KURASA

Monday, August 10, 2009

KICHAA CHA MBWA

KUSAMBAA

Kichaa cha mbwa kinaweza kusambazwa na mate ya wanyama, wengi tumezoea kwamba mbwa ndiye anasambaza kichaa, lakini wanyama wengine kama paka, popo, ng'ombe, mbweha, fisi na wengine wanaweza kukisambaza




DALILI ZA MBWA MWENYE KICHAA

siku 1-3 mbwa hubadilika zile tabia ulizozizoea hapa ni ngumu kidogo kugundua

siku 3-4 mbwa huwa na aibu na pia huwa anakwepa mwanga (photophorbia), anajifichaficha na kung'ata kila kitu kinachopita karibu yake hata kama karatasi limepeperushwa na upepo

siku 5 mbwa huanza kulemaa akianzia miguu ya nyuma (hind quarter paralysis) kisha kufuatia miguu ya mbele, baada ya siku saba mbwa hufariki




CHANJO
Mbwa wachanjwe dhidi ya kichaa angalau mara moja kwa mwaka, watoto wanaozaliwa na mama aliyechanjwa wachanjwe baada ya miezi mitatu baada ya kuzaliwa, unaweza kuwachanja kabla kama kuna mlipuko wa kichaa cha mbwa