KURASA

Thursday, May 17, 2012

MBOLEA VUNDE


1. Namna ya kutayarisha Mboji/Mbolea Vunde/Mbolea Hai
Mboji ni sehemu ya viumbe (mabaki ya mimea na wanyama (matamahuruku)) ambayo imeozeshwa kwa muda mrefu ili kusazwa na viumbe vidogo vidogo. Sehemu za vitu kama majani, matunda na mabaki ya mboga hutengeneza mbolea ya mboji. Matokeo ya kusazwa huku ni tofauti kabisa na zile sehemu zilizowekwa. Mboji iliyoiva hubadilika rangi na kuwa ya hudhurungi, tifutifu na hunukia vizuri.
Mboji ni rahisi kutengeneza, gharama zake ni za chini sana na inafaa mno kuongezwa kwenye udongo ili kuinua mazao ya shamba.
Vipande vya vitu au sehemu ya viumbe mara nyingi huwa vimejazwa nyumbani au shambani bila mpangilio wowote. Hivi vinaweza kutumika kutengenezea mboji lakini itachukua muda mrefu kabla ya kuoza, na hivyo rotuba yake kupotea. Lakini kama muda ukitengwa ili kushugulikia mbolea matokeo yatakuwa mazuri na ya kufaa. Mabaki kutoka shambani na jikoni yanatumika katika kutengenezea mboji.
Mboji iliyotunzwa vyema huwa na rutuba nzuri kwa mimea inapotumiwa shambani. Mboji huchemka hata kiasi cha kuua magonjwa ya mimea na mbegu za magugu.
Majani makavu ya ndizi ni mazuri kwa kutunza vifaa vya mbolea na kuweka ukavu. Hali hii huwa huzuia kupotea kwa maji kabla ya kujenga lundo la mboji na wakati mbolea inapokuwa inaiva.


1.1 Vifaa visivyofaa kuwekwa kwenye mboji
 Sehemu za mimea ambazo zimenyunyiziwa dawa ya kuwaua wadudu (viuatilifu) na kwekwe juzijuzi (Pesticide/herbicides).  Vipande vya nyama kwa sababu vinavutia panya na wadudu wengine. Sehemu nyingi za Mboji ni sehemu ya viumbe (mabaki ya mimea na wanyama (matamahuruku)) ambayo imeozeshwa kwa muda mrefu ili kusazwa na viumbe vidogo vidogo. Sehemu za vitu kama majani, matunda na mabaki ya mboga hutengeneza mbolea ya mboji. Matokeo ya kusazwa huku ni tofauti kabisa na zile sehemu zilizowekwa. Mboji iliyoiva hubadilika rangi na kuwa ya hudhurungi, tifutifu na hunukia vizuri. Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea , Mboji ni rahisi kutengeneza, gharama zake ni za chini sana na inafaa mno kuongezwa kwenye udongo ili kuinua mazao ya shamba. Vipande vya vitu au sehemu ya viumbe mara nyingi huwa vimejazwa nyumbani au shambani bila mpangilio wowote. Hivi vinaweza kutumika kutengenezea mboji lakini itachukua muda mrefu kabla ya kuoza, na hivyo rotuba yake kupotea. Lakini kama muda ukitengwa ili kushugulikia mbolea matokeo yatakuwa mazuri na ya kufaa. Mabaki kutoka shambani na jikoni yanatumika katika kutengenezea mboji.  Mboji iliyotunzwa vyema huwa na rutuba nzuri kwa mimea inapotumiwa shambani. Mboji huchemka hata kiasi mimea na majani ambazo ziliambukizwa ugonjwa.  Vifaa vilivyo na ncha kali kama mwiba ambavyo vyaweza kujeruhi mikono na miguu. Magugu ambayo yanarudiarudia kila mwaka. Magugu kama hayo huuliwa kwa kuanikwa kwenye jua kali ili yakauke baadaye huchomwa ili yasienee na jivu lake huongezwa kwenye biwi, matunda na mabaki ya mboga hutengeneza mbolea ya mboji. Matokeo ya kusazwa huku ni tofauti kabisa na zile sehemu zilizowekwa. Mboji iliyoiva hubadilika rangi na kuwa ya hudhurungi, tifutifu na hunukia vizuri.

