KURASA

Monday, December 22, 2008

MILONGE (moringa oleifera)



Hii ni miti ambayo haiwi mikubwa sana, inakuwa na maua meupe na kisha hutoa mbegu ndogo zinazokuwa kwenye magamba marefu kama kisu. miti hii hustawi zaidi ukanda wa pwani wenye mvua kiasi na joto, hustawi zaidi kwenye udongo usiotuamisha maji na inaweza kustawi kwenye udongo usio na rutuba nyingi na inahimili ukame kwa kiasi kikubwa.

MATUMIZI
Majani yake huweza kupikwa kama mboga na kuliwa, pia yanaweza kuhifadhiwa kwa muda mrefu bila ya kuathiri ubora wake wa virutubisho (nutritional value) majani yake yanavirutubisho vingi kuliko vyakula vingi tulivyozoea mfano


Ina vitamin A nyingi zaidi ya karoti
Ina Calcium nyingi zaidi ya Maziwa
Ina madini ya chuma zaidi ya spinach
Ina vitamin C nyingi zaidi ya Machungwa
Ina madini na pottasium zaidi ya Ndizi
ina protein nyingi zaidi ya nyama na mayai



MATUMIZI MENGINE
Maganda ya mbegu zake yanaweza kutumika kutibu maji(water treatment)unachukua maji yako ambayo unahisi si salama, unachanganya na maganda ya mbegu zilizopondwa pondwa kiasi, unayaacha kwa muda yatuame kisha unayachuja na yanakuwa salama kwa matumizi


Mbegu za milonge zinaweza kutumika kama dawa ya kupunguza sukari mwilini kwa wagonjwa wa kisukari, unachukua mbegu mbili au tatu unazipasua na kuchukua kokwa ya ndani na kutafuna mara 3 kwa siku, matumizi yanaweza kuongezeka au kuzidi kutegemeana na hali ya mgonjwa

Picha hapo chini inaonyesha mbegu za mlonge juu na kulia kwake ni baada ya kupasuliwa na kupata kokwa ya ndani (ambayo ni dawa ya kupunguza sukari mwilini), funguo imewekwa ili kujua ukubwa halisi wa mbegu


Sehemu yoyote ya mmea kama majani, magamba, mizizi, au maua yakipondwa pondwa na kupakwa kwenye sehemu yenye uvimbe ni dawa tosha ya kupunguza hali hiyo, pia dawa hii inauwezo mkubwa wa kupunguza sumu kama umeng'atwa na wadudu kama nyuki, manyigu/dondola, siafu, tandu, nge nk

Mbegu zake zinatoa mafuta (40%) yanayojulikana kama BEN OIL, ambayo hutumika kulainishia mitambo maalum kama saa za ukutani, pia mafuta haya ni dawa ya upele na harara

Monday, December 15, 2008

MAGONJWA YA SAMAKI NA TIBA

Kuna magonjwa mengi ya samaki yanayosababishwa na fangasi, bacteria, protozoa, parasites, virus na mazingira yenyewe. Hapa nitajaribu kuongelea magonjwa machache ambayo mimi ninauzoefu nayo yaani yameshanitokea na nikapambana nayo

Ichthyosporidium (WHITE SPOTS)
Huu ugonjwa kwa kifupi hujulikana kama ICHI, husababishwa na fungus ambao huingia kwa kupitia ngozi na kisha kushambulia maini na figo.




Dalili zake ni samaki kuogelea kwa kupindapinda au kivivu, tumbo kuonekana kama halina kitu (hollow) na alama nyeupe nyeupe kwenye mwili wa samaki

Tiba yake ni pottasium per manganate kwenye maji, Phenoxethol 1% kwenye chakula na Chloromycetin kwenye chakula, dawa zote zinapatikana kwenye maduka (pet shops). kwa kawaida ICHI wana miznguko miwili ya maisha, akizaliwa anaogelea na kujishikiza kwenye mwili wa samaki, kisha anashuka chini kwenda kuzaana (replitications)na kurudi kwenye mwili wa samaki tena. Kwenye hatua hii pottasium per manganate ndio inafanya kazi ya kuzuia ICHI kurudi tena kwenye mwili wa samaki


