KURASA

Tuesday, August 28, 2012

CANINE PARVOVIRUS

Kama jina lake lilivyo ungonjwa huu husababishwa na virusi ambavyo huwaathiri mbwa ka kiasi kikubwa, ugonjwa huu uligundulika miaka ya 1970 na hushambulia zaid seli za kwenye mfumo wa chakula na hewa. virusi vya ugonjwa huu huwa vingi sana kwenye kinyesi cha mbwa mgonjwa na  husambaa baada ya mbwa kugusa kinyesi che nye vidudu kwa mdomo wake, huweza pia kubeba virusi hivi kama atavilalia au kukanyaga kinyesi cha mbwa mwenye ugonjwa huu, na mbwa anaweza pia kuambukizwa ikiwa atagusa kitu chochote ambacho kiligusana na kinyesi chenye vidudu vya parvo.


DOBERMAN PINSCHER

Ugonjwa hushambulia mbwa wa umri wowote lakini watoto wenye umri kati ya wiki 6 - 20 hushambuliwa zaidi na pia mbwa aina ya Doberman Pinschers and Rottweilers hushambuliwa zaidi ya mbwa wengine ha dalili za ugonjwa huu huonekana kirahisi kwao.


ROTTWEILER

Dalili za kwanza huonekana baada ya siku kama 5 ambazo ni kuharisha, kutapika na joto kupanda sana ingawa si mbwa wote ambao watapandisha joto, watoto wataonyesha dalili za kusumbuliwa na maumivu ya tumbo, pia kinyesi hutoka na malenda malenda ambayo wakati mwingine huwa na damu damu kiasi na kwa wataalamu wa mifugo kipimo cha ELISA huweza kutumika kupima na kugundua virusi vya ugnjwa huu

MATIBABU
Hakuna matibabu ya ugonjwa huu ila drip za maji husaidia kurudisha maji yaliyopotea na kumpa nafuu mgonjwa, dawa za kuzuia kuharisha na kutapika ni muhimu na pia wakati mwingine mbwa anaweza kuhitaji kuongezewa damu, antibaiotiks pia ni muhimu kuzuia maambukizi ya bakteria

Kupona kwa mbwa kutategemea vitu vingi kama ukoo wa virusi vya ugonjwa, hatua za maambukizi, uwezo wa mwili wa mbwa kupambana na magonjwa na umri wa mbwa hata uharaka wa kuapata tiba kwa mbwa

KINGA
Kinga kubwa ni chanjo ya DHPP (distemper, hepatitis, parvovirus, and parainfluenza combination)ambayo hupigwa katika umri wa wiki 8 tangu kuzaliwa na kurudiwa baada ya wiki 16 lakini kama wazazi hawakuchanjwa basi ni muhimu kuchanja katika wiki ya 4, usafi wa mabanda pia ni muhimu lakini ukitumia blichi kiasi cha 1:30 katika uchanganyaji na maji ukisafisha na kuiacha kwa zaidi ya dakika 20 kabla ya kuiosha na maji

CANINE DISTEMPER - UGONJWA HATARI WA MBWA

Huu  ni ugonjwa unaosababishwa na virusi vinavyofanana sana na vile vinavyosababisha surua kwa binandamu, distemper hushambulia wanyama jamii ya mbwa (canine) kana simba, mbwa mwitu, fisi, mbweha na mbwa wa kawaida tunaowafua majumbani mwetu. Huu no ugonjwa unaoua zaidi mbwa duniani ingawa hapa nchini haujasababisha madhara makubwa kama kichaa cha mbwa (rabies)


Mbwa aliambukizwa ugonjwa huu hutoa virusi hivi kwa njia ya kinyesi, mkojo, mafua na chafya na njia ya hewa ndio njia kuu ya kusambaza ugonjwa huu kwenda kwa mbwa wengine. Maabukizi makubwa zaidi ni kwenye watoto wasiochanjwa ambao wenye umri kati ya wiki 6 - 12 ambapo kinga toka kwa mama waliyozaliwa nayo hupungua sana na kuwa katika hatari zaidi ya maambukizi.

Mbwa walioambukizwa ugonjwa huu nusu yao wataonyesha dalili kidogo sana au wasionyeshe dalili za ugonjwa huu kabisa na wanaoathirika zaidi ni mbwa ambao hawapati lishe bora na kuwekwa kwenye mazingira mazuri na afya kwa ujumla.Virusi vya ugonjwa huu hushambulia ubongo, sehemu za ndani ya ngozi, macho na utando wa mfumo wa hewa na chakula na dalili za wazi huweza kuonekana baada ya siku 6 - 9 tangu kupata maambukizi

