KURASA

Wednesday, February 18, 2009

MBILIMBI

MTI WA MBILIMBI (M-MBILIMBI)




Huu ni mmea unaopatikana sana sehemu za pwani kama Zanzibar, Tanga, Dar es salaam, Kibaha n.k Ni mmea ambao hauwezi kuhimili ukame wala baridi kali na unastawi zaidi kwenye mvua za kutosha na udongo usiotuamisha maji kabisa.


MATUMIZI


Miaka mingi mbilimbi zimekuwa zikijulikana kwa matumizi ya achali ndio maana sehemu nyingine mbilimbi zilitungwa jina la PICKLE FRUIT. Utengenezaji wa achali uko wa kuchanganya vitu tofauti tofauti kama nyanya, vitunguu, pilipili, ndimu, malimao, chumvi, maembe n.k ambavyo vinankuwa katika vipande vidogo vidigo, unaweka kwenye chupa na kuanika juani kwa siku kadhaa (ingawa baadhi huupika mchanganyiko huu)

Mbilimbi pia hutumika kutengenezea siki (vinegar) na mvinyo, hii mara nyingi hufanyika viwandani na sio majumbani kama ilivyo achali.

Mbilimbi pia ni dawa kwa magonjwa kama chunusi, kifua na kukohoa na mengineyo mengi. Ili kutibu kukohoa unatakiwa utafune mbilimbi kama tunda mara mbili mpaka tatu kwa siku ukichanganya na chumvi kupunguza ukali wake au unaweza kula mbilimbi zilizoiva ambazo ndio zina vitamin C zaidi ya mbichi. Majani na maua yake ni dawa ya vidonda, unaponda ponda na kufunga kwenye kidonda kwa siku kadhaa, pia yanapunguza uvimbe.

MAUA YA MBILIMBI



Mbilimbi mbichi ambazo ni kali huwa na acid ijulikanayo kama OXALIC kwa kiasi kingi hivyo huweza kutumika kungarishia vitu vilivyotengenezwa na chuma, shaba na aluminium kwa kusugulia na kisha kusafisha na maji safi

Monday, February 16, 2009

ALOE VERA - KINGA YA MALARIA


Sina uhakika na jina halisi la mme huu wengi wanauita SHUBIRI au SHUBIRI MWITU wengine huiita LITEMBWE (nafikiri ni jina la kiluga) kuna makala kadhaa zinasema shubiri ni mti kamili na wala si mmea, kama yuko ambaye anajua kwa uhakika naomba atusaidie.

Naomba mkumbuke kwamba kila ninachoandika humu ni kwamba nimehakikisha ukweli wake labda kwa kuona au kutumia mimi mwenyewe na wala sijasoma sehemu na kisha kuandika humu.

Nitaongelea kuhusu Aloe vera kama kinga ya malaria, kwa sababu mimi mwenyewe nilisha wahi kuwaandalia watu hii dawa na ikawasaidia, kwa mfano kuna ndugu yangu mmoja alikuwa anaumwa na malaria kila baada ya miezi 2 - 3. nilimpa hii dawa dozi moja tu na aliweza kukaa miezi 14 (mpaka leo hii)bila kuumwa malaria

Inasemekena kwamba mmea huu unauwezo wa kutibu magonjwa mengi kama vidonda, muwasho wa ngozi na harara, husaidia kusaga chakula, hupunguza uvimbe, hupunguza kiasi cha lehemu (cholestrol) mwilini na mengineyo


Huu ni mmea maarufu sana duniani kutokana na kuwa na uwezo wa kutibu magonjwa mengi, na pia unapatikana sehemu nyingi za dunia hasa zile ambazo hazina baridi. Vipodozi vingi vya ngozi vinachanganywa na mmea huu ili kuvipa uwezo zaidi wa kutunza ngozi


Mmea huu unatumika zaidi kama majani ingawa shina na mizizi yake nayo ni dawa pia, mmea huu huwa na umbo la kama katani/mkonge au mmea wa nanasi ila wenyewe ni mdogo kidogo na huwa laini zaidi


Majani yake yana sehemu mbili, kuna ganda la nje na maji ya ndani (jelly) ganda la nje lina kemikali za kutibu zaidi na ule utando wa ndani una virutubusho vingi sana ambavyo ni kinga za mwili


KINGA YA MALARIA
Kama unasumbuliwa na homa ya malaria mara kwa mara, chukua majani mawili yaliyo komaa, yaoshe vizuri na kata kata katika vipande vidogo.


Changanya na maji vugu vugu kisha saga kwa kutumia kisagio (blender) au twanga kwenye kinu kidogo, chuja na kisha ongeza maji hadi upate bilauri (jug) nzima, unaweza kuhifadhi dawa hii kwenye friji MATUMIZI kunywa vikombe viwili mpaka vitatu kwa kila siku kwa siku 5 - 7. Hii itakusaidia kuongeza kinga ya mwili wako maradufu na unaweza kurudia dozi hii mara baadda ya miezi 3 - 4.