Magonjwa hayo ni ugonjwa wa kukauka miche pamoja na ugonjwa wa mizizi (Eucalyptus root disease)imebainika na wataalamu toka maabara ya Chuo kikuu cha Sokoine (Morogoro) kwamba magonjwa hayo hayatibiki, ila ugonjwa unaweza kudhibitiwa kabla haujaibuka kwa kupiga dawa iana ya Acephate au Confidor wakati miche ipo kitaluni kabla ya kupandwa shambani.

Kitaalamu nashauri kabla ya kuingiza mbegu au miche ni lazima uchunguzi ukafanyika kwa kina ili kugundua kama kuna magonjwa ambukizi, kwa sababu kuna aina zaidi ya 200 za mikaratusi
kwa ushauri zaidi kwa mtu anayetaka miche au mbegu za miti, basi awasailianae na wakala wa mbegu za miti wa taifa (TTSA) ambao wapo Morogoro eneo la kihonda, pamoja na hayo baadhi ya tafiti zimeonyesha kwamba mikaratusi inaathari kwa mazingira kwa sababu inatumia kiasi kikubwa cha maji na kusababisha ukame hasa kipindi hiki cha mabadiliko katika tabia nchi

WITO sehemu kama serengeti ambapo ni urithi wa dunia nashauri makampuni na watu binafsi wajitahidi kupanda miti ya asili na kuachana na hii miti ya kigeni kama mikaratusi, sijaelewa pia kwa nini miti itoke nchi jirani ya Kenya wakati wangeweza kuanzisha vitalu hapa hapa nchini kwa kutumia mbegu ambazo tunazo tena za miti ya asili