KURASA

Monday, November 30, 2009

MABADILIKO YA TABIA YA NCHI KIKWAZO CHA KILIMO KWANZA

Katika miongo kadhaa ijayo kutakuwa na mabadiliko ya kitabia ya nchi katika hali ya hewa, hii inasababishwa na kuongezeka kwa kiwango cha joto katika dunia. Hali hii ina madhara ya moja kwa moja katika maji na uzalishaji wa chakula katika hali mbali mbali. Kuna dalil zilizo wazi zinazoonyesha kwamba nchi masiki zinazoendelea ikiwamo Tanzania ndizo zitakazo athirika zaidi kutokana na mabadiliko haya ya hali ya hewa kitabia.

Jamii zilizoko vijijini ambako ndio kuna watu wengi zaidi na wanategemea kilimo kama ajira yao au chanzo cha mapato ndiyo itakayo athirika zaidi na kusababisha wimbi la kuhamia mijini kuongezeka, Katika kilimo maji ndiyo hutumika sana na kutokana na mabadiliko haya kiasi cha mvua kitapungua kunyesha, kuna watakao amua kuhamia kulima kwenye vyanzo vya maji au maeneo tengefu ili kuweza kuhimili hali ya ukame, kwa kufanya hivyo basi hata upatikanaji wa maji kwenye mito na chemi chemi pia utaathiriwa kwa kiwango kikubwa



Kukoseka kwa maji ya uhakiwa kwa wakazi wa vijijni kutasababisha magonjwa ya milipuko kama kuhara, kichocho na hata kipindupindu kuibuka na hivyo wana vijiji kupoteza maisha, visima vichache ambavyo ni vyaasili na hata vile vya kuchimbwa ambavyo ni vifupi navyo vitakuwa havina maji kwa kipindi kirefu cha Mwaka.

Kuna haja kubwa kwa mamlaka husika za serekali kama Hali ya hewa, kilimo, mifugo, uvuvi, misitu na nyinginezo kujiandaa mapema na kuwaanda wanavijiji na hali hiyo, kuna njia kama kubadili aina ya mazao na wanyama, namna ya ulimaji mfano kuanza kilimo cha umwagiliaji cha uhakika, pia kunahitajika aina mpya za mbegu kulingana na mahitaji ya hali ya hewa zaidi ikiwa ni za muda mfupi na zenye kuhitaji mvua pungufu lakini zenye kuzaa zaidi.

Aina za miti tuayopanda kwa ajili ya misitu yetu pia inabidi ibadilike, baadhi ya miti imelalamikiwa kwamba inaondoa maji mengi sana ardhini na hivyo kuwa chanzo cha ukame, ingawa bado utafiti unaendelea lakini miti kama mikaratusi na misoji ni dhahiri inatumia maji mengi katika ukuaji wake

Thursday, November 26, 2009

VITUNGUU

Ndugu Bunyanza kwa mara nyingine tena alitaka kujua kuhusu zao la vitunguu, na mimi bila hiyana naelezea yale machache ninayoyafahamu.



Zao la vitunguu hulimwa karibu kila mahali hapa nchini. Hata hivyo, mikoa inayolima kwa wingi ni Tanga, Arusha, Iringa, Kilimanjaro, Singida, Morogoro, Mara, Mbeya Dodoma na Manyara. Zao hili ni la biashara na chakula. Ekari moja inaweza kuzalisha gunia 80 – 100 za vitunguu zikitunzwa kitaalam, na mkulima anaweza kulima mara mbili kwa Mwaka kwa mbegu kubwa ambazo huchukua hadi miezi mitano (5) shambani. Bei ya wastani kwa gunia moja ni Tsh 60,000

MAMBO YA KUZINGATIA WA K ATI WA UZALISHAJI

Ili kupata vitunguu bora na vingi ni muhimu kuzingatia kanuni za kilimo bora cha vitunguu.Baadhi ya kanuni hizo ni kama zifuatazo: -



1 - Kuchagua aina ya mbegu

• Chagua aina bora kulingana na matakwa ya soko
• Pamoja na mahitaji ya soko ni muhimu pia kuchagua aina inayovumilia magonjwa, wadudu,kukomaa mapema na kutoa mazao mengi na bora.

