Mbegu hii ya ng'ombe hupatikana zaidi kwenye nchi za Afrika ya magharibi, kaskazini na kati katika nchi za Guinea, Sierra Leone, Liberia, Mali na Ivory Coast ndiko wanakopatikana zaidi. Aina hii ya ng'ombe haina nundu tofauti na ng'ombe wetu wa asili nchini Tanzania, wana pembe kati ya wastani hadi kubwa kabisa na wana miili yenye misuli ya hii huwafanya wawe bora katika uzalishaji wa nyama ingawa hawana miili mikubwa. uzazi wa kwanza kwa majike ni baada ya kufikia miaka mitatu (3)
N'dama wanasifika duniani kote kutokana na uwezo wao wa kuhimili ugonjwa wa ndorobo (trypanosomiasis) unaosambaza wa mdudu ajulikanaye kama mbung'o (tse tse fly) ambaye pia husambaza ugonjwa wa malale kwa binadamu.
Karibuni kwenye blog yangu ambayo najaribu kutoa elimu kidogo niliyo nayo. Kama unataka kufanya kilimo, ufugaji wanyama, ufugaji wa samaki, ufugaji wa nyuki, kilimo cha miti ya mbao, kilimo cha majani na malisho ya mifugo, utaalamu wa mbolea na udongo katika mazingira halisi ya ki Tanzania basi wasiliana nami (mitiki1000@gmail.com) NB sihusiki na habari za masoko ya bidhaa yoyote ya kilimo na mifugo, kabla hujaingia kwenye mradi fanya utafiti wa masoko wewe mwenyewe
Tuesday, May 8, 2012
Wednesday, May 2, 2012
KILIMO BORA CHA UFUTA
Ufuta (sesamum indicum)ni zao linalolimwa kwa wingi katika mikoa ya Lindi, Mtwara, Ruvuma, Pwani, Morogoro, Dodoma, Tanga na ukanda wa chini katika mikoa ya Rukwa na Mbeya. Zao hili hulimwa kwa ajili ya chakula na biashara. Mbegu za zao hili huwa na wastani wa mafuta kiasi cha asilimia 45.

MAMBO YA KUZINGATIA WA KATI WA KUZALISHA MBEGU •
Chagua aina ya mbegu inayotoa mazao mengi na bora, inayovumilia mashambulizi ya magonjwa na wadudu, inayokomaa mapema na kutoa mafuta mengi.
• Chagua mbegu inayokomaa kwa pamoja ili kurahisisha uvunaji na pia kuepuka upotevu wa zao shambani. • Aina nyeupe ya mbegu ya ufuta hupendelewa zaidi kuliko aina nyeusi.
UPANDAJI
Panda mbegu nusu inchi chini ya udongo, inchi sita umbali wa mbegu na mbegu na futi mbili nafasi ya msitari na msitari, kabla ya kupanda hakikisha ardhi imelowana vya kutosha na upande mbegu masaa mawili au matatu baadae
MBOLEA
Ufuta unahitaji rutuba ya kutosha ili kutoa mazao bora. Katika kudumisha rutuba ya udongo, tumia kilimo cha mzunguko wa mazao au weka mbolea za asili pale inapobidi.
PALIZI
Dhibiti magugu kwa kupalilia ili kuruhusu ufuta kutumia vizuri unyevu na virutubishi. Magugu mengine huwa ni maficho ya wadudu waharibifu wa zao la ufuta.
MAGONJWA NA WADUDU
Ufuta hushambuliwa na magonjwa na wadudu mbalimbali ambao huweza kusababisha upungufu na ubora wa mazao. Hivyo kagua shamba mara kwa mara hasa kwenye maua na mapodo ili kuona dalili za mashambulizi. Endapo kuna dalili zamashambulizi, chukua tahadhari mapema kabla ya uharibifu mkubwa haujatokea.
MAANDALIZI KABLA YA KUVUNAKAGUA SHAMBA
• Kagua shamba kuona kama ufuta umekomaa. • Ufuta hukomaa, kati ya miezi mitatu na minne tangu kupanda kutegemea aina.
• Aina ya ufuta usiokuwa na matawi hukomaa mapema kuliko ile yenye matawi.
• Ni muhimu kuwahi kuvuna ili kuepuka ufuta kupukutikia shambani.
DALILI ZA KUKOMAA UFUTA SHAMBANI
• Kwa kawaida majani hubadilika rangi kutoka kijani na kuwa ya manjano na hatimaye kudondoka.
• Mashina hubadilika rangi kutoka kijani na kuwa ya kahawia.
VIFAA VYA KUVUNIA
• Kamba
• Siko
• Panga
VIFAA VYA KUKAUSHIA
• Sehemu ya kukaushia yenye Sakafu ya saruji
• Maturubai
• Sakafu safi
USAFIRI
• Mikokoteni
• Matela ya matrekta
• Magari
KUVUNA
• Vuna ufuta mapema kabla mapodo kukomaa sana na kuanza kupasuka na kuachia punje.Mapodo ya ufuta yaliyokomaa sana yakiguswa au kutikiswa na upepo hupasuka na kuachia mbegu, hali inayosababisha upotevu mkubwa.
• Mbegu za ufuta ni ndogo na zikidondoka chini ni vigumu kuziokota. Vilevile mbegu zilizodondoka ni vigumu kuzitenganisha na uchafu.
• Uvunaji wa ufuta huhusisha ukataji wa mimea yenye mapodo kwa kutumia vyombo vya mkono kama panga kwa kukata mashina.
• Kwa aina za ufuta zenye mapodo yanayopasuka, uvunaji ufanyike wakati mimea bado ni kijani ili kuepuka upotevu wa mbegu.
• Aidha uvunaji ufanyike wakati hakuna upepo wala jua kali.
• Baada ya kukata mashina yafunge katika mizigo midogo na kuweka katika vyombo vya kusafirisha kama vile mikokoteni, matela au magari hadi sehemu ya kukaushia.
• Panga mizigo midogo kwa kusimamisha katika malundo madogo yasiyozidi mizigo minane kwenye sehemu safi za kukaushia.
KUKAUSHA
Mapodo ya ufuta hukaushwa yakiwa yamefungwa katika vitita. Vitita huwekwa kwa kuegeshwa kwenye fremu ya kukaushia kwa muda wa wiki mbili hadi tatu kutegemea hali ya hewa. Fremu hii huwekwa juu ya turubai au sakafu ili kuzuia upotevu wa punje kutokana na kupasuka kwa mapodo.
KUPURA
Upuraji hufanyika kwenye turubai, mkeka au kwenye sakafu safi.
• Vitita hupigwa taratibu kwa kutumia mti au hutikiswa vikiwa vimegeuzwa vichwa chini ili kuruhusu punje za ufuta kudondoka kwenye sakafu safi au turubai.
KUPEPETA NA KUPEMBUA
Kupepeta na kupembua hufanywa ili kuondoa takataka kama vile mawe, vipande vya mapodo,vijiti na vumbi.Njia bora ya kupepeta na kupembua ni kwa kutumia mikono.
• Ufuta huwekwa kwenye vyombo kama vile ungo kwa kiasi cha kilo mbili hadi tatu. Ufuta hurushwa hewani kwa kasi ndogo na takataka nyepesi huchukuliwa na upepo. Zile nzito huondolewa kwa mikono.
KUFUNGASHA
Mbegu za ufuta zilizo safi huwekwa kwenye vifungashio kama vile magunia madogo ya aina ya juti ya ujazo wa kilo 50.
• Fungasha mbegu za ufuta kwenye magunia yenye uzito usiozidi kilo 50. Kabla ya kufungasha hakikisha mbegu zimekauka hadi kufikia unyevu wa asilimia 10.
KUHIFADHI
• Panga magunia ya ufuta juu ya chaga.
• Panga kwa kupishanisha ili kuruhusu mzunguko wa hewa kati ya magunia.
KUSINDIKA MBEGU ZA UFUTA
Ufuta husindikwa kupata bidhaa ya mafuta ambayo hutumika katika mapishi mbalimbali. Mafuta hukamuliwa kwa kutumia njia za asili na kwa kutumia mashine. Njia za asili zina ufanisi mdogo ukilinganisha na zile za kukamua kwa mashine, hivyo ni vyema kutumia mashine. Kuna mashine za aina mbili zinazotumika kukamua mafuta; mashine za mkono na zile zinazoendeshwa kwa injini au mota ya umeme. Mashine za mikono zinazotumika zaidi hapa nchini ni za aina ya daraja (Bridge press) na Ram.
KUKAMUA KWA MASHINE YA DARAJA
Mashine ya daraja ni moja ya mashine za kisasa zinazoweza kukamua mafuta ya ufuta. Mashine hizi huendeshwa kwa mikono na zina uwezo wa kukamua mafuta kwa asilimia 68 hadi 72. Inaweza kukamua kilo 25 za ufuta kwa saa moja. Ili kupata ufanisi mzuri wa mashine hii, ni muhimu ufuta uwe na unyevu wa kati ya asilimia 11 na 13. Iwapo unyevu utakuwa chini ya kiwango hicho inashauriwa kunyunyizi maji kwenye ufuta kabla ya kukamua.

VIFAA VYA KUKAMULIA MAFUTA
• Mashine ya daraja
• Sufuria • Vifungashio
• Mifuko midogo ya nguo au viroba vyenye upana wa sentimita 20 na urefu wa sentimita 20.
• Chombo cha kukinga mafuta.
• Chujio safi
• Lebo
• Lakiri Malighafi
• Mbegu za ufuta safi
• Maji safi
UKAMUAJI MAFUTA
• Nyunyuzia maji kidogo kwenye ufuta ili kuongeza unyevu kufikia asilimia 11 hadi 13. Mafuta hutoka vizuri kwenye kiwango hicho cha unyevu.
• Jaza ufuta kwenye vifuko vya nguo au viroba
• Vipange vifuko hivyo kwenye silinda na kuanza kuzungusha mhimili hadi mafuta yaanze kutoka kupitia matundu ya silinda.
• Acha kwa muda mafuta yaendelee kutoka kisha endelea kuzungusha mhimili hadi mafuta yaishe. Mhimili ukiacha kuzunguka ni dalili kuwa mafuta yamekwisha.
• Kusanya mafuta, chuja na fungasha kwenye chupa safi zilizochemshwa. Hakikisha chupa ni kavu na zina mifuniko.
• Weka lebo na lakiri
• Hifadhi mahali pakavu na pasipo na mwanga mkali.
MASHINE YA RAM
Mashine ya Ram ina uwezo wa kusindika kilo 7 za mbegu za ufuta kwa ufanisi wa asilimia 57%.Aina ya Ram (BP-30) ina uwezo wa kukamua lita 20 za mafuta kwa siku.

VIFAA
• Ndoo
• Mashine ya Ram
• Kichujio au kitmbaa safi
• Vifungashio safi
UKAMUAJI
• Anika mbegu za ufuta juani kwa kuzitandaza kwenye mabati ili zipate joto la kutosha.
• Lengo la kuanika mbegu juani ni kurahisisha ukamuaji wa mafuta.
• Jaza mbegu za ufuta kwenye mpare wa kulishia
• Funga wenzozuia (HANDLE)ili mbegu za ufuta zisitoke.
• Nyanyua wenzozuia mpaka juu ili kuruhusu mbegu za ufuta kuingia kwenye silinda.
• Shusha wenzozuia chini ili kuruhusu pistoni kusukuma mbegu za ufuta ziingie ndani ya eneo la shindilio
. • Nyanyua tena wenzozuia mpaka juu na kushusha na wakati huohuo ukiendelea kujaza mbegu za ufuta kwenye mpare wa kulishia. Wenzoinua ukiwa mzito ni dalili kuwa msukumo wa kutosha umejengeka. Msukumo huo utasababisha mafuta kutoka.
• Mafuta yanapoanza kutoka legeza wenzozuia ili kuruhusu mashudu kutoka.
• Chuja na hifadhi mafuta kwenye vyombo safi vyenye mifuniko vilivyochemshwa.
MASHINE ZA MOTA YA UMEME
Kwa wale wanaohitaji mashine za kukamulia mafuta zinazotumia mota za umeme wakiwa Dar es salaam wafike mtaa wa Nkuruma karibu na clock tower, pale kuna maduka kadhaa yanayouza mashine na zana mbalimbali za kilimo
MATUMIZI
Mafuta ya ufuta hutumika katika mapishi mbalimbali ili kuongeza ladha. Pia husaidia kuleta nguvu na joto mwilini. Mbegu za ufuta huchanganywa na vyakula mbali mbali kama mikate, keki, mboga na kadhalika.

