KURASA

Sunday, August 18, 2013

KUPUNGUZIA MATAWI KWENYE MICHE YA NYANYA

Kuna baadhi ya wasomaji wangu walipenda kufahamu umuhimu wa kupunguzia matawi kwenye zao la nyanya na pia jinsi ya kupunguzia matawi hayo.
Umuhimu wa kupunguzia matawi kwenye zao la nyanya ni kupata nyanya bora, kubwa na zenye afya, ukiacha mti uwe na matawi utatoa maua mengi sana na utaishia kupata nyanya ndogo ndogo ambazo hazina soko zuri, lakini ukipunguzia matawi nyanya zako zitakuwa kubwa na mmea wako utazaa kwa mpangilio na kwa muda mrefu

Jinsi ya kupunguzia matawi ni kwa kutofautisha maua ni yapi na matawi ni yapi kisha unaondoa matawi kwa kutumia mkono tu, usitumie kisu maana itakuwa rahisi kusambaza magonjwa toka mme mmoja hadi mwingine, mara nyini matawi hutoke kati ya shina na jani kama inavyoonekana kwenye picha hapo chini




NYANYA KUBWA ZENYE AFYA


NYANYA DOGO TOKA KWENYE MMEA WENYE MATAWI MENGI


Tuesday, August 13, 2013

UMUHIMU WA MAJIVU KWENYE UDONGO WA BUSTANI

Watu wengi wamekuwa wakiulizia umuhimu wa madini kwenye udongo na namna ya asili ya kuongezea kosefu wa madini kama potasiam, fosforas, kalsiam na mengineyo, njia rahisi ya kuongeza baadhi ya madini kwenye udongo ni kwakutumia majivu

UMUHIMU
Majivu yanakiwango cha wastani wa madini kifuatacho potasiam 5% - 7%, kalsiam 25% - 50%, fosforas 1.5% - 2% na madini mengine kwa kiasi kidogo pia mabaki mabaki ya chenga za mkaa kwenye majivu pia yanasaidia kwenye kunyonya baadhi ya sumu kwenye ardhi, kumbuka mkaa ni kaboni halisi (pure carbon)

KIASI CHA KUTUMIA
Kiasi cha kilo 2.5 mpaka 5 kitumike kwenye eneo la mita za mraba 33 au futi 100 za mraba, na majivu yamwagwe wiki 3 - 4 kabla ya kupanda kitu chochote ardhini.

MADHARA
Kila kitu kikitumiwa zaidi ya kiasi kina madhara na majivu pia yana madhara kwenye udongo kwa sababu yana hali ya kuwa alkaline zaidi (10 - 12 pH)  kwa sababu baadhi ya mchanganyiko wake hauyayuki kwenye maji, kama utahitaji kuongezea kwenye mimea yenye upungufu wa madini kama fosforas na potasiam basi hakikisha majivu hayagusi mashina kwani yanaweza kuuungua haya kama mimea ni michanga.

Pia majivu yanan kiasi kidogo sana cha naitrojeni ambacho hakiwezi kukidhi mahitaji ya mmea wowote ule, kwa hiyo hakikisha pia unatumia vyanzo vingine kwa ajili ya naitrojeni, vyanzo kama mimea jamii ya mikunde, marejea, lukina, na alfalfa

NANE NANE 2013










BLOG AWARDS 2013



Wasomaji wa blog hii ya mitiki-kilimo kwanza, mwaka huu pia blog hii itashiriki kwenye kutafuta blog bora za mwaka 2013 kupitia  http://tanzanianblogawards.blogspot.com/ blog hii itaomba kushiriki kwenye vipengele viwili vya Best AgricultureBlog na Best Educational Blog. 


 



Mkumbuke blog hii kwa mwaka 2012 ndio ilikuwa blog bora kwenye kipengele cha Best Educational Blog, kwa mwaka huu upigajikura utaanza September 1 mpaka September 7 2013 kwa wale wanaoamini hii ni blog bora kwenye vipengele itakavyochaguliwa, nitawaomba watembelee linki hii hapa chini na kupiga kura zao. Aksante

http://tanzanianblogawards.blogspot.com
  

Tuesday, August 6, 2013

SEREKALI KUNUNUA MAZAO YOTE YA NAFAKA


 Serikali imetangaza kuanzia mwakani itaanza kununua mazao yote ya nafaka, ili wakulima nchini  wawe na soko la uhakika. Hatua hii inalenga kuweka ushindani wa biashara baada ya kuhodhiwa wa wanunuzi binafsi.

Mazao yatakayonunuliwa kupitia Bodi Mpya ya Mazao ya Nafaka ni mpunga, maharagwe, karanga, choroko, ulezi, ufuta na mahindi na kwamba yatanunuliwa kwa bei ya ushindani wa soko mwaka huu.
Mchumi wa bodi hiyo, Edwin Mkwenda, alisema hayo kwenye maonyesho ya wakulima yanayofanyika kitaifa  Viwanja vya Nzuguni, Dodoma.
Mkwenda alisema tayari Serikali imeikabidhi bodi hiyo maghala yote yaliyokuwa ya Shirika la Usagishaji la Taifa (NMC), ambayo hayakubinafsishwa kwenye kanda saba za nchi ili kutunza mazao yatakayonunuliwa.
Naye Ofisa Ubora wa Mazao wa Bodi hiyo,  Dendego Abdallah, alisema kuundwa kwa bodi hiyo ni ukombozi kwa wakulima kwani watakuwa na uhakika wa kupata soko la mazao husika.
Abdallah alisema wafanyakazi wa bodi chini ya Mkurugenzi Mkuu, Eliampaa Kilanga, imejipanga kuanza biashara rasmi mwakani na kwamba, wakulima wajiandae kuzalisha mazao hayo kwa wingi kutokana na kuwapo uhakika wa soko.
Wakati huohuo, Shirika la kuendeleza Bonde la Mto Rufiji (Rubada), limetenga Sh300 milioni kujenga kituo cha pili cha kufundisha vijana kilimo cha biashara kwa vitendo eneo la Ngalimila, wilayani Kilombero.
Ofisa Kilimo wa Rubada, Joseph Lyafwila, alisema hayo kwenye maonyesho hayo kuelezea mkakati wa Serikali kubadili kilimo kwa vijana, ili walime kibiashara zaidi  kupitia mafunzo ya vitendo.

