KURASA

Wednesday, June 3, 2009

UJENZI WA BARABARA KISARAWE MPAKA KAZIMZUMBWI




Jumatatu nilikuwa nimeenda Kisarawe maeneo ya visegese (SHAMBA) ndio nikakutana na huu ujenzi wa barabara ambao uko katika hatua za matayarisho. Nilipoongea na wahusika wa kampuni ya ujenzi ya SKYLINK waliniambia barabara hiyo ya lami itakwenda mpaka maeneo ya kijiji cha Kazimzumbwi ambako kunatarajiwa kujengwa kiwanda kipya cha saruji.

UPIMAJI UNAENDELEA


Ujenzi huu utakuwa faraja kwa wakazi wa kazimzumbwi na sisi wakulima wenye mashamba maeneo karibu na hayo, kwa mfano mimi kutoka Kisarawe mjini ambapo lami ilikuwa ndio mwisho wake nilikuwa naendesha kilometa 8 kwenye barabara ya vumbi, kwa sasa nitabakiwa na kilometa zisizozidi 2 kutokea Mpuyani ambapo huwa nachepuka kwenda kwenye barabara inayoelekea Kilvya.


VIJIKO KAZINI






Kiwanda cha saruji pia ni faraja kwa taifa kwani bidhaa hiyo imekuwa ni muhimu sana katika maendeleo ya nchi kwa ujumla, wananchi wataajiriwa kama wafanyakazi na vibarua na hivyo kuongeza ajira, serekali kwa upande wake itanufaika na kodi ya mapato kutoka katika kiwanda hicho

KAMBI YA UJENZI