MAMBO YA KUZINGATIA WA KATI WA KUZALISHA MBEGU •
Chagua aina ya mbegu inayotoa mazao mengi na bora, inayovumilia mashambulizi ya magonjwa na wadudu, inayokomaa mapema na kutoa mafuta mengi.
• Chagua mbegu inayokomaa kwa pamoja ili kurahisisha uvunaji na pia kuepuka upotevu wa zao shambani. • Aina nyeupe ya mbegu ya ufuta hupendelewa zaidi kuliko aina nyeusi.
UPANDAJI
Panda mbegu nusu inchi chini ya udongo, inchi sita umbali wa mbegu na mbegu na futi mbili nafasi ya msitari na msitari, kabla ya kupanda hakikisha ardhi imelowana vya kutosha na upande mbegu masaa mawili au matatu baadae
MBOLEA
Ufuta unahitaji rutuba ya kutosha ili kutoa mazao bora. Katika kudumisha rutuba ya udongo, tumia kilimo cha mzunguko wa mazao au weka mbolea za asili pale inapobidi.
PALIZI
Dhibiti magugu kwa kupalilia ili kuruhusu ufuta kutumia vizuri unyevu na virutubishi. Magugu mengine huwa ni maficho ya wadudu waharibifu wa zao la ufuta.
MAGONJWA NA WADUDU
Ufuta hushambuliwa na magonjwa na wadudu mbalimbali ambao huweza kusababisha upungufu na ubora wa mazao. Hivyo kagua shamba mara kwa mara hasa kwenye maua na mapodo ili kuona dalili za mashambulizi. Endapo kuna dalili zamashambulizi, chukua tahadhari mapema kabla ya uharibifu mkubwa haujatokea.
MAANDALIZI KABLA YA KUVUNAKAGUA SHAMBA
• Kagua shamba kuona kama ufuta umekomaa. • Ufuta hukomaa, kati ya miezi mitatu na minne tangu kupanda kutegemea aina.
• Aina ya ufuta usiokuwa na matawi hukomaa mapema kuliko ile yenye matawi.
• Ni muhimu kuwahi kuvuna ili kuepuka ufuta kupukutikia shambani.
DALILI ZA KUKOMAA UFUTA SHAMBANI
• Kwa kawaida majani hubadilika rangi kutoka kijani na kuwa ya manjano na hatimaye kudondoka.
• Mashina hubadilika rangi kutoka kijani na kuwa ya kahawia.
VIFAA VYA KUVUNIA
• Kamba
• Siko
• Panga
VIFAA VYA KUKAUSHIA
• Sehemu ya kukaushia yenye Sakafu ya saruji
• Maturubai
• Sakafu safi
USAFIRI
• Mikokoteni
• Matela ya matrekta
• Magari
KUVUNA
• Vuna ufuta mapema kabla mapodo kukomaa sana na kuanza kupasuka na kuachia punje.Mapodo ya ufuta yaliyokomaa sana yakiguswa au kutikiswa na upepo hupasuka na kuachia mbegu, hali inayosababisha upotevu mkubwa.
• Mbegu za ufuta ni ndogo na zikidondoka chini ni vigumu kuziokota. Vilevile mbegu zilizodondoka ni vigumu kuzitenganisha na uchafu.
• Uvunaji wa ufuta huhusisha ukataji wa mimea yenye mapodo kwa kutumia vyombo vya mkono kama panga kwa kukata mashina.
• Kwa aina za ufuta zenye mapodo yanayopasuka, uvunaji ufanyike wakati mimea bado ni kijani ili kuepuka upotevu wa mbegu.
• Aidha uvunaji ufanyike wakati hakuna upepo wala jua kali.
• Baada ya kukata mashina yafunge katika mizigo midogo na kuweka katika vyombo vya kusafirisha kama vile mikokoteni, matela au magari hadi sehemu ya kukaushia.
• Panga mizigo midogo kwa kusimamisha katika malundo madogo yasiyozidi mizigo minane kwenye sehemu safi za kukaushia.
KUKAUSHA
Mapodo ya ufuta hukaushwa yakiwa yamefungwa katika vitita. Vitita huwekwa kwa kuegeshwa kwenye fremu ya kukaushia kwa muda wa wiki mbili hadi tatu kutegemea hali ya hewa. Fremu hii huwekwa juu ya turubai au sakafu ili kuzuia upotevu wa punje kutokana na kupasuka kwa mapodo.
KUPURA
Upuraji hufanyika kwenye turubai, mkeka au kwenye sakafu safi.
• Vitita hupigwa taratibu kwa kutumia mti au hutikiswa vikiwa vimegeuzwa vichwa chini ili kuruhusu punje za ufuta kudondoka kwenye sakafu safi au turubai.
KUPEPETA NA KUPEMBUA
Kupepeta na kupembua hufanywa ili kuondoa takataka kama vile mawe, vipande vya mapodo,vijiti na vumbi.Njia bora ya kupepeta na kupembua ni kwa kutumia mikono.
• Ufuta huwekwa kwenye vyombo kama vile ungo kwa kiasi cha kilo mbili hadi tatu. Ufuta hurushwa hewani kwa kasi ndogo na takataka nyepesi huchukuliwa na upepo. Zile nzito huondolewa kwa mikono.
KUFUNGASHA
Mbegu za ufuta zilizo safi huwekwa kwenye vifungashio kama vile magunia madogo ya aina ya juti ya ujazo wa kilo 50.
• Fungasha mbegu za ufuta kwenye magunia yenye uzito usiozidi kilo 50. Kabla ya kufungasha hakikisha mbegu zimekauka hadi kufikia unyevu wa asilimia 10.
KUHIFADHI
• Panga magunia ya ufuta juu ya chaga.
• Panga kwa kupishanisha ili kuruhusu mzunguko wa hewa kati ya magunia.
KUSINDIKA MBEGU ZA UFUTA
Ufuta husindikwa kupata bidhaa ya mafuta ambayo hutumika katika mapishi mbalimbali. Mafuta hukamuliwa kwa kutumia njia za asili na kwa kutumia mashine. Njia za asili zina ufanisi mdogo ukilinganisha na zile za kukamua kwa mashine, hivyo ni vyema kutumia mashine. Kuna mashine za aina mbili zinazotumika kukamua mafuta; mashine za mkono na zile zinazoendeshwa kwa injini au mota ya umeme. Mashine za mikono zinazotumika zaidi hapa nchini ni za aina ya daraja (Bridge press) na Ram.
KUKAMUA KWA MASHINE YA DARAJA
Mashine ya daraja ni moja ya mashine za kisasa zinazoweza kukamua mafuta ya ufuta. Mashine hizi huendeshwa kwa mikono na zina uwezo wa kukamua mafuta kwa asilimia 68 hadi 72. Inaweza kukamua kilo 25 za ufuta kwa saa moja. Ili kupata ufanisi mzuri wa mashine hii, ni muhimu ufuta uwe na unyevu wa kati ya asilimia 11 na 13. Iwapo unyevu utakuwa chini ya kiwango hicho inashauriwa kunyunyizi maji kwenye ufuta kabla ya kukamua.

VIFAA VYA KUKAMULIA MAFUTA
• Mashine ya daraja
• Sufuria • Vifungashio
• Mifuko midogo ya nguo au viroba vyenye upana wa sentimita 20 na urefu wa sentimita 20.
• Chombo cha kukinga mafuta.
• Chujio safi
• Lebo
• Lakiri Malighafi
• Mbegu za ufuta safi
• Maji safi
UKAMUAJI MAFUTA
• Nyunyuzia maji kidogo kwenye ufuta ili kuongeza unyevu kufikia asilimia 11 hadi 13. Mafuta hutoka vizuri kwenye kiwango hicho cha unyevu.
• Jaza ufuta kwenye vifuko vya nguo au viroba
• Vipange vifuko hivyo kwenye silinda na kuanza kuzungusha mhimili hadi mafuta yaanze kutoka kupitia matundu ya silinda.
• Acha kwa muda mafuta yaendelee kutoka kisha endelea kuzungusha mhimili hadi mafuta yaishe. Mhimili ukiacha kuzunguka ni dalili kuwa mafuta yamekwisha.
• Kusanya mafuta, chuja na fungasha kwenye chupa safi zilizochemshwa. Hakikisha chupa ni kavu na zina mifuniko.
• Weka lebo na lakiri
• Hifadhi mahali pakavu na pasipo na mwanga mkali.
MASHINE YA RAM
Mashine ya Ram ina uwezo wa kusindika kilo 7 za mbegu za ufuta kwa ufanisi wa asilimia 57%.Aina ya Ram (BP-30) ina uwezo wa kukamua lita 20 za mafuta kwa siku.

