yatakuwa na mchanganyiko wa jaffer za mwisho na Valencia za mwanzo na kisha mwisho utapata mavuno ya Valencia tu. Kwa hiyo utakuwa na machungwa katika msimu wote wa mavuno na ii itazuia machungwa kuiva yote pamoja na kuharibikia shambani

Tuesday, May 4, 2010

JINSI YA KULIMA BUSTANI KWENYE ENEO LENYE MAJIMAJI

Kutokana na tatizo la bwana Chacha Wambura Ng'wanambiti katika post hii hapa http://mataranyirato.blogspot.com/2010/05/aisifuye-mvua-imemnyea.html nimeamua kutoa maelezo kwa ufupi jinsi ya kukabiliana na sehemu ambazo maji husimama wakati wa mvua



1- Lima na tifua udongo kwa kutumia trekta la mkono (power tiller) kiasi cha inchi 12 chini, udongo mwingine unaweza kuujaza kama matuta na kuweka mifereji pande zote la eneo lako. Kama huna trekta hili pia unaweza kutumia jembe la kukokotwa na ng’ombe (plau)

2- Jaza majani makavu, vijiti, maranda ya mbao n.k kiasi cha inchi 5 -6 halafu mbolea vunde au samadi kiasi cha inchi 4 halafu rudishia udongo wako juu yake na hapo utakuwa umeinyajua ardhi yako kiasi cha inchi 8 juu (kumbuka maranda na mbolea vitadidia kidogo) kisha pitisha harrow au jembe la kukokotwa na ng’ombe ili kuweza kuchanganya vitu hivi



3- Acha udongo wako ukauke kiasi cha siku 3 kisha pitisha harrow au jembe la kukokotwa na ng’ombe tena ili kuvunja vunja mabonge ya udongo yaliyotokea wakati wa udongo kukauka na pia kuchanganya mchanganyiko huu zaidi

4- Weka tena mbolea vunde au samadi kiasi cha nchi mbili juu ya mchanganyiko huu kisha panda mbegu au miche yako na uizungushie udongo kiasi

5- Mwagia maji kadri inavyo hitajika kama udongo utakuwa mkavu, na uendelee kufuata kanuni za kilimo bora kama inavyoshauriwa kitaalamu

Friday, April 30, 2010

MSEELE - delonix elata

Kutokana na maombi ya ndugu Godleader A Shoo alitaka kujua matumizi ya mti wa mdodoma, mti huu hujulikana kitaalam kama delonix elata na jina la kiswahili ni mseele lakini watu wengi wanauita mdodoma kwa sababu imepandwa sana Dodoma na hii inatokana na kuhimili kwake hali ya ukame



Miti hii inauwezo wa kuhimili joto kali na baridi ya wastani kwa hiyo inaweza kuota ukanda wa pwani hadi ukanda wa akti mikoa ya Dodoma, Singida, Shinyanga n.k

MATUMIZI
1- Wengi huipanda kwa ajili ya mapambo na hii hutokana na mwonekano wake mzuri na pia maua yake yanapochanua hupendeza pia
2- Kwenye miti hii tunapata pia kuni kwa ajili ya kupikia na ndio maana hupandwa sana maeneo makame kwa sababu pia inakuwa haraka kiasi
3-Nguzo za kujengea pia zinapatikana kama mti utaacha ukue, nguzo si kubwa sana lakini kwa nyumba za vijijini zinatosha kabisa, pia nguzo hizi huweza kutoa mbao
4- Dawa za magonjwa mbali mbali kama vile majani yakipondwa husaidia kupunguza uvimbe na pia kupunguza sumu ya wadudu kama nyuki, manyigu, na nge. Pia mizizi yake ikichemshwa na kunywewa husaidia matatizo ya tumbo
5- Majani yake huweza kutumika kama chakula cha mifugo, ukipanda miche hii hakikisha hamna wanyama kama mbuzi na Ng'ombe maana wataila ikiwa midogo

MAUA YA MSEELE

Friday, April 23, 2010

FUNGATE LA MKULIMA

Tukiwa na babu na bibi yangu mzee Msumari nyumbani kwake Makorora Tanga, huyu ni mdogo wa mwisho wa Bibi mzaa Baba na ndiye aliyebakia pekee



