KURASA

Sunday, August 18, 2013

KUPUNGUZIA MATAWI KWENYE MICHE YA NYANYA

Kuna baadhi ya wasomaji wangu walipenda kufahamu umuhimu wa kupunguzia matawi kwenye zao la nyanya na pia jinsi ya kupunguzia matawi hayo.
Umuhimu wa kupunguzia matawi kwenye zao la nyanya ni kupata nyanya bora, kubwa na zenye afya, ukiacha mti uwe na matawi utatoa maua mengi sana na utaishia kupata nyanya ndogo ndogo ambazo hazina soko zuri, lakini ukipunguzia matawi nyanya zako zitakuwa kubwa na mmea wako utazaa kwa mpangilio na kwa muda mrefu

Jinsi ya kupunguzia matawi ni kwa kutofautisha maua ni yapi na matawi ni yapi kisha unaondoa matawi kwa kutumia mkono tu, usitumie kisu maana itakuwa rahisi kusambaza magonjwa toka mme mmoja hadi mwingine, mara nyini matawi hutoke kati ya shina na jani kama inavyoonekana kwenye picha hapo chini




NYANYA KUBWA ZENYE AFYA


NYANYA DOGO TOKA KWENYE MMEA WENYE MATAWI MENGI