Karibuni kwenye blog yangu ambayo najaribu kutoa elimu kidogo niliyo nayo. Kama unataka kufanya kilimo, ufugaji wanyama, ufugaji wa samaki, ufugaji wa nyuki, kilimo cha miti ya mbao, kilimo cha majani na malisho ya mifugo, utaalamu wa mbolea na udongo katika mazingira halisi ya ki Tanzania basi wasiliana nami (mitiki1000@gmail.com) NB sihusiki na habari za masoko ya bidhaa yoyote ya kilimo na mifugo, kabla hujaingia kwenye mradi fanya utafiti wa masoko wewe mwenyewe
Thursday, December 22, 2016
Tuesday, July 12, 2016
AGRI-HUB TANZANIA
Agri-Hub Tanzania ilizinduliwa rasmi Oktoba 2012. Uzinduzi huo ulikuwa tukio lenye maana kubwa kwa wote waliokuwepo, ikizingatiwa kwamba ipo haja kubwa ya kushrikiana na kuunganisha juhudi katika uimarishaji wa kilimo. Serikali ilifurahishwa na hatua hii ambayo pia iliungwa mkono na sekta binafsi, jumuiya za wakulima na asasi za kijamii. Wanachama wa Agri-Hub wameunda vikundi-kazi 5 ambavyo vitakuwa na shughuli zifuatazo: uhamasishaji, mafunzo, kuratibu utendaji na mbinu za kibunifu kwa lengo la kuimarisha uzalishaji endelevu wa chakula na kuboresha maisha ya wakulima wa Mkoa wa Arusha.
Shughuli za awali
Kundi la uchanganuzi lililopendekezwa na wanachama kadhaa wa Agri-ProFocus na wadau wengine nchini lilileta msukumo uliowezesha kuanzishwa Agri-Hub Tanzania. Hadi kufikia sasa, tayari jumuiya zipatazo 25 zimeshajiunga na taasisi hii, ikiwa ni pamoja na: SNV, RijkZwaan, TRIAS, Cordaid, Hivos, Agriterra, Farm Africa na Faida Mali. Taasisi zote zina dhamira moja: kuunga mkono shughuli za Agri-Hub Tanzania kwa kujitolea kwa hali na mali katika kuendeleza Agri-Hub. Arusha, jiji lililo kaskazini mwa Tanzania ambalo lina umuhimu mkubwa katika shughuli za kilimo likiwa pia ni makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), liliteuliwa kuwa makao makuu anzilishi ya Agri-Hub.
Upangaji wa agenda: Warsha wa wadau wa sekta mbalimbali
Hafla ya kikazi iliyofanyika tarehe 5, Oktoba ilitayarishwa kwa lengo la kuwaarifu wadau wa kilimo na wengineo wenye ushirika na kilimo katika Mkoa wa Arusha, juu ya mikakati iliyokuwa ikitayarishwa na pia, juu ya warsha wa mipango.
Warsha wa Wadau wa Sekta Mbalimbali (22 – 23 Oktoba, 2012) ilitoa fursa kwa wanachama wa Agri-Hub kupanga Agenda.
Wakati wa warsha, wanachama waliunda vikundi-kazi vifuatavyo:
- Upatikanaji wa Ardhi
- Upatikanaji wa Mitaji
- Upatikanaji wa Pembejeo
- Upatikanaji wa Masoko
- Mtazamo wa Kibiashara kwa Wakulima
Upatikanaji wa ardhi
Ijapokuwa sheria za Tanzania zinatambua haki ya wakulima wadogo kumiliki ardhi na kufanya shughuli za kilimo kwenye ardhi hiyo, wakazi wengi wa vijijini hawajaelimishwa juu ya manufaa mengi wawezayo kuyapata kutokana na ardhi yao.
Kikundi-kazi hiki kina lengo la kuboresha hali ya wakulima kwa kuwapa mafunzo na wadau wengine wa ardhi jinsi ya kutumia kwa manufaaa yao Sheria za Ardhi zilizopo.
Upatikanaji wa mitaji
Huduma za kifedha kwa wakulima ni suala muhimu kwa jamii inayotegemea kilimo kama Tanzania. Kikundi-kazi cha mitaji kimetayarisha mlolongo wa shughuli kwa minajili ya kuunga mkono harakati za utafutaji wa mitaji kwa miaka mingi ijayo. Kikundi hiki kinatazamia kupanga na kujenga ushirikiano na mikakati ambayo tayari ipo (kama vile like Maonyesho ya Kilimo-Biashara, nk) kwa lengo la kuongeza utelekelezaji na utendaji wa kiwango cha juu iwezekanavyo.
Upatikanaji wa Pembejeo
Kulingana na mtazamo wa kikundi-kazi cha pembejeo, upatikanaji na uwepo wa taarifa kamili juu ya pembejeo ni jukumu la pamoja la wakulaima, makampuni mbalimbali na serikali.
Kikundi hiki kimetayarisha shughuli mbalimbali zenye lengo la kuunganisha hawa wadau wote ili waweze kufikia lengo hili:kuwaelekeza wakulima wajue ni wapi pa kupatia pembejeo na waweze kufanya uteuzi sahihi wa pembejeo hizo na jinsi ya kuzitumia.