CHANZO http://www.mwananchi.co.tz/kitaifa/Serikali-kununua--nafaka-zote-nchini/-/1597568/1937656/-/13mbvgmz/-/index.html

Tuesday, July 30, 2013

KILIMO BORA CHA MANANASI

Zao la mananasi hulimwa sana hapa nchini maeneo ya Bagamoyo, Kibaha, Geita, Mwanza, Tanga, Mtwara, Lindi na maeneo mengine. Zao hili lina kiasi kikubwa cha vitamini A na B na kiasi kidogo cha vitamini C, pia kuna madini kama potasiam, kalsiam, chuma na magnesiam

HALI YA HEWA
Manansi hustawi sana ukanda wa pwani usawa usiozini mita 900 toka usawa wa bahari ambapo kuna mvua nyingi kiasi cha milimita 1500 na unyevu wa kutosha, pia unaweza kupanda kwenye maeneo yenye mvua chache lakini kwa kutumia kilimo cha umwagiliaji, Hali ya joto ni kuanzia sentigredi 15 - 32, huwa haya stahimili baridi

UDONGO
Udongo wenye rutuba ya kutosha na usiotuamisha maji ndi unaofaa kwa ajili ya kilimo cha mananasi, unaweza kutumia samadi au mbole vunde ili kuongezea rutuba ya udongo wako.

MSIMU
Kwa ukanda wa pwani wenye mvua mbili kwa mwaka upandaji wa mananasi huanza mara baada ya mvua za kwanza kuanza, ni vizuri kupanda kwa muda mfupi ili uzaaji usipishane sana na pia kusaidia kupata mvua za kutosha kabla ya msimu kuisha.

UPANDAJI
Tumia miche ya aina moja na yenye umri sawa ili huduma zifanane na pia uzaaji uwe wa mpangilio, umbali toka mmea hadi mmea ni sentimeta 30 na mstari hadi mstari ni sentimeta 60, na umbali kila baada ya mistari miwili miwili ni sentimeta 90

Kwa ekari moja unaweza kupanda miche 25,200 na kwa hekta moja unaweza kupanda miche 44,000. ili mananasi yako yastawi vizuri basi tengeneza kama mtaro mdogo na kwenye mitaro ndio upande mananasi yako, hii husaidia kupata unyevu zaidi

MBOLEA
Kwa wale wanaotumia mbolea za viwandani, ni vizuri kutumia NPK na DAP ambazo utaweka miezi miwili baada ya kupanda na miezi 12 baada ya kupanda baada ya hapo hautahitaji mbolea tena, lakini ni vizuri zaidi kama utatumia mbolea za asili

WADUDU
Wadudu wanaoshambulia mananasi ni aina ya mealybug ambao huondolewa kwa kupulizia dawa kama dume na karate.

Ugonjwa wa kuoza moyo wa miche unaweza kuzuiwa kwa kupiga dawa za copper oxychloride au kwa kuzamisha miche kwenye dawa za fungasi (fungicides)kabla ya kupandwa shambani

UVUNAJI
Mananasi huwa tayari kuvunwa miezi 18  mpaka 24 baada ya kupandwa kutegemeana na mbegu na matunzo ikiwemo kiasi cha mvua, mbolea na unyevu shambani, Uvunaji  hufanyika kwa kutumia visu na vibebeo maalum kuhakikisha ubora wa zao hili


Thursday, July 25, 2013

ATHARI ZA MAFUTA YA UBUYU NA TFDA


 
Mamlaka ya chakula na dawa (TFDA) imesisitiza kwamba mafuta ya ubuyu yana athari kubwa za kiafya na ni hatari kwa sababu yana tindikali ya mafuta ijulikanayo kama Clycopropenoic, moya ya madhara ya mafuta ya ubuyu ni pamoja na kusababisha saratani. TDFA imesema pia kutumia unga wa ubuyu na majani yake hakuna athari zozote kiafya kwa hiyo watu wanaweza kuendelea kutumia bila matatizo yoyote.
Kitaalamu tindikali ya Clycopropenoic inaweza kuondolewa kwenye mafuta hayo iwapo tu yatachemshwa katika kiwango cha digrii 180 za sentigredi kwa masaa 8 au kwa teknolojia ya kuyagandisha (hydrogenation) ambapo katika njia hizo zote mbili hakuna hata moja ambayo inatumika hapa nchini.

Miaka ya karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la matumizi ya bidhaa za asili ikiwemo ya aloe vera, ubuyu na bidhaa zake, hii inatokana na matatizo ya kiafya kama kisukari, ugonjwa wa moyo, magonjwa ya ngozi, uzazi, nguvu za kiume na kuongeza kinga mwilini. kutokana na hili matumizi ya ubuyu, majani yake na mafuta yake yaliongezeka zana huku watu wakiamini kwamba ni dawa na kinga ya magonjwa mbali mbali.


Hili walilotuambia TDFA tusilipuuze ila taasisi nyingine za kiutafiti kama SUA na  NIMRI zifanye utafiti wa kutosha sio tu kwa mafuta ya ubuyu bali pia kwenye dawa nyingine na vitu vya asili ili kubaidi madhara yanayoweza kujitokeza kwa waTanzania iwapo watatumia.


Wednesday, July 24, 2013

KILIMO BORA CHA MATUFAA - APPLES

Tufaa ni tunda moja maarufu duniani ambalo hupendwa kuliwa na watu wa jamii zote, hii inatokana na utamu wake pamoja na faida za kiafya zinazopatikana kwa kula matufaa. Matunda haya hustawi zaidi kwenye nyanda za juu ambako joto sio kali, sehemu kama lushoto, Arusha, miteremko ya Kilimanjaro, Mbeya, Iringa, Njombe, Songea nk. Udongo ni wenye rutuba ya kutosha na usiotuamisha maji

Unaweza kupanda kwa kutumia mbegu au kwa kununua miche bora kutoka kwenye taasisiza kilimo mfano Uyole Mbeya. kama utatumia mbegu basi ni bora kununua mbegu bora au ukikosa mbegu basi jaribu kutumia zile utakazopata kutoka kwenye tunda lenyewe

