CHOMBO KINAKUJA
Wadau samahanini sana kwa kupotea humu kijiweni, ilikuwa ni lazima nipotee ili vitu vingine viende, lakini sasa nimerudi rasmi kwenye kijiwe changuWiki hii nilikuwa wilayani
Rufiji nilifika sehemu kama Kibiti, Utete, Ikwiriri, Mkongwa na Nyamwage. Nililala Utete, ni sehemu tulivu na watu wake ni wakarimu kama tulivyo waTanzania wote.
Hali ya utete kwa wakati huu ni joto limepungua sana wala uhitaji kulala na feni kama DSM, kuna mbu wengi sana ni lazima ulalae na chandarua, mji hii uko pembeni ya mto Rufiji

Wakati wa kwenda tulitumia barabara ya Kilwa hadi
Kibiti tukakata kulia kama unaelekea hifadhi ya Selous na kufika kijiji cha
Mkongwa tukakata kulia na kuelekea kwenye kivuko cha Utete, tukasubiri pantoni baaddae tukavuka na kuingia Utete kama saa 3 asubuhi kwa kupitia njia hii ya mkato tuliokoa mwendo wa kilometa kama 40.
Utete tuliona vitu vingi maana kwanza kuna mto huu wa Rufiji, lakini bado hawajaanza kuutumia kiukamilifu, ila nina imani mambo yatakuwa mazuri maana kuna
RUBADA ambayo mamlaka hii imepewa jukumu la kuendeleza bonde la Rufiji.
NAHODHA WA MV UTETE - BWANA ALLI
Wakazi wa Utete ni wakulima wa mazao kama Mpunga, mahindi na shughuli za uvuvi, pia kuna baadhi wanafuga samaki katika mabwawa binafesi ingawa ufugaji wao si mkubwa na si wakitaalam zaidi
TAA ZA BARABARANI - uswazi kwetu hamna hizi
Mji wa Utete una huduma za simu mitandao ya Voda, tigo , Airtel na Zantel, pia kuna umeme na taa mpaka za barabarani ingawa barabara hazina lami, mji una maji ya bomba lakini cha kuchekesha chanzo ni kisima waka mji unapitiwa na mto hapo hapo, maji ni ya chumvi
URITHI WETU
Usafiri ni wa mabasi mawili kwa siku moja saa 12 asubuhi na lapili kwenye saa 6 mchana ukiyakosa hayo, omba lifti kwenye magari madogo madogo ya Serekali au Binafsi au sivyo utalala.
WATAALAMU WA USHAURI KWENYE NYANJA ZOTE
Huduma nyingine ni Hospitali ndogo, pia kuna Magereza, kuna BOma lililojengwa na mkoloni linalotumika kama Ofisi ya Wilaya, Kuna posta, Nyumba za kulala wageni, sehemu za vinywaji, soko, na maduka ya bidhaa mbali mbali.
CHEMCHEM YA MAJI MOTO
Ukifika Utete ulizia wakulete huku, kwa pikipiki ni buku tu unalipia, wenyeji wanaamini maji haya ni yamaajabu na yanaweza kuytibu magonjwa, niliogopa kuwaambia hii ni volcanic feature
USAFIRI TOKA VIJIJI VINGINE KUJA UTETE
MAPATO NI MUHIMU
EWURA WAKIJA HUKU NI BALAA- PETROL INAUZWA KWENYE HIVYO VIDUMU
NILIUKUTA MTIKI IKABIDI NIUHUG
MKONGWA
KILMO KWANZA