KURASA

Wednesday, June 27, 2012

KILIMO BORA CHA MIPAPAI


MAHITAJI
Hali ya  hewa inayofaa kwa mipapai ni ya kitropik ambayo haina baridi kali na joto kiasi . Udongo usiotuamisha maji maji yakisimama kwa masaa 48 tu mpapai unaweza kufa, wenye ruruba ya kutosha kwa sababu mipapai haina mzizi mkuu haihiyaji udongo wenye kina kirefu, kipindi cha jua kali mpapai usiachwe zaidi ya wiki 8 bila kumwagiliwa maji kama hakuna mvua ingawa wakati wa mapapai kuiva kama kuna ukame basi hii huongeza ubora wa papai ikiwamo kutooza mapema sokoni

Mipapai ipandwe sehemu ambazo hazina upepo mwingi kwani huvunjika kirahisi, kama unashamba la mipapai itakubidi kupanda miti ya kukinga upepo kuzunguka shamba lako, miti kama miparachichi, migravilea, vibiriti (leucaena Spp) na miembe pia inafaa. Hakikisha miti ya kukinga upepo inakuwa mirefu kuzidi mipapai kwa mita 10 mpaka 20 juu zaidi

Kuendelea kupanda mipapai kwenye shamba moja kunaweza kusababisha usugu wa magonjwa, nashauri baada ya miaka 3 – 5 ubadilishe zao hili angalau kwa msimu mmoja ili kuua mzunguko wa magonjwa
Mipapai inaweza kuchanganganywa na miembe na mimea jamii ya michungwa, pia mazao ya msimu kama mahindi, mtama, ufuta , alizeti  na  mboga mboga yanaweza kulimwa

Kwa kaida kwenye mipapai kuna mipapai dume, majike  na yenye jinsia zote (multiplesex/hermaphrodite) ambayo huwa na mapapai marefu zaidi, na pia kuna isiyoeleweka ambayo huwa na mapapai mafupi sana

MBEGU
Kusanya mbegu toka kwenye mapai makubwa na yaliyo komaa na kuiva, kausha mbegu vizuri kbla ya kupanda, kama utapata mbegu za  kununua ni vizuri zaidi, baada ya kukausha hakikisha unazipanda ndani ya wiki moja

KUOTESHA MBEGU
Kuna wanaopendelea kuotesha mbegu kwanza na kisha kuhamishia miche shambani, sehemu ya kuoteshea iandaliwe miezi miwili kabla, mbegu zioteshwe kwenye kina kati ya sentimeta 1 – 2 chini ya udongo wenye rutuba au pakiti za plastiki, kiwango bora cha joto ni sentigredi 21 – 27 na itachukua kati ya wiki 1 – 4 kwa mbegu kuota, kwenye kila pakiti weka mbegu 2 – 3. Panda mbegu zako kwenye kitalu kwa umbali wa sentimeta 3 toka shimo hadi shimo na sentimeta 15 kati ya mistari, hakikisha maji hayatuami kabisa, pia unaweza kupiga dawa ya copper oxychloride gramu moja katika lita moja ya maji ilikukinga miche yako na fangasi

UOTESHAJI WA MOJA KWA MOJA
Kabla ya kupanda mbegu weka mchanganyiko wa majivu na mbolea ya kuku sehemu ya kupandia, mbolea husaidia ukuaji haraka na jivu husaidia kukinga mipapai na magonjwa. Panda mbegu 3 – 5 kila shimo maana miche mingine inaweza kufa kwa magonjwa, kuliwa na wadudu au ikaota dume

KUHAMISHA MICHE TOKA KWENYE KITALU
Miche ihamishiwe shambani ikiwa na urefu wa sentimeta 20 – 40, kama udongo unatuamisha maji panda kwenye matuta yenye urefu wa sentimeta 40 – 60 mashimo yawe na ukubwa wa sentimeta 45 upana na sentimeta 30 kina na shimo lichanganywe na udongo na samadi bila kuacha kisahani cha maji, umbali ni mita 3 kwa 3 kwani mipapai inahitaji jua la kutosha

KUPUNGUZA MIPAPAI
Baada ya miezi 3 – 5 baada ya kupanda mipapai itatoa maua na hapo jinsia ya mipapai itajulikana na mingine itabidi ipunguzwe na hasa midume, mipapai yenye jinsi zote inatakiwa isizidi asilimia 10 – 20 na midume ibaki mmoja katika kila mijike 25, mimea yenye magonjwa pia inabidi ing’olewe

RUTUBA YA UDONGO
Weka kiasi chakilo 2 – 5 za samadi kwenye kila mpapai kwa mwaka ili kuongeza ukuaji na uzazi, mabaki ya mimea yanaweza pia kuwekwa kama matandazo na h ii ni muhimu zaidi kipindi cha kiangazi ili kuzuia unyevu usipotee.