Kama utachukua za kwenye tunda basi zikaushe kwenye jua kwanza mpaka zikauke kabisa, zile za kukununua huwa zimekauka kwa hiyo huna haja ya kuzikausha, Chukua karatasi laini (napkins/tissues) iloweshe maji kiasi kidogo kisha chukua mbegu zako na uzifunge na  karatasi hii vizuri kisha ziwekw kwenye jokofu kwa kiasi cha wiki 3-4 zitaanza kuota/kumea, kuziweka kwenye friji husaidia kuua vijidudu vya magonjwa ambavyo huenda vilikuwepo kwenye tunda au mbegu

Chukua mbegu yako na uipande kwenye mifuko au chombo kama ndoo, usipande kwenye vifuko vidogo maana mmea huu hukua mkubwa kiasi na wenye mizizi mikubwa kabla ya kupandwa. Mmea wako ukifikia ukubwa wa futi moja mpaka pili ni kipindi kizuri kuuhamishia shambani,

Umbali wa shimo hadi shimo ni kiasi cha futi 15 mpaka 18 kutoka mti hadi mti. Hakikisha unapanda miche yako wakati wa mvua za kwanza, Mashimo yawe na kina cha futi mbili na upana futi 3. Weka kasi cha debe 1 la samadi au mboji na changanya vizuri na udongo.

kumbuka kuacha kisahani kwa ajili ya kukusanya maji ya mvua au unapomwagilia na utandaze majani/nyasi kiasi cha futi 3 kuzunguka mti wako, hakikisha wanyama kama mbuzi na ng'ombe hawaingii shambani na kula miti yako. Baada ya mwaka hutakuwa tena na haja ya kumwagilia miti yako kwani itaweza kukua yenyewe kwa kutegemea mvua

WADUDU NA MAGONJWA
Wadudu wanaoshambulia zaidi mitufaa ni vidukari (moth) na pia ugonjwa wa madoa meusi (black spot) ndio unaoshambulia zaidi, ili kupambana na ugonjwa na wadudu hawa hakikisha unatuma kiutilifu chochote che nye pareto (pyrethrum) ndani yake
KUVUNA
Uvunaji ni baada ya miaka mitatu lakini miche ya kuunga huanza kuzaa mapema hata ndani ya mwaka, ila nashauri usiruhusu matunda mengi kwenye miti midogo ili kuzuia matawi kuvunjika kwa hiyo punguza matunda kabla hayajawa makubwa na kubakisha machache

Wednesday, July 17, 2013

BLACK QUARTER - CHAMBAVU

Huu ni ugonjwa wa mifugo unaoshambulia ng'ombe, kondoo na mara chache farasi. Unasababishwa na vijidudu  ina ya Clostridium chauvoei  ambavyo hushambulia bila uwepo wa oksijeni ya kutosha (anaerobic) na kuzalisha sumu kwenye mwili wa myama na kusababisha kifo.

KUSAMBAA
Vijidudu husambaa kwa kupitia kwenye udongo ambapo mnyama huvipata anapokula majani, pia huweza kusambazwa kwa njia ya vidonda na mate toka kwa mnyama mwenye ugonjwa huu.

DALILI
-homa kali
-Misuli ya miguu ya nyuma huvimba na kuwa na joto kali, inauma ikiguswa na rangi ya sehemu hiyo ya ngozi hubadilika
-Ukigusa sehemu iliyoshambuliwa inatoa sauti ya kama majani makavu
-Mnayama huchechemea mguu wa nyuma sababu ya maumivu

UCHUNGUZI
Uchunguzi ufanyike na maafisa ugani wa mifugo kwa kufuatilia dalili na historia ya sehemu husika
-Kipande cha msuli na majimaji toka sehemu iliyoathiriwa kwa ajili ya uchunguzi wa kimaabara
-Uchunguzi wa mwili wa myama aliyefariki (post Mortem)

MATIBABU
-Penicilin inasaidia kutibu ugonjwa kama matibabu yataanza katika hatua za mwazo, ukichelewa hutaweza kmtibu mnyama wako.
-Tumia b-complex, na dawa za kupunguza uvimbe  kama visaidizi vya tiba
-Kupachana sehemu iliyoathirika ilikutoa majimaji na kuingiza hewa ili kuharibu mazingira ya kuishi vijidudu

KINGA
-Chanjo ya mara moja kwa mwaka kwa wanyama wakubwa.
-Wanyama wadogo wachanjwe mara wafikishapo umri wa miezi mitatu
-kwa sehemu ambayo kuna mlipuko wa ugonjwa huu wanyama wote wachanjwe kisha wapigwe dozi kubwa ya penicilin (kama ugonjwa hautaibuka ndani ya siku 14 wanyama wako watakuwa salama)
-Miili ya wanyama walikufa ichomwe na kuzikwa kwenye shimo refu sana


Thursday, April 25, 2013

NAMNA YA KUPAMBANA NA HARUFU MBAYA YA MBWA NDANI YA NYUMBA YAKO

Je unafuga mbwa  wako ndani ya nyumba yako kwa usafi wa hali ya juu, lakini umegundua harufu mbaya ya mbwa wako bado ipo ndani ya nyumba yako?  inawezekana ni kwa kiasi kidogo sana lakini bado inakera maana harufu mbaya ni mbaya tuu. Ambacho hujagundua ni kwamba kuna sehemu kadhaa ambapo hii harufu imejificha, sasa hapa nitakupa siri ya kuondoa harufu hii

(a)Matandiko anayolalia mbwa wako hakikisha yanafuliwa kila wiki, na itapendeza kama utakuwa na seti mbili ili wakati moja imefuliwa na kusubiria ikauke na jua basi unamtandikia hii nyingine

(b)Kama tandiko la mbwa huwa lina kaa kwenye kreti maalum basi tumia brashi kulisafisha na sabuni kisha nalo lianikwe, hii iwe angalau mara 1 kwa wiki, pia katikati ya wiki unaweza kuwa unalisafisha mara kwa mara kwa kutumia masine ya vakyum ya kusafishia mazulia

(c)Kama mbwa wako huwa analalia mito ya makochi yako, basi hakikisha ni mito ambayo inaweza kufulika ili nayo iwe inafuliwa mara kwa mara

(d)Midoli ya kuchezea mbwa wako nayo pia iwe ni ile ambayo inaweza kufuliwa na ifuliwe mara kwa mara ili kuondoa harufu

(e)Angalia sehemu ambazo mbwa wako hupenda kujificha mara kwa mara maana wakati mwingine huwa wanasahau mabaki ya chakula  na kusababisha harufu mbaya

(F)Kabla ya kusafisha mazulia yako yanyunyuzie na baking soda (sina jina la kiswahili) kisha safisha kwa kutumia mashine ya vakyum

PAMBANA NA KUNGUNI KWA KUTUMIA MAJANI YA MAHARAGE

Majani ya maharage yameonesha uwezo mkubwa wa kuweza kuwanasa kunguni kama watapita juu yake, majani ya maharage yanaweza kufanikisha zoezi hilo kwa sababu yana vinyweleo ambayo huwanasa kunguni mara wapitapo juu yake. Pia yana uwezo wa kudhoofisha miguu yao na kuwafanya wasiweze kutembea.