2 - Kuweka mbolea
Vitunguu hustawi vizuri kwenye udongo wenye rutuba ya kutosha.
• Tumia mbolea za asili ili kurutubisha udongo kwa lengo la kupata mazao mengi na bora.
• Iwapo ni lazima kutumia mbolea za viwandani muone mtaalam wa kilimo ili akuelekeze namna ya kutumia. Mbolea ikizidi huharibu ubora wa vitunguu.

3 - Kumwagilia maji
• Kagua shamba kuona kama udongo una unyevu wa kutosha. Iwapo unyevu ni mdogo mwagilia maji kufuata mahitaji ya mmea. Vitunguu vinapoanza kukomaa punguza kumwagilia ili kuepuka kuoza



4 - Kupalilia
• Palilia mara kwa mara ili kudhibiti magugu na kuwezesha vitunguu kutumia vizuri unyevu na virutubishi vilivyoko kwenye udongo. Pia magugu mengine huficha wadudu waharibifu kama vile utitiri mwekundu.
• Wakati wa kupalilia epuka kukata mizizi ya mimea.
• Pandishia udongo na kufunika shina la kitunguu wakati wa kupalilia ili kuzuia jua lisiunguze mizizi na kubabua vitunguu. Vitunguu vilivyoungua na kubabuliwa ubora wake hushuka napia huharibika upesi wakati wa kuhifadhi.

5 - Kudhibiti magonjwa na wadudu
Vitunguu hushambuliwa na magonjwa na wadudu mbalimbali ambao huweza kusababisha upungufu na ubora wa mazao. Ili kudhibiti tatizo hilo kagua shamba mara kwa mara kuona dalili za mashambulizi. Endapo kuna dalili za mashambulizi, chukua tahadhari ya kunyunyuzia dawa mapema kabla madhara hayajaleta upotevu mkubwa.

6 - Kupanda kwa nafasi:
Zingatia nafasi ya kupanda inayopendekezwa ili kupata vitunguu vyenye ukubwa uliokusudiwa. Wastani ni inchi 4 - 5 kutoka kitunguu kimoja hadi kingine, na inchi 12 - 18 kutoka mstari hadi mstari na kipandwe inchi 1 - 1.5 chini ya udongo

MAANDALIZI KABLA YA KUVUNA

1 - Kukagua shamba
• Kagua shamba ili kuhakikisha kuwa vitunguu vimekomaa. Vitunguu huwa tayari kuvunwa miezi mitatu hadi mitano tangu kusia mbegu kutegemea aina ya mbegu na hali ya hewa.Dalili za vitunguu vilivyokomaa:

• Majani hunyauka na kuanza kukauka
• Asilimia kumi hadi 20 ya mimea huanguka majani na shingo hulegea.
• Majani hubadilika rangi kuwa ya manjano na baadaye kaki

VITUNGUU VILIVYOKAUKA MAJANI TAYARI KWA KUVUNA



2 - Kuvuna
Vitunguu vinapaswa kuvunwa mapema mara tu vinapokomaa ili kupata mazao mengi na bora.Uvunaji hufanyika kwa mikono ambapo jembe uma hutumika kuchimbua au kulainisha udongo.Udongo ukishalainishwa vitunguu hung’olewa kwa mkono. Inashauriwa uvunaji uanze asubuhi ili vitunguu viweze kunyauka na kukomaza ngozi sehemu za michubuko. Vitunguu visiwekwe juani na inapobidi kukomaza ngozi shambani, majani ya vitunguu yatumike kufunika vitunguu ndani ya matuta yake wakati wa mchana ambapo kuna jua. Kusanya vitunguu kwenye vikapu kisha vipeleke sehemu ya kukaushia. Vitunguu vya kukaushia kwenye kichanja ni bora zaidi, mizizi na majani hupunguzwa na kuachwa urefu wa robo inchi . Vitunguu vya kukausha kwa kunining’iniza havikatwi majani bali hufungwa kwenye mafungu na kupelekwa sehemu ya kukaushia.