Upatikanaji wa Masoko
Maudhui ya kipengele hiki yanajumuisha maudhui mengine kadhaa madogovidogo, kama vile: Mfumo wa taarifa za masoko, kukutana na wanunuzi, kilimo cha mkataba na mengineyo. Hatua inayofuata ni kuangalia ni nini ambacho kila mwanachama wa kikundi-kazi anaweza kuchangia katika majadiliano. Aidha, kunakuwepo na uchunguzi kuona ni jumuiya gani ambazo zingepaswa kuhusishwa lakini bado hazipo, ili ziweze kuunaginshwa na Agri-Hub.
Mtazamo wa kijasiriamali kwa wakulima
Kujengea wakulima mtazamo wa kijasiriamali ndio lengo kuu la Agri-ProFocus. Lakini je, ni kwa vipi tutaweza kutekeleza azma hii katika kiwango cha kimkoa? Kikundi-kazi hiki kinalenga kuwahamasisha wakulima wenye upeo wa juu kuliko wenzao, waweze kuthibitisha wazi kuwa kilimo biashara yenye tija kama biashara zingine, iwapo itaendeshwa kwa njia sahihi.
Je, ungependa kujiunga?
Shughuli za Agri-Hub zimo katika matayarisho na utekelezaji wake utaanza hivi karibuni. Iwapo una nia ya kuingiza mada yako katika agenda, basi jiunge na vikunndi-kazi vilivyoorodheshwa hapo juu mapema iwezekanavyo. Agri-Hub Tanzania itakuwezesha kupata washirika ambao, kwa kujiunga nao, utaweza kufanikiwa katika malengo yako!
Kwa maelezo zaidi:
Apollo Muyanja Mbazzira (SNV)
Mratibu wa Agri-Hub Tanzania
Baruapepe: amuyanja.agrihub@gmail.com
Simu: +255 22 260 0340
Marjolein de Bruin
Mwezeshaji mtandao: mdebruin@agri-profocus.nl
Simu: +31 (0)26 3542056
Jiunge na jukwaa la Intaneti:
http://apf-tanzania.ning.com/ Agri-Hub Tanzania, Plot 1124, Chole Road, Msasani Peninsular, P.O. Box 3941, Dar es Salaam, Tanzania
Agri-ProFocus, Willemsplein 43-II / P.O. Box 108 – 6800 AC ARNHEM (NL)
T: +31 (0)26 354 2074 / E: info@agri-profocus.nl / www.agri-profocus.nl
Shughuli za awali
Kundi la uchanganuzi lililopendekezwa na wanachama kadhaa wa Agri-ProFocus na wadau wengine nchini lilileta msukumo uliowezesha kuanzishwa Agri-Hub Tanzania. Hadi kufikia sasa, tayari jumuiya zipatazo 25 zimeshajiunga na taasisi hii, ikiwa ni pamoja na: SNV, RijkZwaan, TRIAS, Cordaid, Hivos, Agriterra, Farm Africa na Faida Mali. Taasisi zote zina dhamira moja: kuunga mkono shughuli za Agri-Hub Tanzania kwa kujitolea kwa hali na mali katika kuendeleza Agri-Hub. Arusha, jiji lililo kaskazini mwa Tanzania ambalo lina umuhimu mkubwa katika shughuli za kilimo likiwa pia ni makao makuu ya Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), liliteuliwa kuwa makao makuu anzilishi ya Agri-Hub.
Upangaji wa agenda: Warsha wa wadau wa sekta mbalimbali
Hafla ya kikazi iliyofanyika tarehe 5, Oktoba ilitayarishwa kwa lengo la kuwaarifu wadau wa kilimo na wengineo wenye ushirika na kilimo katika Mkoa wa Arusha, juu ya mikakati iliyokuwa ikitayarishwa na pia, juu ya warsha wa mipango.
Warsha wa Wadau wa Sekta Mbalimbali (22 – 23 Oktoba, 2012) ilitoa fursa kwa wanachama wa Agri-Hub kupanga Agenda.
Wakati wa warsha, wanachama waliunda vikundi-kazi vifuatavyo:
- Upatikanaji wa Ardhi
- Upatikanaji wa Mitaji
- Upatikanaji wa Pembejeo
- Upatikanaji wa Masoko
- Mtazamo wa Kibiashara kwa Wakulima
Upatikanaji wa ardhi
Ijapokuwa sheria za Tanzania zinatambua haki ya wakulima wadogo kumiliki ardhi na kufanya shughuli za kilimo kwenye ardhi hiyo, wakazi wengi wa vijijini hawajaelimishwa juu ya manufaa mengi wawezayo kuyapata kutokana na ardhi yao.
Kikundi-kazi hiki kina lengo la kuboresha hali ya wakulima kwa kuwapa mafunzo na wadau wengine wa ardhi jinsi ya kutumia kwa manufaaa yao Sheria za Ardhi zilizopo.