Matumizi ya majani haya kwa kutegesha kwenya chago za vitanda na sehemu nyinginezo yana uwezo mkubwa wa kupunguza uwepo wa kunguni ingawa shaka bado ipo kama yana uwezo wa kuangamiza na kutokomeza kizazi chote.

Kama njia hii itafanikiwa kwa asilimia 100 inamaanisha kupunguza gharama za kutumia kemikali za viwandani ambazo ni aghali ukilinganisha na majani ya maharage ambayo yanapatikana shambani na kwenye bustani zetu

Tatizo pekee ninaloliona kwenye njia hii ni muda wa kutokomeza kunguni kama wamevamia nyumba yako, njia hii inahitaji muda kiasi tofauti na kemikali ambazo zingeweza kuwaua mara upuliziapo, tatizo la kemikali nalo ni gharama, uchafuzi wa mazingira na pia usugu wa wadudu kwenye kemikali hizi ambazo wakati mwingine hupoteza uwezo wa kuangamiza wadudu.

jambo lingine gumu kwenye njia hii ni namna ya kuwafanya kunguni wavutiwe na kupita kwenye majani haya, kwani wasipopita juu yake njia hii haitakuwa na faida yoyote

Friday, April 12, 2013

FLAMINGO WA ZIWA MANYARA HATARINI KUTOWEKA

Ndege aina ya flamingo waliopo katika hifadhi ya taifa ya ziwa manyara wapo hatarini kutoweka, hii ni kwasababu ya matumizi ya mbolea za viwandani na viuatilifu kwenye kilimo katika mazingira yanayozunguka mbuga hii.

Siku hizi kumekuwa na matumizi makubwa sana ya mbolea na madawa ya kilimo katika kuongeza uzalishaji mashambani, baada ya kupuliziwa na kuwekwa ardhini mvua zinaponyesha kemikali hizi husombwa na maji hasa kutoka sehemu za miinuko. Maji haya ambayo mwisho wake huishia kwenye ziwa Manyara na kuchafua maji ya ziwa hili.

Ndege kadhaa hutumia maji ya ziwa hili ambalo lina magadi, wakinywa maji haya yenye kemikali hizo husababisha mapungufu kwenye mfumo wa umeng'enyaji chakula na madini aina ya kalsiam na fosforasi ndio huathirika. matokeo yake ni kwamba ndege hawa hutaga mayai ambayo maganda yake huwa dhaifu na kuathiri utotoaji wa vifaranga vya flamingo hawa.

Kutokana na athari hizi za mabadiliko katika ubora wa maji ya ziwa hili ni kwamba viumbe wote wanaotegemea ziwa hili kwa njia moja au nyingine nao wataathirika hasa baada ya kutokea athari za kiekolojia, kwa kawaida viumbe duniani huishi kwa kutegemeana na kwenye mfumo huu kiumbe kimoja tu kikiathirika maana yake ni kwamba viumbe wengine tegemezi wote wataathirika.
Ushauri muhimu ni kuendeleza kilimo cha asili kwa kutumia mbegu za asili, mbolea vunde au samadi za wanyama na pia kutumia dawa za asili kama utupa, muarobaini na pilipili kwa ajili ya kuulia wadudu waharibifu au kutumia njia za kibailojia kama sukuma vuta ili kukabiliana na wadudu waharibifu mashambani



Thursday, April 11, 2013



JKT (842 KJ) MLALE SONGEA NA JUHUDI ZA KILIMO KWANZA

Katika jitihada za kukabiliana na tatizo la wakulima kuuziwa mbegu za mahindi zisizofaa, kikosi cha Jeshi la Kujenga Taifa (JKT) 842 KJ Mlale cha Songea mkoani Ruvuma, kimeanza uzalishaji wa mbegu za zao hilo ambazo zitakuwa mkombozi kwa wakulima wa Nyanda za Juu Kusini.

Mradi huo utawasaidia wakulima kulima mazao yao kwa uhakika na kwa utaalamu zaidi na kupata mavuno mengi na kuongeza kipato. Bwanashamba wa kikosi hicho Luteni Jackson Otaite, anasema kikosi kinajihusisha na kilimo cha mbegu za mahindi, mahindi ya chakula na kulima bustani za mbogamboga. “Mahindi yameuzwa kwa mkopo kwa Kampuni ya Highland Seed Growers ambayo ndiyo tuliingia mkataba kwa sababu kampuni hiyo haina fedha kwa sasa na bado thamani haijulikani kwa kuwa bado yanaendelea kuchambuliwa Kiwandani,” anasema. Anafafanua zaidi kuwa wanatarajia kuvuna tani 400 za mahindi ya chakula, tani 200 za mahindi ya mbegu na tani 25 za alizeti na mazao yote yanakadiriwa kuwa na thamani ya Sh330 milioni. Luteni Otaite anaeleza zaidi kuwa kikosi kimelima ekari 2.5 za mazao ya bustani na walivuna mbogamboga walizouza Sh7 milioni.

Anasema aina ya mahindi inayozalishwa na Mlale JKT ni Hybrid (H614) ambayo kukomaa baada ya miezi mitano na punje zake ni ngumu na haziliwi kirahisi na wadudu waharibifu, zinavumilia ukame na huzaa mahindi mawili kwa kila mmea na hutoa mavuno kati ya tani 1.5 hadi 2 kwa ekari. “Naiomba Serikali iongeze jitihada zaidi ya kuangalia uwezekano wa kupunguza bei za pembejeo za kilimo zikiwemo mbolea ambazo kwa sasa bei zake ziko juu sana,” anasema Luteni Otaite.