VIFAA
• Ndoo
• Mashine ya Ram
• Kichujio au kitmbaa safi
• Vifungashio safi
UKAMUAJI
• Anika mbegu za ufuta juani kwa kuzitandaza kwenye mabati ili zipate joto la kutosha.
• Lengo la kuanika mbegu juani ni kurahisisha ukamuaji wa mafuta.
• Jaza mbegu za ufuta kwenye mpare wa kulishia
• Funga wenzozuia (HANDLE)ili mbegu za ufuta zisitoke.
• Nyanyua wenzozuia mpaka juu ili kuruhusu mbegu za ufuta kuingia kwenye silinda.
• Shusha wenzozuia chini ili kuruhusu pistoni kusukuma mbegu za ufuta ziingie ndani ya eneo la shindilio
. • Nyanyua tena wenzozuia mpaka juu na kushusha na wakati huohuo ukiendelea kujaza mbegu za ufuta kwenye mpare wa kulishia. Wenzoinua ukiwa mzito ni dalili kuwa msukumo wa kutosha umejengeka. Msukumo huo utasababisha mafuta kutoka.
• Mafuta yanapoanza kutoka legeza wenzozuia ili kuruhusu mashudu kutoka.
• Chuja na hifadhi mafuta kwenye vyombo safi vyenye mifuniko vilivyochemshwa.
MASHINE ZA MOTA YA UMEME
Kwa wale wanaohitaji mashine za kukamulia mafuta zinazotumia mota za umeme wakiwa Dar es salaam wafike mtaa wa Nkuruma karibu na clock tower, pale kuna maduka kadhaa yanayouza mashine na zana mbalimbali za kilimo
MATUMIZI
Sunday, April 15, 2012
KILIMO BORA CHA ALIZETI
Alizeti hulimwa kwa wingi katika mikoa ya Shinyanga, Singida, Dodoma, Iringa, Tabora, Morogoro, Ruvuma, Mbeya, Arusha, Manyara, na Rukwa. Zao hili hulimwa kwa ajili ya chakula na biashara.
MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA WAKATI WA UZALISHAJI
Kuchagua aina bora ya mbegu
• Chagua aina bora ya mbegu inayovumilia magonjwa, wadudu, inayotoa mazao mengi na kiwango kikubwa cha mafuta.
• Vilevile chagua aina ya mbegu ambayo hukomaa kwa wakati mmoja ili kurahisisha uvunaji.
KUWEKA MBOLEA
• Rutubisha udongo kwa kutumia mbolea za mboji na samadi ili kupata mazao mengi na bora.
KUDHIBITI WADUDU NA MAGONJWA
Alizeti hushambuliwa na magonjwa ya majani, mizizi na masuke ambayo husababisha upungufu wa mavuno. Hivyo ni muhimu kuyadhibiti ili kupata mavuno mengi na bora. Pia ndege hupunguza mavuno kwa kiasi cha asilimia 50 au zaidi. Njia ya kudhibiti ndege ni kwa kuwafukuza na kupanda mbegu zinazokomaa mapema.
MAANDALIZI KABLA YA KUVUNA;
UKAGUZI
• Kagua shamba kuona kama alizeti imekomaa. Alizeti hukomaa kati ya miezi minne hadi sita tangu kupanda. Wakati huo punje huwa na unyevu wa asilimia 25. Ni muhimu kuvuna alizeti mapema ili kuepuka mashambulizi ya panya, mchwa na ndege waharibifu.
DALILI ZA ALIZETI ILIYOKOMAA
• Suke hubadilika rangi kutoka manjano na kuelekea kuwa nyeusi.
• Viuwa vya pembeni mwa suke hunyauka na hubadilika kutoka rangi ya manjano na kuwa ya kahawia.
UVUNAJI, UKAUSHAJI NA UBEBAJI
Vifaa vya kuvunia na kubebea kutoka shambani
• Kisu
• Vikapu
• Magunia
• Matenga Vifaa vya kukaushia
• Maturubai
• Mikeka
• Kichanja bora Vyombo vya usafiri kutoka shambani
• Matoroli
• Matela ya matrekta
• Mikokoteni ya kukokotwa na wanyama
• Magari KUVUNA Alizeti huvunwa kwa kutumia mikono ambapo suke hukatwa kwa kutumia kisu. Pia mashine (combine harvester) hutumika kuvunia alizeti katika nchi zinazolima alizeti kwa wingi. Masuke ya alizeti huwekwa kwenye vikapu ambavyo hutumika kusomba alizeti ndani ya shamba. Kisha alizeti hufungashwa kwenye magunia na kusafirishwa hadi nyumbani tayari kwa kukausha.
KUKAUSHA
MAMBO MUHIMU YA KUZINGATIA WAKATI WA UZALISHAJI
Kuchagua aina bora ya mbegu
• Chagua aina bora ya mbegu inayovumilia magonjwa, wadudu, inayotoa mazao mengi na kiwango kikubwa cha mafuta.
• Vilevile chagua aina ya mbegu ambayo hukomaa kwa wakati mmoja ili kurahisisha uvunaji.
KUWEKA MBOLEA
• Rutubisha udongo kwa kutumia mbolea za mboji na samadi ili kupata mazao mengi na bora.
KUDHIBITI WADUDU NA MAGONJWA
Alizeti hushambuliwa na magonjwa ya majani, mizizi na masuke ambayo husababisha upungufu wa mavuno. Hivyo ni muhimu kuyadhibiti ili kupata mavuno mengi na bora. Pia ndege hupunguza mavuno kwa kiasi cha asilimia 50 au zaidi. Njia ya kudhibiti ndege ni kwa kuwafukuza na kupanda mbegu zinazokomaa mapema.
MAANDALIZI KABLA YA KUVUNA;
UKAGUZI
• Kagua shamba kuona kama alizeti imekomaa. Alizeti hukomaa kati ya miezi minne hadi sita tangu kupanda. Wakati huo punje huwa na unyevu wa asilimia 25. Ni muhimu kuvuna alizeti mapema ili kuepuka mashambulizi ya panya, mchwa na ndege waharibifu.
DALILI ZA ALIZETI ILIYOKOMAA
• Suke hubadilika rangi kutoka manjano na kuelekea kuwa nyeusi.
• Viuwa vya pembeni mwa suke hunyauka na hubadilika kutoka rangi ya manjano na kuwa ya kahawia.
UVUNAJI, UKAUSHAJI NA UBEBAJI
Vifaa vya kuvunia na kubebea kutoka shambani
• Kisu
• Vikapu
• Magunia
• Matenga Vifaa vya kukaushia
• Maturubai
• Mikeka
• Kichanja bora Vyombo vya usafiri kutoka shambani
• Matoroli
• Matela ya matrekta
• Mikokoteni ya kukokotwa na wanyama
• Magari KUVUNA Alizeti huvunwa kwa kutumia mikono ambapo suke hukatwa kwa kutumia kisu. Pia mashine (combine harvester) hutumika kuvunia alizeti katika nchi zinazolima alizeti kwa wingi. Masuke ya alizeti huwekwa kwenye vikapu ambavyo hutumika kusomba alizeti ndani ya shamba. Kisha alizeti hufungashwa kwenye magunia na kusafirishwa hadi nyumbani tayari kwa kukausha.
KUKAUSHA
Kuna hatua mbili za kukausha alizeti; kukausha masuke na kukausha mbegu za alizeti. Kukausha masuke
• Masuke hutandazwa kwenye kichanja bora katika kina kisichozidi sentimita 30 ili yaweze kukauka vizuri.
• Vilevile huweza kutandazwa kwenye maturubai, mikeka au sakafu safi.
• Lengo la hatua hii ni kukausha masuke ya alizeti ili kurahisisha upuraji. KUPURA Upuraji hufanyika baada ya kuhakikisha kuwa masuke ya alizeti yamekauka vizuri. Masuke ya alizeti hupurwa kwa kutumia mikono ambapo mbegu hutenganishwa kwa kupiga masuke taratibu kutumia mti. Ni muhimu kupiga masuke taratibu ili kuepuka kupasua mbegu
. • Pura kwenye kichanja bora, maturubai au mikeka.
KUKAUSHA MBEGU
• Mbegu za alizeti hukaushwa juani kwa kutandazwa kwenye vichanja bora, maturubai, mikeka au sakafu safi.
• Tandaza mbegu katika kina kisichozidi sentimita 4 ili ziweze kukauka vizuri.
• Lengo la hatua hii ni kukausha mbegu baada ya kupura ili kufikia kiwango cha unyevu kinachotakiwa kwa hifadhi salama ambacho ni asilimia 8.
JINSI YA KUTAMBUA MBEGU ZILIZOKAUKA VIZURI
Kufikicha mbegu
• Mbegu zilizokauka maganda yake hutoka kwa urahisi zinapofikichwa. Kumimina kwenye chombo kama debe
• Mbegu zilizokauka hutoa mlio mkali zinapomiminwa kwenye vyombo hivyo.
• Mbegu zilizokauka hung’ara Kutumia kipima unyevu.
• Mbegu zilizokauka vizuri kipimo huonyesha asilimia 8
. KUPEPETA NA KUPEMBUA
Kupepeta na kupembua hufanyika ili kuondoa takataka kama vile mawe, wadudu, mapepe, mbegu zilizooza au kupasuka. Mbegu za alizeti hupepetwa kwa kutumia ungo au mashine zinazoendeshwa kwa mkono, injini au umeme. Mashine hizi zina uwezo wa kupepeta na kupembua kilo 60 hadi 350 kwa saa kutegemea aina ya mashine na ukubwa wa mashine yenyewe
KUHIFADHI
Alizeti iliyopurwa huhifadhiwa katika hali ya kichele kwenye maghala bora, yaani vihenge, sailo au bini. Alizeti ya kuhifadhi kwenye maghala ya nyumba ifungashwe kwenye magunia na ipangwe kwenye chaga kwa kupishanisha. Ili kurahisisha kazi ya kukagua ghala, acha nafasi ya mita moja kutoka kwenye ukuta. Ziba sehemu zote za ghala ili kuzuia panya kuingia. Panya hupenda sana kula punje za alizeti, na husababisha upungufu mkubwa wa punje ambao husababisha upotevu wa asilimia 30 kwa kipindi cha miezi mitatu ya hifadhi. Asilimia ya upotevu inaweza kuwa kubwa zaidi kutegemea idadi ya panya na upatikanaji wa vyakula vingine kwa wakati huo. Matumizi ya Mbegu za Alizeti Mbegu za alizeti hasa zenye mistari zinaweza kuliwa baada ya kukaangwa au kukaushwa. Pia zinatumika katika utengenezaji wa mikate. Mbegu za alizeti husindikwa kupata bidhaa ya mafuta.
KUSINDIKA MBEGU ZA ALIZETI KUPATA MAFUTA
KUSINDIKA MBEGU ZA ALIZETI KUPATA MAFUTA
Vifaa
• Mashine ya kukamua mafuta
• Chujio safi
• Ndoo
• Vifungashio
• Sufuria
• Mizani Malighafi
• Mbegu za alizeti
• Maji
• Chumvi
NJIA YA KUKAMUA MAFUTA
• Chagua mbegu bora za alizeti
• Zianike kwenye jua kwa muda wa saa 1 hadi 2
• W eka kwenye mashine ya kukamulia ya daraja au Ram
• Kamua mafuta
• Chuja mafuta kwa kitambaa au chujio safi
• Pima mafuta yaliyokamuliwa.
• Ongeza maji na chumvi. Katika lita 10 za mafuta weka lita moja ya maji na gramu 200 za chumvi. • Weka mafuta kwenye chombo cha kuchemshia (sufuria)
• Chemsha hadi maji yote yaishe
• Sauti ya kuchemka ikiisha ni dalili kuwa maji yamekwisha.
• Ipua, acha yapoe, kisha chuja kwa kitambaa safi au chujio
• Fungasha kwenye vyombo safi na vikavu na vyenye mifuniko
• W eka lakiri na lebo • Hifadhi kwenye sehemu safi, kavu na yenye mwanga hafifu.
MATUMIZI
Mafuta hutumika katika mapishi mbalimbali na yana virutubishi vifuatavyo: - Mafuta gramu 100 Nguvu kilokalori 900
Monday, April 2, 2012
HALI YA KILIMO ILIVYO SASA MKOANI SINGIDA
Hawa ni wale ambao walifuata ushauri wa kitaalam ikiwamo aina ya mbegu, utabiri wa kiasi cha mvua inayotegemewa kunyesha, muda wa upandaji na matumizi sahihi ya mbolea
Monday, December 19, 2011
MGOGORO WA KILIMO CHA MAHINDI MKOANI SINGIDA
Umeibuka mgogoro mkoani Singida mara baada ya mkuu wa mkoa Dr.Parseko Kone kupiga marufuku kilimo cha mahindi mkoani humo. Mmoja wa waliopinga mpango huo ni Mheshimiwa Salome Mwambu mbunge wa Iramba mashariki kwa tiketi ya CCM.
Akitetea kilimo cha mahindi MH Mwambu alisema kwamba hilo silo tamko la mkoa kwa sababu hakuna hata kiongozi mmoja wa mkoa au wilaya ambaye alijaribu kuwashirikisha wananchi kwenye mchakato huo
Pia alisema kwamba kilimo cha mahindi kilikuwepo kwa miaka mingi mkoani humo na zao hilo likiwa ni la biashara na chakula kwa wananchi wenyewe

MAONI YANGU
Viongozi wote wawili walikuwa na nia njema sana kwa wananchi wa Singida, mkuu wa mkoa alikuwa anajitahidi kukabiliana na njaa mkoani mwake na ndio maana akawa anasisitiza kilimo cha mazao ya kinga ya njaa,ambayo ni yale yanayohimili ukame na uhaba wa mvua kama mtama, ufuta na uwele n.k
Mh mbunge naye alikuwa akiwatetea wananchi wake kwa sababu ndio wapigakura wake na yeye ndiye mwakilishi wao, akiangalia anaona kwamba miaka mingi watu wamekuwa wakitegemea mahindi kama zao la chakula na biashara, ndio maana akashauri kwamba watu wasikatazwe kulima mahindi bali walazimishe kupanda na mazao ya kinga ya njaa
Kwa ujumla wote wamefanya maamuzi bila ya kuwashirikisha wataalamu wa kilimo na hali ya hewa, kila mtu alikuwa anatetea kibarua chake. kama wange washirikisha wataalamu basi nina imani kwamba mabo yangekuwa mazuri.
Mkoa wa Singida ni moja ya mikoa inayopata mvua moja kubwa kwa mwaka, na hali yake ni ya ukame kiasi ingawa mvua zinaweza kuwa kubwa zikiambatana na upepo ambao pia huleta madhara kama ya kuharibu mazao na makazi ya watu, mabadiliko tabia nchi yamesababisha kuwe na mvua zisizotabirika na tume shuhudia mara kadhaa zikiwa chini ya kiwango. mkoa huu pia umeathirika na ukataji miti kwa ajili ya kuni, mkaa na matumizi mengine, na pia ufugaji uliokithiri umesababisha uharibifu wa udongo na kusababisha mmong'onyoko wa udongo kwenye baadhi ya sehemu. kwa sababu hizi na nyinginezo zote kwa pamoja zimesababisha madhara kwenye mfumo wa kilimo uliozoeleka na wenyeji wa mkoa huu.

USHAURI
1 - Wakulima walime mahindi kwenye sehemu zilizo tambarare na kwenye mabonde ambako unyevu unachelewa kukauka na wasilime mahindi kwenye uwanda wa juu na milimani kwani sehemu hizo ndizo zinafaa kwa mazao ya kinga ya njaa
2 - Matumizi ya kanuni za kilimo kilimo bora yazingatiwe kama kutumia mbegu bora za mahindi zinazokomaa muda mfupi za zinazoendana na hali ya hewa ya Singida, matumizi ya mbolea za samadi, viuatilifu salama n.k
3 - Upandaji wa mbegu kwa wakati, na kwa kufuata majira ya hali ya hewa, hii ni baada ya kufuata ushauri wa watabiri wa hali ya hewa, hili la hali ya hewa lifanywe na Mbunge akishirikiana na Mkuu wa Mkoa, yaani wafuatilie na wawaeleze wakulima muda sahii wa kuandaa mashamba na kuanza kupanda (wasilete siasa hapa)
4 - Viongozi wa siasa wakae na wakulima/maafisa kilimo na kushauriana nao kuhusu kilimo kwa ujumla, ikiwezekana wasaidie kuanzia upatikanaji wa mbegu bora watakazozichagua kwa pamoja, madawa ya kuua wadudu na taarifa za wadudu au magonjwa ya mazao ili kuzuia kusambaa (wanasiasa wasikae maofisini sana ila watembee kwenye himaya zao kujua matatizo)
Saturday, December 17, 2011
SAMAKI WA MAPAMBO TOKA TANZANIA - (Ornamental Fish From Tanzania)
Tanzania imejaliwa kuwa na aina mbalimbali za samaki wa mapambo wanaopatikana katika maji baridi na maji chumvi. Samaki hawa hupatikana kwa wingi katika maji ya asili na baadhi yao hupatikana humu nchini tu. Kuna samaki wa mapambo ambao wapo katika hatari ya kutoweka. Kwa kiasi kikubwa samaki wa mapambo, wamekuwa wakivuliwa na kupelekwa nje ya nchi na wafanyabiashara.
HALI YA BIASHARA YA SAMAKI WA MAPAMBO
Samaki wengi wa mapambo kwenye maji baridi ni jamii ya Cichlids. Ziwa
Tanganyika lina spishi zaidi ya 200 lakini wanaosafirishwa nje ya nchi kwa ajili ya mapambo ni wastani wa spishi 30 Ziwa Nyasa lina spishi zaidi ya 750 lakini wanaosafirishwa nje ya nchi kama samaki wa mapambo ni takriban spishi 5 ambazo ni Aulo mamelela, A. blue neon, A. hongi, Proto steven na Tropheus ndole. Ziwa Victoria lilikuwa na spishi zaidi ya 300 katika miaka ya 1970 kabla samaki aina ya Sangara aliyepandikizwa hajasambaa na kula jamii ya Cichlid. Hivi sasa baadhi ya spishi zimetoweka na biashara ya samaki wa mapambo haipo Ziwa Victoria.
CICHLIDS TOKA ZIWA TANGANYIKA

Kwa upande wa samaki wa maji chumvi wanaoishi kwenye matumbawe (coral fish species), spishi zilizopo Tanzania ni nyingi lakini idadi kamili haijulikani. Hata hivyo, kati ya spishi takriban 4,000 zilizopo duniani ni spishi 200 – 300 ndio wanaotumika kwa mapambo.
Samaki aina ya “Cichilid” hutumika sana kwa mapambo duniani kote kwa kuwa wana uwezo wa kuzoea mazingira mapya kwa haraka kuliko samaki wengine (Koning, 1995). Hii inatokana na tabia yao ya kuwa na uwezo mkubwa wa kuvumilia hali tofauti ya mazingira ya maji ikiwemo pH na uchumvi chumvi (salinity). Pia, wana tabia ya kula aina mbalimbali za vyakula kutokana na mpangilio wa midomo, meno na taya (Pharyngeal jaws). Kuna wanaokula mwani (algae), mimea (plants), samaki, konokono n.k. Pia, aina hizi za samaki wanaweza kuishi na kusafirishwa kwa muda wa siku tano (5) bila kula alimradi mazingira ya maji yanaruhusu na vifo vinaweza kuwa chini ya asilimia 2 tu wakati wa kuwasafirisha.