Upatikanaji wa mitaji
Huduma za kifedha kwa wakulima ni suala muhimu kwa jamii inayotegemea kilimo kama Tanzania. Kikundi-kazi cha mitaji kimetayarisha mlolongo wa shughuli kwa minajili ya kuunga mkono harakati za utafutaji wa mitaji kwa miaka mingi ijayo. Kikundi hiki kinatazamia kupanga na kujenga ushirikiano na mikakati ambayo tayari ipo (kama vile like Maonyesho ya Kilimo-Biashara, nk) kwa lengo la kuongeza utelekelezaji na utendaji wa kiwango cha juu iwezekanavyo.
Upatikanaji wa Pembejeo
Kulingana na mtazamo wa kikundi-kazi cha pembejeo, upatikanaji na uwepo wa taarifa kamili juu ya pembejeo ni jukumu la pamoja la wakulaima, makampuni mbalimbali na serikali.
Kikundi hiki kimetayarisha shughuli mbalimbali zenye lengo la kuunganisha hawa wadau wote ili waweze kufikia lengo hili:kuwaelekeza wakulima wajue ni wapi pa kupatia pembejeo na waweze kufanya uteuzi sahihi wa pembejeo hizo na jinsi ya kuzitumia.
Upatikanaji wa Masoko
Maudhui ya kipengele hiki yanajumuisha maudhui mengine kadhaa madogovidogo, kama vile: Mfumo wa taarifa za masoko, kukutana na wanunuzi, kilimo cha mkataba na mengineyo. Hatua inayofuata ni kuangalia ni nini ambacho kila mwanachama wa kikundi-kazi anaweza kuchangia katika majadiliano. Aidha, kunakuwepo na uchunguzi kuona ni jumuiya gani ambazo zingepaswa kuhusishwa lakini bado hazipo, ili ziweze kuunaginshwa na Agri-Hub.
Mtazamo wa kijasiriamali kwa wakulima
Kujengea wakulima mtazamo wa kijasiriamali ndio lengo kuu la Agri-ProFocus. Lakini je, ni kwa vipi tutaweza kutekeleza azma hii katika kiwango cha kimkoa? Kikundi-kazi hiki kinalenga kuwahamasisha wakulima wenye upeo wa juu kuliko wenzao, waweze kuthibitisha wazi kuwa kilimo biashara yenye tija kama biashara zingine, iwapo itaendeshwa kwa njia sahihi.
Je, ungependa kujiunga?
Shughuli za Agri-Hub zimo katika matayarisho na utekelezaji wake utaanza hivi karibuni. Iwapo una nia ya kuingiza mada yako katika agenda, basi jiunge na vikunndi-kazi vilivyoorodheshwa hapo juu mapema iwezekanavyo. Agri-Hub Tanzania itakuwezesha kupata washirika ambao, kwa kujiunga nao, utaweza kufanikiwa katika malengo yako!
Kwa maelezo zaidi:
Apollo Muyanja Mbazzira (SNV)
Mratibu wa Agri-Hub Tanzania
Baruapepe: amuyanja.agrihub@gmail.com
Simu: +255 22 260 0340
Marjolein de Bruin
Mwezeshaji mtandao: mdebruin@agri-profocus.nl
Simu: +31 (0)26 3542056
Jiunge na jukwaa la Intaneti:
http://apf-tanzania.ning.com/ Agri-Hub Tanzania, Plot 1124, Chole Road, Msasani Peninsular, P.O. Box 3941, Dar es Salaam, Tanzania
Agri-ProFocus, Willemsplein 43-II / P.O. Box 108 – 6800 AC ARNHEM (NL)
T: +31 (0)26 354 2074 / E: info@agri-profocus.nl / www.agri-profocus.nl
Tuesday, September 15, 2015
KILIMO BORA CHA MTAMA
Mtama ni kundi
la mbegu ndogo aina ya mazao ya nafaka au nafaka ambayo kwa jina la kisayansi unajulikana kama
(Sorghum bicolor), ni mazao yanayolimwa sana duniani kote kwa ajili ya chakula na lishe Mtama hutoa
mazao mengi hata kwenye hali ambayo haifai kwa kilimo cha aina nyingine za
mazao ya nafaka. Mtama una uwezo mkubwa wa kustahimili ukame.
Mtama
unaweza kutumika kwa kuchemshwa na kuliwa kama ulivyo, kusagwa na kutumika kwa
uji, kutengenezea vinywaji kama vile bia, kuoka mikate, na aina nyinginezo za
vitafunwa. Mmea wa mtama pia hutumika kwa ajili ya malisho ya mifugo kama vile
hay na sileji. Mtama unastawis vizuri kwenye mazingira yenye wastani wa
milimita 400 – 700 za mvua kwa mwaka. Pia mtama unavumilia sehemu
zinazotuhamisha maji, na unaweza kulimwa sehemu zenye mvua nyingi.
