KURASA

Tuesday, January 26, 2010

SIMBA MWENYE FADHILA



Mwaka 1969 John Rendall na Ace berg walimuona mtoto wa simba (dume) aliyekuwa anauzwa huko Harrods alionekana mpweke ndani ya kibanda chake kidogo na wakaamua kumnunua na kwenda naye nyumbani kwao ambako ni ghorofani na wakampa jina la Christian. Paroko wa kanisa moja aliwaruhusu kucheza naye katika viwanja vya kanisa lakini ndani ya muda mfupi simba alikuwa haraka na kuwa mkubwa ambako kwenye nyumba yao asingeweza kuendelea kuishi zaidi ya hapo.

Wakaamua kumrudisha kwenye mazingira yake ya asili kwenye mbuga za Afrika na baada ya Mwaka walipotaka kumtembelea waliambiwa ya kwamba amekuwa mkubwa na kuwa na milki yake na sasa amegeuka mnyama pori kamili kwa hiyo ni hatari kama simba wengine kwa maana hiyo wasingeweza kumsogelea karibu tena, pamoja na hayo bado waliamua kwenda kumuangalia hivyo hivyo, baada ya kumtafuta kwa masaa kadhaa walifanikiwa kumuona…….. ukiangalia kwenye video hii utaona jinsi alivyo warukia kwa furaha akiruka ruka, kucheza nao huku nao wakimkumbatia na wala hakuwa mkali au hatari kwao kama walivyoambiwa, na mwisho alikuja simba mwingine jike ambaye alikuwa ni mke wake kwenye hiyo milki yake na huyo simba jike naye akabaki akiwaangalia tu na wala hakuwashambulia ( ni kama naye alitambulishwa)

Saturday, January 23, 2010

VODACOM NA WAATHIRIKA WA MAFURIKO



Katika kuthamini waliopatwa na maafa ya mafuriko pote nchini kampuni ya simu ya VODACOM imeanzisha kampeni inayojulikana kama RED ALERT itakayowawezesha wateja wake kuchangia kadri wawezavyo ili kuwasaidia waathirika wa mvua na mafuriko pote nchini

Kwa ufupi ni kwamba ukitaka kuchangia waliopatwa na maafa pote hapa nchini kama Kilosa, Same, Tanga na Dodoma basi tuma neno MAAFA kwenda namba 15599 na hapo utakatwa shilingi 250/= (PAMOJA NA KODI) kama mchango wako kwa waathirika wa mvua na mafuriko.

Serekali imefanya tathmini na kutangaza kwamba kiasi cha shilingi billioni 10 zinahitajika ili kuweza kuwasaidia wale walioathirika mpaka hali itakapo tengemaa, na kampeni hii ni kuanzia tarehe 24th January 2010 paka 30th January 2010 (wiki moja tu)

MTI MZEE ZAIDI DUNIANI

Mti mzee kuliko yote duniani ulio hai ni bristlecone pine (Pinus longaeva) unaoitwa Methuselah mti huu unapatikana marekani California katika mlima mweupe, mti huu ambao uko futi 11,000 juu ya usawa wa bahari una miaka 4838 na sio tu ni mti mzee zaidi bali ni kiumbe kizee zaidi duniani cha asili (non-cloned) kilicho hai
Kabla ya Methuselah haujagunduliwa kwamba ni mti mzee zaidi duniani Mwaka 1957 na Edmund Schulman iliaminika kwamba mti mkubwa aina ya Sequoias ndio mti wenye umri mkuwa zaidi ukiwa na miaka 2000

MITI AINA YA METHUSELAH HUKO CALIFORNIA KATIKA MLIMA MWEUPE


Mti mwingine aina ya Prometheus uligunduliaka baada ya mwanafunzi wa Mwaka wa mwisho chuoni 1964 ajulikanaye kama , Donald R. Currey alipokuwa akifanya majaribio ya kisayansi na kifaa chake cha kuchimbia viini vya miti miti kuvunjika ndani ya mti, aliomba ruhusa ya kuukata mti huo (iliauchunguze zaidi) kutoka idara ya misitu na alistaajabu alipokubaliwa (wenzetu hawakati miti hovyo hovyo bila sababu maalum) na baada ya kuukata mti huo ndipo walipogundua kwamba ni mti wenye umri mkubwa zaidi duniani ukiwa na zaidi ya miaka 5000.

