Samaki wa urembo wako aina nyingi, wanamahitaji na tabia tofauti, tumezoea kuona wengi wakifugwa kwenye vyombo vya kioo (aquarium) na mara chache kwenye mabwawa. Mara nyingi majumbani wanakuwa kwenye aquarium na kwa wale wazalishaji (breeders) wnazalisha na kukuza kwenye mabwawa, mara chache sana wanatumika kwa ajili ya urembo kwenye mabwawa

Samaki wako aina nyingi lakini kwa hapa Tanzania waliozoeleka sana ni goldfish, koi, angels, cichlids, barbs, sharks, parots, catfish, gupies, sotas, zebra na kadhalika, na mimi nitajaribu kuwachambua ufugaji na mazingira wanayohitaji kwa baadhi ya samaki ingawa mahitaji yao hayatofautiani sana