KURASA

Saturday, May 24, 2008

MICHE BORA KWENYE KITALU




SPECIE tectona grandis (teak)
SEEDS SOURCE Bombani Muheza Tanga
DATE PLANTED January 2008
AGE 3 moths from germination
GERMINATION RATE 70%
USED SEEDS TREATMENT METHOD deep soaking & changing water after 12hrs for 4 days



Friday, May 23, 2008

KITALU CHA MITIKI














Ninashauri kitalu kiwe karibu na shamba na pia chanzo cha maji kiwe karibu. Kitalu cha mitiki kinaweza kuwa katika tuta lolote lile la juu au la chini, udongo unaofaa ni ule wenye rutuba na usiotuamisha maji. Tuta liwe kwenye sehemu yenye mwanga wa kutosha na kusiwe na kitu kitakachokinga mwanga wa jua, hii ni kwa sababu mbegu na miche ya mitiki inahitaji mwanga wa jua wa kutosha.




UOTESHAJI


Mbegu za mitiki zioteshwe kwa mistari zifukiwe kiasi cha kama sentimeta moja chini ya udongo, hakikisha kwamba mbegu haziwi chini sana ya udongo hii itasaidia katika uchipuaji wa mbegu zako. Nafasi kati ya msitari na msitari ni sentimeta kumi (10).




Uotaji wa mbegu huchukua muda kiasi cha siku 30 - 45, wakati wote huu kabla na baada ya kuota kitalu inabidi kimwagiwe maji ya kutosha angalau mara moja kila siku, maji yamwagiwe taratibu kwa kutumia vyombo vya kuwagilia (watering can) ili kuzuia kuzifukua mbegu zilizopo ardhini. Mara baada ya mbegu kuota ziendelee kumwagiwa maji ya kutosha.




Maara baada ya miche kufikia uefu wa sentimea 8- 10, mbolea za kukuzia zinaweza kuwekwa ili kuhahkikisha miti inakuwa na nguvu, wkati huu unaweza kupunguza kiasi cha maji ya kumwagilia ili kuzuia mbolea kuchkuliwa na maji.




UTUNZAJI


Muda wote hakikisha magugu yanang'olewa ili yasinyang'a nyane chakula na miche yako, hakikisha pia kingo za tuna zinanyanyuliwa muda wote kuzuia upotevu wa maji. Huna haja ya kutandaza nyasi juu ya tutalako kwa ajili ya kuzuia upotevu wa maji, kumbuka mbegu za mitiki zinahitaji mwanga wa kutosha na hewa ili ziweze kuchipua.






Kama utagundua kuna wadudu wanaoshambulia kitalu chako, omba ushauri kwa mabwana shamba dawa gani utumie ingawa ni nadra sana mitiki kushambuliwa na wadudu.




Kwa wale watakaouza miche hii au wanategemea kuisafirisha umbali mrefu, basi itawalazimu kuiweka kwenye vifuko, hii iatahisisha usafirishaji mpaka shambani, ingawa kitaalamu miche ya kwenye vifuko huwa inakufa mingi zaidi na huwa inapindapinda wakati wa ukuaji. Uhamishaji wa miche kwenye vifuko hufanyka wakati miche ina urefu wa sentimeta za wastani 2

Thursday, May 22, 2008

MBEGU

Mbegu za mitiki lazima zikusanywe kutoka katika miti iliyokomaa, hii itasaidia katika uotaji kwa sababu mbegu za miti hii ni ngumu kidogo kuota. Unaweza kupata mbegu kutoka kwenye mashmba makubwa ya miti au ukanunua kutoka kwa wakala wa mbegu za miti wa taifa (TTSA) ambao wana matawi yao katika kanda tofauti nchini (Morogoro, Lushoto na Iringa) http://www.ttsa.co.tz/

Mbegu zilizo bora ni zile zilizohifadhiwa mahali pakavu, kabla ya kupanda mbegu inabidi ziloekwe kwenye maji yanayo tembea kama mto kwa siku 3 (masaa 72) au unaweza kuzitia kwenye gunia na kuloweka kwenye chomba chenye maji kwa masaa 72, huku ukibadilisha maji kila baada ya masaa 8 -12. Hakikisha unapoloweka mbegu, lile gunia unalifunga na kitu kizito kama jiwe ili ziweze kuzama kabasa ndani ya maji.

Kila unapobadilisha maji utagundua kwamba maji unayomwaga yanakuwa na rangi nyekundu, hii ni kawaida kwa miti hii huwa inaacha alama ya rangi nyekundu (red dye) kama utakata matawi yake kwa mkono.

Ukisha maliza kuloweka mbegu kwa masaa yasiyopungua 72, mbegu zianikwe kwenye jua ili ziweze kukauka kabisa. Unaweza kuzianika juu ya bati ili kuharakisha ukaukaji, hakikisha unazi tandaza ili zikauke vizuri, hii inaweza kuchukua hata siku mbili kama hamna jua la kutosha. Mara baada ya kukauka mbegu zikusanywe na kuhifadhiwa mahali pakavu na pasipo na joto tayari kwenda kupandwa kwwenye kitalu.

UTANGULIZI

Watu wengi siku hizi wamekuwa wakijihusisha na upandaji miti katika mashamba binafsi, miti hii ina matumizi mbali mbali ikitumika kama mipaka, chanzo cha kuni, mbao, chakula cha mifugo, urembo n.k.

Miti ya mitiki ni moja ya miti inayotoa mbao ngumu na aghali zaidi duniani, vitu kama boti na mashua, vitako vya bunduki, fimbo za askari, milango na samani mbalimbali za majumbani hutengenezwa kutokana na miti hii.

Mti hii inasifika kwa uimara wa kutoliwa na wadudu kama mchwa na kuoza kutokana na maji kwa sababu ina hali ya mafuta mafuta. Mbao zake zina rangi nyekundu iliyokolea na kama mti litunzwa vituri kwa kupunguziwa matawi mapema, mbao zinakuwa hazina vidoda vidonda.

Kwa hapa nchni mashamba makubwa yanapatikana Kilombero, mtibwa na longuza (Lushoto) pia kuna wakulima wadogo wadogo katika mikoa ya Tanga, Morogoro na Pwani.

Kwa kawaida miti hii hustawi zaidi katika ukanda wa pwani wenye joto na mvua nyingi, hustawi katika udongo wa kitifu tifu wenye mbolea ya kutosha na usio tuamisha maji kabisa. Miti inayopandwa mabondeni inakuwa haaraka sana kuliko iliyopandwa sehemu za miinuko, ingawa miti ilipondwa kwenye miinuko inatoa mbao bora zaidi kutokana na kukua taratibu kidogo.

Uvunaji unaanza baada ya miaka 6-7 kwa kutoa miti ya kujengea ambayo hupatikana kwa kupunguza miti ya kati ili ile inayobaki iweze kukua zaidi. Mbao huanza kuvunwa baada ya miaka 12 - 15, ikifuatiwa na miaka 18. 20, 25, kumbuka uvunaji huu unafanywa kwa kupunguza nusu ya miti (kati ya mti na mti) na kuacha inayobaki iendelee kukua zaidi
.