Takwimu za biashara ya samaki wa mapambo duniani sio sahihi sehemu nyingi. Hata hivyo takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa Uingereza mwaka 1987 waliuza samaki wa kiasi cha Paundi za Uingereza milioni 17 na Marekani waliuza samaki wa thamani ya Dola za Kimarekani milioni 739 mwaka 1988. Hata hivyo taarifa zilizopo zinaonyesha kuwa tabia ya kupenda (hobby) kufuga samaki wa mapambo inaongezeka kwenye nchi mbalimbali zikijumuisha, Japan, China, Australia, Afrika ya Kusini, Korea, Ujerumani na Malaysia. Mara nyingi ufugaji hufanyika kwenye mabwawa na matanki (aquarium).
Kwa upande wa Tanzania, takwimu za biashara ya samaki wa mapambo kutoka kwenye maji baridi kuanzia mwaka 2006 mpaka mwaka 2009 ni kama ifuatavyo: Kwa ujumla biashara ya samaki hawa huingizia Serikali pesa kidogo sana. Samaki wengi waliosafirishwa nje ya nchi katika mwaka 2006 walitoka Ziwa Nyasa. Jumla ya samaki 12,661 ambao walikuwa na thamani ya shilingi 100 87,143,451.25 waliingizia Serikali ushuru wa shilingi 6,541,825.56 tu. Jumla ya samaki 9,080 kutoka Ziwa Tanganyika waliokuwa na thamani ya shilingi 58,770,742.7 waliingizia Serikali kiasi cha shilingi 4,292,456.39. Mwaka
2009 samaki wengi walitoka Ziwa Tanganyika jumla ya samaki 23,500 wenye thamani ya shilingi 131, 356,148.5 waliingizia Serikali jumla ya shilingi 13,018,338.19 kama ushuru. Samaki kutoka Ziwa Victoria walisafirishwa wachache tu mwaka 2007, walikuwa 12 tu. Samaki wa mapambo kutoka Ziwa Victoria wako hatarini kutoweka kutokana na kuliwa na Sangara kwa hiyo wameingizwa kwenye “Red list” chini ya CITES,
hawasafirishwi tena. Kinachohimizwa ni ufugaji wa hao samaki.

FURSA YA UWEKEZAJI KATIKA SAMAKI WA MAPAMBO
i) Kuna fursa kubwa ya uwekezaji katika samaki wa mapambo wa Ziwa Tanganyika kwa kuwa samaki hao wapo wengi (Watson, 2000) na baharini kwenye matumbawe (Coral reef fish species)
ii) Kuwepo kwa masoko ya uhakika na mazingira mazuri ya kuvutia biashara Ili uendeleza na kuimarisha uwekezaji katika eneo hili ni muhimu kuhamasisha wananchi na wawekezaji kutoka nje katika kuwekeza kwenye biashara ya samaki wa mapambo. Pia, ni lazima kufanya utafiti wa kufahamu spishi zilizopo na wingi wa samaki wa mapambo ili kuepuka kumaliza baadhi ya samaki hao.
UMUHIMU WA BIASHARA YA SAMAKI WA MAPAMBO KATIKA KUONDOA UMASIKINI
Takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa mapato ya biashara ya samaki wa mapambo kwenye nchi mbalimbali duniani ina thamani ya takriban Dola za Marekani milioni 186 na samaki wengi wanatoka nchi zinazoendelea (Watson, 2000). Kati ya hizi fedha Zinazobaki kwa jamii wanaokusanya samaki hao ni kidogo sana. Hata hivyo, kama jamii itawezeshwa kupata mtaji na teknolojia sahihi itaweza kujiongezea kipato na kupunguza umaskini. Asilimia 90 ya samaki wa mapambo duniani huzalishwa kwenye mabwawa hasa kwenye nchi zilizoendelea na samaki hao wametolewa kutoka kwenye nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania. Ili mwananchi aweze kunufaika na biashara ya samaki wa mapambo kuna umuhimu wa kuwaelimishwa kuhusu njia bora za kuwavua, kuwahifadhi na kuwasafirisha kwa ajili ya kuongeza kipato chao na taifa kwa ujumla.
SAMAKI WA UREMBO TOKA ZIWA NYASA

ATHARI ZITOKANAZO NA BIASHARA YA SAMAKI WA MAPAMBO
Shirika la Kimataifa la Hifadhi ya Viumbe na Mazingira kupitia kitabu cha “Red List’’ (IUCN, 1988) kimeainisha aina za samaki wa mapambo ambao wapo hatarini Kutoweka. Samaki hao ni pamoja na aina ya furu (Haplochromine). Athari za biashara hiyo ni kama ifuatavyo:
i) Kupungua wingi na makazi ya samaki waliopo kwenye maeneo ya asili ikiwa ni pamoja na maziwa, mito na bahari kwa njia mbalimbali. Hali ya aina hii imekwishatokea kwenye nchi ambazo biashara ya samaki wa mapambo ni kubwa kama vile Sri Lanka na Malaysia (Banister, 1989). Kwa upande wa Tanzania tathmini ya athari za biashara ya mapambo bado haijafanyika.
ii) Kuharibika kwa mfumo mzima wa ikolojia na kuharibu makazi ya samaki asilia (indigenous species). Hali hii hutokana na samaki wa mapambo kupelekwa kwenye maeneo ambayo sio ya asili yao kama vile mabwawa. Wakati mwingine samaki hawa huingia kwenye mito iliyo karibu na mabwawa wanayofugiwa na kwenda kwenye maziwa ambako
huchanganyika na samaki ambao ni wa asili kwenye maeneo hayo. Pia, biashara hii inaweza kuhatarisha ikolojia ya maji ya nchi waliyopelekwa.
CHANGAMOTO
i) Kuimarisha na kuendeleza miundombinu kwenye maeneo yenye vivutio kwa ajili ya utalii ikolojia ikiwa ni pamoja na barabara, umeme na maji safi;
ii) Upatikanaji wa mitaji na uwekezaji katika utalii ikolojia na biashara ya samaki wa mapambo;
iii) Kuweka bayana umiliki wa fukwe za bahari ambazo ziko nje ya Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu ili kuharakisha uwekezaji wa maeneo haya kwa nia ya kukuza utalii ikolojia;
iv) Kufanya utafiti wa kufahamu ikolojia, aina, wingi wa samaki wa mapambo n.k.;
v) Kuboresha mazingira ya utalii ikolojia na biashara ya samaki wa mapambo.
MAPENDEKEZO YANGU
i) Kufanya utafiti wa kufahamu wingi wa spishi mbalimbali za samaki wa mapambo ili uvunaji uwe endelevu;
ii) Kuhamasisha wananchi na wadau wengine kuwekeza katika biashara ya samaki wa mapambo na utalii ikolojia;
iii) Kuhamasisha wananchi kutembelea Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu ili kukuza utalii wa ndani; na
iv) Kufanya jitihada za kuhifadhi spishi za viumbe wa kwenye maji zilizo hatarini kutoweka.
HALI YA BIASHARA YA SAMAKI WA MAPAMBO
Samaki wengi wa mapambo kwenye maji baridi ni jamii ya Cichlids. Ziwa
Tanganyika lina spishi zaidi ya 200 lakini wanaosafirishwa nje ya nchi kwa ajili ya mapambo ni wastani wa spishi 30 Ziwa Nyasa lina spishi zaidi ya 750 lakini wanaosafirishwa nje ya nchi kama samaki wa mapambo ni takriban spishi 5 ambazo ni Aulo mamelela, A. blue neon, A. hongi, Proto steven na Tropheus ndole. Ziwa Victoria lilikuwa na spishi zaidi ya 300 katika miaka ya 1970 kabla samaki aina ya Sangara aliyepandikizwa hajasambaa na kula jamii ya Cichlid. Hivi sasa baadhi ya spishi zimetoweka na biashara ya samaki wa mapambo haipo Ziwa Victoria.
CICHLIDS TOKA ZIWA TANGANYIKA

Kwa upande wa samaki wa maji chumvi wanaoishi kwenye matumbawe (coral fish species), spishi zilizopo Tanzania ni nyingi lakini idadi kamili haijulikani. Hata hivyo, kati ya spishi takriban 4,000 zilizopo duniani ni spishi 200 – 300 ndio wanaotumika kwa mapambo.
Samaki aina ya “Cichilid” hutumika sana kwa mapambo duniani kote kwa kuwa wana uwezo wa kuzoea mazingira mapya kwa haraka kuliko samaki wengine (Koning, 1995). Hii inatokana na tabia yao ya kuwa na uwezo mkubwa wa kuvumilia hali tofauti ya mazingira ya maji ikiwemo pH na uchumvi chumvi (salinity). Pia, wana tabia ya kula aina mbalimbali za vyakula kutokana na mpangilio wa midomo, meno na taya (Pharyngeal jaws). Kuna wanaokula mwani (algae), mimea (plants), samaki, konokono n.k. Pia, aina hizi za samaki wanaweza kuishi na kusafirishwa kwa muda wa siku tano (5) bila kula alimradi mazingira ya maji yanaruhusu na vifo vinaweza kuwa chini ya asilimia 2 tu wakati wa kuwasafirisha.

Takwimu za biashara ya samaki wa mapambo duniani sio sahihi sehemu nyingi. Hata hivyo takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa Uingereza mwaka 1987 waliuza samaki wa kiasi cha Paundi za Uingereza milioni 17 na Marekani waliuza samaki wa thamani ya Dola za Kimarekani milioni 739 mwaka 1988. Hata hivyo taarifa zilizopo zinaonyesha kuwa tabia ya kupenda (hobby) kufuga samaki wa mapambo inaongezeka kwenye nchi mbalimbali zikijumuisha, Japan, China, Australia, Afrika ya Kusini, Korea, Ujerumani na Malaysia. Mara nyingi ufugaji hufanyika kwenye mabwawa na matanki (aquarium).
Kwa upande wa Tanzania, takwimu za biashara ya samaki wa mapambo kutoka kwenye maji baridi kuanzia mwaka 2006 mpaka mwaka 2009 ni kama ifuatavyo: Kwa ujumla biashara ya samaki hawa huingizia Serikali pesa kidogo sana. Samaki wengi waliosafirishwa nje ya nchi katika mwaka 2006 walitoka Ziwa Nyasa. Jumla ya samaki 12,661 ambao walikuwa na thamani ya shilingi 100 87,143,451.25 waliingizia Serikali ushuru wa shilingi 6,541,825.56 tu. Jumla ya samaki 9,080 kutoka Ziwa Tanganyika waliokuwa na thamani ya shilingi 58,770,742.7 waliingizia Serikali kiasi cha shilingi 4,292,456.39. Mwaka
2009 samaki wengi walitoka Ziwa Tanganyika jumla ya samaki 23,500 wenye thamani ya shilingi 131, 356,148.5 waliingizia Serikali jumla ya shilingi 13,018,338.19 kama ushuru. Samaki kutoka Ziwa Victoria walisafirishwa wachache tu mwaka 2007, walikuwa 12 tu. Samaki wa mapambo kutoka Ziwa Victoria wako hatarini kutoweka kutokana na kuliwa na Sangara kwa hiyo wameingizwa kwenye “Red list” chini ya CITES,
hawasafirishwi tena. Kinachohimizwa ni ufugaji wa hao samaki.

FURSA YA UWEKEZAJI KATIKA SAMAKI WA MAPAMBO
i) Kuna fursa kubwa ya uwekezaji katika samaki wa mapambo wa Ziwa Tanganyika kwa kuwa samaki hao wapo wengi (Watson, 2000) na baharini kwenye matumbawe (Coral reef fish species)
ii) Kuwepo kwa masoko ya uhakika na mazingira mazuri ya kuvutia biashara Ili uendeleza na kuimarisha uwekezaji katika eneo hili ni muhimu kuhamasisha wananchi na wawekezaji kutoka nje katika kuwekeza kwenye biashara ya samaki wa mapambo. Pia, ni lazima kufanya utafiti wa kufahamu spishi zilizopo na wingi wa samaki wa mapambo ili kuepuka kumaliza baadhi ya samaki hao.
UMUHIMU WA BIASHARA YA SAMAKI WA MAPAMBO KATIKA KUONDOA UMASIKINI
Takwimu zilizopo zinaonyesha kuwa mapato ya biashara ya samaki wa mapambo kwenye nchi mbalimbali duniani ina thamani ya takriban Dola za Marekani milioni 186 na samaki wengi wanatoka nchi zinazoendelea (Watson, 2000). Kati ya hizi fedha Zinazobaki kwa jamii wanaokusanya samaki hao ni kidogo sana. Hata hivyo, kama jamii itawezeshwa kupata mtaji na teknolojia sahihi itaweza kujiongezea kipato na kupunguza umaskini. Asilimia 90 ya samaki wa mapambo duniani huzalishwa kwenye mabwawa hasa kwenye nchi zilizoendelea na samaki hao wametolewa kutoka kwenye nchi zinazoendelea ikiwemo Tanzania. Ili mwananchi aweze kunufaika na biashara ya samaki wa mapambo kuna umuhimu wa kuwaelimishwa kuhusu njia bora za kuwavua, kuwahifadhi na kuwasafirisha kwa ajili ya kuongeza kipato chao na taifa kwa ujumla.
SAMAKI WA UREMBO TOKA ZIWA NYASA