Saturday, November 21, 2009

MAHINDI NA MPUNGA KIPI KINA FAIDA ZAIDI

Kutokana na maombi ya Ndugu Buyanza ya kutaka kufahamu kati ya kilmo cha mahindi na Mpunda kipi kina faida zaidi, nami nimejaribu kuchambua kidogo kati ya mazao haya mawili

MPUNGA
Katika hecta moja ya mpunga unaweza kuzalisha mpaka kilo 3675 kwa mkupuo mmoja, kama shamba ni jipya itakuchukua miezi 6 mpaka kuanza uvunaji, hii ni kwa sababu ya kuliandaaa shamba lako, baada ya mvuno wa kwanza utaweza kuvuna mara 3 kwa Mwaka. Hii inamaanisha kwamba unaweza kuvuna kiasi cha tani 10 -11 kwa Mwaka kama utafanya kilimo cha umwagiliaji.



Kilo ya mpunga sasa hivi ni shilingi 700 – 800 ingawa bei hupanda baadae kama utahifadhi mpunga wako kwa maana hiyo kwa Mwaka unaweza kupata kati ya shilingi milioni 7 mpaka milioni 8, gharama za kulima mpunga ni wastani wa asilimia 20- 22 ya mauzo, kwa maana hiyo kwa Mwaka kilimo chako kitatumia si zaidi ya shilingi milioni 2 kwa mara zote 3 utakazolima, hii ikijumuisha vibarua na mbolea.



MAHINDI


Kama utalima mahindi, ambayo unaweza kulima mara 2 kwa Mwaka kwa ukanda wa pwani na mara moja kama nisehemu zenye baridi, MAvuno kwa hecta moja ni kilo 7500 kwa maeneo yenye baridi na kilo 5000 kwa ukanda wa pwani ambapo utavuna kilo 10,000 kwa Mwaka. Bei ya mahindi kwenye soko ni wastani wa shilingi 400 kwa maana hiyo unaweza kupata shilingi milioni 4 kwa Mwaka.



Matumizi ya mbolea za viwandani ni lazima ili kufikia mavuno haya, Mbolea kama UREA itawekwa mara mbili wakati wa kupandia na kukuzia ikichanganywa na DAP (diamonium phosphate) ghara jumla ya mbolea hizi kwa mpando mmoja hufikia kiasi cha shilingi laki 7 mara mbili ni shilingi 1,400,000 ukongeza na gharama za kuandaa shamba na kupalilia kama 200,000 unapata jumla ya 1,600,000 kwa hiyo utabakiwa na kama shilingi 2,400,000



HITIMISHO
Mpunga ukilimwa kitaalam unawezza kukupatia faida shilingi milioni 5 kwa Mwaka, wakati mahindi yatakupatia shilingi milioni 2.5, faida ya mpunga inakuwa kubwa kwa sababu utalima mara 3 kwa Mwaka lakini kama utategema mvua utalima mamra 2 tu kwa Mwaka na utapata faida ya shilingi 3,300,000 kwa Mwaka

Hizi data ni kwa uzoefu wangu tu wa haraka haraka, bei ya mazao inaweza kupanda au kushuka na kiasi cha uzalishaji kwa hecta kinaweza kupanda au kushuka kutokana na aina ya mbegu, hali ya hewa na uzoefu wa mkulima mwenyewe. Kwa sasa hivi kilo ya unga wa mahindi ni shilingi 700 na debe la mpunga wa kyela ni shilingi 20,000, unaweza kupata faida zaidi kama utaachana na madalali na kupeleka mazzao yako sokoni mwenyewe

Thursday, November 19, 2009

MIGRAVILLEA

Kutokana na maombi ya ndugu Leonard Kisenha mwenye shamba lake pale Goba, alitaka kujua kati ya Mitiki/misoji na migavilea (GRAVILLEA ROBUSTA), je ni miti gani itamfaa kupanda kwenye shamba lake? Jibu ni rahisi ukuaji mpaka kuvuna umri ni karibia sawa sawa ila wakati wa kuvuna mwenye mitiki atapa faida nyingi sana (maradufu) kutokana na bei ya mitiki kuwa juu sana, pia hali ya hewa ya pwani kwenye joto inafaa zaid kwa mitiki tofauti na migravilea ambayo hukua vizuri zaidi kwenye baridi