Mtaama
unafaa pia kwa sehemu kame zenye wastani wa joto la chini kiasi cha nyuzi joto
18°C, ili kuweza kuota vizuri, na kiasi cha nyuzi joto 25-30°C ili kukua
vizuri. Mtama hauwezi kuvumilia barafu. Mtama unaweza kukua kwenye aina zote za
udongo. Kwa kiasi kikubwa unafaa zaidi kwenye udongo wa mfinyanzi, lakini pia kwenye
udongo ambao una kiasi kidogo cha mchanganyiko wa kichanga. Mtama unaweza
kuvumilia uchachu kwenye udongo kuanzia pH 5.0-8.5, na inavumilia udongo wenye
chumvi kuliko yalivyo mahindi.
Aina za
mtama
Kwa jumla kuna aina zaidi ya 30 za mtama zinazolimwa kama
chakula. Mtama hustawi vizuri kwenye joto ikivumilia pia ukame. Hivyo ni nafaka
muhimi kwenye maeneo yabisi za Afrika. Katika miaka ya nyuma kilimo chake
kiliachwa mara nyingi kwa ajili ya mahindi kwa sababu mahindi huleta mazao
makubwa zaidi kwa ekari. Lakini wakati wa ukame mahindi ni hasara na watu
hurudi-rudi kwenye kilimo cha mtama.
Aina za
mtama zinatofautiana kulingana na rangi zake, kuna nyeupe, nyekundu, na
kahawia. Mbegu za asili huwa zinachavushwa kwa urahisi zaidi lakini mavuno yake
huwa ni hafifu ukilinganisha na mbegu za kisasa. Hata hivyo, aina za kisasa
zinazalishwa kwa gharama nafuu zaidi zinapopandwa kwa kufuata kanuni za kilimo
bora.
Serena:
Ina punje za kahawia. Aina hii hustawi kwenye eneo lenye mvua za wastani na
hukomaa katika kipindi cha siku 110. Aina hii huwa na shina na mizizi imara,
ambapo huweza kuzalisha kiasi cha kilo 3,000 kwa hekari moja. Ambapo
zinahitajika kilo 5 za mbegu kwa hekari moja. Aina hii ina uwezo wa kukabiliana
na ugonjwa milia, kutu, na madoa ya kahawia kwenye majani.
Seredo:
Hii ni aina nyingine yenye punje za kahawia, na inapendekezwa Kulimwa kwenye
eneo lenye mwinuko wa mita 1,500 kutoka usawa wa bahari. Aina hii huchanua
baada ya siku 71 na hukomaa katika kipindi cha siku 120. Aina hii huwa ni
ndefu, na ina uwezo wa kuzalisha kilo 5000 kwa hekari moja. Ina uwezo wa
kukabiliana na ugonjwa wa milia, kutu, mabaka kwenye majani, na madoa ya
kahawia kwenye majani.
Gadam: Inafanya
vizuri katika sehemu ambazo si kame sana. Katika nchi nyingi mfano Kenya, aina
hii ya mtama hutumika kutengenezea bia na pia kwa chakula. Aina hii huvumilia
bungo na ugonjwa wa majani.
Hakika na
Wahi: Hizi ni aina mbili za mtama ambazo zimezalishwa na kituo
cha Utafiti wa Kilimo cha Ilonga kwa ajili ya kuoteshwa kwenye mashamba
yalioathiriwa na viduha. Mbegu hizi zina rangi ya manjano iliyopauka. Unga wa
aina zote mbili zinafaa sana kwa kupika ugali.
Utayarishaji
wa shamba na kupanda
Kwa
kawaida mtama hupandwa kwa kutumia mbegu. Mbegu hupandwa shambani moja kwa moja
baada ya shamba kuandaliwa, lakini pia zinaweza kurushwa shambani, kasha
zikavurugwa pamoja na udongo. Unapaswa kutayarisha shamba la kupanda mtama, iwe
ni kwa ajili ya malisho au chakula kabla mvua za msimu hazijaanza. Zao hili
hufanya vizuri zaidi kwenye udongo ulio laini. Linaweza pia kupandwa kwenye
udongo ambao haukulimwa vizuri na bado ukaota vizuri.
Nafasi:
Mtama unaopandwa kwa ajili ya malisho, unaweza kupandwa kwa nafasi ya sentimita
75×10. Aina za mtama ambazo zinalengwa kwa ajili ya lishe kwa binadamu na
wanyama, zinahitaji nafasi kiasi cha sentimita 60×20. Nafasi hutoa mwanya wa
kuwa na kiwango kikubwa cha malisho. Mkulima anaweza kupanda mbegu za mtama
kiasi cha kilo 2.4-3.3 kwa hekari moja. Ni mara chache sana mbegu hupandwa
kwenye vitalu na kuhamishiwa shambani baadaye.
Kupanda:
Mtama hupandwa mvua zinapoanza kunyesha. Mbegu ni lazima zifukiwe ardhini usawa
wa sentimita 3 kwenda chini, hii itasaidia kuepuka kuota wakati ambao si msimu
kamili wa mvua. Pia zinaweza kufukiwa kiasi cha sentimita 2 wakati ardhi
inapokuwa na unyevu. Mtama unahitaji rutuba ya hali ya juu wakati wa kupanda na
wakati wa kuota. Ni vizuri kutumia samadi au mboji iliyooza vizuri wakati wa
kuandaa shamba.
