Karibuni kwenye blog yangu ambayo najaribu kutoa elimu kidogo niliyo nayo. Kama unataka kufanya kilimo, ufugaji wanyama, ufugaji wa samaki, ufugaji wa nyuki, kilimo cha miti ya mbao, kilimo cha majani na malisho ya mifugo, utaalamu wa mbolea na udongo katika mazingira halisi ya ki Tanzania basi wasiliana nami (mitiki1000@gmail.com) NB sihusiki na habari za masoko ya bidhaa yoyote ya kilimo na mifugo, kabla hujaingia kwenye mradi fanya utafiti wa masoko wewe mwenyewe
Friday, November 15, 2013
Tuesday, October 8, 2013
Tuesday, October 1, 2013
FARASI WANAUZWA - HORSES FOR SALE
Jumla kuna farasi watano, wote bado vijana hakuna aliyezeeka, 1. jike mweusi wa miaka minne ana mimba bei Tsh 5,500,000/= 2. jike mweupe wa miaka miwili Tsh 4,200,000/= 3. Jike wa miaka miwili rangi ya hudhurungi isiyokooza bei Tsh 4,200,000/= 4. Dume wa miaka miwili rangi ya kahawia bei Tsh 4,200,000/= kwa mawasiliano zaidi piga simu namba +255 786 763 265
5 Young horses for sale. 1. Black pregnant female 4 years old. - 5, 500, 000 TSHS 2. White female horse 2 years old. 3. Greyish white male for sale 2 years old. 4. A light brown mixed white foal of 2 months Contact: : +255 786 763 265 All others are for $2500 0r 4, 200 000 Tsh
Friday, September 27, 2013
NG'OMBE - KWA TAARIFA YAKO
Ng'ombe mwenye afya kwa kawaida pua yake huwa na unyevu unyevu au kama vile inatoa jasho jembamba sana.Ukiona ng'ombe wako ana pua iliyokauka na haina unyevuunyevu basi ujue
hiyo ni dalili kwamba kuna tatizo katika mwili wake, hii inaweza pia
kuwa dalili ya maambukizi au magonjwa
Pua ya ng'ombe inauwezo wa kunusa umbali wa kilometa 8 au maili 5, ndio maana wanaweza kukimbia machungoni au hata kuvunja banda na kufuata mazao mashambani sababu ya harufu, msimu wa membe tatizo la kutoroka ndio huwa kubwa hasa maembe yapaoanza kuiva
Kwa siku hutumia masaa 6 kula chakula na hutumia masaa 8 kucheua na na kutafuna tena na hunywa maji kiasi cha lita 12 mpaka 25 kutegemeana na ukubwa na hula kiasi cha kilo mpaka 45 kwa ng'ombe wakubwaNg'ombe mwenye kilo 1000 huweza kuzalisha kiasi cha tani 10 za mbolea kwa mwaka
Mpwapwa breed ni mbegu ya ng;ombe iliyo patikana nchini Tanzania baada ya tafiti kadhaa za kitaalam
Thursday, September 19, 2013
MBWA - KWA TAARIFA YAKO
Kama unafuga mbwa na umemzoea basi kila mara unapokaa naye mchunguze namna macho yake yanavyo jaribu kuwasiliana na wewe kila mara, mara zote macho haya hofuatana na lugha ya mwili (body language)
Anapokuwa na furaha, anahitaji kitu, kuna hatari, joto au baridi sana au hata anaumwa ishara ya macho pia huonekana
Kama umemzoea mbwa wako unaweza kuanza kuhisi kama kuna kitu hakiko sawa kwa kumuangalia kwenye macho, cha muhimu ni kujua akiwa kwenye hali ya kawaida macho yake yanakuwa kwenye hali gani au huwa anakuangalia vipi?