Asili ya miti hii ni nchini Australia lakini nchini Coasta rica na Guantemala (mita 1000 kutoka usawa wa bahari) Afika Mashariki (1200m – 1800m) Sri lanka (600m – 2000m) Israel, Cyprus na Afrika ya Kusini huota yenyewe ikichanganyika na miti ya mikaratusi. Miti hii hustawi zaidi kwenye maeneo yasiyo na joto na inahimili hali ya hewa hata kufikia kuganda ndio maana ukanda wetu hustawi zaidi mikoa ya Mbeya, iringa, Songea, Arusha, Kilimanjaro, Tanga (Lushoto)

Miti hii hukua hadi kufikia mita 30 – 35 ikiwa na kipenyo cha wastani 50cm – 60cm, inakuwa na majani kipindi chote cha Mwaka huwa na magamba ya kahawia huku mbao zake zikiwa na rangi nyekundu kuelekea hudhurungi iliyo kolea, huweza kuhimili kuota kwenye mchanga na udongo wenye asidi 5 – 7ph ingawa hukua vizuri zaidi kwenye udongo wenye rutuba na usiotuamisha maji.



Kiasi cha mvua kinachohitajika ni wastani wa 1200mm – 1800mm kwa mwaka, hutoa maua yenye rangi ya njano na kishubaka cha mbegu huwa na urefu wa senti meta 2 ambazo kwa Tanzania hukomaa kuanzia mwezi 5 mpaka 8, mbegu zake ni nyembamba kama karatasi (kilo moja huwa na mbegu 50,000 mpaka 150,000)

Umri mzuri wa kuvuna tangu kupandwa ni miaka 15 ambapo mbao nzuri hupatikana, lakini mti unaweza kuvunwa kabla ya hapo kama utahitajika kwa matumizi mengine kama kuni au nguzo za kujengea, mti huu unaweza kupandwa kwa ajili ya kivuli, mapambo au hata mipaka ya shamba na kuzuia upepo



Gamba la mbegu zake huwa gumu kiasi, njia nzuri ya kuhakikisha zinaota kwa wingi ni kwa kuzipitisha kwenye moto kidogo (heat seed scarification) mbegu zikiachwa wazi huweza kukaa bila kuharibika kwa miezi 2 – 3 lakini kama zitahifadhiwa kwenye mifuko ya plastic kwenye hali joto ya sentigredi 4 na unyevu kiasi cha asilimia 60 kisha mfuko ukazikwa kwenye mchangamkavu ulio ndani ya chombo maalum, basi mbegu huweza kuhifadhiwa mpaka miaka miwili

Thursday, November 12, 2009

KASUKU - DONDOO ZA KUMFUNDISHA KUONGEA



Watu wengi wamekuwa wakipenda kufuga kasuku lakini utakuta wanalalamika kwamba kasuku wake haongei, nimeamua kuweka vidokezo muhimu ili mfugaji aweze kuzingatia wakati wa kumfundisha
Kuna aina nyingi za kasuku duniani wengine wakiwa na rangi za kawaida na wengine wakivutia sana, kwa kawaida huwa hawaishi sehemu zenye baridi kali kwani hupendelea hali ya joto wastani

UCHAGUZI WA KASUKU
Mbegu kubwa ni waongeaji wazuri, mbegu ndogo ni wavivu kujifunza,
Akiwa mdogo anajifunza vizuri zaidi, ukiweza mpate yule anayetoka kulelewa kwenye kiota na ndio anajifunza kuruka/kupaa
Kasuku muoga hawezi kujifunza vizuri.
Kasuku mwenye tabia ya kung'ata anauwezo mkubwa wa kujifunza kungea.




MAZINGIRA
Kumbuka kasuku hujifunza maneno machache tu hawezi kuongea kama mtu.
Sehemu nzuri ya kumuweka nyumbani ni jikoni, kwa sababu kuna shughuli nyingi.
Huanza kuongea katika umri wa miezi 4-6.