MITI AINA YA METHUSELAH WENYE MIAKA 4838



Kwa hiyo Prometheus ndio mti mzee zaidi kugunduliwa lakini umekufa baada ya kukatwa na Methuselah ndio mti mzee zaidi duniani ulio hai mpaka sasa. Miti ya Methuselah iko mingi na yote ikiwa na umri zaidi ya miaka 4000 na ipo California katika mlima mweupe lakini mahali ulipo kutwa mti wa Prometheus pamefanywa siri kwani bado wanaendelea kulichunguza eneo hili wakiamini wataukuta mti mwingine wenye umri unaofanana na ule walioukata

KISIKI CHA MTI WA PROMETHEUS BAADA YA KUKATWA

Tuesday, January 19, 2010

MTI MPWEKE ZAIDI DUNIANI

Mti aina ya acacia ulioota kwenye jangwa la sahana nchini Niger ndio mti ulio mpweke zaidi baada ya kuwa umbali wa zaidi ya maili 250 pande zote bila kukutana na mti mwingine. Mti huu uligunduliwa Mwaka 1970 lakini uliota mahala hapo wakati jangwa halijawa kavu kama lilivyo sasa, kwa miaka hiyo ambako mti huu uliota haukuwa peke yake bali kulikuwa na miti mingine ila yenyewe ilikufa baada ya jangwa hili kuendelea kuwa kavu zaidi na kupata kiasi kidogo cha mvua

MTI MPWEKE PICHANI



Mtii huu Ulikufa baada ya dreva wa lori kutoka Libya alipougonga, inasemekana dreva huyo alikuwa akiendesha lori hilo huku akiwa amelewa pombe. Baada ya mti huu kufa wana sayansi walichimba pembeni yake na kugundua mizizi ilikwenda chini kiasi cha futi 120 (mita 36) mpaka kufikia maji ya chini ya ardhi (water table) Sasa hivi sehemu ulipoota mti huo imejengwa nguzo ya chuma kama kumbukumbu ya mti mpweke zaidi duniani

NGUZO MAHALI ULIPOKUWA MTI MPWEKE

Sunday, January 17, 2010

UGONJWA WA MIGUU NA MIDOMO - FOOT AND MOUTH DISEASE

KWATO ZA MNYAMA MWENYE FMD


Ugonjwa huu husababishwa na virusi jamii ya Aphtovirus vinavyoambukiza binadamu pia (Aphtae epizooticae) ambavyo vipo kwenye Makundi ya A, O, C, SAT1, SAT2, SAT3, Asia1, vinauwezo wa kuishi kwenye matezi na ndani ya mifupa (bone marrow) madhali PH isiwe chini ya 6 na vinauwezo wa kuendelea kuishi kwenye mwili wa mnyama aliyekufa au kwenye udongo kwa mwezi mzima madhali PH isizidi 6. Kama lilivyo jina lake ugonjwa huu hushambulia kwato na midomo (fizi)
Ugonjwa huua zaidi ndama kuliko wanyama wakubwa, hushambulia wanyama wenye kwato kama ng’ombe, mbuzi, kondoo, punda, farasi, nguruwe, nyati maji, na wanyama wengine wenye kwato wanyama jamii ya ngamia, llama na nyati pori, huwa hawasumbuliwi sana na ugonjwa huu

MIKONO YA MTU ALIYEAMBUKIZWA UGONJWA


KUSAMBAA
Ugonjwa hussambazwa kwa njia ya mate, machozi, kinyesi, viatu, vifaa vya kuhudumia wanyama, nyama, maziwa, magari na hata hewa hasa kwa ukanda wa pwani usizidi futi 300 kutoka usawa wa bahari, wanyama ambao wana vijidudu na hawaumwi (carriers) kama nyati pori pia husambaza ugonjwa huu.

DALILI KUU
Toka mnyama aambukizwe huchukua siku 2 -14 na dalili kuu ni uzalishaji wa maziwa kushuka, kusaga meno, joto hupanda, mnyama huchechemea na kurusha mateke, ukiangalia fizi na kati kati ya kwato utaona kama vipele ambavyo baadae hupasuka na kuwa vidonda, wanyama hutoa mimba na wanyama wadogo (ndama )hufa

DAWA
Ugonjwa huu hauna dawa, bali unaweza kutibu vidonda kwa kutumia dawa (antibiotic) kama ulipo hakuna dawa unaweza kutumia chumvi au magadi ukiyeyusha kwenye maji na kuosha kwenye fizi na kwato za mnyama