Tunapata msosi na my wife wangu tukiwa kijijini kwetu, hapa ni Ugali, kuku wa kienyeji na Mchunga bila kusahau ngogwe na chachandu la mbilimbi halafu tunashushia na mnazi au boha



Kaburi la Marehemu Baba yangu mzee Reginald Bennet huko Muhinduro Tarafa ya Maramba Wilaya ya Mkinga Mkoa wa Tanga




Hili ni kaburi la marehemu Bibi mzaa Baba aitwaye Perpetua Mohamed kijijini kwetu Muhinduro Tarafa ya Maramba Wilaya ya Mkinga Mkoa wa Tanga


Wife akishangaa machungwa, yakiwa madogo hivi tunaita mawashata taa



NB Picha za tukiwa Lushoto na Pangani sitaziweka humu kutokana na maombi ya mke wangu (privacy)

Friday, March 26, 2010

KONDOO AKISAIDIWA KUZAA WATOTO MAPACHA

JINSI YA KUKATA MICHE YA MISOJI (MITIKI)

Kwa kawaida miche ya misoji mara baada ya kutolewa kwenye kitalu huitaji kukatwa, mjasiliamali aliyeko jijini Mwanza aitwae NAYMA aliniomba nimwelekeze kwa picha na mimi bila hiyana nilikwenda shamba na kung,oa mche mmoja na kuukata na kuupiga picha kabla ya kuukata na baada ya kuukata ili kupata kipandikizi

MCHE KABLA YA KUKATWA (angalia mishale kujua sehemu za kukata)


Mche wangu niliukata na kuacha kiasi cha nchi mbili au pingili mbili za vidole kwa sehemu ya juu ya mzizi na kwenye mzizi niliondoa ile sehemu nyembamba ya chini, kwa kawaida hii sehemu ya chini hufa mara baada ya kupandwa kwa sababu sehemu nene/kubwa ya mzizi inayoachwa ndiyo huifadhi maji na chakula cha mmea, nadhani hapa nitakuwa nimemsaidia kama bado nipigie kwenye ile namba niliyokupa

KIPANDIKIZI TAYARI KWA KUPANDWA


Kumbuka wakati wa kupandwa lazima uweke kisahani ili kiweze kukusanya maji kwa ajili ya ukuaji mzuri, kama ni udongo unaotuamisha maji usiweke kisahani bali wekea kama tuta au mwinuko

WEKA KISAHANI KAMA UDONGO HAUTUAMISHI MAJI


WEKA TUTA KAMA UDONGO UNATUAMISHA MAJI

Friday, March 19, 2010

MBWA WAKIPANDANA KWA NINI HUNASIANA AU KUNATANA?



Nadhani karibia kila mtu ameshawahi kuona mbwa wakipandana, kama bado basi maelezo haya yatakusaidia siku ukiwaona, mara baada ya mbwa dume kumpanda jike utaona dume anageuka na kupeana mgongo na jike kila mmoja akiangalia upande wake wakati huo huo, uume ukiwa bado ndani ya uke, wanakuwa kama wanavutana na wakati mwingine wanaweza kutoa milio kama wanalalamika, unaweza kuhisi wanaumia na ukataka kuwatenganisha ACHA na wala usijaribu kufanya hivyo utawaumiza.

Kwa kawaida mbwa dume anapoanza kumpanda jike uume unakuwa haujasimama bali husaidiwa na kiuongo kijulikanacho kama baculum, hii ni tishu kama mfupa na iko ndani ya uume wa mbwa. Wakati mbwa dume anapotaka kumwaga manii ndani ya uke ndipo damu hujaa kwenye uume na hapo uume hutanuka (kudinda) kwa hiyo akimaliza kutoa manii uume hunasa ndani ya uke kwa sababu ya kule kutanuka.



Mbwa dume anapogeuka anazipa muda Mbegu za kiume ziweze kuingia vizuri kwenye uke na hivyo kusababisha ujauzito, ukitumia nguvu kuwaachanisha, mbali na kuumia pia jike hataweza kupata ujauzito. Hiki ni kitu cha asili kwa hiyo husaidia pia kuzuia madume mengine yasiingilie tendo hili na kulikatisha wakati Mbegu bado zinaogelea na kuyafuata mayai kwenye mji wa mimba, kwa kawaida hata kama mbwa madume walikuwa wanapigana kila mmoja akitaka kumpanda jike, mara baada ya Yule aliyefanikiwa kupanda na kugeuka wale wengine huacha vurugu zote.

