Hupendelea kwenye maji yenye kina kifupi au yasiyotembea, kama kwenye vijito na mito, mabwawa, majaluba ya mpunga na sehemu yoyote ambayo maji hujikusanya. Hukua hadi sentimeta 30 (urefu wa rula ya mwanafunzi) hana magamba kama kambale wengine bali ngozi yake huwa na ulenda ulenda unaomsaidia atembeapo nchi kavu, ana rangi ya kijivu mpaka kahawia iliyokolea kabisa. Tofauti na yake na kambale wengine yeye hana mapezi ya kwanza juu ya mgongo bali pezi lake la pili huwa refu mpaka karibu na mwisho wa mkia, unapomvua kambale huyu usimshike akiwa hai au hata kama kafa mshike kwa umakini sababu ana miiba iliyojificha kwenye mapezi ya chini karibu na mkia

Hupendela halijoto kati ya 10c mpaka 28c, chakula chao kikuu ni samaki wadogo, wadudu, konokono wasio na magamba na mimea ya kwenye maji, kambale hawa wanatabia ya ulafi inayowafanya wawe hatari kwa viumbe wengine wa kweye maji

5 comments:
Habari nzuri, lakini hao samaki mbona wanatisha!!
Upepo mwanana hujawahi kuwaonja tu. hasa ukute waliokaushwa wa kutoka ifakara huko, na mpunga mpya. utaacha michips hiyo. usisahau nazi kwenye wali.
Hahahahaaa John. No wonder profile photo yako unacheka.
Asante kwa mara ya tena Kaka Benett lwa uelimishaji huu.
Kwa hiyo huyu ndiye apendaye na awezaye kuishi kwenye tope zaidi?
Upepo mwanana ni kweli samaki huyu anatisha lakini sio sana
JM hawa samaki kwa kweli ni watamu sana kwa wasafiri wa kuja DSM wanaweza kuwanunua pale Ruvu darajani
Mzee wa changamoto kambale wote huweza kuishi kwenye tope pale ambako maji hukauka kwa ukame, lakini huyu ninaye mwongelea yeye anaweza kuhamia bwawa au dimbwi lolote lili karibu na alipo kama maji yatakauka
kaka leo nimeanza kuchimba bwawa la kufuga samaki.naomba unishauri pa kupata mbegu bora za samaki. pia nna shamba langu mkuranga ningependa kufuga huko samaki pia bila kusakafia bwawa any advice?
Post a Comment