KURASA

Monday, November 30, 2009

MABADILIKO YA TABIA YA NCHI KIKWAZO CHA KILIMO KWANZA

Katika miongo kadhaa ijayo kutakuwa na mabadiliko ya kitabia ya nchi katika hali ya hewa, hii inasababishwa na kuongezeka kwa kiwango cha joto katika dunia. Hali hii ina madhara ya moja kwa moja katika maji na uzalishaji wa chakula katika hali mbali mbali. Kuna dalil zilizo wazi zinazoonyesha kwamba nchi masiki zinazoendelea ikiwamo Tanzania ndizo zitakazo athirika zaidi kutokana na mabadiliko haya ya hali ya hewa kitabia.

Jamii zilizoko vijijini ambako ndio kuna watu wengi zaidi na wanategemea kilimo kama ajira yao au chanzo cha mapato ndiyo itakayo athirika zaidi na kusababisha wimbi la kuhamia mijini kuongezeka, Katika kilimo maji ndiyo hutumika sana na kutokana na mabadiliko haya kiasi cha mvua kitapungua kunyesha, kuna watakao amua kuhamia kulima kwenye vyanzo vya maji au maeneo tengefu ili kuweza kuhimili hali ya ukame, kwa kufanya hivyo basi hata upatikanaji wa maji kwenye mito na chemi chemi pia utaathiriwa kwa kiwango kikubwa



Kukoseka kwa maji ya uhakiwa kwa wakazi wa vijijni kutasababisha magonjwa ya milipuko kama kuhara, kichocho na hata kipindupindu kuibuka na hivyo wana vijiji kupoteza maisha, visima vichache ambavyo ni vyaasili na hata vile vya kuchimbwa ambavyo ni vifupi navyo vitakuwa havina maji kwa kipindi kirefu cha Mwaka.

Kuna haja kubwa kwa mamlaka husika za serekali kama Hali ya hewa, kilimo, mifugo, uvuvi, misitu na nyinginezo kujiandaa mapema na kuwaanda wanavijiji na hali hiyo, kuna njia kama kubadili aina ya mazao na wanyama, namna ya ulimaji mfano kuanza kilimo cha umwagiliaji cha uhakika, pia kunahitajika aina mpya za mbegu kulingana na mahitaji ya hali ya hewa zaidi ikiwa ni za muda mfupi na zenye kuhitaji mvua pungufu lakini zenye kuzaa zaidi.

Aina za miti tuayopanda kwa ajili ya misitu yetu pia inabidi ibadilike, baadhi ya miti imelalamikiwa kwamba inaondoa maji mengi sana ardhini na hivyo kuwa chanzo cha ukame, ingawa bado utafiti unaendelea lakini miti kama mikaratusi na misoji ni dhahiri inatumia maji mengi katika ukuaji wake