ATHARI ZITOKANAZO NA BIASHARA YA SAMAKI WA MAPAMBO
Shirika la Kimataifa la Hifadhi ya Viumbe na Mazingira kupitia kitabu cha “Red List’’ (IUCN, 1988) kimeainisha aina za samaki wa mapambo ambao wapo hatarini Kutoweka. Samaki hao ni pamoja na aina ya furu (Haplochromine). Athari za biashara hiyo ni kama ifuatavyo:
i) Kupungua wingi na makazi ya samaki waliopo kwenye maeneo ya asili ikiwa ni pamoja na maziwa, mito na bahari kwa njia mbalimbali. Hali ya aina hii imekwishatokea kwenye nchi ambazo biashara ya samaki wa mapambo ni kubwa kama vile Sri Lanka na Malaysia (Banister, 1989). Kwa upande wa Tanzania tathmini ya athari za biashara ya mapambo bado haijafanyika.
ii) Kuharibika kwa mfumo mzima wa ikolojia na kuharibu makazi ya samaki asilia (indigenous species). Hali hii hutokana na samaki wa mapambo kupelekwa kwenye maeneo ambayo sio ya asili yao kama vile mabwawa. Wakati mwingine samaki hawa huingia kwenye mito iliyo karibu na mabwawa wanayofugiwa na kwenda kwenye maziwa ambako
huchanganyika na samaki ambao ni wa asili kwenye maeneo hayo. Pia, biashara hii inaweza kuhatarisha ikolojia ya maji ya nchi waliyopelekwa.
CHANGAMOTO
i) Kuimarisha na kuendeleza miundombinu kwenye maeneo yenye vivutio kwa ajili ya utalii ikolojia ikiwa ni pamoja na barabara, umeme na maji safi;
ii) Upatikanaji wa mitaji na uwekezaji katika utalii ikolojia na biashara ya samaki wa mapambo;
iii) Kuweka bayana umiliki wa fukwe za bahari ambazo ziko nje ya Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu ili kuharakisha uwekezaji wa maeneo haya kwa nia ya kukuza utalii ikolojia;
iv) Kufanya utafiti wa kufahamu ikolojia, aina, wingi wa samaki wa mapambo n.k.;
v) Kuboresha mazingira ya utalii ikolojia na biashara ya samaki wa mapambo.
MAPENDEKEZO YANGU
i) Kufanya utafiti wa kufahamu wingi wa spishi mbalimbali za samaki wa mapambo ili uvunaji uwe endelevu;
ii) Kuhamasisha wananchi na wadau wengine kuwekeza katika biashara ya samaki wa mapambo na utalii ikolojia;
iii) Kuhamasisha wananchi kutembelea Hifadhi za Bahari na Maeneo Tengefu ili kukuza utalii wa ndani; na
iv) Kufanya jitihada za kuhifadhi spishi za viumbe wa kwenye maji zilizo hatarini kutoweka.
Wednesday, November 23, 2011
MAGONJWA MAKUU YA NDEGE
Magonjwa huainishwa kulingana na baiolojia yao,kama Virusi,Bakteria,Kupe,ukungu,na chanzo chao,kwa mfano magonjwa ya lishe yaliyoangaliwa hapo juu.Hata hivyo,magonjwa makuu katika ndege yamegawanywa katika makundi matatu kulingana na makali yao na umuhimu katika mfumo wa uzalishhaji mdogo katika vijiji.Vitu muhimu kama tabia zao wakati wa mlipuko(dalili),na matibabu yanayowezekana(kuzuia ama kudhibiti)vile vile wakati wa kutokea magonjwa hayo.Umuhimu wa ugonjwa huthaminiwa na idadi ya vifo na athari kwa uzalishaji,na itatofautiana kutoka eneo hadi eneo na msimu hadi msimu.
MCHANGANYIKO WA MAGONJWA
Magonjwa kadhaa yasiyo maku yanaweza kukutana na magonjwa mengine na kusababisha madhara makali kwa ndege.Hii ndio hali kwa mfano maambukizo ya E.coli, utapiamlo na kupe wa ndani.Magonjwa kama haya ni vigumu kuua ndege lakini huwa na madhara makubwa kwa kinga ya ndege dhidi ya magonjwa,na kujenga msingi wa maambukizo rahisi ya magonjwa mengine baada ya kuwafanya ndege kuwa dhaifu kiafya.
Umuhimu mkubwa huashiria ugonjwa wa kawaida wenye vifo vingi(zaidi ya asilimia 30 ya kundi),husambaa kwa urahisi na ni vigumu kutibu au hautibiki kabisa.Umuhimu wa wastaani kawaida ,vifo vya wastani(10-30%) kwa kundi na /ama vigumu kutibu.Ugonjwa usio mkuu huashiria wa kawaida, vifo vichache na /ama rahisi kutibu.
UGONJWA WA KUAMBUKIZANA WA KUKU UNAOSHAMBULIA MAPAFU NA MFUMO WA NEVA - NEWCASTLE DISEASE (NCD)
Ugonjwa huu huua, ni wa kawaida katika msimu wa mvua,na hutokea mara kwa mara katika vifaranga wachanga,lakini pia katika kuku waliokomaa.Vifo vya juu katika kundi,mara kwa mara baina ya aslimia 30 na asilimia 80 ya ndege hufa,ugonjwa unapowakumbaKuku hupoteza hamu ya kula na usagaji mbaya wa chakula tumboni.Unaweza kuonyesha upumuaji mzito,kinyesi cha kijani na wakati mwingine kuhara damu. Unaweza kuonyesha dalili za kuchanganyikiwa,kiharusi na hufa ghafla.Dalili zinaweza kutokea zote wakati mmoja.Ugonjwa huu ni wa virusi (virus)kwa hivyo hauna tiba,lakini unaweza kuzuiwa kwa kuwachanja ndege wote ukijumuisha vifaranga wa kutoka wiki mbili.
HOMA YA NDEGE - AVIAN INFLUENZA(AI)
Ugonjwa huu hubebwa na bata na bata maji,na unaweza kusambaa kwa urahisi na ni hatari sana kwa kuku.Vifo vya juu katika kundi,ndevu na panga za jogoo huvimba na kuwa na rangi ya kibuluu (samawati).Husambaa kupitia chakula na maji yaliyochafuliwa katika madimbwi na vyombo vya maji/chakula.Ugonjwa huu husababishwa na virusi (virus),kwa hivyo hauna tiba.
Ili kujikinga na ugonjwa huu zingatia usafi kwenye banda lako na vyombo vya kuku, ukiona dalili za ugonjwa huu waondoe kuku wagonjwa, wachinjwe na kuchomwa moto. Kabla ya kuingiza kundi lingine la kuku kwenye banda lenye ugonjwa hakikisha unapulizia dawa za kuua virusi ka a VIRU KILL. Mara uonapo dalili za ugonjwa huu muite afisa ugani wa mifugo (Veterinarian)
NDUI YA KUKU - FOWL POX
Huonekana mara kwa mara katika vifaranga wadogo,lakini pia kwenye kuku waliokomaa na huonekana uvimbe mdogo mdogo kwenye ndevu,panga na uso wa kuku.joto la kuku hupanda,uchovu unaoambatana na vifo vya ghafla.Ugonjwa huu ni wa kawaida wakati wa msimu wa kiangazi,lakini pia unaweza kutokea mwaka mzima.Ugonjwa huu ni virusi kwa hivyo hauna tiba.Chanjo inapatikana kwenye maduka ya pembejeo za kilimo.
UGONJWA WA MAREK - MAREK DISEASE
Huonekana tu katika ndege walio na zaidi ya wiki 16 kwa hiyo hauwapati kuku wa nyama labda kama umewafuga kwa ajili ya uzalishaji (parent stock).Mwanzoni ndege wanaweza kuonyesha bawa moja kushuka au yote mawili.Ama mguu mmoja ama yote inaweza kupooza.Ugonjwa huu ni virusi,kwa hivyo hauna tiba,lakini Chanjo inapatikana kwenye maduka ya pembejeo za kilimo
MAAMBUKIZO YA BAKTERIA WA E.coli
Hutokea sana sana katika vifaranga walioanguliwa (Day old chicks),na husababisha maambukizo katika tumbo.Dalili katika ndege wakubwa:kupumua kwa tabu au maambukizo katika mayai na kupungua au kuacha kabisa kwa utagaji kwa kuku wa mayai, kinga bora ni usafi katika mayai kwa ajili ya .Tiba kwa vifaranga wagonjwa inawezekana ukiwa na kiua vijisumu (antibiotics) kama OTC 10%, 20%, 30%.
KIPINDUPINDU CHA KUKU - pasteurellosis
Unaweza kutokea wakati wowote na kwa rika zote.Dalili ni kuharisha sana kwa kuku,kupumua kwa tabu,kukosa hamu ya kula,ndevu na panga za jogoo huwa na rangi ya kibuluu(samawati).Unaweza kutokea kama ugonjwa sugu na kuku kufariki ghafla .Mambukizo kupitia chakula na maji yaliyochafuliwa.Hauna tiba.kinga ni usafi wa hali ya juu na chanjo.Ua na uchome moto kuku wote walioathirika.Chanjo inapatikana kwenye maduka ya pembejeo za kilimo.
UGONJWA WA KUHARA VIFARANGA
Ugonjwa huu unasababishwa na bacteria aina ya salmonella pullorum(Bacillary white bacteria)
Hutokea sana sana katika vifaranga wadogo.Vifaranga hutembea kwa tabu sana,tumbo huvimba na hukokota mbawa zao.Kinyesi chao huwa maji maji na hugeuka cheupe.Hauna tiba.Kuzuia ni kutilia usafi maanani.Ikiwa ugonjwa utatokea,tenga ama ua na uchome ndege.Ugonjwa huu husambazwa kwa kifaranga kutoka kwa mayai ya kuku aliyeathirika,ambaye haonyeshi daalili zozote za kuwa mgonjwa.
HOMA YA MATUMBO YA KUKU - TYPHOID
Huonekana zaidi kwenye kuku wakubwa.Dalili:joto huwa kali,uchovu,panga na ndevu za kuku huwa za kibuluu (samawati).Hauna tiba.Kinga ni kutilia usafi maanani na kuua kuku wagonjwa.Usinunue vifaranga kutoka kwenye vyanzo ambavyo hauvijui,na usitumie mayai kwa ajili ya kuanguliwa kutoka kwenye kuku wagonjwa.
GUMBORO - Infectious Bursal Disease(IBD)
Huonekana tu katika vifaranga walio chini ya wiki 6,na ni wa kawaida katika makundi makubwa ambayo yamefugwa katika sehemu zilizofungwa (indoor).Sio wa kawaida katika mfumo mdogo wa ufugaji vijijini.Dalili za kawaida: kuharisha.Ugonjwa huu ni virusi ,kwa hivyo hauna tiba.Chanjo inapatikana kwenye maduka ya pembejeo za kilimo.
UGONJWA WA KUPUMUA
Dalili:Pua inayotoka makamasi,uvimbe chini ya macho,macho yaliyojifunga,upungufu katika utagaji wa mayai.Tiba ni kuongeza kiua vijisumu (antibotics) katika maji ya kunywa.
UGONJWA SUGU WA KUPUMUA - Mycoplsmosis
Dalili:Pua inayotoka makamasi ama iliyoziba,uso uliovimba,macho yaliyojifunga,upungufu katika utagaji wa mayai,vifo visivyo vya kawaida.Tiba ni kuongeza kiua vijasumu (antibotics)katika maji ya kunywa.
COCCIDIOSIS
Ugonjwa huu unaweza kutokea wakati wowote na katika rika zote,lakini unaweza kuzuiwa kwa kusafisha kwa makini nyumba za ndege.Dalili:hali dhoofu ya kuku,kuchoka,kutembea kichwa chini ,manyoya yaliyotimka,kuhara damu.Vifo katika vifaranga wachanga.Ikiwa vifaranga wataendelea kuishi watabakia kuwa wembamba na watachelewa kutaga.Tiba:Weka dawa ya Coccidiostatics katika maji ya kunywa au chakula.Kuzuia:Usiweke ndege wengi pamoja.Epuka kuweka ndege wa rika mbalimbali katika nyumba moja kwani ugonjwa unaweza kusambaa kutoka kwenye kuku wakubwa hadi kwa vifaranga.
MINYOO
Minyoo ni vimelea vya ndani na ni vya kawaida katika umri wote katika mfumo wa uzalishaji vijijini na mjini.Vimelea hivi husababisha afya mbovu,kupoteza uzito,kupungua kwa uzalishaji wa mayai.Tiba bora ni kuongeza dawa ya minyoo kama piperazine katika maji ya kunywa mara moja ama mbili kwa mwaka,ikiwezekana wiki mbili kabla ya chanjo yoyote.
CHAWA, KUPE, VIROBOTO NA UTITIRI
Huvamia rika zote wakati wowote,lakini hutokea mara kwa mara katika nyumba za kuku zenye unyevunyevu na uchafu.Ndege waliokomaa husumbuliwa na hutumia wakati mwingi wakidonoa na kujikuna.Vifaranga wachanga wanaweza kufa kwa sababu ya upungufu wa damu (anaemia).Kama hautatibiwa utitiri,chawa,viroboto,kupe watasababisha kuku kupungua uzito na pia kuna uwezekano wa kupoteza manyoya kwa sababu ya kunyonywa damu na vimelea na kuwashwa na ngozi.Chawa wanaweza kuonekana karibu na macho na pua.Viroboto vinaweza kuonekana kwenye tumbo.Tiba:Nyunyiza dawa ya kuua vimelea kama Akheri powder,jivu na mafuta.Jivu na poda ya salfa inaweza kutumiwa mahali ambapo kuku huoga na mchanga.Viota vinaweza kulindwa kwa kuwekewa majani kadhaa ya tumbaku yaliyochanganywa na jivu katika viota.
MAGAMBA KWENYE MIGUU
Miguu yenye magamba husababishwa na vimelea vya nje vinavyowasha ngozi kwenye miguu ya ndege.Dalili:Miguu ina magamba yanayoonekana na majeraha na anaweza kulemazwa katika kutembea.Tiba:Weka miguu kila siku kwenye mafuta taa,ama katika dawa kuogeshea mifugo hadi magamba yatoweke.
LISHE DUNI
Ndege wanaoathirika zaidi ni wale wanaofugwa ndani kuliko wale wanaojtafutia chakulaDalili:mifupa kukua vibaya na kunyonyoka manyoya.Ndege hutembea kwa tabu;huchopea .Tiba,ukigundua mapema wape ndege wako vitamini na kalsiam ya ziada kwenye chakula, pia wape majani, mabaki ya mboga za majani au kinyesi cha ng'ombe
MCHANGANYIKO WA MAGONJWA
Magonjwa kadhaa yasiyo maku yanaweza kukutana na magonjwa mengine na kusababisha madhara makali kwa ndege.Hii ndio hali kwa mfano maambukizo ya E.coli, utapiamlo na kupe wa ndani.Magonjwa kama haya ni vigumu kuua ndege lakini huwa na madhara makubwa kwa kinga ya ndege dhidi ya magonjwa,na kujenga msingi wa maambukizo rahisi ya magonjwa mengine baada ya kuwafanya ndege kuwa dhaifu kiafya.
Umuhimu mkubwa huashiria ugonjwa wa kawaida wenye vifo vingi(zaidi ya asilimia 30 ya kundi),husambaa kwa urahisi na ni vigumu kutibu au hautibiki kabisa.Umuhimu wa wastaani kawaida ,vifo vya wastani(10-30%) kwa kundi na /ama vigumu kutibu.Ugonjwa usio mkuu huashiria wa kawaida, vifo vichache na /ama rahisi kutibu.
UGONJWA WA KUAMBUKIZANA WA KUKU UNAOSHAMBULIA MAPAFU NA MFUMO WA NEVA - NEWCASTLE DISEASE (NCD)
Ugonjwa huu huua, ni wa kawaida katika msimu wa mvua,na hutokea mara kwa mara katika vifaranga wachanga,lakini pia katika kuku waliokomaa.Vifo vya juu katika kundi,mara kwa mara baina ya aslimia 30 na asilimia 80 ya ndege hufa,ugonjwa unapowakumbaKuku hupoteza hamu ya kula na usagaji mbaya wa chakula tumboni.Unaweza kuonyesha upumuaji mzito,kinyesi cha kijani na wakati mwingine kuhara damu. Unaweza kuonyesha dalili za kuchanganyikiwa,kiharusi na hufa ghafla.Dalili zinaweza kutokea zote wakati mmoja.Ugonjwa huu ni wa virusi (virus)kwa hivyo hauna tiba,lakini unaweza kuzuiwa kwa kuwachanja ndege wote ukijumuisha vifaranga wa kutoka wiki mbili.
HOMA YA NDEGE - AVIAN INFLUENZA(AI)
Ugonjwa huu hubebwa na bata na bata maji,na unaweza kusambaa kwa urahisi na ni hatari sana kwa kuku.Vifo vya juu katika kundi,ndevu na panga za jogoo huvimba na kuwa na rangi ya kibuluu (samawati).Husambaa kupitia chakula na maji yaliyochafuliwa katika madimbwi na vyombo vya maji/chakula.Ugonjwa huu husababishwa na virusi (virus),kwa hivyo hauna tiba.
Ili kujikinga na ugonjwa huu zingatia usafi kwenye banda lako na vyombo vya kuku, ukiona dalili za ugonjwa huu waondoe kuku wagonjwa, wachinjwe na kuchomwa moto. Kabla ya kuingiza kundi lingine la kuku kwenye banda lenye ugonjwa hakikisha unapulizia dawa za kuua virusi ka a VIRU KILL. Mara uonapo dalili za ugonjwa huu muite afisa ugani wa mifugo (Veterinarian)
NDUI YA KUKU - FOWL POX
Huonekana mara kwa mara katika vifaranga wadogo,lakini pia kwenye kuku waliokomaa na huonekana uvimbe mdogo mdogo kwenye ndevu,panga na uso wa kuku.joto la kuku hupanda,uchovu unaoambatana na vifo vya ghafla.Ugonjwa huu ni wa kawaida wakati wa msimu wa kiangazi,lakini pia unaweza kutokea mwaka mzima.Ugonjwa huu ni virusi kwa hivyo hauna tiba.Chanjo inapatikana kwenye maduka ya pembejeo za kilimo.
UGONJWA WA MAREK - MAREK DISEASE
Huonekana tu katika ndege walio na zaidi ya wiki 16 kwa hiyo hauwapati kuku wa nyama labda kama umewafuga kwa ajili ya uzalishaji (parent stock).Mwanzoni ndege wanaweza kuonyesha bawa moja kushuka au yote mawili.Ama mguu mmoja ama yote inaweza kupooza.Ugonjwa huu ni virusi,kwa hivyo hauna tiba,lakini Chanjo inapatikana kwenye maduka ya pembejeo za kilimo
MAAMBUKIZO YA BAKTERIA WA E.coli
Hutokea sana sana katika vifaranga walioanguliwa (Day old chicks),na husababisha maambukizo katika tumbo.Dalili katika ndege wakubwa:kupumua kwa tabu au maambukizo katika mayai na kupungua au kuacha kabisa kwa utagaji kwa kuku wa mayai, kinga bora ni usafi katika mayai kwa ajili ya .Tiba kwa vifaranga wagonjwa inawezekana ukiwa na kiua vijisumu (antibiotics) kama OTC 10%, 20%, 30%.
KIPINDUPINDU CHA KUKU - pasteurellosis
Unaweza kutokea wakati wowote na kwa rika zote.Dalili ni kuharisha sana kwa kuku,kupumua kwa tabu,kukosa hamu ya kula,ndevu na panga za jogoo huwa na rangi ya kibuluu(samawati).Unaweza kutokea kama ugonjwa sugu na kuku kufariki ghafla .Mambukizo kupitia chakula na maji yaliyochafuliwa.Hauna tiba.kinga ni usafi wa hali ya juu na chanjo.Ua na uchome moto kuku wote walioathirika.Chanjo inapatikana kwenye maduka ya pembejeo za kilimo.
UGONJWA WA KUHARA VIFARANGA
Ugonjwa huu unasababishwa na bacteria aina ya salmonella pullorum(Bacillary white bacteria)
Hutokea sana sana katika vifaranga wadogo.Vifaranga hutembea kwa tabu sana,tumbo huvimba na hukokota mbawa zao.Kinyesi chao huwa maji maji na hugeuka cheupe.Hauna tiba.Kuzuia ni kutilia usafi maanani.Ikiwa ugonjwa utatokea,tenga ama ua na uchome ndege.Ugonjwa huu husambazwa kwa kifaranga kutoka kwa mayai ya kuku aliyeathirika,ambaye haonyeshi daalili zozote za kuwa mgonjwa.
HOMA YA MATUMBO YA KUKU - TYPHOID
Huonekana zaidi kwenye kuku wakubwa.Dalili:joto huwa kali,uchovu,panga na ndevu za kuku huwa za kibuluu (samawati).Hauna tiba.Kinga ni kutilia usafi maanani na kuua kuku wagonjwa.Usinunue vifaranga kutoka kwenye vyanzo ambavyo hauvijui,na usitumie mayai kwa ajili ya kuanguliwa kutoka kwenye kuku wagonjwa.
GUMBORO - Infectious Bursal Disease(IBD)
Huonekana tu katika vifaranga walio chini ya wiki 6,na ni wa kawaida katika makundi makubwa ambayo yamefugwa katika sehemu zilizofungwa (indoor).Sio wa kawaida katika mfumo mdogo wa ufugaji vijijini.Dalili za kawaida: kuharisha.Ugonjwa huu ni virusi ,kwa hivyo hauna tiba.Chanjo inapatikana kwenye maduka ya pembejeo za kilimo.
UGONJWA WA KUPUMUA
Dalili:Pua inayotoka makamasi,uvimbe chini ya macho,macho yaliyojifunga,upungufu katika utagaji wa mayai.Tiba ni kuongeza kiua vijisumu (antibotics) katika maji ya kunywa.
UGONJWA SUGU WA KUPUMUA - Mycoplsmosis
Dalili:Pua inayotoka makamasi ama iliyoziba,uso uliovimba,macho yaliyojifunga,upungufu katika utagaji wa mayai,vifo visivyo vya kawaida.Tiba ni kuongeza kiua vijasumu (antibotics)katika maji ya kunywa.
COCCIDIOSIS
Ugonjwa huu unaweza kutokea wakati wowote na katika rika zote,lakini unaweza kuzuiwa kwa kusafisha kwa makini nyumba za ndege.Dalili:hali dhoofu ya kuku,kuchoka,kutembea kichwa chini ,manyoya yaliyotimka,kuhara damu.Vifo katika vifaranga wachanga.Ikiwa vifaranga wataendelea kuishi watabakia kuwa wembamba na watachelewa kutaga.Tiba:Weka dawa ya Coccidiostatics katika maji ya kunywa au chakula.Kuzuia:Usiweke ndege wengi pamoja.Epuka kuweka ndege wa rika mbalimbali katika nyumba moja kwani ugonjwa unaweza kusambaa kutoka kwenye kuku wakubwa hadi kwa vifaranga.
MINYOO
Minyoo ni vimelea vya ndani na ni vya kawaida katika umri wote katika mfumo wa uzalishaji vijijini na mjini.Vimelea hivi husababisha afya mbovu,kupoteza uzito,kupungua kwa uzalishaji wa mayai.Tiba bora ni kuongeza dawa ya minyoo kama piperazine katika maji ya kunywa mara moja ama mbili kwa mwaka,ikiwezekana wiki mbili kabla ya chanjo yoyote.
CHAWA, KUPE, VIROBOTO NA UTITIRI
Huvamia rika zote wakati wowote,lakini hutokea mara kwa mara katika nyumba za kuku zenye unyevunyevu na uchafu.Ndege waliokomaa husumbuliwa na hutumia wakati mwingi wakidonoa na kujikuna.Vifaranga wachanga wanaweza kufa kwa sababu ya upungufu wa damu (anaemia).Kama hautatibiwa utitiri,chawa,viroboto,kupe watasababisha kuku kupungua uzito na pia kuna uwezekano wa kupoteza manyoya kwa sababu ya kunyonywa damu na vimelea na kuwashwa na ngozi.Chawa wanaweza kuonekana karibu na macho na pua.Viroboto vinaweza kuonekana kwenye tumbo.Tiba:Nyunyiza dawa ya kuua vimelea kama Akheri powder,jivu na mafuta.Jivu na poda ya salfa inaweza kutumiwa mahali ambapo kuku huoga na mchanga.Viota vinaweza kulindwa kwa kuwekewa majani kadhaa ya tumbaku yaliyochanganywa na jivu katika viota.
MAGAMBA KWENYE MIGUU
Miguu yenye magamba husababishwa na vimelea vya nje vinavyowasha ngozi kwenye miguu ya ndege.Dalili:Miguu ina magamba yanayoonekana na majeraha na anaweza kulemazwa katika kutembea.Tiba:Weka miguu kila siku kwenye mafuta taa,ama katika dawa kuogeshea mifugo hadi magamba yatoweke.
LISHE DUNI
Ndege wanaoathirika zaidi ni wale wanaofugwa ndani kuliko wale wanaojtafutia chakulaDalili:mifupa kukua vibaya na kunyonyoka manyoya.Ndege hutembea kwa tabu;huchopea .Tiba,ukigundua mapema wape ndege wako vitamini na kalsiam ya ziada kwenye chakula, pia wape majani, mabaki ya mboga za majani au kinyesi cha ng'ombe
Thursday, November 10, 2011
KILIMO BORA CHA MINAZI