Kamanda wa kikosi hicho Meja Thomas Mpuku ameiomba Serikali kuanzisha utaratibu wa kutoa mbolea za ruzuku kwa vikosi vya JKT ili vizalishe mazao ya chakula na biashara kwa wingi pamoja na mahindi ya mbegu. Meja Mpuku, ameitaka Serikali kuwapa ruzuku za pembejeo ili waongeze uzalishaji badala ya utaratibu wa sasa wa kutoa ruzuku kwa wakulima pekee bila kuangalia wadau wanaowazalisha mbegu. Anasema baadhi ya matatizo ni upungufu wa wataalamu wa kilimo, kupanda kwa gharama za uzalishaji, uchakavu wa maghala, mchwa wanaoshambulia mahindi na kucheleweshwa kwa malipo.

JKT kuongeza uzalishaji
Anabainisha kwamba mipango ya baadaye ya kikosi hicho ni kuongeza ukubwa wa shamba kutoka ekari 650 hadi 800. Pia kupanua eneo la kulima bustani kutoka ekari 2 .5 hadi ekari 5 na kujenga bwawa litakalotumika kwa umwagiliaji. Mkuu wa Wilaya ya Songea Joseph Mkirikiti amekipongeza kikosi hicho kwa jitihada hizo ambazo zinaonekana kuwa mkombozi wa kilimo. “Nimevutiwa na miradi yote ya maendeleo niliyoiona, nawatia moyo mkazane na jitihada hizo mtafika mbali, kwani miradi yenu ni madhubuti na hii iwe chachu kwa wanaohitimu, mkirudi majumbani kwenu mkawe mfano wa kuigwa kwa kilimo bora,” anasema Mkirikiti.

Wednesday, April 10, 2013

KUMUANDAA MNYAMA KABLA YA KUCHINJWA - STUNNING






Hii ni njia inayotumika kumuandaa mnyama kabla ya kuchinjwa, nia kuu ya stuning ni kumpunguzia mnyama maumivu wakati wa kuchinjwa, pia huondoa uwezekano wa mnyama kumuumiza mchinjaji na mwisho ni kuongeza ubora wa nyama.

Zipo njia nyingi au vifaa vingi vya kumuandaa mnyama kabla ya kuchinjwa lakini leo nitaongelea kifaa kijulikana cho kitaalam kama CAPTIVE BOLT PISTOL/GUN. Hiki ni kifaa kama bunduki ndogo ambapo ndani huwekwa baruti maalum au hutumia nguvu ya upepo ambayo ukifyatua kuna chuma imara chenye ncha kali  mbele (bolt)kina toka mara moja na kurudi ndani.

Boriti hii inakazi moja tu ya kutoboa sehemu ya mbele ya ubongo wa mnyama na kumfanya abung'ae na kupoteza fahamu, hii hurahisisha zoezi la uchinjaji na kufanya mnyama achinjwe bila kusikia maumivu yoyote. Kila mnyama anasehemu maalum ya kufanya stunning kama inavyoonyeshwa hapo kwenye michoro ya makala hii
http://www.youtube.com/watch?v=nr00arV2XIw kwenye link hii ya you tube unaweza kuona jinsi zoezi hili linavyofanyika kwa kutumia mashine maalum ya upepo

Tuesday, April 9, 2013

KILIMO BORA CHA VIAZI VITAMU

Utangulizi
Viazi vitamu ni moja kati ya mazao makuu ya mizizi nchini Tanzania ambalo hulimwa kwa ajili ya chakula. Zao hili ni moja kati ya mazao ya kinga ya njaa kutokana na sifa yake ya kuvumilia ukame. Zao la viazi vitamu, asilia yake ni Amerika ya Kati na ya Kusini. Nchini Tanzania, zao hili hulimwa zaidi katika mikoa ya Mwanza, Shinyanga, Dodoma, Morogoro,Kagera,Arusha na Ruvuma.

Matumizi
Viazi vitamu hutumika kama chakula kwa kutayarishwa katika njia mbalimbali kama vichembe, na Matobolwa. Pia Unga wa viazi vitamu hutumika kutengeneza vyakula kama keki, maandazi, kalimati na tambi. Majani ya viazi huliwa kama mboga pia hutumika katika kutayarisha mboji.

Aina za viazi vitamu
Kuna aina nyingi za viazi vitamu zinazolimwa ulimwenguni. Hapa nchini Tanzania aina zinazolimwa zaidi ni Ukerewe, Simama, Kakamega, Karoti C, Mwananjemu, Ali mtumwa mayai, Mavuno, Pananzala, Kibakuli, Sinia,Vumilia na Polista

Uzalishaji
Zao hili hustawi maeneo mengi Nchini Tanzania. Viazi hustawi vizuri katika maeneo ya tambarare yenye udongo tifutifu, unaoruhusu maji kupenya kwa urahisi. Udongo wa mfinyazi na wenye kokoto nyingi haufai kwani huzuia mizizi kupenya na kupanuka.

Shamba jipya litayarishwe vizuri kwa kufyeka vichaka na kung’oa visiki. Majani yafukiwe wakati wa kutengeneza matuta ili kuongeza rutuba ya udongo.

Viazi vipandwe kwa kutumia Marando yenye urefu wa sentimita 30 kwa mavuno bora. Inashauriwa kutumia sehemu ya juu ya shina kwa mavuno zaidi. Marando yapandwe katika umbali wa sentimita 25 hadi 30 kutoka mmea hadi mmea na sentimita 60 hadi 75 kutoka tuta hadi tuta. Viazi pia vyaweza kupandwa kwa kutumia viazi vyenye afya vyenye uzito wa kati ya gramu 20 hadi 30. Hata hivyo inashauriwa kutumia marando ili kupata mavuno zaidi na kuepuka kuenea kwa magonjwa.

Kutunza shamba
Ni muhimu kupalilia viazi vitamu katika miezi miwili ya mwanzo ili kuupa mmea nguvu ya kutambaa vizuri. Baada ya muda huo, viazi huweza kufunika ardhi na hivyo huzuia uotaji wa magugu.

