KURASA

Sunday, December 7, 2008

UPANGAJI (AQUARIUM ARRANGEMENTS)

Upangaji wa tank lako ni muhimu ili kuwapa samaki mazingira mazuri kwa matokeo bora, wakati wa kupanga kuna vitu vya msingi na muhimu vya kuzingatia, na kabla ya kununua au kujenga tank lako lazima ujue ni samaki gani unataka kuweka na idadi yao. Baadhi ya samaki kama Goldfish,, Shaks, Koi n.k huwa wakubwa mpaka kufikia futi moja, kwa hiyo wanahitaji chombo kikubwa zaidi.


WATER PUMP
Hii hukaa nje na kusukuma hewa ndani kwa kupitia mawe ya hewa (air stones) ambazo lazima zikae katikati ya tank, pia kuna aina mbali mbali za urembo ambazo nazo zinaingiza hewa, hizi zinaweza kuwekwa kokote ila ni muhimu zisambae ndani ya tank.

WATER FILTER
Ni vizuri kama itawekwa upande mmoja wa tank na kusukuma maji kwa urefu kuelekea upande mwingine, hii husaidia kuweka mzunguko wa maji ambapo chini maji yanavutwa na na juu yanatolewa na pump.

SAKAFU
Sakafu ya tank lako lazima iwe na mchanganyiko wa mchanga na changarawe, ambao hutumika kwa ajili ya mimea kujishikiza. Mchanga na changarawe pia zinatumika kama filter kwa sababu zinachuja uchafu na mabaki ya chakula

MAPAMBO
Hii inajumuisha mimea, urembo na sehemu za kujificha samaki, mapambo yawe ya kutosha ili samaki wajisikie huru kwa sababu inawafanya waone kama wako kwenye mazingira yao halisi



MAJI
Kama unatumia maji ya bomba ni vizuri yawe yamekaa angalau masaa 12 baada ya kukingwa toka bombani. Hii ni kwa sababu huwa yanatiwa chlorine ili kuuyafanya yawe salama kuyanywa, hii chlorine huua samaki. Ukiyaweka wazi kwa masaa zaidi ya 12 chlorine huondoka kwa njia ya mvuke (evaporation), maji wazuri zaidi kutumia ni ya visima vya kuchimba (drilled water wells)kwa sababu yana chumvi chumvi za asili zinazosaidia kuwakinga na magonjwa

baada ya kuweka maji ya bomba kwenye tank unaakiwa uweke chumvi ya mezani kijiko kidogo kwa lita kwa lita 25 za maji, ukianzia na kumuweka samaki mmoja na kumwacha kwa saa zima huku ukimchunguza, ukimwona yuko salama unaweza kuwaweka samaki wote waliobakia

MAJANI NA MIMEA (aquatic plants)

Majani ni kitu muhimu sana katika ufugaji wa samaki, kazi ya majani ni kusafisha maji na kuweka mazingira ya uhasilia kwa samaki, kuna majani ya bandia lakinioiyanabakia kama urembo tu kwa sababu hayawezi kusafisha maji. Ili majani yakue kwa kiwango kizuri ni lazima mahitaji yafuatayo yazingatiwe


MWANGAZA
Mwanga wa kutosha unahitajika kwa ajili ya ukuaji wa majani na mimea ya majini, hii husaidia katika tengenezaji wa chakula kwa kutumia majani yake, mwanga wa tube lights ni mzuri zaidi ila usiwe mwingi sana kwa sababu utachangia ukuaji wa algae kwenye maji. kiwango cha mwanga kinachoshauriwa ni 1.5 watts kwa kila galon ya maji (1.5wpg), mfano tank la galon 20 linahitaji taa ya watts 30




MIZIZI
Mizizi ya mimea na majani inahitaji kujishikiza kwenye sakafu yenye udongo, changarawe au mchanga ili iweze kufyonza virutubisho, inashauriwa usiweke changarawe tu bali uchanganye na mchanga


VIRUTUBISHO
Ili mimea iweze kukua vizuri inahitaji virutubisho kama nitrogen, potasium, phosphorus, chuma na kadhalika, nitogen ambacho ni kirutubisho kikuu kinapatikana kwenye vinyesi vya samaki amabvyo vinatoka kama ammonia. Pia maji yenyewe na chakula cha samakikina madini haya kwa kiasi kidogo



CARBON-DIOXIDE
Hii ndio hewa inayotumiwa na mimea na inapatikana kutokana na samaki wanavyo pumua (respiration). Kwa kawaida samaki wanavuta oxygen na kutoa CO2 ambayo ndio inatumiwa na mimea, wingi wa upatikanaji wa hewa hii ya co2 inategemeana na wingi wa samaki.