Mseto:
Unaweza kupanda mtama mseto na mazao jamii ya mikunde, na kuongeza mboji
shambani mwako. Hii inaweza kuwa njia nzuri zaidi ya kupata virutubisho
vinavyohitajika. Mseto wa mazao jamii ya mikunde inashauriwa iwe ni kama vile
maharagwe, kunde, n.k
Uangalizi
na utunzaji
Ni lazima
kung’oa baadhi ya mimea inapokuwa na urefu wa sentimita 30, au siku 30 baada ya
kupanda, ili kuwa na uhakika wa nafasi ya sentimita 10 kati ya mstari na mstari
kwa mtama unaokusudiwa kwa ajili ya malisho, na nafasi ya sentimita 20 kati ya
mstari kwa mtama uliokusudiwa kwa ajili ya chakula na lishe ya mifugo.
Palizi ya
mkono ifanyike walau mara mbili. Shamba la mtama ni lazima liwekwe katika hali
ya usafi na kutokuruhusu magugu wakati wote hasa katika kipindi cha mwanzoni.
Monday, September 7, 2015
PATA USHAURI WA BURE KUPITIA SIMU YAKO
Pata ushauri wa bure kuhusiana na kilimo kwa njia ya simu kupitia mtandao wa ushauri kwa wakulima (MUWA).
MUWA inaratibiwa na mradi wa EPINAV - 'MOBILE FOR IMPROVING AGRICULTURE EXTENSION SERVICE'(http://ushaurikilimo.org/) uliopo Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo.
MUWA inawawezesha wakulima kupata ushauri katika mambo mbalimbali yanayohusu kilimo kama vile ukulima, uvunaji, ufugaji wa wanyama, utuzaji wa misitu, maendeleo ya jamii, masoko na msaada wa kiuchumi katika kuendeleza kilimo.
Kama unapenda kupewa ushauri kupitia simu yako ya mkononi unaweza kutuma swali lako kupitia namba 0688099408 na mabwana na mabibi shamba watakujibu mara moja!
NB: Huduma hii ni bure ila mkulima utalipia gharama ya ujumbe mfupi wa simu kwa kampuni husika ya simu. Mradi utalipia gharama ya ujumbe mfupi wa simu wenye majibu ya swali la mkulima.
TOVUTI: http://ushaurikilimo.org/
Bofya hapa chini kuona maswali na majibu yaliyokwisha jibiwa: http://ushaurikilimo.org/ maswalimajibu.php
MUWA inaratibiwa na mradi wa EPINAV - 'MOBILE FOR IMPROVING AGRICULTURE EXTENSION SERVICE'(http://ushaurikilimo.org/) uliopo Chuo Kikuu cha Sokoine cha Kilimo.
MUWA inawawezesha wakulima kupata ushauri katika mambo mbalimbali yanayohusu kilimo kama vile ukulima, uvunaji, ufugaji wa wanyama, utuzaji wa misitu, maendeleo ya jamii, masoko na msaada wa kiuchumi katika kuendeleza kilimo.
Kama unapenda kupewa ushauri kupitia simu yako ya mkononi unaweza kutuma swali lako kupitia namba 0688099408 na mabwana na mabibi shamba watakujibu mara moja!
NB: Huduma hii ni bure ila mkulima utalipia gharama ya ujumbe mfupi wa simu kwa kampuni husika ya simu. Mradi utalipia gharama ya ujumbe mfupi wa simu wenye majibu ya swali la mkulima.
TOVUTI: http://ushaurikilimo.org/
Bofya hapa chini kuona maswali na majibu yaliyokwisha jibiwa: http://ushaurikilimo.org/
Monday, April 27, 2015
JINSI YA KUANDAA MBEGU ZA MITIKI
Hizi ni mbegu kutoka kwa wakala wa mbegu wa taifa (TTSA) wanaopatikana eneo la Kihonda Morogoro Mjini
Nilinunua jumla ya kilo 4 kwenye mifuko ya kilo mojamoja kwa kila mfuko
Nilifungua mifuko yangu na kuweka mbegu zote kwenye kiroba kimoja
Nikaweka mawe ndani ya kiroba ili kukipa uzito utakao nihakikishia mbegu kuzama zitakapo kuwa ndani ya maji
weka kwemye pipa na utie maji, kilo moja ya maji inahitaji kama lita 20 ambazo utabadilisha kila baada ya masaa 12 yaani asubuhi na jioni kwa muda wa siku 7 kisha utazitoa na kuzianika kwa siku moja kabla ya kuzipanda kwe ye kitalu

Tuesday, September 16, 2014
TRACTOR FOR SALE - TREKTA LINAUZWA
Tractor Massey Ferguson 3080, 2 wheel drive 90 HP kama mpya inauzwa kwa bei poa sana, na imewasili Tanzania tayari kutoka denmark, (serious buyers only) kwa mawasiliano zaidi na bei piga 004560248586 au 004553901576
Thursday, May 22, 2014
JINSI YA KUKATA MICHE YA MISOJI (MITIKI) marudio
