KURASA

Tuesday, August 13, 2013

UMUHIMU WA MAJIVU KWENYE UDONGO WA BUSTANI

Watu wengi wamekuwa wakiulizia umuhimu wa madini kwenye udongo na namna ya asili ya kuongezea kosefu wa madini kama potasiam, fosforas, kalsiam na mengineyo, njia rahisi ya kuongeza baadhi ya madini kwenye udongo ni kwakutumia majivu

UMUHIMU
Majivu yanakiwango cha wastani wa madini kifuatacho potasiam 5% - 7%, kalsiam 25% - 50%, fosforas 1.5% - 2% na madini mengine kwa kiasi kidogo pia mabaki mabaki ya chenga za mkaa kwenye majivu pia yanasaidia kwenye kunyonya baadhi ya sumu kwenye ardhi, kumbuka mkaa ni kaboni halisi (pure carbon)

KIASI CHA KUTUMIA
Kiasi cha kilo 2.5 mpaka 5 kitumike kwenye eneo la mita za mraba 33 au futi 100 za mraba, na majivu yamwagwe wiki 3 - 4 kabla ya kupanda kitu chochote ardhini.

MADHARA
Kila kitu kikitumiwa zaidi ya kiasi kina madhara na majivu pia yana madhara kwenye udongo kwa sababu yana hali ya kuwa alkaline zaidi (10 - 12 pH)  kwa sababu baadhi ya mchanganyiko wake hauyayuki kwenye maji, kama utahitaji kuongezea kwenye mimea yenye upungufu wa madini kama fosforas na potasiam basi hakikisha majivu hayagusi mashina kwani yanaweza kuuungua haya kama mimea ni michanga.

Pia majivu yanan kiasi kidogo sana cha naitrojeni ambacho hakiwezi kukidhi mahitaji ya mmea wowote ule, kwa hiyo hakikisha pia unatumia vyanzo vingine kwa ajili ya naitrojeni, vyanzo kama mimea jamii ya mikunde, marejea, lukina, na alfalfa

NANE NANE 2013










BLOG AWARDS 2013



Wasomaji wa blog hii ya mitiki-kilimo kwanza, mwaka huu pia blog hii itashiriki kwenye kutafuta blog bora za mwaka 2013 kupitia  http://tanzanianblogawards.blogspot.com/ blog hii itaomba kushiriki kwenye vipengele viwili vya Best AgricultureBlog na Best Educational Blog. 


 



Mkumbuke blog hii kwa mwaka 2012 ndio ilikuwa blog bora kwenye kipengele cha Best Educational Blog, kwa mwaka huu upigajikura utaanza September 1 mpaka September 7 2013 kwa wale wanaoamini hii ni blog bora kwenye vipengele itakavyochaguliwa, nitawaomba watembelee linki hii hapa chini na kupiga kura zao. Aksante

http://tanzanianblogawards.blogspot.com