Hatua ya kwanza ya ugonjwa huu joto hupanda kufikia sentigredi 39.4 - 40.5 mbwa hupoteza hamu ya kula, hutoa machozi na majimaji puani, lakini dalili hizi ni kama za ugonjwa wa kawaida wa mafua (colds) kwenye mbwa kwa hiyo zinaweza kukuchanganya kidogo. baada ya siku chache macho huwa na matongo tongo na sio machozi tena na puani atatoa makamasi mazito na sio majimaji tena, mbwa huwa na kikohozi kikavu, hutapika, kuharisha na hii husababisha upungufu wa maji mwilini. ndani ya wiki moja au zaidi mbwa ataonekana kupata nafuu na hii hutokea zaidi kwa mbwa waliotibiwa na dawa za antibaiotiki kama OTC  na Gentamycin, lakini hali hubadilika baada ya mashambulizi ya juu kutokea kwenye njia ya hewa na mfumo wa chakula

Hatua ya pili ni baada ya wiki mbili au tatu mbwa wengi wataonyesha dalili za magonjwa ya akili, kushambulia ghafla, kutingisha kichwa, kutafuna kama vile anatafuna bazoka/chewing gum, kukimbia kwa kujizungusha mduara na kuanguka chini, kupiga mateke miguu yote minne, kuona aibu na wakati mwingine anakua haoni vitu vizuri sababu ya kushambuliwa macho. Dalili nyingine ni kuvimba kwa pua na nyayo za mbwa ingawa hii haitokei sana

MATIBABU
Matibabu yanakuwa ya uhakika zaidi kama mbwa atatibiwa mapema wakati wa dalili za mwanzo kabisa, antibaiotiks husaidia sana kupunguza mashambulizi ya juu (secondary infections) ingawa hazitaua virusi vinavyosababisha ugonjwa huu, Mbwa pia watahitaji drip ya maji ili kufidia upungufu mkubwa wa maji uliosababishwa na kutapika/kuharisha, pia apewe dawa za kuzuia kuharisha na kutapika pamoja na dawa za usingizi ili apumzishe ubongo wake vya kutosha



KINGA
Hii ndio njia sahihi ya kupambana na ugonjwa huu, siku hizi kuna chanjo moja kwa ajili ya magonjwa manne DHPP (distemper, hepatitis, parvovirus, and parainfluenza combination) ambapo chanjo hii wapigwe watoto wa mbwa kabla ya kufikisha wiki 8 toka wazaliwe au wapigwe kabla kama mama yao hakuchanjwa kabisa



Thursday, August 23, 2012

SILAGE - CHAKULA BORA CHA MIFUGO WAKATI WA KIANGAZI

Silage ni chakula maalum kinachotengenezwa kwa kutumia aina yoyote ya malisho yanayofaa kwa mifugo kama majani, nyasi, mabua ya mahindi, mtama na ufuta. Kwa kawaida silage hutengenezwa wakati wa mvua ambapo majani hukua kwa haraka na kukatwa tena na tena mpaka kiangazi kitakapoanza, kama una shamba binafsi la majani ya napier unaweza ukawa unayaka kila baada ya wiki sita katika kipindi cha mvua. Silage utokea baada ya majani kuozeshwa na vimelea katika mfumo usiotumia oxijeni (anaerobic fermentation)

VIFAA
1- Majani na mabua kama chakula cha mifugo
2- Molasses ambayo hupatikana kwenye viwanda nya miwa
3- Panga au mashine ya kukata kata majani
4- Maji
5- Mfuko mkubwa mweusi wa plastiki au shimo liliojengewa kuta zake

NAMNA YA KUTENGENEZA SILAGE
1- Katakata malisho yako katika vipande vidogo vodogo kwa kutumia panga au mashine maalum.
2- Changanya molasses kiasi cha kila lita moja kwa lita mbili za maji au lita mbili na nusu za maji kama malisho ni makavu kiasi na lita tatu za maji kama malisho ni makavu zaidi
3- Changanya mchanganyiko wa maji na molasses pamoja na malisho kiasi malisho yako yalowane kisasi tu
4- Weka kwenye mfuko wako au kwenye shimo lililo jengewa na shindilia vizuri
5- Funga vizuri mfuko wako na uuweke mahali pasipo na jua
6- Kama unatuma shimo lililojengewa lifunike vizuri na plastiki na unaweza kuweka udongo kiasi juu yake
7- Hakikisha kwamba hamna hewa inayoopenya kwenye mchanganyiko wako

SILAGE ILIYOTENGENEZWA KWENYE DUMU LA PLASTIKI



MATUMIZI
Silage huwa tayari baada ya miezi 3 - 4 kutegemeana na aina ya malisho yaliyotumika, umri wa malisho, ubora wa uchanganyaji na mengineyo. Baada ya kuwa tayari unaweza kuanza kulisha mifugo yako silage uliyotengeneza wakati wa mvua nyingi, silage inauwezo wa kukaa hadi miaka minne tangu kuanza kutengenezwa kwake

