KURASA

Tuesday, September 10, 2013

KILIMO BORA CHA MATANGO - KWENYE VYOMBO

Kilimo hiki kinaweza kufanyika kwa watu wanaoishi ghorofani au sehemu yenye ardhi ambayo haifai kwa kilimo, mfano mchanga mwingi hasa sehemu ambazo zipo karibu na bahari au ardhi yenye mawe mawe

 Nimetumia boksi la mbao (upana sentimeta 25) ambalo lilitumika kujengea nguzo za nyumba, baada ya hapo lilikuwa limekaa bila kazi yoyote. nikatoa mbao ya juu, nikaziba pembeni na keweka udongo wenye rutuba ndani yake nikichanganya na mbole vunde, nikaweka nguzo mbili na kuweka nyavu ya vibox box ambayyo imeondolewa kwenye ukarabati wa nyumba, wewe unaweza kutumia waya za kawaida na kuzishona shona, hakikisha chini ya box lako kuna matundu ya kupitisha maji ili maji yasituame.




Matango ni vizuri kama mbebu zake ukapanda moja kwa moja, sia mbegu moja kiasi cha sentimita moja chini ya udongo na umbali kati ya mbegu na mbegu usipungue sentimeta 30 na zaidi, Sehemu ya kupandia iwe na jua la kutosha kwani matango huhitaji kiasi cha jua kisichopngua masaa 6 - 8 kwa siku, mwagia maji ya kutosha angalau mara moja kwa siku hasa nyakati za jioni


 Baada ya wiki moja mbegu zako zitaanza kuota, endelea kumwagia maji kila siku, baada ya wiki mbili mpaka tatu mimea itakua na kuanza kutaka kutambaa, hakikisha haitambai sehemu moja na kuanza kubanana, itenganishe na ikue kwa kupeana nafasi


 Hakikisha matawi yote unayaondoa kwa kuyavunja na mikono yakiwa madogo, mmea wenye mayawi mengi utakupa mazao dhaifu kwa sababu ya kutumia rutuba nyingi na mimea itabanana na kuanza kugombea nish ti ya jua

 Mmea wa matango huwa na majani, kamba za kujishikiza, maua na matawi, kabla ya kuondoa matawi ni lazima ujue kutofautisha kati ya maua na matawi maana hufanana sana yakiwa madogo na huota sehemu moja kati ya tawi na jani, kama huna uhakika lipi ni tawi na lipi ni ua subiri siku moja au mbili na utaona tofauti maana matawi hukua haraka sana kuliko maua






 MAUA YAKIWA YAMEBAKI YENYEWE BILA YA MATAWI



Monday, August 26, 2013

FISH CENTRE & AQUARIUM


 Samaki wa aina mbali mbali kama Gold (aina zote), koi, Salasa, Sotas, Angels, Gupies, zebra nk


 Vyakula vya aina mbali mbali kwa ajili ya samaki wako. kwa ajili ya ukuaji mzuri, kinga ya magonjwa na utoaji wa rangi


Filter na pampu za aina na ukubwa mbalimbali

Urembo na mapambo ya kuweka ndani ya vyombo vya kufugia

Vyombo vya kufugia samaki (aquarium) aina na ukumbwa tofauti tofauti kulingana na matakwa yako












 Hii ni aquarium ya kusimama, ndefu kwenda juu zaidi ya upana
 Kwa mawasiliano zaidi piga simu namba 0753-151811, 0787151811, 0715151813

Sunday, August 18, 2013

KUPUNGUZIA MATAWI KWENYE MICHE YA NYANYA

Kuna baadhi ya wasomaji wangu walipenda kufahamu umuhimu wa kupunguzia matawi kwenye zao la nyanya na pia jinsi ya kupunguzia matawi hayo.
Umuhimu wa kupunguzia matawi kwenye zao la nyanya ni kupata nyanya bora, kubwa na zenye afya, ukiacha mti uwe na matawi utatoa maua mengi sana na utaishia kupata nyanya ndogo ndogo ambazo hazina soko zuri, lakini ukipunguzia matawi nyanya zako zitakuwa kubwa na mmea wako utazaa kwa mpangilio na kwa muda mrefu

Jinsi ya kupunguzia matawi ni kwa kutofautisha maua ni yapi na matawi ni yapi kisha unaondoa matawi kwa kutumia mkono tu, usitumie kisu maana itakuwa rahisi kusambaza magonjwa toka mme mmoja hadi mwingine, mara nyini matawi hutoke kati ya shina na jani kama inavyoonekana kwenye picha hapo chini




NYANYA KUBWA ZENYE AFYA


NYANYA DOGO TOKA KWENYE MMEA WENYE MATAWI MENGI


Tuesday, August 13, 2013

UMUHIMU WA MAJIVU KWENYE UDONGO WA BUSTANI

Watu wengi wamekuwa wakiulizia umuhimu wa madini kwenye udongo na namna ya asili ya kuongezea kosefu wa madini kama potasiam, fosforas, kalsiam na mengineyo, njia rahisi ya kuongeza baadhi ya madini kwenye udongo ni kwakutumia majivu

UMUHIMU
Majivu yanakiwango cha wastani wa madini kifuatacho potasiam 5% - 7%, kalsiam 25% - 50%, fosforas 1.5% - 2% na madini mengine kwa kiasi kidogo pia mabaki mabaki ya chenga za mkaa kwenye majivu pia yanasaidia kwenye kunyonya baadhi ya sumu kwenye ardhi, kumbuka mkaa ni kaboni halisi (pure carbon)

KIASI CHA KUTUMIA
Kiasi cha kilo 2.5 mpaka 5 kitumike kwenye eneo la mita za mraba 33 au futi 100 za mraba, na majivu yamwagwe wiki 3 - 4 kabla ya kupanda kitu chochote ardhini.

MADHARA
Kila kitu kikitumiwa zaidi ya kiasi kina madhara na majivu pia yana madhara kwenye udongo kwa sababu yana hali ya kuwa alkaline zaidi (10 - 12 pH)  kwa sababu baadhi ya mchanganyiko wake hauyayuki kwenye maji, kama utahitaji kuongezea kwenye mimea yenye upungufu wa madini kama fosforas na potasiam basi hakikisha majivu hayagusi mashina kwani yanaweza kuuungua haya kama mimea ni michanga.

Pia majivu yanan kiasi kidogo sana cha naitrojeni ambacho hakiwezi kukidhi mahitaji ya mmea wowote ule, kwa hiyo hakikisha pia unatumia vyanzo vingine kwa ajili ya naitrojeni, vyanzo kama mimea jamii ya mikunde, marejea, lukina, na alfalfa

NANE NANE 2013