MBWA WALIONASIANA BAADA YA KUPANDANA


Tendo hili huchukua kati ya dakika 20 – 30 na mbwa hufanikiwa kunasuka mara baada ya damu kupungua kwenye uume na uume kusinyaa na kupungua ukubwa. Kwa mbwa dume ambaye ni mara yake ya kwanza kupanda basin a hata yeye huchanganyikiwa atakapoona amenasa, anaweza hata kujaribu kujinasua au kupiga kelele, unachotakiwa ni kumshika shika shika mbwa wako kichani huku ukimuongelesha kwa upole, yaani jaribu kumpunguza presha ili atulie

Monday, March 8, 2010

KILIMO CHA UYOGA

Miaka ya karibuni, utaalamu wa kuotesha uyoga umeanza hapa Tanzania baada ya watu kutilia maanani lishe bora ya protini na manufaa mengine ya zao hilo. Kwa kuwa uyoga upo wa aina mbalimbali, usitawishaji wake hutofautiana katika mahitaji yake, ikiwa ni pamoja na hali ya hewa, malighafi za kuoteshea, urahisi wa teknologia ya kuotesha katika mazingira ya Tanzania na soko lake kwa wananchi na katika hotel. Hata hivyo ni wananchi wachache tu wanaojua kilimo cha uyoga.



Uyoga unaozalishwa unafahamika. Aina zinazofaa kwa Tanzania ni zile ambazo hustawi vizuri, kwenye maeneo ya joto la wastani wa nyuzi joto 20C hadi 33C. Kwa mfano uyoga aina ya mamama n.k. Aina hizi za uyoga pia uhitaji hali ya unyevu hewani (moisture) wa kiasi cha asilimia 75%.

UOTESHAJI WA UYOGA
Kabla ya kuanza kuzalisha uyoga inabidi kuwa na chumba chenye paa ambalo litazuia jua, mvua, na vumbi. Chumba hiki kinatakiwa kiwe na sakafu inayohifadhi unyevunyevu pamoja na sehemu ya giza ambayo ni muhimu kwa kuotesha utando wa uyoga. Mkulima
wa kawaida anaweza kutumia kasha kama sehemu ya giza.

Mbegu za uyoga huzalishwa kwenye maabara zenye vifaa vinavyowezesha kuotesha mbegu hizo bila kuchafuliwa au kuchanganyika na vimelea kama bakteria, ukungu au jamii
nyingine za uyoga ambazo haziliwi. Hapa Tanzania hivi sasa maabara hizo zipo Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo (SUA), Chuo Kikuu cha Dar es Salaam, kituo cha utafiti wa kilimo-Uyole na taasisi ya utafiti wa kilimo cha bustani- Tengeru (HORTI
Tengeru, Arusha).


HATUA MUHIMU ZA KUOTESHA UYOGA
Hatua muhimu za kuotesha uyoga baada ya kupata mbegu ni kama ifuatavyo:
Kusanya masalia ya mazao kama vile mabua, majani ya mpunga, ngano, pumba za mpunga au mahindi, masalia ya miwa baada ya kukamua nk. Vitu hivi hutumika kama mali
ghafi kwa kuoteshea uyoga.
Mabua, majani ya mpunga au migomba yakatwe kwa urefu usiozidi sm 6, au urefu wa vidole kwa kutumia panga au kisu.
Loweka mali ghafi kwenye maji ya kawaida kwa muda wa siku nzima (masaa 24).
Kisha yachemshe kwa muda wa saa mbili ili kuua vijidudu pamoja na vimelea vilivyomo.
Ipua na umwage maji yote halafu tandaza kwenye kichanja kisafi ili yapoe bila kuchafuliwa na vumbi au vijidudu.
Kisha jaza mali ghafi hii katika mifuko ya nailoni tayari kwa
kupanda mbegu.