LEECHES
Ugonjwa huu husababishwa wadudu wa nje (external parasites)ambao hujishikiza kwenye mapezi na mikia ya samaki. Dalili yao ni kuwaona wakiwa wamejishikiza kwenye sehemu zilizotajwa na ndani ya ngozi, huwa na umbo la kama moyo na rangi ya kijivu/nyeupe



Kwa sababu dalili zinaonekana wazi kwa macho, mara nyingi ugonjwa huu huingia kwenye tank lako kwa njia ya konokono na majani

Matibabu ni kuwaweka samaki ndani ya maji yenye chumvi kiasi cha asilimia 2.5, baada ya dakika 15 leeches wengi watakuwa wamedondoka chini na wale watakaobaki unaweza kuwatoa kwa kutumia kibanio (forceps)
Tiba nyingine ni kwa kutumia Trichlorofon kiasi cha 0.25m/l (robo miligram kwa lita moja ya maji) majani yanaweza kuondolewa ugonjwa kwa kutumia potassium permanganate kiasi cha 5mg/l (miligram 5 kwa lita moja ya maji)

KUOZA MKIA NA MAPEZI
Huu ni ugonjwa unaosababishwa na bakteria, dalili zake kubwa ni kuwa na rangi nyekundu au rangi ya udongo (hudhurungi) kama damu imevilia kwenye kona za mapezi na mkia na kisha baadae sehemu hizi hunyofoka na kubakia kibubutu.




Sababu kubwa ni kuumia kunakosababishwa na kujigonga au madume kupigana, TB pia inaweza kusababisha hali hii

Tiba yake ni kwa kutumia antibiotics kama tetracycline au chloramphenicol kiasi cha 20-30mg/l (miligramu 20-30 za dawa kwa lita moja ya maji)au mili gramu 250 (1 capsule) kwa chakula cha gramu 25

ingawa magonjwa mengi yanasababishwa na vimelea lakini mazingira nayo pia yanachangi katika kuongeza kasi ya magonjwa, ukizingatia yafuatayo unaweza kuwakinga samaki wako.
(a)Nunua samaki wako toka kwa mtu mwenye uzoefu wa kufuga na ambaye unauhakika samaki wake hawana magonjwa

(b)Samaki wapya watengwe kwa muda kwenye chombo kingine (hospital tank0 kwa siku kadhaa kabla ya kuchanganywa na wengine

(c)hakikisha samaki wako hawali zaidi ya kiwango chao na kuvimbiwa, lisha kwa kipimo sahihi

(d)Epuka kuwaweka samaki kwenye mazingira mabaya kama maji machafu, kuweka samaki wasiopatana pamoja, kuwasumbua kwa kuwashikashika na kugonga gonga tanki

(e)Samaki wagonjwa watengwe kwenye tank lingine (hospital tank)

(F)Nyavu zilizotumika kutolea samaki wagonjwa ziwekwe dawa (disinfection) zikaushwe juani na zioshwe vizuri hii ni pamoja na tank na vitu vyake

(g)hakikisha tank halina kitu chochote cha chuma (metal) na maji ya hospital tank yasiingie kwenye tank kuu

Sunday, December 7, 2008

UPANGAJI (AQUARIUM ARRANGEMENTS)

Upangaji wa tank lako ni muhimu ili kuwapa samaki mazingira mazuri kwa matokeo bora, wakati wa kupanga kuna vitu vya msingi na muhimu vya kuzingatia, na kabla ya kununua au kujenga tank lako lazima ujue ni samaki gani unataka kuweka na idadi yao. Baadhi ya samaki kama Goldfish,, Shaks, Koi n.k huwa wakubwa mpaka kufikia futi moja, kwa hiyo wanahitaji chombo kikubwa zaidi.


WATER PUMP
Hii hukaa nje na kusukuma hewa ndani kwa kupitia mawe ya hewa (air stones) ambazo lazima zikae katikati ya tank, pia kuna aina mbali mbali za urembo ambazo nazo zinaingiza hewa, hizi zinaweza kuwekwa kokote ila ni muhimu zisambae ndani ya tank.

