KURASA

Saturday, June 13, 2009

MAZIWA YA NGAMIA NA KISUKARI

AINA ZA KISUKARI
Aina ya kwanza ya kisukari ni pale mgonjwa anapohitaji kutumia insulin kila siku, aina hii huwa ni asilimia isiyozidi 10 ya wagonjwa wote wa kisukari, miili yao huzalisha insulin kidogo sana au haizalishi kabisa.Aina ya pili ni ile ambayo mwili mgonjwa wa mgonjwa huzalisha insulin lakini mwili unashindwa kuitumia na baada ya miaka kadhaa mwili hushindwa kuzalisha insulin na kusababisha aina ya kwanza ya kisukari


MDAU AKIMKAMUA NGAMIA


Maziwa ya ngamia yamekuwa yakisifika katika kuwasaidia wagonjwa wa kisukari aina ya kwanza kama watakunywa maziwa haya kiasi cha nusu lita kwa siku. Kwa kawaida mgonjwa wa kisukari aina ya kwanza huitaji kiasi cha ankara 20 za insulin kwa siku lakini akitumia maziwa haya huitaji kiasi cha ankara 6 – 7 za insulin kwa siku.



Huko india katika jimbo la Rajasthan kuna jamii/ kabila linayoitwa Raica ambalo husifika kwa ufugaji wa ngamia, jamii hii husifika kwa kutokuwa na wagonjwa wa kisukari isipokuwa kati ya wale wachache ambao huwa hawatumii kabisa maziwa ya ngamia




Maziwa ya ngamia pia husifika kwa kusaidia wagonjwa wa shinikizo la juu la moyo, pia husaidia katika kupambana na vimelea kama virusi na bakteria. Kwa mfano mgonjwa wa kifua kikuu anayaetumia dawa na maziwa ya ngamia hupata nafuu haraka zaidi ya yule asiyetumia maziwa ya ngamia