KURASA

Saturday, October 9, 2010

KITUO CHA KUZALISHA NA KUFUGA SAMAKI KINGOLWIRA - MOROGORO



MSAIDIZI WA BWANA KALINGA akiwalisha kambale kwenye bwawa la kufugia








BUSTANI ya mipapai, maji yakitolewa kwenye mabwawa hutumika kumwagilia bustani hii


BATA akiogelea na kusaidia mzunguko wa oksijen kwenye maji


BWAWA lililochimbwa tayari kwa matumizi, mabanda ya bata na kuku yakiwa pembeni tayari


TANKI LIKIJENGWA


TANKI LA KULELEA VIFARANGA VYA SAMAKI


MTAALAMU BWANA KALINGA AKINIPA MAELEZO


MTAMBO WA KUTOTOLESHEA MAYAI YA KAMBALE MAABARA






MASHINE YA KUSAGIA CHAKULA CHA SAMAKI


CHAKULA CHA SAMAKI


KWA MAWASILIANO NA BW KALINGA
0757891761 au 0787596798
BEI YA KIFARANGA CHA SAMAKI NI KATI YA SHILINGI 30 - 50 KUTEGEMEA UKUBWA

KITUO CHA KUFUGIA SAMAKI MOROGORO MJINI BOMA ROAD

Nilibahatika kutembelea vituo vya ufugaji na uzalishaji wa samaki huko Morogoro mjini barabara ya boma na Kingolwira, mwenyeji wangu alikuwa ni Bwana Melton Kalinga ambapo tulishinda karibia kutwa nzima akinionyesha vitu mbali mbali huku tukibadilishana uzoefu na utaalamu wa kuzalisha samaki, wakati yeye alikuwa akinifundisha namna ya kuzalisha Sato na Kambale, mimi nilimfundisha namna ya kuzalisha samaki wa mapambo hasa Gold fish na Angels

HAPA NI MOROGORO MJINI BOMA ROAD kwenye kituo cha kufugia samaki, kuna mabwawa ambapo samki hufugwa baada ya kuzalishwa katika kituo cha Kingolwira


CHANZO CHA MAJI ni kutoka katika kisima cha kuchimbwa na maji huvutwa kwa pampu ya umeme





BANDA LA BATA kinyesi chao chakula cha samaki, pia wakiogelea husaidia kuingiza hewa kwenye bwawa (aeration)


SEHEMU YA KUWEKEA CHAKULA CHA SAMAKI sehemu hii imejengwa kwa kutumia miti na inahamishika


SEHEMU YA KUWEKEA CHAKULA CHA SAMAKI imejengwa kwa saruji, ni sehemu ya kudumu


BATA pia hufukuza ndege wanaokula samaki na kuwala vyura wala samaki


NDEGE MLA SAMAKI naye alikuwepo