Mboji ni rahisi kutengeneza, gharama zake ni za chini sana na inafaa mno kuongezwa kwenye udongo ili kuinua mazao ya shamba.
Vipande vya vitu au sehemu ya viumbe mara nyingi huwa vimejazwa nyumbani au shambani bila mpangilio wowote. Hivi vinaweza kutumika kutengenezea mboji lakini itachukua muda mrefu kabla ya kuoza, na hivyo rotuba yake kupotea. Lakini kama muda ukitengwa ili kushugulikia mbolea matokeo yatakuwa mazuri na ya kufaa. Mabaki kutoka shambani na jikoni yanatumika katika kutengenezea mboji.
Mboji iliyotunzwa vyema huwa na rutuba nzuri kwa mimea inapotumiwa shambani. Mboji huchemka hata kiasi cha kuua magonjwa ya mimea na mbegu za magugu.
Majani makavu ya ndizi ni mazuri kwa kutunza vifaa vya mbolea na kuweka ukavu. Hali hii huwa huzuia kupotea kwa maji kabla ya kujenga lundo la mboji na wakati mbolea inapokuwa inaiva.


1.1 Vifaa visivyofaa kuwekwa kwenye mboji
 Sehemu za mimea ambazo zimenyunyiziwa dawa ya kuwaua wadudu (viuatilifu) na kwekwe juzijuzi (Pesticide/herbicides).  Vipande vya nyama kwa sababu vinavutia panya na wadudu wengine. Sehemu nyingi za Mboji ni sehemu ya viumbe (mabaki ya mimea na wanyama (matamahuruku)) ambayo imeozeshwa kwa muda mrefu ili kusazwa na viumbe vidogo vidogo. Sehemu za vitu kama majani, matunda na mabaki ya mboga hutengeneza mbolea ya mboji. Matokeo ya kusazwa huku ni tofauti kabisa na zile sehemu zilizowekwa. Mboji iliyoiva hubadilika rangi na kuwa ya hudhurungi, tifutifu na hunukia vizuri. Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea , Mboji ni rahisi kutengeneza, gharama zake ni za chini sana na inafaa mno kuongezwa kwenye udongo ili kuinua mazao ya shamba. Vipande vya vitu au sehemu ya viumbe mara nyingi huwa vimejazwa nyumbani au shambani bila mpangilio wowote. Hivi vinaweza kutumika kutengenezea mboji lakini itachukua muda mrefu kabla ya kuoza, na hivyo rotuba yake kupotea. Lakini kama muda ukitengwa ili kushugulikia mbolea matokeo yatakuwa mazuri na ya kufaa. Mabaki kutoka shambani na jikoni yanatumika katika kutengenezea mboji.  Mboji iliyotunzwa vyema huwa na rutuba nzuri kwa mimea inapotumiwa shambani. Mboji huchemka hata kiasi mimea na majani ambazo ziliambukizwa ugonjwa.  Vifaa vilivyo na ncha kali kama mwiba ambavyo vyaweza kujeruhi mikono na miguu.huwa vimejaa nyumbani au shambani bila mpangilio wowote. Hivi vinaweza kutumika kutengenezea mboji lakini itachukua muda mrefu kabla ya kuoza, na hivyo rotuba yake kupotea. Lakini kama muda ukitengwa ili kushugulikia mbolea matokeo yatakuwa mazuri na ya kufaa. Mabaki kutoka shambani na jikoni yanatumika katika kutengenezea mboji.
 Mboji iliyotunzwa vyema huwa na rutuba nzuri kwa mimea inapotumiwa shambani. Mboji huchemka hata kiasi mimea na majani ambazo ziliambukizwa ugonjwa.
 Vifaa vilivyo na ncha kali kama mwiba ambavyo vyaweza kujeruhi mikono na miguu.
 Magugu ambayo yanarudiarudia kila mwaka. Magugu kama hayo huuliwa kwa kuanikwa kwenye jua kali ili yakauke baadaye huchomwa ili yasienee na jivu lake laweza kuongezwa kwenye lundo la mbolea.
 Vitu visivyo kua na uhai kama plastiki na chuma. 


1.2 Mfano wa vitu vinavyoweza kutumiwa kutengenezea mboji nyumbani





2. Namna ya kutengeneza mboji ya mimea
Kusanya vitu na vifaa vinavyohitajika katika utengenezaji wa mboji ambayo ni;
 Majani mengi mabichi/kijani na makavu. Majani jamii ya mikunde ni mazuri sana kwani hutengeneza kirutubishi cha naitrojeni (N) kwa wingi.
 Mabua ya mahindi au vitawi vya miti
 Udongo wa kawaida wa juu
 Samadi, mbolea yoyote ya wanyama au mboji ya zamani
 Majivu au vumbi la mkaa
 Maji

