KURASA

Tuesday, July 30, 2013

KILIMO BORA CHA MANANASI

Zao la mananasi hulimwa sana hapa nchini maeneo ya Bagamoyo, Kibaha, Geita, Mwanza, Tanga, Mtwara, Lindi na maeneo mengine. Zao hili lina kiasi kikubwa cha vitamini A na B na kiasi kidogo cha vitamini C, pia kuna madini kama potasiam, kalsiam, chuma na magnesiam

HALI YA HEWA
Manansi hustawi sana ukanda wa pwani usawa usiozini mita 900 toka usawa wa bahari ambapo kuna mvua nyingi kiasi cha milimita 1500 na unyevu wa kutosha, pia unaweza kupanda kwenye maeneo yenye mvua chache lakini kwa kutumia kilimo cha umwagiliaji, Hali ya joto ni kuanzia sentigredi 15 - 32, huwa haya stahimili baridi

UDONGO
Udongo wenye rutuba ya kutosha na usiotuamisha maji ndi unaofaa kwa ajili ya kilimo cha mananasi, unaweza kutumia samadi au mbole vunde ili kuongezea rutuba ya udongo wako.

MSIMU
Kwa ukanda wa pwani wenye mvua mbili kwa mwaka upandaji wa mananasi huanza mara baada ya mvua za kwanza kuanza, ni vizuri kupanda kwa muda mfupi ili uzaaji usipishane sana na pia kusaidia kupata mvua za kutosha kabla ya msimu kuisha.

UPANDAJI
Tumia miche ya aina moja na yenye umri sawa ili huduma zifanane na pia uzaaji uwe wa mpangilio, umbali toka mmea hadi mmea ni sentimeta 30 na mstari hadi mstari ni sentimeta 60, na umbali kila baada ya mistari miwili miwili ni sentimeta 90

Kwa ekari moja unaweza kupanda miche 25,200 na kwa hekta moja unaweza kupanda miche 44,000. ili mananasi yako yastawi vizuri basi tengeneza kama mtaro mdogo na kwenye mitaro ndio upande mananasi yako, hii husaidia kupata unyevu zaidi

MBOLEA
Kwa wale wanaotumia mbolea za viwandani, ni vizuri kutumia NPK na DAP ambazo utaweka miezi miwili baada ya kupanda na miezi 12 baada ya kupanda baada ya hapo hautahitaji mbolea tena, lakini ni vizuri zaidi kama utatumia mbolea za asili

WADUDU
Wadudu wanaoshambulia mananasi ni aina ya mealybug ambao huondolewa kwa kupulizia dawa kama dume na karate.

Ugonjwa wa kuoza moyo wa miche unaweza kuzuiwa kwa kupiga dawa za copper oxychloride au kwa kuzamisha miche kwenye dawa za fungasi (fungicides)kabla ya kupandwa shambani

UVUNAJI
Mananasi huwa tayari kuvunwa miezi 18  mpaka 24 baada ya kupandwa kutegemeana na mbegu na matunzo ikiwemo kiasi cha mvua, mbolea na unyevu shambani, Uvunaji  hufanyika kwa kutumia visu na vibebeo maalum kuhakikisha ubora wa zao hili


Thursday, July 25, 2013

ATHARI ZA MAFUTA YA UBUYU NA TFDA


 
Mamlaka ya chakula na dawa (TFDA) imesisitiza kwamba mafuta ya ubuyu yana athari kubwa za kiafya na ni hatari kwa sababu yana tindikali ya mafuta ijulikanayo kama Clycopropenoic, moya ya madhara ya mafuta ya ubuyu ni pamoja na kusababisha saratani. TDFA imesema pia kutumia unga wa ubuyu na majani yake hakuna athari zozote kiafya kwa hiyo watu wanaweza kuendelea kutumia bila matatizo yoyote.
Kitaalamu tindikali ya Clycopropenoic inaweza kuondolewa kwenye mafuta hayo iwapo tu yatachemshwa katika kiwango cha digrii 180 za sentigredi kwa masaa 8 au kwa teknolojia ya kuyagandisha (hydrogenation) ambapo katika njia hizo zote mbili hakuna hata moja ambayo inatumika hapa nchini.

Miaka ya karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la matumizi ya bidhaa za asili ikiwemo ya aloe vera, ubuyu na bidhaa zake, hii inatokana na matatizo ya kiafya kama kisukari, ugonjwa wa moyo, magonjwa ya ngozi, uzazi, nguvu za kiume na kuongeza kinga mwilini. kutokana na hili matumizi ya ubuyu, majani yake na mafuta yake yaliongezeka zana huku watu wakiamini kwamba ni dawa na kinga ya magonjwa mbali mbali.


Hili walilotuambia TDFA tusilipuuze ila taasisi nyingine za kiutafiti kama SUA na  NIMRI zifanye utafiti wa kutosha sio tu kwa mafuta ya ubuyu bali pia kwenye dawa nyingine na vitu vya asili ili kubaidi madhara yanayoweza kujitokeza kwa waTanzania iwapo watatumia.