Mbwa hunywa maji kwa kuukunja ulimi wake kwa nyuma na kuyachota kisha kuyaingiza mdomoni, tofauti na wengi wanavyojua kwamba huwa analamba maji
Mbwa haonyeshwi upendo kwa kukumbatiwa, kama ulikuwa unafanya hivyo acha mara moja maana mbwa hutafsiri kukumbatiwa kawa kuonyesha utawala wako, mbwa anayetawala ndio hukumbatia wenzake kama ishara ya ukuu
Mikanda ya mbwa ya shingoni iligunduliwa zama za ugiriki ya zamani, nia kuu ilikuwa kuwalinda mbwa dhidi ya mashambulizi ya wanyama wengine kama mbweha na fox
Tuesday, September 10, 2013
KILIMO BORA CHA MATANGO - KWENYE VYOMBO
Kilimo hiki kinaweza kufanyika kwa watu wanaoishi ghorofani au sehemu yenye ardhi ambayo haifai kwa kilimo, mfano mchanga mwingi hasa sehemu ambazo zipo karibu na bahari au ardhi yenye mawe mawe
Nimetumia boksi la mbao (upana sentimeta 25) ambalo lilitumika kujengea nguzo za nyumba, baada ya hapo lilikuwa limekaa bila kazi yoyote. nikatoa mbao ya juu, nikaziba pembeni na keweka udongo wenye rutuba ndani yake nikichanganya na mbole vunde, nikaweka nguzo mbili na kuweka nyavu ya vibox box ambayyo imeondolewa kwenye ukarabati wa nyumba, wewe unaweza kutumia waya za kawaida na kuzishona shona, hakikisha chini ya box lako kuna matundu ya kupitisha maji ili maji yasituame.
Matango ni vizuri kama mbebu zake ukapanda moja kwa moja, sia mbegu moja kiasi cha sentimita moja chini ya udongo na umbali kati ya mbegu na mbegu usipungue sentimeta 30 na zaidi, Sehemu ya kupandia iwe na jua la kutosha kwani matango huhitaji kiasi cha jua kisichopngua masaa 6 - 8 kwa siku, mwagia maji ya kutosha angalau mara moja kwa siku hasa nyakati za jioni
Baada ya wiki moja mbegu zako zitaanza kuota, endelea kumwagia maji kila siku, baada ya wiki mbili mpaka tatu mimea itakua na kuanza kutaka kutambaa, hakikisha haitambai sehemu moja na kuanza kubanana, itenganishe na ikue kwa kupeana nafasi
Hakikisha matawi yote unayaondoa kwa kuyavunja na mikono yakiwa madogo, mmea wenye mayawi mengi utakupa mazao dhaifu kwa sababu ya kutumia rutuba nyingi na mimea itabanana na kuanza kugombea nish ti ya jua
Mmea wa matango huwa na majani, kamba za kujishikiza, maua na matawi, kabla ya kuondoa matawi ni lazima ujue kutofautisha kati ya maua na matawi maana hufanana sana yakiwa madogo na huota sehemu moja kati ya tawi na jani, kama huna uhakika lipi ni tawi na lipi ni ua subiri siku moja au mbili na utaona tofauti maana matawi hukua haraka sana kuliko maua
MAUA YAKIWA YAMEBAKI YENYEWE BILA YA MATAWI
Sunday, September 8, 2013
BLOGS AWARDS 2013
Monday, August 26, 2013
FISH CENTRE & AQUARIUM
Samaki wa aina mbali mbali kama Gold (aina zote), koi, Salasa, Sotas, Angels, Gupies, zebra nk
Vyakula vya aina mbali mbali kwa ajili ya samaki wako. kwa ajili ya ukuaji mzuri, kinga ya magonjwa na utoaji wa rangi
Filter na pampu za aina na ukubwa mbalimbali
Urembo na mapambo ya kuweka ndani ya vyombo vya kufugia
Vyombo vya kufugia samaki (aquarium) aina na ukumbwa tofauti tofauti kulingana na matakwa yako
Hii ni aquarium ya kusimama, ndefu kwenda juu zaidi ya upana
Kwa mawasiliano zaidi piga simu namba 0753-151811, 0787151811, 0715151813
Subscribe to:
Posts (Atom)