FAIDA
1- Hupunguza tatizo la chakula wakati wa kiangazi
2- Huongeza utoaji wa maziwa wakati wa kiangazi
3- Mifugo huwa na afya bora hata wakati wa jua kali na malisho duni
4- Mifugo yenye afya bora huzaliana vizuri wakati wote
5- hupunguza gharana ya mashudu kwani silage ina virutubisho vingi
6- Mayai ya minyoo hufa wakati wa kutengeneza silage

Wednesday, August 22, 2012

NG'OMBE ALIYE KWENYE JOTO - JINSI YA KUMTAMBUA

Kwa kawaida ng'ombe jike aliyebalehe huingia kwenye joto kila baada ya siku 14 - 24 au wastani wa siku 21 kama hatapandwa na kushika mimba, hii hutegemea na aina ya ng'ombe, mazingira, lishe na hali ya hewa. kuna masaa kati ya 6 - 10 kabla hajaingia vizuri kwenye joto (pre heat) na joto lenyewe huchukua kati ya masaa 4 - 30 pia kutegemeana na aina ya ng'ombe, mazingira, lishe na hali ya hewa na yai hupevuka kwa wastani wa masaa 10 - 12 baadae

Kama utataka kumpandisha ng'ombe jike wako kwa kutumia madume bora ya kuazima au kwa kutumia  kupandisha kwa njia ya chupa, basi ni muhimu kuzijua dalili kuu ambazo huonekana ng'ombe jike anapokuwa kwenye joto, dalili hizi zinaweza kuonekana kabla ya joto, wakati wa joto ana hata baada ja joto kupita kidogo, kwa hiyo ni muhimu kuzitambua mara zinapoanza ili usiweze kupitiliza na kulikosa joto halisi

DALILI KUU

  1. Sehemu ya nje ya kizazi/uke huwa kubwa zaidi kama imeumuka na kutuna zaidi ya ile saizi yake ya kawaida.
  2. Sehemu ya nje ya kizazi/uke huwa na rangi nyekundu inayoelekea kukooza zaidi ya kawaida yake.
  3. Ute ute hutoka kwenye kizazi na huwa mzito wenye kunata nata.
  4. Ng'ombe huwa hatulii, mwenye kuzunguka zunguka na hata kulia lia zaidi ya kawaida yake.
  5. Ingawa ni jike lakini pia hujaribu kuyapanda majike mengine yaliyopo bandani, kana kuna mabanda mengine zaidi, ukimuhamisha hali hii ya kuwapanda wenzie hizi.
  6. Hunyanyua nyanyua mkia na kwenye ncha mkia huwa imevurugika (rough)
  7. Ukimgandamiza mgongoni kwa kutumia mikono sehemu ya nyuma kabisa karibu na mkia hutulia na kusikilizia kama anapandwa, mwanzo hatatulia ila ukifikia wakati sahihi atatulia na hapo ndipo unapoweza kumuwekea mbegu kwa njia ya chupa na kama unatumia dume lenyewe litatambua hali hii kwa hiyo ukiona dalili tu zinaanza mpeleke kwa dume na lenyewe litapanda kwa wakati sahihi.

Wednesday, August 15, 2012

SUKUMA VUTA -Njia bora ya kupambana na kiwavi mshambulia mabua ya mahindi (maize stalk borer)


Kiwavi anayeshambulia mabua ya mahindi anajulikana pia kama maize stalk borer (Sesamia fusca) kiwavi huyu hutokana na vipepeo weupe wanao onekana kwenye mashamba ya mahindi, vipepeo hawa hutaga na baada ya mayai yao kuanguliwa ndipo viwavi hawa waharibifu hutokea na kuanza kushambulia mahindi shambani



Viwavi hawa hushambulia katikati ya mabua na kusababisha mmea kudumaa na kisha kufa, hali huwa mbaya zaidi kama mashambulizi yatatokea wakati mimea ikiwa bado michanga maana mkulima hatavuna kabisa katika mimea iliyoshambuliwa na pia hupunguza mavuno kwenye mimea iliyokomaa na kutoa mbelewele



Njia hii ya sukuma vuta ni njia yenye mafanikio kwa asilimia kupambana na viwavi hawa kama utafuata maelekezo kwa usahihi, na hii itakusaidia kupambana na viwavi hawa kwa njia ya kibaiolojia bila kutumia kemikali zozote shambani mwako
 Ilikupambana na viwavi hawa waharibifu kwenye shamba lako la mahindi, panda mimea ya desmodium kila baada ya mistari mitano ya mahindi, desmodiuM husaidia kufukuza vipepeo na viwavi kutokana na harufu yake kali na wakati huo huo kuongeza nitrjeni kwenye udongo shambani

Panda majani aina ya napier kuzunguka shamba lako, kwani majani haya huwavutia pia vipepeo na viwavi hawa waharibifu, wakati desmodium inawafukuza nje ya shamba lako viwavi hawa, majani ya napier yanakuwa yanawavuta nje ya shamba lako na ndio maana njia hii ya kibaiolojia hiutwa SUKUMA VUTA