KURASA

Wednesday, May 27, 2009

VUNJA - JUNGU




Huu ni msimu ambao huku kwetu wanakuwa wengi sana, hiki ni kipindi ambacho mvua zinaishia na kuelekea kwenye majira ya baridi (joto kupungua) hawa wadudu huzaana sana kipindi hiki na hujazana kwenye taa za majumbani na wakati mwingine huingia ndani

DUME



Kuna baadhi ya jamii huwakamata na kuwala kama vile kumbi kumbi na senene, lakini si wengi waliozoea kuona wakiliwa, ukimshika vibaya na anakapata nafasi anaweza kuku ng'ata ingawa hana sumu yoyote na kidonda chake ni kidogo kinachoweza kupona chenyewe.

JIKE



Kama una bustani ya maua na mboga mboga na unasumbuliwa na wadudu kuvamia mara kwa mara, basi unaweza kuwapandikiza wadudu hawa na wakakusaidia katika kuondoa wadudu waharibifu kwa njia ya kibaiolojia, kwa sababu wana tabia ya kula wadudu wengine kama chakula chao. ili kuweza kujua madume na majike angalia rangi zao, madume huwa na rangi zilizokooza na kijivu wakati majike huwa na rangi ya kijani kibichi


WAKIPANDANA