NAMNA YA KUPANDA
Kuna aina mbili za upandaji

AINA YA KWANZA


Chukua mfuko wa nailoni wenye upana wa cm 40 - 45 na kimo cm 75. Weka tabaka la mali ghafi ya kuoteshea yenye kina cha sm 10 katika mfuko halafu tawanya mbegu ya uyoga juu yake. Baada ya kuweka mbegu, weka tena tabaka nyingine ya vioteshea na kuweka
mbegu juu yake. Endelea kuongeza tabaka kwa namna hii mpaka ifike ujazo wa robo tatu ya mfuko.

AINA YA PILI

Changanya malighafi ya kuoteshea (baada ya kuchemshwa na kupoa) na mbegu ya uyoga katika uwiano wa 1: 25 (mbegu : malighafi ya kuoteshea) kwa uyoga aina ya mamama (Pleurotus spp.)Kisha mchanganyiko huo ujazwe katika mifuko ya nailoni mifuko hii
iwe na ukubwa wa cm 20 kwa cm 40 ambamo unaweza kujaza kilo 1 – 1.5 ya mali ghafi ya kuoteshea.

Funga mifuko na toboa matundu kwenye mifuko yenye kipenyo cha cm 1 kwa kila umbali wa cm 6 hadi 10 kwa kila mfuko.Matundu yawe mengi ili kuingiza hewa ya kutosha ndani ya mifuko. Kumbuka uyoga ni kiumbe hai hivyo unahitaji kupumua kama inavyoonekana kwenye picha hapo chini.



MATUNZO
Weka mifuko kwenye chumba cha giza. Kwa mkulima wa kawaida waweza kutumia kasha lisilopitisha mwanga kama chumba cha giza. Acha mifuko humo kwa muda wa siku 14 - 21 bila kufunua ili ukungu mweupe uweze kutanda vizuri.Utando wa uyoga ukishatanda vizuri kwenye mali ghafi ya kuoteshea, hamishia kwenye chumba chenye mwanga na hewa ya kutosha kisicho pigwa na jua. Katika chumba chenye mwanga, mifuko inaweza kuwekwa
kwenye, meza, chanja la waya au miti. Mifuko inaweza pia kuning’inizwa kwenye kamba toka kwenye boriti za paa la chumba hicho. Unatakiwa kudumisha hali ya unyevu kwenye chumba hicho cha mwanga kwa kumwaga maji sakafuni. Ukiona vipando vinakauka
unaweza kunyunyizia maji yaliyochemshwa na kupoa juu ya mifuko mara tatu au zaidi kwa siku. Tumia bomba la mkononi lenye ukubwa wa lita moja kunyunyizia maji.
Tafadhali: usizidishe maji kwani maji yakiwa mengi sana yaweza kuozesha uyoga uliyoanza kuota. Aina nyingi za uyoga huanza kutoa vichwa (pini) siku 2 - 3 baada
ya kuwekwa kwenye mwanga.

UVUNAJI
Uyoga huwa tayari kuchumwa siku tatu baada ya vichwa /pini kuonekana.
Uyoga uvunwe kwa mkono kwa kushika katikati ya shina la uyoga kisha zungusha hadi uyoga ung’oke. Usiondoe kichwa peke yake katika kuvuna uyoga kwani kubakiza shina huzuia uyoga mwingine kutokea. Mkulima anatakiwa ajue soko la uyoga kabla ya kuvuna ili kuepuka gharama za kuhifadhi. Kwani uyoga ukishavunwa unatakiwa uliwe
kabla haujaharibika.

JINSI YA KUHIFADHI
i) Unaweza ukauweka uyoga kwenye mifuko ya karatasi na kuhifadhi kwenye jokofu.
ii) Unaweza ukauanika juani hadi ukauke na kuweka kwenye mifuko ya nailoni liyofungwa vizuri ili isipitishe hewa na unyevu.

SOKO LA UYOGA
i) Watu wengi hupenda uyoga mbichi uliotoka shambani wakati huo huo kama kitoweo, kwa kutumia kama nyama, samaki, au kama kiungo.
ii) Unaweza kuuza uyoga mbichi kwa bei ya shilingi 3000/= hadi 5000/= kwa kilo kwa uyoga aina ya mamama.
Pia unaweza kuuza nje ya nchi ikiwa uyoga wako ni kiasi kikubwa na uko katika viwango vinavyo kubalika kimataifa.



