KURASA

Thursday, March 26, 2009

MHALINTA - Mti unaotoa povu la sabuni

MTI WENYEWE



Huu mti niliukuta mkoani Tanga wilaya ya Mkinga tarafa ya Maramba kijiji cha Muhinduro mtaa wa Majengo, ni mti unaokuwa mkubwa kama miti mingi tuliyoizoea ukiwa na majani ya wastani na unakuwa na majani muda wote wa mwaka (ever green)



MBEGU ZAKE
Ndizo hutumika kufulia nguo mbadala wa sabuni, unachotakiwa kufanya ni kukusanya mbegu kama 5 kwa ajili ya kufulia nguo moja, weka nguo yako ndani ya maji kiasi kisha chukua mbegu zako na uzipasue. Toa ile mbegu ya ndani na ubakie na maganda yake kisha tumia haya maganda kutengeneza povu ndani ya maji yako kisha fua nguo yako kama kawaida.



Wenyeji waliniambia kuwa mti huu unazaa kwa misimu miwili kwa mwaka kutokana na majira ya mvua sehemu za pwani yaani masika na vuli, na kila msimu huwa miti inazaa mbegu nyingi na za kutosha

OMBI kwa wanaoujua mti huu kwa majina mengine, jina la kiingereza na jina la kisayansi ninaomba wanifahamishe kwa kupitia blogu hii