KURASA

Monday, August 26, 2013

FISH CENTRE & AQUARIUM


 Samaki wa aina mbali mbali kama Gold (aina zote), koi, Salasa, Sotas, Angels, Gupies, zebra nk


 Vyakula vya aina mbali mbali kwa ajili ya samaki wako. kwa ajili ya ukuaji mzuri, kinga ya magonjwa na utoaji wa rangi


Filter na pampu za aina na ukubwa mbalimbali

Urembo na mapambo ya kuweka ndani ya vyombo vya kufugia

Vyombo vya kufugia samaki (aquarium) aina na ukumbwa tofauti tofauti kulingana na matakwa yako












 Hii ni aquarium ya kusimama, ndefu kwenda juu zaidi ya upana
 Kwa mawasiliano zaidi piga simu namba 0753-151811, 0787151811, 0715151813

Sunday, August 18, 2013

KUPUNGUZIA MATAWI KWENYE MICHE YA NYANYA

Kuna baadhi ya wasomaji wangu walipenda kufahamu umuhimu wa kupunguzia matawi kwenye zao la nyanya na pia jinsi ya kupunguzia matawi hayo.
Umuhimu wa kupunguzia matawi kwenye zao la nyanya ni kupata nyanya bora, kubwa na zenye afya, ukiacha mti uwe na matawi utatoa maua mengi sana na utaishia kupata nyanya ndogo ndogo ambazo hazina soko zuri, lakini ukipunguzia matawi nyanya zako zitakuwa kubwa na mmea wako utazaa kwa mpangilio na kwa muda mrefu

Jinsi ya kupunguzia matawi ni kwa kutofautisha maua ni yapi na matawi ni yapi kisha unaondoa matawi kwa kutumia mkono tu, usitumie kisu maana itakuwa rahisi kusambaza magonjwa toka mme mmoja hadi mwingine, mara nyini matawi hutoke kati ya shina na jani kama inavyoonekana kwenye picha hapo chini




NYANYA KUBWA ZENYE AFYA


NYANYA DOGO TOKA KWENYE MMEA WENYE MATAWI MENGI


Tuesday, August 13, 2013

UMUHIMU WA MAJIVU KWENYE UDONGO WA BUSTANI

Watu wengi wamekuwa wakiulizia umuhimu wa madini kwenye udongo na namna ya asili ya kuongezea kosefu wa madini kama potasiam, fosforas, kalsiam na mengineyo, njia rahisi ya kuongeza baadhi ya madini kwenye udongo ni kwakutumia majivu

UMUHIMU
Majivu yanakiwango cha wastani wa madini kifuatacho potasiam 5% - 7%, kalsiam 25% - 50%, fosforas 1.5% - 2% na madini mengine kwa kiasi kidogo pia mabaki mabaki ya chenga za mkaa kwenye majivu pia yanasaidia kwenye kunyonya baadhi ya sumu kwenye ardhi, kumbuka mkaa ni kaboni halisi (pure carbon)

KIASI CHA KUTUMIA
Kiasi cha kilo 2.5 mpaka 5 kitumike kwenye eneo la mita za mraba 33 au futi 100 za mraba, na majivu yamwagwe wiki 3 - 4 kabla ya kupanda kitu chochote ardhini.

MADHARA
Kila kitu kikitumiwa zaidi ya kiasi kina madhara na majivu pia yana madhara kwenye udongo kwa sababu yana hali ya kuwa alkaline zaidi (10 - 12 pH)  kwa sababu baadhi ya mchanganyiko wake hauyayuki kwenye maji, kama utahitaji kuongezea kwenye mimea yenye upungufu wa madini kama fosforas na potasiam basi hakikisha majivu hayagusi mashina kwani yanaweza kuuungua haya kama mimea ni michanga.

Pia majivu yanan kiasi kidogo sana cha naitrojeni ambacho hakiwezi kukidhi mahitaji ya mmea wowote ule, kwa hiyo hakikisha pia unatumia vyanzo vingine kwa ajili ya naitrojeni, vyanzo kama mimea jamii ya mikunde, marejea, lukina, na alfalfa

NANE NANE 2013










BLOG AWARDS 2013



Wasomaji wa blog hii ya mitiki-kilimo kwanza, mwaka huu pia blog hii itashiriki kwenye kutafuta blog bora za mwaka 2013 kupitia  http://tanzanianblogawards.blogspot.com/ blog hii itaomba kushiriki kwenye vipengele viwili vya Best AgricultureBlog na Best Educational Blog. 


 



Mkumbuke blog hii kwa mwaka 2012 ndio ilikuwa blog bora kwenye kipengele cha Best Educational Blog, kwa mwaka huu upigajikura utaanza September 1 mpaka September 7 2013 kwa wale wanaoamini hii ni blog bora kwenye vipengele itakavyochaguliwa, nitawaomba watembelee linki hii hapa chini na kupiga kura zao. Aksante

http://tanzanianblogawards.blogspot.com
  

Tuesday, August 6, 2013

SEREKALI KUNUNUA MAZAO YOTE YA NAFAKA


 Serikali imetangaza kuanzia mwakani itaanza kununua mazao yote ya nafaka, ili wakulima nchini  wawe na soko la uhakika. Hatua hii inalenga kuweka ushindani wa biashara baada ya kuhodhiwa wa wanunuzi binafsi.

Mazao yatakayonunuliwa kupitia Bodi Mpya ya Mazao ya Nafaka ni mpunga, maharagwe, karanga, choroko, ulezi, ufuta na mahindi na kwamba yatanunuliwa kwa bei ya ushindani wa soko mwaka huu.
Mchumi wa bodi hiyo, Edwin Mkwenda, alisema hayo kwenye maonyesho ya wakulima yanayofanyika kitaifa  Viwanja vya Nzuguni, Dodoma.
Mkwenda alisema tayari Serikali imeikabidhi bodi hiyo maghala yote yaliyokuwa ya Shirika la Usagishaji la Taifa (NMC), ambayo hayakubinafsishwa kwenye kanda saba za nchi ili kutunza mazao yatakayonunuliwa.
Naye Ofisa Ubora wa Mazao wa Bodi hiyo,  Dendego Abdallah, alisema kuundwa kwa bodi hiyo ni ukombozi kwa wakulima kwani watakuwa na uhakika wa kupata soko la mazao husika.
Abdallah alisema wafanyakazi wa bodi chini ya Mkurugenzi Mkuu, Eliampaa Kilanga, imejipanga kuanza biashara rasmi mwakani na kwamba, wakulima wajiandae kuzalisha mazao hayo kwa wingi kutokana na kuwapo uhakika wa soko.
Wakati huohuo, Shirika la kuendeleza Bonde la Mto Rufiji (Rubada), limetenga Sh300 milioni kujenga kituo cha pili cha kufundisha vijana kilimo cha biashara kwa vitendo eneo la Ngalimila, wilayani Kilombero.
Ofisa Kilimo wa Rubada, Joseph Lyafwila, alisema hayo kwenye maonyesho hayo kuelezea mkakati wa Serikali kubadili kilimo kwa vijana, ili walime kibiashara zaidi  kupitia mafunzo ya vitendo.

CHANZO http://www.mwananchi.co.tz/kitaifa/Serikali-kununua--nafaka-zote-nchini/-/1597568/1937656/-/13mbvgmz/-/index.html