UPANDAJI
Uko wa ina mbili kuna wa vibox na wa pembetatu lakini kwa aina zote mbili umbali wa kupanda ni mita 7.6 kutoka shimo hadi shimo la mnazi, kiasi cha mashimo 175 kwa hecta huingia na kama utatumia mtindo wa pembetatu basi mashimo 13 zaidi yataingia kwa hecta.

Ukubwa wa shimo uwe futi tatu kwa kina, upana na urefu hi kwa maeneo yenye udongo mzuri na wakaida lakini maeneo yenye changarawe, mawe mawe na miamba ukubwa uongezeke hadi futi4 kwa mapana , urefu na kina, Shimo lijazwe majani kiasi cha kilo 15 – 20 unaweza kukisia kama theluthi moja ya shimo au futi moja baada ya kushindilia majani, weka juu yake kama, weka udongo wa juu (top soil) kiasi cha futi moja tena ongezea kiasi cha kilo 10 – 20 cha mbolea ya samadi.

Hakikisha haijai na kufunika shimo lote, pia kama utapata ule udongo mwekundu ambao wengi hupenda kuutumia kwenye bustani zao, pia weka humu kiasi kama utaukosa basi acha vivo hivyo, anza kumwagilia maji wiki moja kabla ya kupanda mbegu yako, kama shimo litatitia ongezea udongo wenye rutuba ya kutosha, kumbuka kuacha kisahani kwa ajili ya kukusanyia maji, ila kama ni sehemu ambazo hufurika kipindi cha mvua jaza udongo hadi kuweka tuta ili maji yasituame.
UPANDAJI
Ni vizuri kutumia mbegu ya nazi moja kwa moja kuliko kutumia miche, hii ni kwa sababu mbili kubwa, kwanza ukinunua mche unakuwa hujui imetoka mnazi gani, wenye ubora gani na hata uzaaji wake huujui, lakini inashauriwa kununua nazi kutoka kwenye mnazi moja kwa moja kwa kuchagua mnazi bora na unaozaa nazi nyingi na kubwa, chagua nazi kubwa zaidi kutoka katika kila mnzi bora.