Viazi hushambuliwa na wadudu mbalimbali wakiwemo kipepeo, mbawa kavu, fukusi na minyoo fundo.Pia hushambuliwa na magonjwa yakiwemo magonjwa yanayotokana na virusi kama Sweet Potato Chlorotic Stunt virus (SPCSV). Magonjwa na wadudu yaweza kudhibitiwa kwa kuzingatia usafi wa shamba, kubadilisha mazao, na kuzingatia udhibiti sango.

Uvunaji
Viazi vitamu huwa tayari kuvunwa miezi mitatu hadi minne tangu kupanda kutegemea hali ya hewa. Viazi vinaweza kuvunwa kidogo kidogo kwa kutumia mikono, vijiti, jembe, au rato kadri vinavyohitajika. Aidha inashauriwa viazi visiachwe ardhini muda mrefu bila kuvunwa kwani vitakomaa sana na kuwa na nyuzi, na hivyo kuharibu ubora wake. Pia kuacha viazi muda mrefu hukaribisha mashambulizi ya wadudu kama fukusi na kuoza. Kwa maeneo makubwa zaidi, inashauriwa kutumia mashine ya kukokotwa na ng’ombe. Uvunaji ufanywe kwa uangalifu ili kuhakikisha viazi visikatwekatwe wala kuchubuliwa wakati wa kuvuna.

Mavuno ya viazi hutofautiana kulingana na aina, hali ya hewa, na udongo. Mavuno ya viazi yanakadiriwa kufikia tani 20 kwa hekta


Tuesday, September 18, 2012

SABABU ZA KASUKU/CHIRIKU KUJINYOFOA MANYOYA

SABABU

1 - Lishe duni, upweke na kukosa matunzo ya jumla

2 - Kama atakuwa anatafuna kucha zako unapomshika

3 - Viroboto au utitiri

4- Maambukizi ya bakteria au fangasi

5 - Banda dogo sana

6 - Lishe yenye vitamini A kwa wingi zaidi

NINI KIFANYIKE
1 - Hakikisha ndege wako anapata mlo kamili, unaweza kununua chakula kwenye maduka au ukachanganya mwenyewe baada ya kupata utaalam, apate matunzo yote muhimu na pia asiwe mwenyewe ni vizuri ukafuga dume na jike.

2 - Kama unatabia ya kumshika ndege wako hakikisha unavaa kitu cha kukinga asiweze kula kucha zako kama vile gloves

3 - Viroboto na uttiiri vidhibitiwe kwa kutumia dawa maalum kama vile akheri powder

4 - Maambukizi ya bakteria na fangasi yadhibitiwe mara moja kwa kutumia dawa kama ancobal

5 - Hakikisha ndege wako anaishi kwenye banda lenye ukubwa wa kutosha

6 - Punguza vyakula vyenye vitamini A kwa wingi kama vile karoti na mapapai

Tuesday, September 11, 2012

KILIMO BORA CHA MIHOGO


Zao la muhogo ni  muhimu sana kwa Tanzania zaidi kwa wakulima wadogo wenye kipato cha chini. Wakulima wengi huchanganya zao la muhogo na mazao mengine kama vile kunde, mbaazi, njugumawe, n.k. Umuhimu wa zao hili ni kutupatia cahakula na wakati mwingine kwa biashara. Kwa kanda ya kusini muhogo ni chakula kikuu ambacho kinachukua asilimia 75 ya chakula kwa maeneo yote ya mikoa ya pwani

Muhogo hustawi vizuri katika maeneo yaliyopo kwenye maeneo ya mita 0 – 1500 kutoka usawa wa bahari. Vile vile muhogo hustawi vizuri kwenye maeneo yanayopata mvua ya wastani wa mm 750  - mm1200 kwa mwaka. Muhogo hustawi vizuri kwenye ardhi ya kichanga. Vili vile zao la muhogo ni maarufu sana kwa uvumilivu wa hali ya ukame.

TEKNOLOJIA ZILIZOPO
  1. Mbegu bora za muhogo
Mpaka sasa hivi kuna aina mbili za mbegu bora ambazo zimathibitishwa kwa wakulima. Mbegu hizi huvumilia magonjwa, (batobato na matekenya), pia huzaa sana ukilinganisha na mbegu za kienyeji.
    • Naliendele
                 Huzaa tani 19 kwa hekta moja, na inaweza kuvunwa kuanzia miezi 9 toka ipandwe.


    • Kiroba
Huzaa tani 25 – 30  kwa hekta moja, na inaweza kuvunwa kuanzia miezi 9 toka ipandwe.

  1. Mbinu bora za kilimo cha muhogo
    • Uandaaji wa shamba
Shamba liandaliwe kabla ya msimu wa kuanza. Uandaaji wa shamba bora hufuata hatua zifuatazo:
- Kufyeka shamba
- Kung’a na kuchoma visiki
- Kulima na kutengeneza matuta
·         Uchaguzi wa mbegu bora za kupanda
Mbegu zinatakiwa zisiwe na magojwa yeyote, pia chagua mashina ambayo yamelomaa vizuri.
·         Upanadaji
Kuna njia tatu za upandaji wa muhogo:
-          Kulaza ardhini (Horizontal)
-          Kusimamisha wima (Vertcal)
-          Kuinamisha ( Inclined/Slunted)

Urefu wa kipande cha shina cha kupanda:
 Inashauriwa urefu uwe sm 30; lakini urefu wa kipande cha kupanda unategemea sana idadi ya macho yaliyopo kwenye hicho kipande, inashauriwa kipande kiwe na macho (4 – 6).

Nafasi ya kupanda:
Kwa upandaji wa shamba muhogo tupu, shina hadi shina ni mita 1 na mstari hadi mstari ni mita 1.Kwa shamba la mchanganyiko na mazao mengine, inategemeana na zao linalochanganywa; mstari hadi mstari ni mita 2 – mita 4 na shina hadi shina ni mita 1.


·         Palizi:
-          Palizi ya kwanza ifanyike mapema (mwezi 1) baada ya kupanda ili kuepukana na magugu yanayochipua haraka baada ya mvua kunyesha. Ndani ya miezi mine ya mwanzo mihogo haitakiwi kuwa na magugu ili kuepuka ushindni wa mahitaji muhimu (mwanga, mbolea, maji, n.k) kati ya muhugo na magugu.
-          Palizi hufanyika kwa kutumi jebe la mkono au dawa ya kuuwa magugu.
-          Wakati mwingine udhibiti wa magugu kufanyika kwa kutumia majani kwa kutandazwa juu ya udongo.
-          Plaizi hufanyika mara 2 – 3 hadi muhugo kukomaa.