MAGUGU
Mipapai inapopandwa tu inaweza kuwekewa matandazo kuizunguka ili kuzuia uoataji wa magugu, magugu yang’olewe yakiwa machanga na epuka kuchimbua chini sana maana mizizi ya mipapai huwa juu juu, njia nzuri ni kuweka matandazo kwenye shamba lote ili kuzuia outaji wa magugu

UANGALIZI
  • Mipapai iangaliwe dhidi ya magonjwa, ing’olewe na kuchomwa au kufukiwa chini ikiwa itabainika kuwa na maonjwa, piga dawa dhidi ya magonjwa ya fangasi na virusi mara yanapoibuka ili kuongeza uzaaji nakipato chako
  • Ondoa matawi yote yatakayojitokeza pembeni ya mpapai wako, na hii ifanyike mapema kabla ya tawi kuwa kubwa.
  • Ondoa mapapi yote ambayo yatakuwa hayakuchavuliwa vizuri na acha yale yenye afya tu
  • Weka miti ya kuegemea kama mpapai utazaa matunda mengi na hasa wakati wa upepo mwingi ili kuzuia mipapai isivunjike
  • Mipapai ikitunzwa inaweza kuishi mika mingi, ila kwa ajili ya mazao bora ondoa mipapai na upande mingine baada ya kila miaka mitatu (3) kwani mpapai unapo kuwa mkubwa basi rutuba yote huishia kwenye mti wenyewe

21 comments:

emuthree said...

Mkuu kwanini wewe usichaguliwe kuwa mbunge, wa `kilimo kwanza' maana hii kilimo kwanza naona kama ngonjera ya kufikirika!

Bennet said...

Nashukuru sana kwa ushauri wako

Anonymous said...

Uncle,

Napenda sana pos zako.

Je, naweza kukupata vipi kwa ushauri zaid juu ya kilimo?

Mr. Primus said...

Papai zao zuri sana na kama ukipanda eka moja kwa 1000 mapapai utapata 1kila wiki, ukiuza 1000 kwa 300 tu ni laki 3 sasa ukiweka eka 5 ni 1.5m kwa wiki...dahhhh....Tanzania nzuri unataka kenda wapi? Lima ww?

wajibu said...

wewe Mr primus umelima? you should lead by example.where is your shamba darasa tuje kujifunza kwa cc wajasilia mali.

Unknown said...

kaka nakukubali cna,
nimegraduate from Sua bt still am learning a lot from ur site,
keep it up !!

Kohelplus said...

napenda post zako, keep it up

Unknown said...

mwaka jana mwezi wa 12 nilipanda papai katika shamba,mpaka hii leo nina mipapai 300 ambayo sasa inatengeneza matunda lakin kuna miti ambayo tayali ilisha zaa na matunfa meng nimeuza na kula...jaman kama unashamba komaa upande mipapai inalipa sana. wakati wa upandaj changamoto ni kidogo cha msing aldh alimwe vizur kwa trecta au ngo'mbe ili udongo uwe lain kwa mizizi ya mipapai ni lain sana haiwezi kupambana na aridh ngumu sana..

Unknown said...

nashkuru mtaalam kwa maalezo yako ila ss wengine ndo kwanza tunataka tuanze ukulima wa mipapai ila sijui nianzeje maana nina eneo la wastani nataka nipande ila naomba maelezo zaidi vipi nianze.

Unknown said...

Yanachukua muda gan kukua

Unknown said...

George
naona una uzoefu tyr,kwenye zao hili kwa sababu unalima tyr,unapatikana wapi wewe nahitaji nione shamba lako nipate elimu zaidi kwa vitendo.

Unknown said...

Hi George
Tunashukuru kwakuwa mwenzetu unao uzoefu wa papai kwasasa mana umeshalima , ombi langu je mbegu bora za papai ulipata wap na kwa bei gan? mana ,kuna makala ya Mkulima mbunifu yeye kazungumzia mbegu ya Red royal F1 ila bei yake pale kuna wadau walisema punje 50 ni elf 18, na Mkilima mbunifu akasema mbegu hii huvunwa mapema zaidi na na mfululizo kwa miaka 5 hadi 7 hivyo tunaomba ushauri kwako ambaye umeshapanda jee umetumia mbegu gan?.

Unknown said...

Pia kuna na mtu nilimpgia cm akanambia gram 50 ya mbegu ya papai anauza 250,000/=, sasa wewe ukitusaidia itakuwa vizuri kujua eka moja unaweza panda miche mingapi.

Paul said...

Watanzania wenzangu wapenda fursa kwa heshima na Taadhima napenda niwapongeze sana kwa kupenda fursa hii ya kilimo pia ningependa kuwakaribisha kwa undani zaidi katika Group letu maalum lifahamikalo kama Bunge la uchumi BU huku utakutana na watekelezaji wa fursa kama hii Kuna spika pamoja na naibu spika wanaotoa mafunzo haya yakinifu zaidi follow my contacts to be directed

Unknown said...

Naomba contact za Hilo group, je ni WhatsApp?

Unknown said...

Mipapai yangu ina kama miezi miwil hv na nusu tokea nipande, na ukubwa wake kwa inayoenda vinzur ni sm kama 50-70 hv, je kwel itakuwa na uwezo wa kuzaa ndan ya miez mitano? Na kama sio tatizo litakuwa ni nini?

Ahsante

khamis said...

Naomba na Mimi kuunganishwa katika hilo group

khamis said...

Naomba na Mimi kuunganishwa katika hilo group

Unknown said...

Asante kwa maelezo mazuri nimekuelewa

Unknown said...

Asante kwa maelezo mazuri nimekuelewa

Wills Tanibali said...

naomba kujiunga na group la kilimo hilo.