MCHE KABLA YA KUKATWA (angalia mishale kujua sehemu za kukata)
Mche wangu niliukata na kuacha kiasi cha nchi mbili au pingili mbili za vidole kwa sehemu ya juu ya mzizi na kwenye mzizi niliondoa ile sehemu nyembamba ya chini, kwa kawaida hii sehemu ya chini hufa mara baada ya kupandwa kwa sababu sehemu nene/kubwa ya mzizi inayoachwa ndiyo huifadhi maji na chakula cha mmea, nadhani hapa nitakuwa nimemsaidia kama bado nipigie kwenye ile namba niliyokupa
KIPANDIKIZI TAYARI KWA KUPANDWA
Kumbuka wakati wa kupandwa lazima uweke kisahani ili kiweze kukusanya maji kwa ajili ya ukuaji mzuri, kama ni udongo unaotuamisha maji usiweke kisahani bali wekea kama tuta au mwinuko
WEKA KISAHANI KAMA UDONGO HAUTUAMISHI MAJI
WEKA TUTA KAMA UDONGO UNATUAMISHA MAJI
Tuesday, April 29, 2014
UANDAAJI WA MBEGU ZA MITIKI
Mbegu za mitiki ni lazima ziandaliwe kabla ya kusia kitaluni, hakikisha umeshaanda kitalu chako mapema na kiwe na udongo wenye rutuba ya kutosha, mwagia maji ya kutosha ili kama kuna magugu yaanze kuota na kung'olewa mapema, hii inasaidia kwa sababu mbegu za mitiki huchukua muda mrefu kuota, sasa ukianza kung'olea na mbegu hazijaota au miche ni midogo utakuwa unaing'oa na yenyewe
Kwa kila kilo moja ya mbegu ina hitaji ndoo ya maji lita 20, weka mbegu zako kwenye gunia au kiroba, kisha weka vitu vizito kama mawe ili kuhakikisha mbegu zako zinakuwa chini ya maji, kinyume na hapo zitaelea juu na hutapata matokeo mazuri katika uotaji, bila kufanya hivi mbegu zko hazitaota kwa wingi
Hili ni pipa la lita 200, linatosha kwa kilo 10, badilisha maji yako kila jioni na asubuhi kwa muda wa siku 7. kama utaweka maji mara mbili zaidi unaweza kubadilisha maji mara moja kwa siku, yaani kilo moja kwa maji lita 40. Kama kuna maji yanayotembea kama vijito vidogo basi unaweza kuloweka humo bila kuziondoa kwa siku 7.
Siku ya 8 anika mbegu zako juani, ni vizuri kama utaziweka kwenye bati ili zipasuke gamba lake na kusaidia uotaji
Panda mbegu zako kwa msitari, chora mfereji wenye kina cha sentimeta moja na uziweke kwenye huo mfereji mwanzo mpaka mwisho bila kuruka nafasi, acha nafasi ya sentimeta 18 - 20 kati ya fereji na mfereji kama inavyoonekena kwenye picha juu na chini
Baada ya wiki tatu mbegu zitaanza kuota na zitaacha kuota baada ya siku 65, uotaji ni kiasi cha 45% mpaka 50%, kilo moja ina wastani wa mbegu 800 mpaka 1000, kwa hiyo unaweza kupata mpaka miche 500 kwa kilo moja, Mbegu zinapatika kwa WAKALA WA MBEGU WA TAIFA kwa bei ya shilingi 9000/= kwa kilo, wanapatikana Morogoro mjini, eneo la Kihonda ukitokea msamvu kama unaelekea Dodoma ni kama kilometa 3, unaweza kupanda daladala, bodaboda au hata taxi na ukafika
Friday, March 28, 2014
TOGGENBURG - AINA BORA YA MBUZI WA MAZIWA
Hii ni aina ya mbuzi wa maziwa ambao asili yake ni uswizi
katika eneo la Obertoggenburg kama wanavyoitwa, hii ndio mbegu ya mbuzi wa
maziwa wa zamani zaidi kuliko zote. Kwa hapa Tanzania wanapatikana Uyole, SUA
na Tengeru (hivi vyote ni vyuo vya mifugo)
UZALISHAJI
Mbuzi hawa wanauwezo wa kuzalisha maziwa wastani wa lita
mbili kwa siku au zaidi, hawatoi maziwa mengi kama Saanen ila maziwa yao yana
kiasi cha mafuta kati ya 3% - 4%
MAUMBILE
Mbuzi hawa wana umbile la wastani lakini ni wakubwa kuliko
mbuzi wa kienyeji, kilo 55 kwa majike na kilo 75 kwa madume, wana rangi ya
kahawia (khaki) mpaka hudhurungi (brown)
pia wana mistari miwili usni yenye rangi ya maziwa au nyeupe kuanzia juu
mpaka kwenye pua (kama duma) huwa na viwele (udder) vikubwa na pia ni wazazi na
walezi wazuri, mara nyingi huweza kuzaa mapacha
HALI YA HEWA
Mbuzi hawa hawawezi kuhimili hali ya joto, bali hufanya
vizuri kwenye maeneo yanye baridi kama mikoa ya Mbeya, Iringa, Ruvuma, Njombe,