KINGA
Kuna chanjo za ugonjwa huu ambazo hupigwa , sindano ya pili hupigwa baada ya siku 30 na baada ya hapo ni kila baada ya miezi 6 ( waone maafisa ugani wa mifugo) unaweza kuwakinga wanyama wako kwa kuzuia mwingiliano na wanyama wengine na kabla ya kuleta mnyama mpya hakkisha amepata chanjo zote (sijui wangapi wanafanya hii) pia karantini zitumike mara mlipuko wa ugonjwa huu unapotokea, wanyama wenye ugonjwa wauwawe na kuchomwa moto (incineration)

MFANO WA KIBAO CHA KARANTINI


WANYAMA WENYE UGONJWA WAKICHOMWA MOTO

Tuesday, January 12, 2010

KAMBALE ANAYETEMBEA

Hii ni aina ya kambale inayopatikana sana bara la Asia na Africa, amepewa jina la kambale anayetembea sababu ya uwezo wake wa kujikongoja na kuhama toka sehemo moja hadi nyingine kupitia nchi kavu kwa dhumuni la kutafuta chakula au mazingira mazuri, sio kwamba anatembea bali hujinyanyua juu kwa kutumia mapezi yake na kujinyonga nyonga kama nyoka na ii humuwezesha kusogea mbele, ana uwezo wa kuka muda mrefu nje ya maji madhali ardhi isiwe kavu bali iwe na unyevu

Hupendelea kwenye maji yenye kina kifupi au yasiyotembea, kama kwenye vijito na mito, mabwawa, majaluba ya mpunga na sehemu yoyote ambayo maji hujikusanya. Hukua hadi sentimeta 30 (urefu wa rula ya mwanafunzi) hana magamba kama kambale wengine bali ngozi yake huwa na ulenda ulenda unaomsaidia atembeapo nchi kavu, ana rangi ya kijivu mpaka kahawia iliyokolea kabisa. Tofauti na yake na kambale wengine yeye hana mapezi ya kwanza juu ya mgongo bali pezi lake la pili huwa refu mpaka karibu na mwisho wa mkia, unapomvua kambale huyu usimshike akiwa hai au hata kama kafa mshike kwa umakini sababu ana miiba iliyojificha kwenye mapezi ya chini karibu na mkia



Hupendela halijoto kati ya 10c mpaka 28c, chakula chao kikuu ni samaki wadogo, wadudu, konokono wasio na magamba na mimea ya kwenye maji, kambale hawa wanatabia ya ulafi inayowafanya wawe hatari kwa viumbe wengine wa kweye maji

Saturday, January 9, 2010

ADHA YA MVUA JIJINI DAR ES SALAAM


Kuwasha taa ni muhimu maana madereva hawaoni vizuri mbele kwa sababu ya ukungu kwenye vioo vya mbele





Hapo hata dala dala hazitanui maana inaweza kudumbukia kwenye mtaro, njia haionekani




Ukiwa na mwamvuli hautaloana labda miguuni ndio kasheshe


Magari (hasa ya petroli) nayo hupata hitilafu na kuzimika, hii husababisha adha kwa wenye kuyamiliki na gharama za ziada kama kusukumwa na kuyatengeneza tena


Limebuma


Jamaa anashuka......


Jamaa hana la kufanya anatafakari.... nyuma foleni kama treni


Jamaa anafurahia mvua kwa sababu lazima atauza makoti na mabuti ya mvua hahahahhe!!!!! kufa kufaana


Vituo vya kuwekea mafuta navyo vimefurika maji, je yakiingia kwenye matanki ya mafuta si tutauziwa maji-balaa hili........



Hata zoezi la kuzoa taka hufanyika kwa tabu na jamaa hawana vifaa vya kujikinga angalau gum boot

Sunday, January 3, 2010

MVUA NA MIUNDO MBINU YETU

Jamani heri ya mwaka mpya kwenu nyote, namshukuru MUNGU niko buheri wa afya, Leo nitawaonyesha baadhi ya picha zinazoonyesha tabu tunayopata tukiwa field kutokana na madhara ya mvua kwenye barabara ambazo si za lami, kwa kweli kuna sehemu hata gari ikiwa na 4wheel drive inaweza isipite, pia kunatakiwa uzoefu wa kuendesha kwenye barabara hizo, kama wewe ni dereva wa mjini kwenye lami tu basi kazi utakuwa nayo

TANGA







MANYARA


RUKWA





RUVUMA


Hivi mnategemea kwa kutumia barabara hizi mkulima ataweza kweli kusafirisha mazao yake na kuyapeleka mjini kwenye masoko au mazao hasa yale yanayooza haraka kama matunda na mboga mboga si yataharibikia shambani.