KURASA

Friday, September 18, 2009

NYUNGUNYUNGU JINSI YA KUWAKUZA KWA AJILI YA CHAKULA CHA SAMAKI

Kuna msomaji mmoja wa Zanzibar Bwana Ali Makame Juma (POLO) wa mahinda kaskazini B, ambaye alifurahishwa na maelezo ya ufugaji wa samaki na akaniomba nimwelekeze pia uzalishaji wa nyungunyungu



MAHITAJI
Nyungunyungu
Chombo cha kufugia
Udongo wa juu (top soil)
Mahindi (dona)
Majani makavu

JINSI YA KUFANYA

(A) Andaa chombo chako ambacho hakivuji mfano sinki la bafu, pipa la plastiki (likatwe nusu)
(B) Jaza udongo kiasi cha inchi 4 – 8 kwenye chombo
(C) Weka inchi moja ya majani makavu
(D) Weka mchanganyiko wa dona na vegetable shortenings
(E) Weka nyungunyungu
(F) Funika juu
(G) Ongeza mchanganyiko wa dona na vegetable shortenings baada ya mwezi mmoja na kila baada ya wiki mbili weka 1qt ya maji kila unapoongeza mchanganyiko huu
(H) Weka chombo chako pasipo na mwanga wa jua



KUKUZA NYUNGUNYUNGU KWA AJILI YA CHAKULA CHA SAMAKI NA MBOLEA
MAHITAJI

(a) nyungunyungu
(b) Mabaki ya jikoni/chakula
(c) Kinyesi cha mnyama ambaye hajatoka kupewa dawa za minyoo
(d) Ndoo 3 zenye matobo nusu sentimeta

JINSI YA KUFANYA
(a) Tafuta minyoo kutoka eneo ulilopo, chimba chini au kwenye vinyesi vya wanyama vilivyo lundikana, usi chukue minyoo wa sehemu nyingine kuzuia kuvamia mazingira mapya na kubadili mfumo wa maisha ya viumbe (biodiversity)
(b) Ndoo moja weka minyoo, ya pili weka mabaki ya jikoni nay a tatu iwe tupu
(c) Zipange kwa mpangilio huu ya chini iwe tupu, ya kati iwe na minyoo na ya juu iwe na mabaki ya chakula
(d) Ndoo ya juu ijazwe mabaki ya chakula mpaka juu, na inyunyuziwe maji kidogo kufanya mabaki yawe na unyevu, maji mengi yataua minyoo.
(e) Baada ya muda minyoo itapanda kwenye ndoo ya juu na kuanza kula chakula, chakula kikipungua na kubakia theluthi mbili, toa ndoo ya chini utakachokikuta ni mbolea uiweke bustanini/shambani na uiweke juu
(f) Ndoo yenye minyoo ambayo sasa iko chini itabaki na chakula kidogo na baadhi ya minyoo, minyoo irudishe ndoo ya kati ambayo mwanzo ilikuwa na chakula sababu minyoo mingi itakuwa huko
(g) Ndoo ya juu ijazwe na mabaki ya jikoni tena na endelea na mzunguko huu kwa muda wa miezi 3 minyoo itakuwa mingi tayari kwa ajili ya kulisha samaki
(h) Katikati ya zoezi hili unaweza kutumia baadhi ya minyoo kwa ajili ya kupandishia zamaki (breeding) kumbuka kuweka ndoo hizi kwenye kivuli wakati wote



NJIA NYINGINE RAHISI
Chukua kiroba cha katani na weka pumba za mahindi kama kilo 5 ziloweshe na maji kodogo, tafuta kwenye shina lamigomba mikubwa, chimba pembeni yake na uzike gunia lako, hakikisha mgomba wako haumwagiliwi na maji ya sabuni hata kidogo na wala hauwekewi kemikali yoyote. Acha gunia lako kwa muda wa mwezi mmoja nenda kachimbe ukiwa umevaa gloves za shamba pekua pekua na utakuta nyungunyungu kibao wamezaana, hamisha na ulishe samaki wako, endelea kuvuna kila baada ya mwezi mmoja na kuongeza pumba nyingine kiasi
Hii njia inafaa zaidi kwa ajili ya wale wanaohitaji nyungunyungu kidogo tu kwa ajili ya kulisha samaki wanaopandishwa (breeding stock)