·         Uvunaji:
Mihogo inaweza kuanza kuvunwa baada ya miezi 9 – 12 tangu kupandwa. Inashauriwa kuvuna katika katika kipindi cha jua; kwani wakati wa mvua kiwango cha wanga kwenye muhogo hupungua.

·         Usindikaji bora
Usindikaji bora wa muhogo unafanyika kwa sababu kuu mbili:
-          Kurahisisha/kuharakisha ukaushaji
-          Kuondoa sumu (cyanide) ilyoko kwenye baadhi ya aina za mihogo
-          Kuongeza ubora wa unga utokanao muhogo wenyewe.

Njia bora za usindikaji
-          Kwa kutumia mashine aina ya Grater
Hii hutoa chembechembe laini za muhogo, ambazo baadae hukamuliwa kwa kutumia kifaa kingine kiitwacho “presser” ili kuondo sumu iliyoko kwenye muhogo. Mashine hii hutumika hususani kwa muhogo mchungu.
-          Kwa kutumia mashine aina ya chipper
-          Mashine hii hutoa vipande vidogo vidogo (chips). Mashine hii hutumika hasa hasa kwa ajili ya mihogo mitamu/baridi.

Matumizi ya Muhogo
-          Muhogo unaweza kupikwa wenyewe kama chakula au kutengeneza unga
-          Unga wa muhogo unaweza kutengeneza vitu vyotekama vinavyotengenezwa na unga wa ngano kama vile biskuti, chapatti, maandazi, chichili, keki n.k.
-          Pia muhogo huweza kutumika viwandani kutengeneza bidhaa nyingine kama vile wanga.

  
iii         MAGONJWA NA WADUDU WAHARIBIFU
·         Magonjwa
Kuna magonjwa mawili ambayo ni muhimu sana na yanapunguza uzalishaji wa zao la muhogo.
a) Ugonjwa wa Matekenya au Ugonjwa wa michirizi ya kahawia
      katika    muhogo
  Ugonjwa huu ni maarufu kwenye sehemu zenye miinuko iliyo na urefu  chini ya mita 300 na unapatikana kidogo sana kwenye miinuko ya mita 500 na kuendelea ambako uenezaji wake wa kawaida hautokei kabisa.

            Visababishi:
            Matokeo ya uchunguzi wa awali unaonyesha kwamba ugonjwa huu ulienezwa na mdudu mweuupe au inzi mweupe (whitefly) mwenye mabawa madogo.

Dalili za Ugonjwa
Sehemui zote za muhogo zinaweza kuonyesha dalili za uambukizo wa ugonjwa huu lakini ni vipengele gani vya ugonjwa na ni kwa kiwango gani hutegemea hali ya mzingira, hatua ya kukua kwa mmea kwa kulinganisha.

-          Kwenye majani
Dalili ya kwanza: Chlorosis rangi ya njani hutokea kwanza pembezoni mwa vena ndogo baadae huathtiri vena ndogo zaidi na inaweza kuwa doa (chlorosis) la rangi ya njano.
Dalili ya pili: Rangi ya njano ambayo haihusishwi vizuri na vena isipokuwa katika mbaka ya mviringo kati ya vena kuu kwenye hatua za mwisho za ugonjwa sehemu kubwa ya lamin inaweza isiathirike, majni yenye ugonjwa hubaki yameshikilia kwenye mmea kwa muda wa wiki kadhaa.

-          Kwenye shina
Huonekana kwenye tisu ya shina changa la kijani, jeraha la zambarau au kahawia linweza kuoneakan nje na kuingia ndani hadi kwenye gamba baaada ya kubandua gome la nje. Pia jeraha la nekrotiki kwenye kovu la shina hutokea baada ya majni kudondoka kutokana na umri wa mmea. Tawi/shina hufa kuanzia kwenye nch kuelekea chini na kusababisha kufa kwa mmea wote.

-          Kwenye mizizi
Kwa kawaida hutokea baada ya dalili za majani na wakati wa kipindi kati ya uambukizo na kufa, amabpo kifo cha mizizi hutokea kuanzia miezi 5 toka kupandwa. Dalili za mizizi zinabadilika nje ya mizizi na zinaweza kuwa kama kizuizimwanga au shimo au kufa kwenye gome.

Tishu inayo zunguka mshins ina doa la rangi ya kahawia au nyeusi. Wakati mwingine mizizi huonekana kuwa yenye afya kwa nje bila kuwa na matatizo yaliyowazi au bila kupungua ukubwa, lakini ikikatwa huonekana kufainakufa au rangi ya njano.

Uambukizaji na ueneaji

Ugonjwa wa CBSD unaambukizwa kwa njia ya vipandikizi vinavyotokea kwenye mimea iliyoathiriwa vinavyosababisha mmea kuonesha kwenye majani dalili za ugonjwa.
Kwa kuwa muhogo kwa kawaida huzalishwa kwa njia ya vipandikizi ugonjwa huu huingizwa kwenye sehemu mpya zilizopandwa kwa kutumia vipandikizi vilivyoambukizwa.
Kwa aina zinazovumilia sana kwenye hali za mabondeni, dalili mbaya sana hutokea wakati ugonjwa ukigundulika  katika hatua za mwanzo.
Uchunguzi umeonesha kwamba Bemisia afer ni mdudu/kisababishi ambacho ndicho kinachohusiana na maendeleo ya hivi karibuni kuhusu uhamishaji wa visababishi kama “ipomovirus”. Mara nyingine inaonesha nzi weupe (White flies) na kutokana na hali hiyo bado uchunguzi unaendelea zaidi.