Dodoma, Singida n.k. Wanahitaji chakula chakutosha ili kutoa maziwa mengi, pia
chakula kiwe na virutubisho kamili. Ingawa pia wanaweza kuchungwa kwenye maeneo
yenye ukame kiasi na wakaweza kufanya vizuri (good foragers)
TABIA
Mbuzi hawa huishi kwa makundi wakitoroka au kuingia kwenye
shamba la mazao basi huenda wote na hufundishika kirahisi sana hii husababisha
urahisi wa kuwafundisha kukamuliwa na mashine
FAYC KAY TRADING LTD - WAUZAJI WA MATREKTA NA ZANA ZA KILIMO
Hawa ni wajasiliamali wa kiTanzania waishio nchini Denmark, wanauza zana za kilimo zilizotumika (used) kama matrekta na majembe yake, matrailer, irrigation water pumps, Chemicals sprayer, harrows, planters, combining harvesters n.k
Unaweza kuwasiliana nao kwa namba zifuatazo wakiwa Denmark 0004560248586 au 0004527201580 unaweza kuwapigia au kwa kutumia whats up. pia wana email zifuatazo charlesurban00@hotmail.com au sweetfaydat@gmail.com
Wanazo brand za kimataifa zenye ubora wa hali ya juu kama Massey Ferguson, John Deere, New Holland, Ford na nyinginezi nyingi
Wednesday, March 26, 2014
KILIMO BORA CHA MDALASINI - CINNAMON
Mti wa mita 10 au zaidi. Hutoa machipukizi na kuota miti zaidi ya mmoja kwenye shina moja na kuongeza mavuno mengi, haya mashina mapya yasing'olewe bali yaachwe yakue na kuwa mti mkubwa.
AINA
Mchanganyiko; za kienyeji (ndogo) na za kigeni ( kubwa)
HALI YA HEWA NA UDONGO
· Mvua nyingi za kutosha 2000mm -2500mm kwa mwaka
· Udongo wenye rutuba
· Joto kwa wingi
· Hewa yenye unyevunyevu
KUSIA MBEGU KWENYE VITALU
· Mbegu hupatikana kwenye miti iliyokomaa
· Sia mbegu kwenye kitalu zikiwa nusu sentimeta chini ya udongo
· Baada ya kuchipua, mbegu huchukua miezi 6 hadi mwaka mmoja kufikia umri wa kupandikiza shambani
· Panda miche wakati wa masika
· Panda kwa nafasi ya 2m x2m. Nafasi hizi huwezesha miti kutoa machipukizi mengi. Nafasi kubwa hufanya miti kuwa na matawi mengi pia mashina hayanenepi wala kurefuka
UTUNZAJI
· Acha machipukizi kwenye shina
· Toa matawi kwenye mashina ili kunenepesha mashina
· Weka shamba katika hali ya safi
· Zuia magonjwa kama.
- Vinundu (galls)wanaosababishwa na utitiri na wadudu scales na mealbugs kwa kutumia dawa za sumu kama Selecron, Karate nk.
KUVUNA
· Anza kuvuna miaka 3 baada ya kupanda
· Mazao ya mdalasini ni maganda ya mashina ya miti
· Kata shina la mti,na tenganisha maganda na mti kwa njia ya kumenya
· Kuwa mwangalifu ili ganda litoke vizuri bila kupasukapasuka
· Seli za nje ya ganda la mdalasini ni chungu hivyo ni vizuri ziondolewe kwa kukaruza kwa kisu
· Kausha vizuri siyo kwenye jua kali Mavuno
· 0.25 kg – 10kg maganda yaliyokaushwa kwa mti mmoja. Kiasi cha mazao hutegemea ukubwa na umri wa mti
· Ubora wa mdalasini hushuka kulingana na umri wa mti. Mti wa umri mkubwa hutoa mganda yenye ubora wa chini
MATUMIZI
Mdalasini baada ya kukaushwa ikiwa umesagwa au bila kusagwa hutumika kama:
· Kiungo kwenye chakula na vitafunwa kama keki, mandazi,vitumbua
· Vikolezo kwenye vinjwaji km. chai, kahawa
· Dawa ya tumbo hasa wakati wa kuvimbiwa, kutoa hewa tumboni pia kuongeza hamu ya chakula
· Dawa ya ngozi
JINSI YA KUTUMIA
· kiungo kwenye chakula
Tumia maganda au saga magada yaliyokauka. Tumia ili kuongeza ladha kwenye vyakula kama pilau, ndizi, mchuzi nk
· Kutengenezea kinywaji
Weka vipanda vichache 2-3 (30gm) vya maganda kwenye kikombe ongeza maji yanayochemka, funika kwa dakika 15, ongeza vipande vya limao. Kunywa kila baada ya kula
MANUFAA
· Miti hudumu shambani zaidi ya miaka 20. Miti huchipua na kutoa machipukizi mengine kila baada ya kuvuna
· Gharama ndogo ya uzalishaji
· Mazao yaweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu
· Magonjwa na wadudu ni kidogo
· Rahisi kuchanganya na mazao mengine
· Nguvu kidogo, kipato kikubwa.