Nazi ambayo haijafuliwa inakuwa na pembe tatu, moja ya pembe hizi huwa kubwa zaidi na mbili zilizobaki hufanan ukubwa, ule upande mkubwa ulazwe chini wakati wa kupandwa, na upande ule wenye kikonyo ambako nazi hujishika katika matawi ya mnazi (mahanda) ndipo ambapo huota, utatakiwa upatate au upapunguze kwa kisu ili kurahisisha kuota, wakati wa kupanda hakikisha nazi ina maji, ikiwa na maji kidogo sana usiipande, panda miezi miwili au mitatu kabla ya mvua kuanza, nazi inauwezo wa kuota yenyewe bila mvua kwa sababu ina maji ndani yake, ila baada ya kuanza kuota kama hakuna mvua ni muhimu kumwagilia ama sivyo mbegu yako itakufa.
Pia ni muhimu kutumia dawa za kuua mchwa au oil chafu wakati wa kupanda, pia kunadaadhi ya mimea ambayo mizizi yake hufukuza mchwa inaweza kupandwa pamoja na nazi yako. Kama utaamua kutumia miche basi hakikisha miche yako haipungui umri wa miezi sita tangu mbegu kupandwa ili kuzuia miche mingi kufa.
MAGONJWA YA MINAZI
- KUOZA VIKONYO
Huanza kwa majani machanga mawili ya mwanzo kubadilika rangi na kuwa njano na baadae huwa na vidoti vyeusi hutokea kwenye ukingo, majani hunyauka na kukauka na kisha sehemu ya chini linapoanzia jani huoza na kutoa harufu mbaya ambapo baadae mnazi wote hufa.

Ili kuzuia ugonjwa huu mara tu unapoona dalili za mwanzo tengeneza mchanganyiko ufuatao (gramu 100 za copper sulphate changanya na nusu lita ya maji) + (Gramu 100 za chokaa changanya na nusu lita ya maji) kila moja itengenezwe peke yake halafu kisha vichanganywe pamoja baadae kisha pulizia kwenye minazi iliyoanza kushambuliwa, kama mnazi umeshambuliwa sana ukatwe na kuchomwa moto kuzuia maambukizi zaidi. Pia pulizia mchanganyiko huu msimu wa baridi kuanzi mwezi wa 5 hadi wa 9 kwenye shamba lako kama kinga.
- KUOZA MAJANI
Majani huwa meusi kwenye ukingo na kuti likiliwa zaidi kati kati, majani machanga yakichomoza huwa dhaifu na kisha huchanguka, mnazi haufi ila mazao huwa duni kama ni mnazi unaozaa

ili kuzuia tumia dawa yoyote ya kuzuia fangasi za mimea kama Hexaconazol, Mancozeb au Dithane - M5, muhimu ukufika duka la pembejeo ulizia dawa ya kuua fangasi wa mimea utapata dawa na maelekezo ya kuchanganya usikariri haya majina ya dawa nilizotaja
Monday, November 7, 2011
MPWAPWA BREED - Mbegu bora ya ng'ombe iliyosahaulika
ASILI
Mbegu hii inatokana na mchanganyiko wa mbegu ya ng’ombe jike aina ya Zebu toka Tanzania na Red madume ya Sindhi na Sahiwal wenye asili ya india na Pakistan lakini waliotolewa nchini Kenya hii ilikuwa ni mwaka 1940 ambapo uzalishaji wa mbegu hii ulifanyika kwa mara ya kwanza katika kituo cha utafiti wa mifugo Mpwapwa Dodoma nchini Tanzania
Mwaka 1958 uboreshaji wa mbegu hii ulifanyika kwa kuongezea damu za ng’ombe wa ulaya (Bos Taurus) aina ya Ayshire na Jersey na mpaka kufikia mwaka 1960 mbegu ya Mpwapwa ikawa na na uwiano wa 20% Tanganyika Zebu 10% Boran 5% Ankole 55% Red Sindhi na Sahiwal na 10% Ayshire na Jersey. Mpaka mwaka 1971 mbegu hii ikawa na mchanganyiko wa 32% Red Sindhi, 30% Sahiwal, 19% Tanganyika Zebu 10% Boran na 10% Ayshire na Shorthorn, utagundua kwamba mbegu ya Jersey iliondolewa na kuingizwa short horn
MWONEKANO
Wanaonekana zaidi kama Sahiwal wakiwa na rangi nyekundu iliyofubaa mpaka kukooza sana au Nyekundu na nyeupe, Wana nundu kama ng’ombe wetu wa kienyeji, ngozi ya chini yashingo ijulikanayo kama DEWLAP ni ndogo zaidi ya Zebu lakini kubwa zaidi ya Ng’ombe wa kigeni, wana kiwele kikubwa zaidi ya ngombe wa kienyeji chenye kukamilika kirahisi ANGALIZO nundu na dewlap huwasaidia kupambana na mazingira ya Afrika hasa joto kali
MBEGU YA MPWAPWA

Madume yana uzito kati ya kilo 450 – 600 na majike kilo 275 – 300 wakati wa uzazi wa kwanza na huongezeka hadi kufikia kilo 450 hapo baadae, mbegu hii inauezo wa kuzalisha maziwa mengi kuliko ng’ombe wa kienyeji na pia uhimili mazingira ya joto na magonjwa kuliko Tanganyika Zebu
Serekali imeshindwa kusambaza mbegu hii kwa wafugaji na inasemekena karibia itapotea kwa sababu ng’ombe wa Mpwapwa waliobakia ni wachache sana na wanapatikana kwenye baadhi ya vituo vya utafiki kama Mpwapwa kwenyewe. Pia kuna tetesi kwamba kwa sasa hakuna MBEGU HALISI (pure breed) ya ng’ombe hawa kutokana na kuachwa wakapandana ndugu kwa ndugu (Inbreeding)
Mbegu hii inatokana na mchanganyiko wa mbegu ya ng’ombe jike aina ya Zebu toka Tanzania na Red madume ya Sindhi na Sahiwal wenye asili ya india na Pakistan lakini waliotolewa nchini Kenya hii ilikuwa ni mwaka 1940 ambapo uzalishaji wa mbegu hii ulifanyika kwa mara ya kwanza katika kituo cha utafiti wa mifugo Mpwapwa Dodoma nchini Tanzania
Mwaka 1958 uboreshaji wa mbegu hii ulifanyika kwa kuongezea damu za ng’ombe wa ulaya (Bos Taurus) aina ya Ayshire na Jersey na mpaka kufikia mwaka 1960 mbegu ya Mpwapwa ikawa na na uwiano wa 20% Tanganyika Zebu 10% Boran 5% Ankole 55% Red Sindhi na Sahiwal na 10% Ayshire na Jersey. Mpaka mwaka 1971 mbegu hii ikawa na mchanganyiko wa 32% Red Sindhi, 30% Sahiwal, 19% Tanganyika Zebu 10% Boran na 10% Ayshire na Shorthorn, utagundua kwamba mbegu ya Jersey iliondolewa na kuingizwa short horn
MWONEKANO
Wanaonekana zaidi kama Sahiwal wakiwa na rangi nyekundu iliyofubaa mpaka kukooza sana au Nyekundu na nyeupe, Wana nundu kama ng’ombe wetu wa kienyeji, ngozi ya chini yashingo ijulikanayo kama DEWLAP ni ndogo zaidi ya Zebu lakini kubwa zaidi ya Ng’ombe wa kigeni, wana kiwele kikubwa zaidi ya ngombe wa kienyeji chenye kukamilika kirahisi ANGALIZO nundu na dewlap huwasaidia kupambana na mazingira ya Afrika hasa joto kali
MBEGU YA MPWAPWA

Madume yana uzito kati ya kilo 450 – 600 na majike kilo 275 – 300 wakati wa uzazi wa kwanza na huongezeka hadi kufikia kilo 450 hapo baadae, mbegu hii inauezo wa kuzalisha maziwa mengi kuliko ng’ombe wa kienyeji na pia uhimili mazingira ya joto na magonjwa kuliko Tanganyika Zebu
Serekali imeshindwa kusambaza mbegu hii kwa wafugaji na inasemekena karibia itapotea kwa sababu ng’ombe wa Mpwapwa waliobakia ni wachache sana na wanapatikana kwenye baadhi ya vituo vya utafiki kama Mpwapwa kwenyewe. Pia kuna tetesi kwamba kwa sasa hakuna MBEGU HALISI (pure breed) ya ng’ombe hawa kutokana na kuachwa wakapandana ndugu kwa ndugu (Inbreeding)
Wednesday, September 28, 2011
LEO NI SIKU YA KICHAA CHA MBWA DUNIANI -
Wakati leo tunaazimisha siku ya kichaa cha mbwa duniani, ugonjwa huu hapa nchini kwetu bado umekuwa tatizo sugu. Katika wilaya ya Temeke pekee watu 202 waling'atwa na kati ya hao 19 waliugua kichaa cha mbwa. Wilaya hii inajumla ya mbwa 4500, paka 1500 ambapo kati ya hao 3418 walifanikiwa kuchanjwa.
CHANJO YA KICHAA CHA MBWA (RABIES) KWA AJILI YA WANYAMA

Ugonjwa huu huweza kumpata viumbe vingi ikiwemo binadamu, ng'ombe, mbuzi, kondoo na kadhalika, na wasmbazaji wakuu wakiwa mbwa na paka ingwa kuna baadhi ya poo (vampire bats) nao pia husambaza ugonjwa huu kwa kung'ata na kusambaza vimelea vya kichaa cha mbwa.
ugonjwa huu upo kila sehemu ya dunia ambapo kwa mwaka huua jumla ya watu 55,000 kote duniani ambapo Afrika watu 21,000 hufa kila mwana na wengine 34,000 hufa barani Asia na kwingineko
Kauli mbiu ya mwaka huu ni TUSHIRIKIANE KUFANYA KICHAA CHA MBWA KUWA HISTORIA na njia pekee ni kuwachanja wanyama wetu, na pia kuwazuia wasizurure hovyo mitaani, MUONE MTAALAM WA MIFUGO ALIYE KARIBU NAWE ILI MBWA NA PAKA WAKO WAPATE CHANJO KAMILI
CHANJO YA KICHAA CHA MBWA (RABIES) KWA AJILI YA WANYAMA

Ugonjwa huu huweza kumpata viumbe vingi ikiwemo binadamu, ng'ombe, mbuzi, kondoo na kadhalika, na wasmbazaji wakuu wakiwa mbwa na paka ingwa kuna baadhi ya poo (vampire bats) nao pia husambaza ugonjwa huu kwa kung'ata na kusambaza vimelea vya kichaa cha mbwa.
ugonjwa huu upo kila sehemu ya dunia ambapo kwa mwaka huua jumla ya watu 55,000 kote duniani ambapo Afrika watu 21,000 hufa kila mwana na wengine 34,000 hufa barani Asia na kwingineko
Kauli mbiu ya mwaka huu ni TUSHIRIKIANE KUFANYA KICHAA CHA MBWA KUWA HISTORIA na njia pekee ni kuwachanja wanyama wetu, na pia kuwazuia wasizurure hovyo mitaani, MUONE MTAALAM WA MIFUGO ALIYE KARIBU NAWE ILI MBWA NA PAKA WAKO WAPATE CHANJO KAMILI
WILAYA ZA NGORONGORO NA LONGIDO ZAKUMBWA NA UGONJWA HATARI WA HOMA YA MAPAFU YA NGOMBE

Wilaya za Ngorongoro na Longido ambazo zipo mpakani na Kenya zimekumbwa na ugonjwa wa mapafu wa ng'ombe, hali hii imefanya jumla ya ng'ombe milioni moja (1,000,000) kuwa katika hatari ya kukumbwa na ugonjwa huu.
Ugonjwa huu ulitangazwa kama janga la kitaifa mnamo mwaka 2001 kwa sababau ni hatari sana na unaua ng'ombe kwa kasi sana, na unaweza kudhibitiwa kwa kuchanja mifugo mara unapoonyesha dalili za mlipuko.
Kutokana na hilo serekali imechukua hatua za dharura za kuwachanja ng'ombe wote katika wilaya ya Ngorongoro, Longido na zile za jirani kama Karatu na nyinginezo.
Historia ya ugonjwa huu inaanzia enzi za ukoloni mnamo mwaka 1905 na uliweza kudhibitiwa, lakini mnamo mwaka 1964 mwaka ambao ndio wa muungano wa Tanganyika na Zanzibar ulitokea na Tanzania kuzaliwa, ugonjwa huu ulilipuka tena nchini mwetu. mnamo mwaka 1990 ugonjwa huu ulilipuka tena katika Wilaya ya Loliondo mpakani na Kenya.