MAMBO YA KUZINGATIA
Uzalishaji wa uyoga huzingatia sana hali ya hewa na vifaa ulivyonavyo, hivyo basi, kabla hujachagua aina ya uyoga unaotaka kupanda pata ushauri kwa wataalamu walio
karibu nawe.

Ukishanunua mbegu, kama hupandi kwa muda huo, hakikisha umehifadhi mbegu hiyo kwenye jokofu. Kama huna jokofu la kuhifadhia, nunua mbegu baada ya kuandaa kila kitu. Hata hivyo, uotaji wa mbegu huwa mzuri kama zitakaa nje ya jokofu kwa siku mbili.

Mbegu za uyoga huwekwa ndani ya chupa yenye ujazo wa mililita 300, waweza kutumia chupa moja katika kupanda kwenye kilo 15 ya mali ghafi ya kuoteshea. Hakikisha
unamaliza mbegu yote iliyo ndani ya chupa kwani ikibaki itapata maambukizo ya vimelea.
Hakikisha unaponunua mbegu iwe ni nyeupe. Mbegu ambayo siyo nyeupe ni dalili za maambukizo ya vimelea vingine na hivyo haifai kwa kupanda.

Hakikisha chumba cha kupandia ni kisafi na hakipati vumbi toka nje ili kuzuia maambukizo ya magonjwa ya uyoga.

Usimwagilie uyoga maji yasiyochemshwa kwani maji hayo mara nyingi si salama. Yaweza kusababisha vimelea vingine kuota, kwani uyoga ni dhaifu kuhimili ushindani wa
vimelea.

Pia waweza kusababisha magonjwa ya uyoga ambayo kutibu kwake kunahitaji kutumia dawa za viwandani ambazo ni sumu na hivyo kusababisha madhara kwa mlaji. Unaweza kupata faida nyingi kutokana na uzalishaji wa uyoga,

FAIDA ZA UYOGA:-
Lishe kama protini inayolingana na ile ipatikanayo kwenye maziwa, samaki na kunde. Pia utapata vitamini B, C, na D, na madini ya joto, phosphoras, chuma na potashi.

Uyoga husadikika kutibu maradhi kama kifua kikuu, kisukari, moyo, shinikizo la damu na figo.

Masalia ya mazao hutumika katika kuzalishia uyoga, na baada ya kilimo cha uyoga yanaweza kutumika kama mbolea asili kwa kilimo cha bustani. Masalia ya kilimo cha uyoga pia hutumika kama chakula cha mifugo kama ng’ombe.

Kilimo hiki huhitaji eneo dogo sana la ardhi na kiasi kidogo cha maji, hivyo hupunguza tatizo la ukosefu wa ardhi na ugomvi katika jamii ambao unatokana na tatizo hilo.

Kilimo hiki ni njia nyepesi ya kutoa ajira kwa familia kutokana na gharama ndogo, teknolojia rahisi inayotumika na pato lake kubwa.

Sunday, February 21, 2010

MAKAKARA - PASSION FRUITS

Ni mimea inyotambaa na kuhimili hali nyingi za hewa (sio ukame) mme huu hustawi zaidi ukanda usio na baridi wastani wa 20c – 30c na kiasi cha mvua 1500mm za ujazo kwa Mwaka, tunda huwa na ukubwa wa sentimeta 10 kwa kipenyo na uzito gramu 90, kuna aina kadhaa za matunda haya lakini yale ya kijani/manjano hustawi zaidi ukanda wa pwani na yale yenye wekundu Fulani hustawi zaidi maeneo ya misitu, hupendelea udongo wa kichanga wenye mbolea na usiotuamisha maji, pia udongo usiwe na chumvi nyingi na pia kusiwe na mwamba chini kasi cha mita moja tu.