Thursday, December 19, 2013
NDIKANA KALI - EAST COAST FEVER
Ugonjwa huu hushambulia wanyama kama ng'ombe, mbuzi na kondoo na husababishwa na vimelea vijulikanavyo kama Theileria parva ambavyo vusambazwa na kupe wekundu wa kwenye masikio wajulikanavyo kama Rhepicephalus Appendiculatus, ugonjwa huu usipodhibitiwa unaweza kusababisha vifo vya wanyama wengi sana na pia ni aghali kuutibu kulinganisha na magonjwa mengine
Homa kali, mnyama kushindwa kupumua vizuri, kukohoa pamoja na kutoa makamasi, kuharisha na kuvimba matezi
MATIBABU
Mnyama inabidi apigwe sindano ya dawa za PARVAQUONE au BUTALEX kiasi cha ml 20 (soma kimbatanisho cha dawa kwa maelezo zaidi) na kurudia baada ya siku moja kupita, yaani ukuchoma leo unarudia dozi kesho kutwa, pia mnyama achomwe dawa ya OTC20% kipindi chote cha matibabu
KINGA
Kinga kubwa ya ugonjwa huu ni kuhakikisha kwamba mifugo yako inaoga mara kwa mara kwenye majosho au kwa kuwanyunyuzia dawa za kuua wadudu wa mifugo
KUPE WEKUNDU KWENYE MASIKIO YA NG'OMBE
DALILI ZA UGONJWA HUUHoma kali, mnyama kushindwa kupumua vizuri, kukohoa pamoja na kutoa makamasi, kuharisha na kuvimba matezi
MATIBABU
Mnyama inabidi apigwe sindano ya dawa za PARVAQUONE au BUTALEX kiasi cha ml 20 (soma kimbatanisho cha dawa kwa maelezo zaidi) na kurudia baada ya siku moja kupita, yaani ukuchoma leo unarudia dozi kesho kutwa, pia mnyama achomwe dawa ya OTC20% kipindi chote cha matibabu
KINGA
Kinga kubwa ya ugonjwa huu ni kuhakikisha kwamba mifugo yako inaoga mara kwa mara kwenye majosho au kwa kuwanyunyuzia dawa za kuua wadudu wa mifugo
NG'OMBE WAKIOGESHWA KWENYE DAWA
KUPUNGUZIA MATAWI MITI YA MITIKI - PRUNING TEAK TREES
Umuhimu wa zoezi hili ni kuhakkisha miti yako inanyooka, kukua kwa haraka na kuwa na mbao bora, miti inapokuwa na matawi haikui kwa haraka maana chakula kinagawanywa pamoja na matawi, lakini kama mti hauna matawi mengi basi hunenepa na kurefuka kwa haraka, pia kwa kuondoa matawi yakiwa machanga unoaongeza ubora wa mbao maana hazitakuwa na vidonda vinavyo sababishwa na matawi
Tuesday, November 26, 2013
IVOMEC / IVERMECTIN
Hii ni dawa inayukuja na majina kadhaa kama Ivomec, Ivermectin, Zimectin, Iverhart au Tri-heart kutegemea na iana ya mtengenezaji wa dawa hii.
Dawa hii imeonesha mfanikio makuwa katika kupambana na minyoo duara, minyoo bata, minyoo ya moyo, viroboto na ukurutu.Dawa hii huweza kutumika kwenye wanyama kama Mbuzi, Ng'ombe na Nguruwe na kutokomeza kabisa minyoo, ukurutu na hata kuua viroboto wanaonyonya damu kwenye wanyama hawa.
Dawa hii pia huweza kuja katika namna mbali mbali za matumizi kama sindano (injectable), ya kunywa (oral drench) na ya kupaka (pour/spot on) na mfugaji anaweza kuamua kununua kwa kadri ya mahitaji yake, urahisi au namna anavyopendelea yeye
Kwa njia ya sindano hupigwa chini ya ngozi (subcutaneous) ambapo kwa Ng'ombe na Mbuzi unaweza kupiga mahala popote ila kwa Nguruwe inapigwa nyuma ya sikio sababu ndio sehemu pekee mbayo haina mafuta
Dawa hii imeonesha mfanikio makuwa katika kupambana na minyoo duara, minyoo bata, minyoo ya moyo, viroboto na ukurutu.Dawa hii huweza kutumika kwenye wanyama kama Mbuzi, Ng'ombe na Nguruwe na kutokomeza kabisa minyoo, ukurutu na hata kuua viroboto wanaonyonya damu kwenye wanyama hawa.
Dawa hii pia huweza kuja katika namna mbali mbali za matumizi kama sindano (injectable), ya kunywa (oral drench) na ya kupaka (pour/spot on) na mfugaji anaweza kuamua kununua kwa kadri ya mahitaji yake, urahisi au namna anavyopendelea yeye
Kwa njia ya sindano hupigwa chini ya ngozi (subcutaneous) ambapo kwa Ng'ombe na Mbuzi unaweza kupiga mahala popote ila kwa Nguruwe inapigwa nyuma ya sikio sababu ndio sehemu pekee mbayo haina mafuta
Friday, November 22, 2013
Subscribe to:
Posts (Atom)