Wednesday, July 24, 2013

KILIMO BORA CHA MATUFAA - APPLES

Tufaa ni tunda moja maarufu duniani ambalo hupendwa kuliwa na watu wa jamii zote, hii inatokana na utamu wake pamoja na faida za kiafya zinazopatikana kwa kula matufaa. Matunda haya hustawi zaidi kwenye nyanda za juu ambako joto sio kali, sehemu kama lushoto, Arusha, miteremko ya Kilimanjaro, Mbeya, Iringa, Njombe, Songea nk. Udongo ni wenye rutuba ya kutosha na usiotuamisha maji

Unaweza kupanda kwa kutumia mbegu au kwa kununua miche bora kutoka kwenye taasisiza kilimo mfano Uyole Mbeya. kama utatumia mbegu basi ni bora kununua mbegu bora au ukikosa mbegu basi jaribu kutumia zile utakazopata kutoka kwenye tunda lenyewe

Kama utachukua za kwenye tunda basi zikaushe kwenye jua kwanza mpaka zikauke kabisa, zile za kukununua huwa zimekauka kwa hiyo huna haja ya kuzikausha, Chukua karatasi laini (napkins/tissues) iloweshe maji kiasi kidogo kisha chukua mbegu zako na uzifunge na  karatasi hii vizuri kisha ziwekw kwenye jokofu kwa kiasi cha wiki 3-4 zitaanza kuota/kumea, kuziweka kwenye friji husaidia kuua vijidudu vya magonjwa ambavyo huenda vilikuwepo kwenye tunda au mbegu

Chukua mbegu yako na uipande kwenye mifuko au chombo kama ndoo, usipande kwenye vifuko vidogo maana mmea huu hukua mkubwa kiasi na wenye mizizi mikubwa kabla ya kupandwa. Mmea wako ukifikia ukubwa wa futi moja mpaka pili ni kipindi kizuri kuuhamishia shambani,

Umbali wa shimo hadi shimo ni kiasi cha futi 15 mpaka 18 kutoka mti hadi mti. Hakikisha unapanda miche yako wakati wa mvua za kwanza, Mashimo yawe na kina cha futi mbili na upana futi 3. Weka kasi cha debe 1 la samadi au mboji na changanya vizuri na udongo.

kumbuka kuacha kisahani kwa ajili ya kukusanya maji ya mvua au unapomwagilia na utandaze majani/nyasi kiasi cha futi 3 kuzunguka mti wako, hakikisha wanyama kama mbuzi na ng'ombe hawaingii shambani na kula miti yako. Baada ya mwaka hutakuwa tena na haja ya kumwagilia miti yako kwani itaweza kukua yenyewe kwa kutegemea mvua

WADUDU NA MAGONJWA
Wadudu wanaoshambulia zaidi mitufaa ni vidukari (moth) na pia ugonjwa wa madoa meusi (black spot) ndio unaoshambulia zaidi, ili kupambana na ugonjwa na wadudu hawa hakikisha unatuma kiutilifu chochote che nye pareto (pyrethrum) ndani yake
KUVUNA
Uvunaji ni baada ya miaka mitatu lakini miche ya kuunga huanza kuzaa mapema hata ndani ya mwaka, ila nashauri usiruhusu matunda mengi kwenye miti midogo ili kuzuia matawi kuvunjika kwa hiyo punguza matunda kabla hayajawa makubwa na kubakisha machache

Wednesday, July 17, 2013

BLACK QUARTER - CHAMBAVU

Huu ni ugonjwa wa mifugo unaoshambulia ng'ombe, kondoo na mara chache farasi. Unasababishwa na vijidudu  ina ya Clostridium chauvoei  ambavyo hushambulia bila uwepo wa oksijeni ya kutosha (anaerobic) na kuzalisha sumu kwenye mwili wa myama na kusababisha kifo.

KUSAMBAA
Vijidudu husambaa kwa kupitia kwenye udongo ambapo mnyama huvipata anapokula majani, pia huweza kusambazwa kwa njia ya vidonda na mate toka kwa mnyama mwenye ugonjwa huu.

DALILI
-homa kali
-Misuli ya miguu ya nyuma huvimba na kuwa na joto kali, inauma ikiguswa na rangi ya sehemu hiyo ya ngozi hubadilika
-Ukigusa sehemu iliyoshambuliwa inatoa sauti ya kama majani makavu
-Mnayama huchechemea mguu wa nyuma sababu ya maumivu

UCHUNGUZI
Uchunguzi ufanyike na maafisa ugani wa mifugo kwa kufuatilia dalili na historia ya sehemu husika
-Kipande cha msuli na majimaji toka sehemu iliyoathiriwa kwa ajili ya uchunguzi wa kimaabara
-Uchunguzi wa mwili wa myama aliyefariki (post Mortem)

MATIBABU
-Penicilin inasaidia kutibu ugonjwa kama matibabu yataanza katika hatua za mwazo, ukichelewa hutaweza kmtibu mnyama wako.
-Tumia b-complex, na dawa za kupunguza uvimbe  kama visaidizi vya tiba
-Kupachana sehemu iliyoathirika ilikutoa majimaji na kuingiza hewa ili kuharibu mazingira ya kuishi vijidudu

KINGA
-Chanjo ya mara moja kwa mwaka kwa wanyama wakubwa.
-Wanyama wadogo wachanjwe mara wafikishapo umri wa miezi mitatu
-kwa sehemu ambayo kuna mlipuko wa ugonjwa huu wanyama wote wachanjwe kisha wapigwe dozi kubwa ya penicilin (kama ugonjwa hautaibuka ndani ya siku 14 wanyama wako watakuwa salama)
-Miili ya wanyama walikufa ichomwe na kuzikwa kwenye shimo refu sana