2.1 Hatua
1) Chagua sehemu karibu na eneo ambalo mboji itaenda kutumika na ambapo kuna hifadhi ya kutosha kukinga dhidi ya upepo, jua na mvua.
2) Katakata majani yawe madogo madogo ili yaweze kuoza haraka. Tengeneza msingi kama mita sita (6) urefu na upana wake mita 2 kwa kutumia majani magumu kama matawi/vijiti. Hii itahakikisha maji yanatiririka na hewa ina zunguka vizuri. Hakikisha kuna nafasi ya kutosha kufanyia kazi kwenye biwi bila kulikanyaga.
3) Weka sentimita 10 ya majani ambayo hayaozi haraka kwa mfano mabua vya mahindi au mimea mibichi/kijani.
4) Weka sentimita 10 ya vifaa ambavyo huoza haraka kwa mfano maganda ya mboga na matunda.
5) Weka sentimita 2 ya samadi (mbolea-hai ya wanyama), mabaki ya mbolea ya zamani kama yaweza kupatikana.
6) Weka udongo wa juu sentimita 10 kutoka kwenye shamba ambalo hulimwa.
7) Majivu na mkojo vyaweza kunyunyuziwa juu ili kufanya biwi/lundo kuoza haraka. Kukatakata majani
8) Nyunyizia maji kwenye biwi mpaka lilowe.
9) Rudia mpangilio huu kuanzia namba nne (4) mpaka lundo lifike mita moja (1.m) hadi moja na nusu (1.5m) kwenda juu isipokuwa vijiti/matawi ya kwanza.

2.2 Zingatia
Biwi/lundo cha mboji kinatakiwa kifunukwe ili kupunguza/kuzuia mvuke ama mvua nyingi ambayo hubeba rotuba kutoka kwenye mbolea. Weka gunia, nyasi ama matawi ya ndizi yaliyokauka.



 Kila tabaka/kunjo/safu yafaa kupangwa kuanzia kwenye ukingo ili lundo la mbolea lisiporomoke.
 Namna nyigine ya kuzuia lundo kuporomoka ni kwa kuweka vipande vya mbao kando ya biwi. Wavu wa nyuzi za chuma utafanya biwi kukauka.



3. Wadudu wenye manufaa na mazingira yanayohitajika kwenye Biwi
3.1 Wadudu ambao husaidia kufanya biwi kuoza
Viumbe wengi wanaohusika na kazi hii ya kuoza ni wadogo hawaonekani kwa macho matupu. Ila viumbe hawa huhitaji maji, hewa na vipande/sehemu ya viumbe wengine ambazo kwao ni chakula. Viumbe hawa hula vipande hivyo na hutoa hewa ya carbon dioxide, maji na joto.
Kuna hatua tatu kubwa wakati biwi linapooza; hatua ya kupanda joto, hatua ya kupoa/kuwa baridi na hatua ya kukomaa.
Wakati ya hatua ya kupanda joto, joto hufikia kiwango cha juu sana katikati mwa biwi. Uzuri wa joto hili ni kwamba magonjwa yaliyokuwa kwenye viungo vya biwi na mbegu za magugu huchomwa hadi kufa. Hatua ya pili ya kuwa baridi; uyoga (fungi) huwa na faida nyingi kwa sababu kazi yake ni kuzisaga nyuzi ngumu ambazo zimo kwenye viungo vya mimea au majani.
Kwenye hatua ya tatu, ‘hatua ya kukomaa’ viumbe wakubwa kama mchwa na nyungunyungu husaidia kusaga na kuchanganya mbolea.
Hali ya anga ikiwa na joto jingi viumbe hawa hufanya kazi haraka kuliko wakati ambapo hali ya anga ni baridi. Aina ya viungo vilivyotumika kujenga/kukuza biwi na ukali/uchungu (pH) wa udongo pia huathiri kiwango cha mbolea kuoza.
3.2 Mazingira yanayohitajika kwenye biwi
Biwi huhitaji vitu vitatu: hewa, maji na joto.

Hewa
Viumbe wadogo kwenye biwi huhitaji hewa ili waweze kuishi. Hewa ya carbon dioxide (CO2) ambayo imetolewa na wadudu hawa huhitaji kutolewa nje. Ikiwa hewa safi itakosekana, viumbe wengine wasiohitajika huingia na kutoa harufu mbaya na pia kufanya mbolea isioze haraka.

Maji
Kazi ya viumbe wadogo huwa polepole ikiwa biwi ni kavu. Aidha ikiwa biwi litalowa maji basi viumbe wadogo watakufa na kufanya biwi kuwa na uchachu badala ya kutengeneza mbolea. Hivyo basi kukagua kiwango halisi cha maji huhitaji ujuzi fulani.
Joto
Biwi hutoa joto wakati linaoza. Lundo likiwa na joto jingi viumbe wadogo hutoka, kisha huweza kurudi pindi linapopoa.
4. Matunzo ya Biwi
Ili kupata mbolea nzuri, biwi linapojengwa yafaa lishughulikiwe kwa utaratibu. Biwi hilo litahitaji maji, kupinduliwa, joto na muda unaofaa wa kukomaa.