WATER FILTER
Ni vizuri kama itawekwa upande mmoja wa tank na kusukuma maji kwa urefu kuelekea upande mwingine, hii husaidia kuweka mzunguko wa maji ambapo chini maji yanavutwa na na juu yanatolewa na pump.

SAKAFU
Sakafu ya tank lako lazima iwe na mchanganyiko wa mchanga na changarawe, ambao hutumika kwa ajili ya mimea kujishikiza. Mchanga na changarawe pia zinatumika kama filter kwa sababu zinachuja uchafu na mabaki ya chakula

MAPAMBO
Hii inajumuisha mimea, urembo na sehemu za kujificha samaki, mapambo yawe ya kutosha ili samaki wajisikie huru kwa sababu inawafanya waone kama wako kwenye mazingira yao halisi



MAJI
Kama unatumia maji ya bomba ni vizuri yawe yamekaa angalau masaa 12 baada ya kukingwa toka bombani. Hii ni kwa sababu huwa yanatiwa chlorine ili kuuyafanya yawe salama kuyanywa, hii chlorine huua samaki. Ukiyaweka wazi kwa masaa zaidi ya 12 chlorine huondoka kwa njia ya mvuke (evaporation), maji wazuri zaidi kutumia ni ya visima vya kuchimba (drilled water wells)kwa sababu yana chumvi chumvi za asili zinazosaidia kuwakinga na magonjwa

baada ya kuweka maji ya bomba kwenye tank unaakiwa uweke chumvi ya mezani kijiko kidogo kwa lita kwa lita 25 za maji, ukianzia na kumuweka samaki mmoja na kumwacha kwa saa zima huku ukimchunguza, ukimwona yuko salama unaweza kuwaweka samaki wote waliobakia

MAJANI NA MIMEA (aquatic plants)

Majani ni kitu muhimu sana katika ufugaji wa samaki, kazi ya majani ni kusafisha maji na kuweka mazingira ya uhasilia kwa samaki, kuna majani ya bandia lakinioiyanabakia kama urembo tu kwa sababu hayawezi kusafisha maji. Ili majani yakue kwa kiwango kizuri ni lazima mahitaji yafuatayo yazingatiwe


MWANGAZA
Mwanga wa kutosha unahitajika kwa ajili ya ukuaji wa majani na mimea ya majini, hii husaidia katika tengenezaji wa chakula kwa kutumia majani yake, mwanga wa tube lights ni mzuri zaidi ila usiwe mwingi sana kwa sababu utachangia ukuaji wa algae kwenye maji. kiwango cha mwanga kinachoshauriwa ni 1.5 watts kwa kila galon ya maji (1.5wpg), mfano tank la galon 20 linahitaji taa ya watts 30




MIZIZI
Mizizi ya mimea na majani inahitaji kujishikiza kwenye sakafu yenye udongo, changarawe au mchanga ili iweze kufyonza virutubisho, inashauriwa usiweke changarawe tu bali uchanganye na mchanga


VIRUTUBISHO
Ili mimea iweze kukua vizuri inahitaji virutubisho kama nitrogen, potasium, phosphorus, chuma na kadhalika, nitogen ambacho ni kirutubisho kikuu kinapatikana kwenye vinyesi vya samaki amabvyo vinatoka kama ammonia. Pia maji yenyewe na chakula cha samakikina madini haya kwa kiasi kidogo



CARBON-DIOXIDE
Hii ndio hewa inayotumiwa na mimea na inapatikana kutokana na samaki wanavyo pumua (respiration). Kwa kawaida samaki wanavuta oxygen na kutoa CO2 ambayo ndio inatumiwa na mimea, wingi wa upatikanaji wa hewa hii ya co2 inategemeana na wingi wa samaki.