UPANDAJI
Mbegu zipandwe kwanza kwenye mifuko ya plastiki yenye udongo wenye rutuba ya kutosha , kiasi cha Mbegu 3 kwa kila mfuko na mara zinapoota mimea ikingwe na jua kali na ikifikia urefu wa sentimeta 30, huweza kuhamishiwa shambani
Kwenye shamba lako hakikisha kuna nguzo zenye waya mmoja kwa ajili ya mimea kutambaa juu yake, sehemu ya juu baada ya nguzo kuzikwa chini ibakie kama mita mbili na kati ya msatari na mstari iwe ni mita 2 (ukanda wa pwani ) na mita 3 ukanda wa juu kiasi, na umbali kati ya nguzo na nguzo kwenye mstari ni mita 6, na mimea ipandwe umbali wa mita 3 kati ya nguzo na nguzo kufuata mstari.



UANGALIZI
MBOLEA

Mbolea za viwandani ziwekwe kutokana na hali ya udongo, muone afisa ugani kilimo ili afanye vipimo kujua mahitaji na upungufu wa udongo,

MAGONJWA WADUDU
Wadudu kama chawa wa mimea na mchwa wekundu ndio adui wa makakara, pia fangasi husshambulia sana maua ya makakara. Dawa za jamii ya kopa zitumike mara dalili za magonjwa au wadudu kuonekana, kiasi cha kilo 2.8 – 3 hutosha kwa hekta moja au gramu 225 kwa ajili ya dumu moja la lita 20

MAGUGU
Makakara yanatakiwa yawe kwenye shamba safi lisilo na majani na magugu, jembe la Mkono au madawa kama ROUND-UP na GRAMOXONE ynaweza kutumika mimea ikishaefuka na kuwa juu kwenye waya

KUFUNDISHA MIMEA
Ni lazima kuyafundisha matawi mawili ya kwanza kwa kuyaelekeza kutambaa kwenye waya kila moja likielekea upande wake na matawi yatakayoota kutokana na matawi makuu nayo yaelekezwe juu kwenye waya yakifikia ukubwa wa sentimeta 30 – 40



KUPUNGUZA MATAWI
Silazima kupunguza matawi kwa sababu mmea mkubwa zaidi ndio hutoa matunda mengi zaidi, labda kama kuna matatizo katika uchumaji ndio unaweza kupunguza baadhi ya matawi kiasi.

UVUNAJI

Uvunaji huanza baada ya miezi 8 – 9 baada yam mea kupandwa na matunda hukusanywa baada ya kudondoka yenyewe chini baada ya kuiva kila baada ya wiki moja, matunda yahifadhiwe sehemu kavu na isiyo na joto , kiasi cha tani 5 – 10 huweza kupatikana katika hakta moja kwa msimu

Monday, February 8, 2010

DARAJA LINALOISHI



Huko nchini INDIA sehemu za CHERAPUNJEE ambako ni eneo tengefu lenye majimaji ambako wanapatikana watu jamii ya KHASIS huwa wanatumia mizizi ya miti jamii ya mipira kutengeneza madaraja kwa ajili ya matumizi ya kila siku.



Wanachofanya ni kuielekeza mimizi ya mti husika kukua kuelekea upende wa pili wa mto, kwa kawaida miti hii huwa na mizizi ya chini ya udongo na ile ambayo hutokea kwenye matawi na kuelea elea hewani, kwa hiyo mizizi hii inayoelea hewani huongozwa kukua kufuatana na matakwa ya watu hao mpaka upande wa pili na hapo huachiwa ikue kwa kuingia ardhini ili kupata uimara unaohitajika.



Ili kupata daraja kamili na lenye uimara unaohitajika zoezi hili huchukua kati ya miaka 10 hadi 15, na yapo madaraja yenye hadi refu wa futi 100 na huwa na uwezo wa kuhimili jumla ya watu 50 kwa pamoja kama wote watakaa juu ya daraja husika. Kati ya madaraja hayo lililo maarufu zaidi hujulikana kama UMSHIANG DOUBLE DECKER ROOT BRIDGE ambalo kama jina lake lilivyo lina njia mbili ya juu na chini

DARAJA LA UMSHIANG


Sunday, February 7, 2010

MBUZI WA MOROCCO

Mbuzi unaowaona pichani hupatikana nchini MOROCCO, inasemekana ni kawaida kuwaona mbuzi wakiwa wamepanda juu ya hivyo vichaka ni kwa sababu wanafuata matunda yajulikanayo kama ARGO, kutokana na kuyapenda sana matunda hayo basi mbuzi hao hudandia juu ya matawi ya vichaka ili kupata matunda hayo