KURASA

Wednesday, May 13, 2009

UFUGAJI WA SAMAKI WA CHAKULA KWENYE BWAWA-SEHEMU YA KWANZA

BWAWA LA KUCHIMBA KWA AJILI YA SAMAKI WA CHAKULA


Ufugaji wa samaki ni kama ufugaji mwingine wowote wa wanyama, kwa sababu wanahitaji uangalizi kama wanyama wengine mfano vitu kama kula, usafi, tiba na mengineyo yote yanahitajika kwa ajili ya ufugaji wa samaki

VITU MUHIMU
Baada ya kuamua kufuga samaki ili kuchagua sehemu ya kufugia ni lazima uzingatie mambo yafuatayo
(a)MAJI- Ufugaji wa samaki unahitaji maji mengi ya kutosha kwa hiyo sehemu ya kufugia lazima iwe na chanzo cha uhakika cha maji kwa mwak a mzima, vyanzo kama ziwa, bwawa, mto, kisima ni vyanzo vizuri sana lakini maji ya bomba hayawezi kutumika moja kwa moja kwa sababu huwa yanatiwa dawa ya chlorine ambayo huua samaki. Ukitaka kutumia maji ya bomba ni lazima uyakinge kwanza sehemu kama kwenye matanki yakikaa kwa masaa kama 12 chlorine huondoka. Tatizo la maji ya mto, ziwa na bwawa ni maambukizi ya magonjwa kwa samaki.

BWAWA LA ASILI


(b)UDONGO- Sehemu utakayochagua kwa ajili ya bwawa lako la samaki lazima iwe na udongo unaotuamisha maji ili kuzuia upotevu wa maji na kupunguza gharama za uendeshaji, unaweza pia kujenga kwa simenti

(c)MAFURIKO-Sehemu ya bwawa isiwe ambayo inaweza kupatwa na mafuriko kila msimu wa mvua sababu samaki wataondoka na mafuriko, pia magonjwa na kemikali zisizohitajika zitaingia bwawani na kuua samaki wako

BWAWA LILOJENGWA KWA AJILI YA SAMAKI WA UREMBO


(d)JOTORIDI-Ni muhumu kujua aina ya samaki unaotaka kufuga kama wataweza kuishi kulingana na kiasi cha joto cha sehemu husika.

(e) MIPANGO YA BAADAE- Seehemu husika lazima iendane na mipango ya baadae hasa kama unampango wa kutanua ufugaji wako, ni muhimu mradi uwe sehemu moja kupunguza gharama za usimamizi

MFANO WA BWAWA LILOJENGWA KWA AJILI YA UZALISHAJI WA SAMAKI WA CHAKULA