Mwaka 1994 ugonjwa huu ulilipuka tena na kusambaa hadi mkoa wa Morogoro katika wilaya za kilosa na Mahenge. na mwaka 1998 ugonjwa huu ulisambaa katika mikoa 11 ya nchi yetu
Ugonjwa huu hujulikana kama contagious bovine pleural pneumonia au CBPP kwa kifupi na kama unataka mifugo yako ichanjwe wasiliana na maofisa ugani waliokaribu nawe au ofisi za wizara ya mifugo
Saturday, September 17, 2011
MBEGU BORA YA MIHOGO YAGUNDULIWA
SHAMBA DARASA LA MIHOGO

Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika ikishirikiana na taasisi ya kimataifa ya kilimo cha kitropiki (IITA) kwa pamoja zimezalisha aina mpya ya mbegu za mihogo zenye kustahimili magonjwa makubwa ya zao hilo. Mbegu hiyo mpya inayojulikana kama KIROBA inatoa wanga mzuri kwa ajili ya lishe na kuhimili magonjwa, pia inaweza kutoa mazao kufikia tani 35 kwa hecta.
MIHOGO BORA TAYARI KUVUNWA

Akiongea hayo Meneja wa mradi wa Shirika la chakula Duniani (FAO) BW. Raphael Laizer wakati anakagua mashamba darasa ya mihogo huko Mkuranga, alisistiza kutumia mashamba darasa ya zao la muhogo kwa ajili ya majaribio ili kupata mbegu bora ambazo zitalimwa karibu mikoa yote na ziwe zenye uwezo wa kuhumili ukame na magonjwa pia.
MIHOGO YA KUKAUSHA (makopa) KWA AJILI YA UNGA

Wizara ya Kilimo, Chakula na Ushirika ikishirikiana na taasisi ya kimataifa ya kilimo cha kitropiki (IITA) kwa pamoja zimezalisha aina mpya ya mbegu za mihogo zenye kustahimili magonjwa makubwa ya zao hilo. Mbegu hiyo mpya inayojulikana kama KIROBA inatoa wanga mzuri kwa ajili ya lishe na kuhimili magonjwa, pia inaweza kutoa mazao kufikia tani 35 kwa hecta.
MIHOGO BORA TAYARI KUVUNWA

Akiongea hayo Meneja wa mradi wa Shirika la chakula Duniani (FAO) BW. Raphael Laizer wakati anakagua mashamba darasa ya mihogo huko Mkuranga, alisistiza kutumia mashamba darasa ya zao la muhogo kwa ajili ya majaribio ili kupata mbegu bora ambazo zitalimwa karibu mikoa yote na ziwe zenye uwezo wa kuhumili ukame na magonjwa pia.
MIHOGO YA KUKAUSHA (makopa) KWA AJILI YA UNGA

Saturday, August 13, 2011
KILIMO CHA VITUNGUU TWAUMU - garlic

UDONGO
Vitunguu twaumu vinahimili aina nyingi za udongo, ila vinastawi zaidi katika udongo usiotuamisha maji kabisa na wenye mbolea asili, kama mbolea si ya kutosha kwenye udongo, tumia samadi iliyokwisha oza vizuri usitoe samadi bandani na kuipeleka shambani moja kwa moja kwenye shamba la vitunguu thwaumu, labda kama utaliacha shamba bila kulimwa kwa zaidi ya miezi 6, pia unaweza kutumia mbolea za viwandani kama ammonium nitrate, ammonium sulphate, urea n.k wakati wa kupanda na kila baada ya wiki 4 – 6 mara mbili zaidi
UPANDAJI
Kipindi kizuri kwa upandaji ni kipindi ambacho hakuna joto hasa miezi ya May mpaka August kwa Tanzania, Unachukua kitunguu twaumu na kutenganisha vitunguu kimoja kimoja (bulbs) na kuchagua vile vikubwa maana hivi ndivyo vitakavyo kupa mazao mengi na bora, nafasi kati ya kitunguu na kitunguu ni sentimeta 10 na kati ya mistari ni sentimeta 30. Baada ya kupanda pandishia udongo na uukandamize kuhakikisha kwamba kimekaa vizuri na hakiwezi kuathiriwa na mvua au maji wakati wa kumwagilia ili kisikae upande au kungolewa kabisa. Uotaji mzuri hutegemea pia namna vitunguu thwaumu vilivyo hifadhiwa kabla ya kupandwa, kama vilihifadhiwa sehemu zenye joto na hewa finyu uotaji wake utakuwa duni na dhaifu.

UMWAGILIAJI
Kama kuna upungufu wa mvua au ni kipindi cha kiangazi basi ni vizuri ukamwagilia shamba lako, wakati mzuri wa kumwagilia vitunguu twaumu ni asubuhi na sio jioni au mchana, hii inasaidia vitunguu twaumu kujijengea uwezo wa kupambana na magonjwa, baada ya mizi miwili unaweza kupunguza umwagiliajai huku ukiangalia kwa kuchimba kidogo kama vitunguu twaumu vimezaliana vya kutosha na kuanza kukomaa, ukiona vimekomaa acha kabisa kumwagilia ili visioze
UANGALIZI
Aina nyingi za vitunguu twaumu vitakuwa kama vinatoa mbegu kwenye mmea (angalia picha chini), ingawa kuna nadharia nyingi lakini inashauriwa kukata hizi mbegu chini kabisa kwa kisu kikali na kisafi, usikate mapema mara baada ya kutokeza bali subiri mpaka mmea unapoanza kama kujikunja ndipo ukate, kwa wale wanaoacha mbegu hizi ukiamua kuzipanda kwa msimu wa kwanza zitazaa kitunguu kimoja tu cha duara lakini chenyewe ukikipanda tena kwenye mzunguko wa pili kitazaa vitunguu vingi kama kawaida

Ungoleaji wa magugu na majani ni muhimu muda wote ili kuondoa kugombea rutuba, hewa na maji shambani, kwa wenye mashamba makubwa wanaweza kutumia dawa za kemikali kama ROUNDUP na nyinginezo ili kudhibiti magugu, ingawa mimi sishauri hivyo.
MAGONJWA
Magonjwa kama botrytis (kuoza shingo) blue mould na fusarium (kuoza kwa vitunguu) husababisha hasara kubwa kama hayatadhibitiwa kwa kutumia viuatilifu mara unapoona dalili, pia magonjwa kama white rot huchukua zaidi ya miaka 20 kuondoka kama yatavamia shamba lako, inashauriwa kufanya mabadiliko ya zao kila baada ya miaka mitano kwa kupanda mazao mengine yasiyo jamii moja kama vitunguu maji, unaweza kupanda maharage, mahindi, karoti na kabichi katika mzunguko huo. Pia magonjwa kama kutu ya majani husababisha na unyevu mwingi hasa kama mimea itakuwa kwenye udongo unaotuamisha maji au mimea kumwagiliwa jioni au usiku, kumbuka kumwagilia asubuhi tu Ili kudhibiti ugonjwa huu wa kutu mimea ingolewe na ichomwe au utumie viuatilifu vya kuulia fangasi wa mimea.
Monday, August 8, 2011
NANE NANE NA MELTON KALINGA
Leo ni siku ya wakulima yaani nane nane na maadhimisho kitaifa yanafanyika Dodoma, mimi niko na mtaalam wa Samaka Bw Melton Kalinga kwenye kituo cha Kingolwira nje kidogo ya Morogoro mjini kama km12. Kinachofanyika kwa leo ni upandishaji wa Samaki aina ya kambale
Unaanza kwa kutafuta majike makubwa yenye mayai tumboni, kisha unatafuta na Madume yaliyokomaa, ili kupandisha kwa njia ya kimaabara kambale dume inabidi umuue kisha unachukua pituitari gland na kumwingizia jike mwenye mayai aliye hai, baada ya masaa 24 mayai yanakuwa yame komaa, unayakamua toka kwa jike kisha unachanganya na mbegu za kiume toka kwa samaki uliyemuua jana yake, kwa kutumia mtambo wa maabara wenye maji ya vuguvugu unatotolesha mayai hayo kwa njia ya kitaalam.
Vifaranga wa samaki aina ya sato wanapatikana pia kwa shilingi 50 tu, kwa mawasiliano zaidi mpigie Bw Kalinga 0757891761 au 787596798
KAMBALE WAKIVULIWA KWENYE BWAWA


UKAGUZI NA UCHAMBUZI KUJUA MADUME NA MAJIKE WANAOFAA

SAMAKI JIKE MWENYE MAYAI
SAMAKI DUME

UTOAJI WA MBEGU TOKA KWA DUME
MTAMBO WA KUTOTOLESHEA MAYAI YA KAMBALE
Unaanza kwa kutafuta majike makubwa yenye mayai tumboni, kisha unatafuta na Madume yaliyokomaa, ili kupandisha kwa njia ya kimaabara kambale dume inabidi umuue kisha unachukua pituitari gland na kumwingizia jike mwenye mayai aliye hai, baada ya masaa 24 mayai yanakuwa yame komaa, unayakamua toka kwa jike kisha unachanganya na mbegu za kiume toka kwa samaki uliyemuua jana yake, kwa kutumia mtambo wa maabara wenye maji ya vuguvugu unatotolesha mayai hayo kwa njia ya kitaalam.
Vifaranga wa samaki aina ya sato wanapatikana pia kwa shilingi 50 tu, kwa mawasiliano zaidi mpigie Bw Kalinga 0757891761 au 787596798
KAMBALE WAKIVULIWA KWENYE BWAWA
UKAGUZI NA UCHAMBUZI KUJUA MADUME NA MAJIKE WANAOFAA
SAMAKI JIKE MWENYE MAYAI

SAMAKI DUME

UTOAJI WA MBEGU TOKA KWA DUME

MTAMBO WA KUTOTOLESHEA MAYAI YA KAMBALE
Thursday, July 7, 2011
MATIKITI MAJI - water melon

Ili kulima matikiti maji, inakubidi uwe na sehemu ya kutosha, yenye jua la kutosha, maji mengi na ardhi yenye rutuba ya kutosha, matikiti maji hukua haraka kama mimea mimgine ya jamii yake itambaayo mfano Matango, maboga na maskwash.
Kwa mtu ambaye anaanza kilimo yatampa tabu kidogo tofauti na Yule ambaye ana ujuzi kidogo na mambo ya kilimo kwa sababu yanahitaji umakini kiasi.
HALI YA HEWA
Mimea hii haihimili hali ya joto kali sana, mvua nyingi na udongo unaotuamisha maji, magonjwa ya fangasi na wadudu waharibifu, inastawi vizuri kwenye kuanda wa pwani na miinuko kidogo kama DSM,Tanga, Morogoro, Mtwara, lindi na Pwani ambapo kuna jua la kutosha. Muda mzuri wa kupanda ni kipindi cha kipupwe mwezi wa machi mpaka wa septemba .
UPANDAJI
Panda kwa kutumia Mbegu zinazouzwa madukani, ukitumia Mbegu kutoka kwenye tikiti ulilonunua linaweza likawa ni hybrid na matokeo yake matikiti yatakayozaliwa hayatakuwa bora kwa sababu yatakuwa ni kizazi cha pili (F2)
Panda Mbegu yako moja kwa moja kwenye shamba, usinunue miche au kupanda Mbegu kwenyemifuko ya plastiki halafu ndi uhamishie shambani, panda Mbegu mbili sentimeta 2 chini ya udongo kwa umbali wa sentimeta 30 kutoka shina hadi shina na mita 2 - 3 kutoka mstari hadi mstari, baada ya siku chache Mbegu zitaanza kuota, baada ya kama wiki 2 katika Mbegu mbili ulizopanda kata moja na uache ule mche wenye afya zaidi, angalizo using’oe mche bali ukate ili kuzuia kusumbua mizizi ya mche uliobaki.
Unaweza kupandishia udongo kwenye mashina na hii itasaidia kupunguza maji yasituame kwenye mimea yako, pia unaweza kuweka samadi badala ya kupandishia udongo ukiwa na nia ileile ya kuzuia maji yasituame na kuongeza rutuba.
Kama una sehemu ndogo ya shamba unaweza kuyawekea matikiti waya wa kutambalia, ila inabidi uwe imara kwa sababu ya kuhimili uzito wa matunda yenye, na wakati wa kuanza kutambaa kwenye waya ni lazima uifundishe mimea kwa kuielekezea kwenye waya na kufungia
MCHE ULIOCHIPUA

UANGALIZI
Miche ikiwa imetambaa kiasi unaweza kuweka matandazo kwenye udongo ili kuzuia upotevu wa unyevu, unaweza kuweka samadi au mbolea za viwandani, mimea ikiwa midogo tumia zaidi mbolea zenye nitrojen na utumie zaidi mbolea za potasiam mara baada ya maua kutokeza hadi matunda kukomaa, matawi yakifikia urefu wa mita 2 kata mbele ilikuruhusu kutoa matawi na hivyo kupata maua mengi zaidi hatimaye mavuno zaidi
MAUA NA MATUNDA
Matikiti hutoa maua dume na jike kwenye tawi moja, maua dume ambayo ni madogo zadi hutoka kwanza yakifuatiwa na maua jike ambayo ni makubwa zaidi, usipoona maua dume na jike kuna tatizo mfano maji kidogo yalimwagiliwa, upungufu wa viritubisho kwenye udongo, hali ya hewa ni joto/baridi sana n.k
Uchavushaji kwenye matikiti hufanyika na wadudu, kama huwaoni wakifanya kazi yao unaweza kufanya mwenyewe, muda mzuri ni wa asubuhi, unakata maua dume kwa kisu na kufanya uchavushaji kwenye maua jike, maua jike ya mwanzo kwenye tawi ndiyo yenye ukuaji bora zaidi, unaweza kukata tawi lisiendelee kukua baada ya matunda kutokeza hii husababisha kuwa na matunda makubwa zaidi
UCHAVUSHAJI KWA MKONO

UVUNAJI MATIKITI
Ili kujua matikiti yamekomaa inahitaji ujuzi kidogo, upande wa chini wa tunda huanza kuwa na rangi ya njano, pia kikonyo juu ya tunda hukauka kabisa na kuwa kijivu, ila njia nzuri ni kuyapiga kwa kiganja na kusikiliza mlio wake kama tunavyofanya kwenye mafenesi, hii nayo ni shule nyingine. Tumia kisu wakati wa kuvuna matikiti, yabebwe na kuhifadhiwa vizuri kwenye makasha tayari kuuzwa au kwa matumizi binafsi
MAGONJWA NA WADUDU
Wadudu wa matikiti wako wanaoshambulia majani na maua, na wengine hushambulia matunda , pia kuna magonjwa ya fangasi ambayo hushambulia mimea, ili kujua dawa za magonjwa ni vizuri kuchukua sampuli na kwenda nayo kwenye duka la dawa na pembejeo za kilimo ili kjupata dawa sahii, dawa aina ya KARATE itasaidia kuua wadudu wa majani, maua na matunda na FUNGICIDE itasaidia kwa mashambulizi ya fangasi
Sunday, June 26, 2011
LINDI - MTWARA
Subscribe to:
Posts (Atom)