UFUNDISHAJI
Wakati wa kumfundisha zima radio na TV (kusiwe na kelele)
Muda mzuri wa mafunzo ni asubuhi na jioni.
Mfundishe kupiga miluzi baada ya kuweza kuongea baadhi ya maneno na si kabla ya hapo.
Kumbuka kasuku hujifunza vizuri zaidi kwa vitendo mfano unamtoa nje ya kibanda chake huku unamwambia " toka nje mmmh" ukirudia rudia, jitahidi kutumia Mmmh kila baada ya neno, hii humsaidia kujifunza kwa urahisi.
Hakikisha anapata mlo kamili maji na matibabu

Saturday, November 7, 2009

SAANEN MBUZI BORA WA MAZIWA




ASILI Switzerland katika ukanda wa Saanen

RANGI nyeupe au maziwa

UZITO kilo 65-68

MAZINGIRA yasiyo na joto, wanapendelea baridi chini ya sentigredi 15c



UZAZI mtoto moja au mapacha (kila mwaka mara mbili)

UZALISHAJI lita 4 mpaka 7 kwa siku (mikamuo miwili)

MASIKIO yamesimama wima

MKIA umelala tofauti na mbuzi wengi ambao husimamisha mkia

NDEVU majike yana ndevu mara chache ingawa si nyingi kama madume

PEMBE ndefu zilizosimama wima

Monday, November 2, 2009

BORAN - MBEGU BORA YA NG'OMBE WENYE ASILI YA AFRIKA MASHARIKI

Asili yake ni maeneo ya borana kusini mwa Ethiopia ambako alipatikana baada ya mbegu tatu za ng’ombe zilichanganyika kwa bahati mbaya kutoka kwa wafugaji wa kienyeji waliotoa ngombe wao kutoka pande tofauti za afrika, hiyo ilikuwa zaidi ya miaka 1300 iliyopita lakini sasa hivi kuna taasisi inayoitwa Boran cattle breeder’s society iliyopo nchini Kenya.

DUME BORA LA BORAN


Taasisi hii iliamua sasa itafute mbegu bora ya Boran kwa kutumia njia za kitaalam tofauti na hapo mwanzo ambako Boran alitokea tu bila hata wafugaji kujua kwamba wanatengeneza mbegu bora ya ng’ombe.

JIKE BORA LA BORAN


Waalamu wa kupandisha (breeders) waliamua kuangalia vinasaba bora zaidi na kumfanya Boran awe wa kisasa zaidi na kuweza kuhimili hali ya Afrika mashariki huku uzalishaji wa maziwa na nyama ukiongezeka zaidi kuliko ule wa ng’ombe wetu wa kienyeji, Boran wa kisasa ana damu za aina tatu katika uwiano ufuatao N’gombe wa ulaya wasio na nundu (european bos taurus) 24% Ng’ombe wa Afrika mashariki wenye nundu wajulikanao kama Zebu (bos indicus)64% na ngombe wafrika wasio na nundu (african bos taurus ) 12%



SIFA
-Ni mkubwa kuliko ng’ombe wa kienyeji
-Ana kiwele cha wastani na chuchu ni kubwa kidogo
-Anazaa ndama wa wastani (kilo 25 – 28) kwa hiyo hakuna matatizo wakati wa kujifungua lakini watoto hukua haraka na ni mara chache sana ndama kufariki
-Anahimili hali ya mazingira ya Afrika kuliko ng’ombe wa kisasa (joto na magonjwa)
-Ngombe jike anaweza kuzaa bila matatizo mpaka akiwa na miaka 15, madume yanauwezo wa kuzalisha mpaka miaka 16
-Majike hubalehe baada ya siku 385 (mwaka na siku chache)
-Ni wapole na wenye nguvu kwa hiyo hufaa kwa shughuli za kulima na kukokota mikokoteni (maksai)
-Anaongezeka uzito haraka hata kama anakula majani makavu, majike yanayo nyonyesha hupungua uzito kidogo sana kipindi cha kunyonyesha
-Wanakula kwa mshikamano na hawatawanyiki wakiwa machungoni kiasi kwamba inakuwa vigumu kumuiba mmoja au kumtenganisha na wenzake

BORAN WAKICHUNGWA KATIKA KUNDI LENYE MSHIKAMANO



Wafugaji wengine wamejaribu kuchanganya mbegu hii na mbegu nyingine za kisasa kutoka bara la ulaya ili kuongeza uzalishaji wa maziwa au nyama kama wanavyoonekana hapo chini kwenye picha

BORAN NA FRIESIAN (maziwa)


BORAN NA BEEFMASTER (nyama)



BORAN NA JERSEY (maziwa)


BORAN NA DRANKENSBERGER (nyama na maziwa)