4.1 Maji
Wakati wa kiangazi biwi/lundo la mboji huhitaji kumwagiliwa maji kila wiki. Maji katika lundo la mbolea hupimwa kwa kuweka fungu dogo la nyasi na kulitoa baada ya dakika tano. Nyasi isipoonyesha majimaji au unyevu itabidi maji yamwagwe kwenye lundo hilo.
Kuna njia kadha za kuzuia mvuke kuinuka kutoka kwenye biwi, hali kadhalika kiwango cha maji yanayomwagiliwa:
 Funika lundo kwa majani ya ndizi ama nyasi.
 Funika lundo kwa udongo.
 Lundo lisigeuzwegeuzwe

Biwi likilowa maji itabidi kifunuliwe na kuachwa kikauke kwenye jua kabla ya kujengwa tena.

4.2 Kupindua/kugeuza
Katika muda wa wiki tatu (3) baada ya kujenga/kukuza biwi/lundo ukubwa wake utakuwa umepungua sana. Kupindua biwi uhakikishe ya kwamba majani yaliyo kando yameoza pia hewa safi imerejeshwa. Kupindua biwi huchanganya majani yaliyotengenezwa na kukijenga upya. Majani yalivyo kando huwekwa katikati, ikiwa kuna ukavu, maji mengi na majani/viungo vikavu huongezwa. Kupindua kunatikiwa kufanyike kila baada ya wiki tatu.
Hali ya joto na kiwango cha maji yafaa kupimwa siku chache baada ya kupinduliwa. Kupinduliwa kwa mara ya tatu kutahitajika ikiwa viungo havitakuwa vimeoza kikamilifu. 


Mbolea yaweza kutengenezwa bila kupinduliwa ila viungo vilivyo kando havitaoza. Mbegu za magugu na viungo na magonjwa ya mimea hayatakufa. Viungo vilivyobaki hutengwa na kutumiwa kwenye biwi lingine. Japokuwa kugeuza hakuna lazima, kunapendekezwa ili kupata mbolea nzuri.

4.3 Kiwango cha Joto
Kupima kiwango cha joto kwenye biwi kunahitaji kijiti kirefu kichomwe ndani ya lundo siku kumi (10) baada ya kujengwa. Kijiti yafaa kionyeshe joto la kutosha kinapoguswa kwa mkono, la sivyo kuoza bado hakujaanza kufanyika. Katika hali kama hii, maji ama hewa itahitajika kwenye biwi na biwi kuachwa kwa muda. Ikiwa biwi lina joto jingi, biwi linaoza basi viumbe hai wanaweza kufa. Katika hali hii, hewa na maji itabidi kuongezwa ili kufanya biwi lipoe. Kiasi cha joto yafaa kupimwa mara kwa mara kwa kutumia kijiti.



Chini ya 57C
Joto hili linaweza kuivisha mboji lakini haliwezi kuua mbegu za magugu na magonjwa.

57-71C
Joto muafaka kwaajili ya kuivisha mbojj na kuua mbegu za magugu na magonjwa. Katika kiwango hiki cha joto, mbegu zote na vijimelea vyote vya magonjwa vilivyoko kwenye mchanganyiko wa mboji hufa na hivyo kutokuwepo pale mboji inapokuwa imeiva.

Zaidi ya 71C
Joto hili ni kali sana na huweza kusababisha madhara mengineyo kama vile kuzalishwa kwa gesi zenye madhara pia wadudu wenye manufaa ambao husaidia mboji kuiva huweza kukimbia. 


Muhimu kuhakikishakuwa joto halizidi sana ili kuweza kuwa na mboji bora yenye virutubisho




2 comments:

socialesungrand@gmail.com said...

hongera juu ya elimu inayo itoa kwa jamii kwani jamii yetu hasa vijana bado wana mfumo hasi juu ya kilimo na kutaka ajila tu za kuvaa tai.

said...

Kwa zaidi ya miaka 13 ya ndoa sikuweza kuzaa, naendelea kuharibika hata nikipata mimba, madaktari wote hawakuweza kunisaidia, hadi dada yangu akanielekeza kwa Dr DAWN, ambaye alinisaidia nikapata ujauzito na sasa hivi kuwa na mtoto mzuri wa kike,
Anasaidia pia marafiki zangu wengi niliowaelekeza, Dr DAWN ni baraka kwa kila mtu anayewasiliana naye,
*Kama unataka kupata mimba.
*Ukitaka kuacha kuharibika kwa mimba.
*Ukitaka kumrudisha mpenzi wako.
*Kama unataka mume/mkeo arudishwe.
*Kama unataka kurejesha mali yako iliyoibiwa au Pesa.
*Ukitaka kutibu aina yoyote ya ugonjwa,
Wasiliana naye kwa WhatsApp: +2349046229159