Udhibiti/Kuzuia
ü  Njia ya msingi ya kuzuia/kudhibiti ugonjwa wa CBSD ni kuchagua mbegu kutoka kwenye mimea isiyo na dalili ya ugonjwa.
ü  Ubora wa mashina unahitaji kutunzwa kwa kuendelea kuchagua na kuangamiza ile iliyoambukizwa ambayo inaonekana wakati wa kuchipua.
ü  Hakikisha kuwa unapanda mbegu bora za mhogo ambazo zinastahimili uambukizo wa magonjwa.
ü  Hakikisha kuwa wakati wa uvunaji uonapo hali ya kuoza kwa mizizi ya mhogo ichome moto ili kutokomeza ugonjwa huo.
ü  Kuelewa dalili za ugonjwa wa CBSD kwa ajili ya kuchukua tahadhari ya kutokomeza ugonjwa huu.
ü  Hakikisha kuwa unaendelea kutunza mbegu bora zinazoonekana kuvumilia magonjwa sana.
ü  Hakikisha kuwa shamba la mhogo linakuwa safi kwa ajili ya kupunguza visababishi vya ugonjwa wa CBSD
      


b) Ugonjwa wa batobato au ukoma wa majani
      Ni ugonjwa ambao ulienezwa kwamara ya kwanza hapa Tanzani mwaka 1894, na baadae uliripotiwa katika nchi nyingine nyingi za Afrika Mashriki, Afrika Magharibi na Afrika ya Kati na sasa unafahamika kuwa upo maeneo yote yanayolimwa muhogo Afrika.

Katika viwango vya kuwepo kwa ugonjwa wa CMD na katika uwingi wa hasara zinazopatikana kutokana na CMD ni kati ya 15% – 20%. Hii ni sawa na tani milioni 15 – 18 zikilinganishwa na makadirio ya shirika la kilimo na chakula  duniani ya tani milioni 85 ya mwaka 1997.

Visababishi
Tangu ugonjwa wa CMD ulipoenezwa kwa mara ya kwanza, visababishi vilichukuliwa  kuwa ni virusi kwa sababu ya kukosekana kisababishi kingine. Kwa hiyo kutokana na kuwa mtazamo huu unalingana na matokeo ya uchunguzi wa awali inaonesha kwamba ugonjwa huu huenezwa na nzi mweupe (white fly).
Pia uchunguzi wa mara kwa mara umesababisha utambuzi wa virusi vya aina mbalimbali na tofauti kama ifuatavyo:
·         Ugonjwa wa batobato unaosababishwa na virusi vya Africa cassava mosaic virus
·        Ugonjwa wa batobato unaosababishwa na virusi vya Afrika mashariki (East Africa cassava mosaic virus)
·         Ugonjwa wa batobato unaosababishwa na virusi vya India (Indian cassava mosaic virus)


                  Dalili za ugonjwa wa batobato (Cassava Mosaic Disease-CMD)
                  
                  Dalili hutokea kwenye jani lenye uwaraza wa michirizi ambazo huathiri         
                   Sehemu zisizokunjamana za kutolea hewa na hufahamika katika hatua za    
                  Awali za ukuaji wa jani.
                  Sehemu za kloritiki hushindwa kutanuka hadi mwisho, hivyo mvutano unaji-
                  tokeza kutokana na ukuaji usiolingana na jani au majani madogo yaliyoharibika.
                
                  Majani yaliyoathirika sana hupungua ukubwa wa umbo, na hujikunja na kujitenga kwa
                  Sehemu zenye rangi ya njano na zenye rangi ya kawaida ya kijani.
                  Mmea hudumaa na majani machanga hupatwa na uvimbe.
                  Kloritiki ya jani inaweza kuwa ya rangi ya manjano nyepesi au rangi inayokaribia nyeupe
                  yenye kijani kidogo au kupauka kuliko ilivyo kawaida.

                 Uambukizaji na uenezaji
                  Ukoma wa mhogo huambukizwa kwenye vipandikizi vya shina ambavyo kwa kawaida
                  hutumika kuzalishia mmea.
                  Pia huenezwa na inzi mweupe (white fly) aitwae Bemisia tabaci G. Aina mbili za inzi au
                  Mbu hao Bemisia (Preisner Hhosny na Aleorodius disperses R) pia huambukiza mihogo
                  katika nchi za Afrika na India
                  Usambazaji wa vipandikizi unaweza kusababisha kuenea kwa ugonjwa wa CMD katika
                  Maeneo mapya.



                
 UHIBITI NA KUZUIA
                  -Hatua ya msingi ya kuzuia ugonjwa wa CMD ni kwa kuchagua vipandikizi kutoka kwa
                   Mmea ambao hauna uambukizo wowote.
                  -Ubora wa mashina unahitajika kwa kuendelea kuchagua na kuangamiza kwa kung’oa ile
                   Mihogo iliyoambukizwa ambayo inaonekana wakati wa kuchipua
                  -Hakikisha kuwa wakati wa kuvuna mihogo kwa ile iliyoathirika na ugonjwa wa CMD
                   inaangamizwa kwa kuchomwa moto.
                  -Hakikisha kuwa unatunza shamba na kuwa safi ili kupunguza wadudu waenezao CMD.
                  -Hakikisha una elimu ya kutosha juu ya dalili za ugonjwa wa CMD>

·         WADUDU NA WANYAMA WAHARIBIFU
-          Cassava Mealy Bug (CMB)

Wadudu hawa hushambulia kwenye ncha za mashina/matawi kwenye majani machanga. Athari zake ni kwamba majani ynadumaa na kujikusanya pamoja, hivyo basi kupunguza ukuaji wa mmea kwa ujumla. Vile vile urefu kati ya pingili na pingili huwa fupi sana.

-          Cassava Green Mites (CGM)

Wadudu hawa hushambulia majani mapya sehemu za chini. Madhara yake sio makubwa.

-          White Scales


Hawa ni weupe na hujishika kwenye shina na kufyonza maji kutoka kwenye mti wa muhogo. Vili vile wadudu hawa madhara yake sio muhimu.

-          Mchwa
Hawa hutafuna/hula mashina ya muhogo hasa wakati wa jua kali/kiangazi.
-          Wanyama waharibifu
Hawa hushambulia muhogo ukiwa shambani kwa kuula, kama vile nguruwe, panya, wezi, n.k

Udhibiti/Kuzuia
Kwa upande wa wadudu wanweza kudhibitiwa kwa njia zifuatazo:
ü  Kutumia dawa za kuulia wadudu
ü  Kutumia wadudu marafiki wa wakulima
      Kwa upande wa wanyama ni kuweka walinzi.