KURASA

Monday, May 17, 2010

ZANZIBAR HAKUNA MBUNG'O

Ni miaka zaidi ya sita (6) tokea mbung’o waache kuonekana katika visiwa vya Zanzibar na tokea kipindi hicho ng’ombe kadhaa wamekuwa wakipimwa damu ili kujua kama wana ugonjwa wa ndigana/nagana unaosambazwa na mbung’o lakini matokeo yamekuwa mazuri yakionyesha kwamba ng’ombe hawana vimelea vya ugonjwa huo hatari kwa mifugo

MBUNG'O WAKIPANDANA


Hii imesababisha uzalishaji wa maziwa kuongezeka mara tatu zaidi, uzalishaji wa nyama marambili zaidi, matumizi ya samadi ya mifugo nayo yameongezeka mara tano zaidi na hii inamaanisha kwamba wafugaji wa ng’ombe kipato chao kimeongezeka zaidi. Je sababu ya haya yote na mbung’o kupotea ni nini?

Kwa kawaida mbung’o jike akishapandwa mara moja hawezi kupandwa tena maisha yake yote, yaani inamaanisha kwamba huwa wana mzao mmoja tu katika maisha yao yote. Sasa kinachofanyika kitaalam ni kwamba mbung’o wanakamatwa wakiwa hai kisha wana tengwa majike na madume, majike yanauwawa na madume yanapelekwa kwenye maabara na kupigwa mionzi ya gamma kutoka katika cobalt 60, baada ya hapo yanakuwa yanapanda majike kama kawaida ila yanapoteza uwezo wa kuwazalisha kwa maana hiyo watapandana bila kuzalishana na pole pole kizazi kinapotea na kufutika kabisa

MTEGO WA KUKAMATIA MBUNG'O



Kwa Zanzibar zoezi lilifanikiwa asilimia 100 kwa sababu mbung’o hawawezi kutoka sehemu nyingine na kuhamia Zanzibar kwa kuwa ni kisiwa, pia wao walizalisha madume mengi kwenye maabara na kuyaachia baada ya kuyaua kizazi, njia hii inajulikana kama sterile male technique