Saturday, December 6, 2008

WATER FILTER AND PUMP

WATER PUMP



Hiki ni chombo muhimu sana katika ufugaji wa samaki, kazi yake kubwa ni kuingiza hewa ndani ya chombo cha samaki. Kwa kawaida aquarium huwa inafunikwa sehemu kubwa ya juu na hivyo kupunguza kiwango cha hewa inayoingia. Water pump inaongezea hewa katika style tofauti, hewa inaingia kupitia mawe ya hewa(air stones) na pia kwa kupitia urembo mbali mbali ambao unakuwa ukicheza, kuzunguka au kufunuka na kuruhusu hewa kuingia

mirija ya pump


Kwa kawaida water pump inakuwa nje na inaingiza hewa kwa kutmia mirija inayoingia ndani ya maji mpaka kwenye sakafu ya chombo, ambako huunganishwa na vitu husika kama mawe ya hewa na urembo mbalimbali, pump pia husaidia kuleta mzunguko wa maji na kujenga hali ya mazingira ya uhalisia kwa samaki kama wako mtoni au bwawani/ziwani.

WATER FILTER
Hii hfanya kazi zote kama pump ila tofauti ni kwamba yenyewe ina kazi ya ziada ya kusafisha na kuchuja uchafu kwenye maji

Kwa filter ndogo huwa zinazama ndani ya maji (submeged) kwa sababu huwa zinapoozwa joto na maji hayo hayo,Sehemu ya chini ya filter huvuta maji na hewa huvutwa kutokea juu kwa kutumia mrija mdogo unaokuwa nje ya maji na sehemu ya kati huwa inatoa mchanganyiko wa maji na hewa.

Filter kubwa hukaa nje na mipira ya kutoa maji na kuingiza maji na hewa ndio huingia kwenye maji, hizi mara nyingi huwa zinatumiaka kwa ajili ya aquarium kubwa na mabwawa au vyombo vingi kwa mara moja kwa sababu vinaweza kusafisha vyombo zaidi ya kimoja kwa wakati

Ndani ya filter kuna chujio ambalo husafishwa kwa urahisi mara linapochafuka kwa wastani wa mara moja kwa wiki na likichoka huwa lina badilishwa

Friday, December 5, 2008

GOLD FISH

Hawa wapo aina nyingi sana duniani, lakini hapa kwetu Tanzania kuna aina ambazo ni maarufu zaidi aina hizo ni Gold, Black Moor, Bubbles eye,Oranda, Telescope eye Shibunkins, Red cap n.k


RED CAP




Ni samaki wagumu kiasi wanaoweza kuhimili mazingira ya wastani, wanahitaji joto la wastani mpaka baridi kiasi, kwa mazingira ya tanzania hawahitaji heater na wala wasiwekwe sehemu amabayo watapata mwanaga wa jua moja kwa moja (direct sunlight) labda kama uko sehemu zenye baridi sana

SHUBUNKINS


Hakikisha chombo cha kufugia kina nafasi ya kutosha, gold fish mkubwa nahitaji kiasi cha lita 25 za maji peke yake ili aweze kuishi maisha mazuri. kwa kaida samaki hawa huwa wanachafua sana maji kwa sababu ya tabia yao ya kula sana wakati wote (piggy), na inamchukua muda mfupi kukitoa chakula kwa njia ya kinyesi

BLACK MOOR


Chombo cha kufugia kinatakiwa kiwe na sehemu za kujificha samaki kiasi cha 50% - 70% ili samaki wajione wako salama. Hakikisha unapunguza maji 25% kila baada ya wiki na kuweka maji mapya, na kila baada ya wiki 4 unatoa maji yote, unasafisha chombo chako, mawe, filter pamoja na urembo uliopo ndani na kuweka maji mapya 100%

TELESCOPE EYES

Gold fish huwa wanakula mara mbili kwa siku, tumia chakula maalum ambacho kinauzwa madukani, vyakula kama uduvi, dagaa na ubongo vinaweza kulishwa kama wako kwenye bwawa tu kwa sababu huchafua sana vioo na maji. Gold fish huwa wanakula chochote kile (omnivorous)ila inabidi uwe makini usije ukawalisha zaidi (overfeeding) kwa sababu wanaweza kufa

GOLD



Hakikisha chombo kina mfumo wa kusafisha maji (filter) na mfumo wa uingizaji hewa (pump)ili kujua kipimo halisi cha ukubwa wa filter na pump itabidi usome mwongozo wa mtumiaji na mtengenezaji (user manual)

BUBBLES