KURASA

Tuesday, September 4, 2012

SOTOKA YA MBUZI - Peste des Petits Ruminants (PPR)

Ugonjwa huu husababishwa na virusi na hushambulia kondoo na mbuzi ukiwa na dalili zote kama sotoka (rinderpest) inayoshambulia wanyama kama ng'ombe, nyati, ngamia nk. kwa taarifa tu ni kwamba ugonjwa wa sotoka (rinderpest) ulitokomezwa duniani mwaka 2011 na shirika la afya duniani WHO kudhibitisha hilo. Ugonjwa wa PPR ulisambaa sana miaka ya 1980 na kuathiri sehemu kubwa ya Afrika na duniani kote na ugonjwa wa PPR huwashambulia zaidi mbuzi kuliko kondoo na kwenye ng'ombe unaweza kuukuta kwa kupima damu lakini ng'ombe hawataonyesha dalili wala kuweza kusambaza ugonjwa huu wa PPR.

Ugonjwa huu huweza kuua wanyama kwa kiwango cha mpaka asilimia 100% kutegemeana na umri wa wanyama, afya, lishe na kuchoka kutokana na kufuata malisho   umbali mrefu sana. kwa wanyama wenye umri kati ya miezi 4 - 8 hali huwa mbaya zaidi na pia wanyama wenye maradhi mengine ni rahisi kushambuliwa kutokana na kinga kuwa chini

KUSAMBAA
Ugonjwa PPR husambaa kwa njia ya kugusana na virusi vya ugonjwa huu huwa kwenye matongotongo, makamasi, mate na kinyesi cha wanyama, kwa hiyo mnyama mwingine akigusa kimoja kati ya hivi ataambukizwa ugonjwa huu

DALILI
Dalili kwa wanyama ni kama kuharisha, homa kati ya siku 5 - 8, mnyama hutoa makamasi ya kawaida na baadae kubadilika rangi na kuwa ya kahawia kuziba pua na kusababisha ugumu wakati wa kupumua, michubuko kwenye pua na midomo na pia kusababisha wanya kutoona vizuri na matongo tongo kwenye macho, mnyama kuishiwa maji mwilini na pia mimba kutoka

UCHUNGUZI
Uchunguzi wa kitaalamu kugundua ugonjwa huu utafanywa na maafisa ugani wa mifugo kwa kuukagua mwili kuona uwepo wa makamasi ya kahawia, mnyama kutoa kinyesi cha maji maji chenye harufu mbaya, pia watachunguza njia ya hewa, chakula na sehemu ya juu ya mdomo (hard palate) kwney utumbo wa mnyama huwa na mistari kama ya pundamilia, kuvimba kwa mitoki na usaha kwenye mapafu, baada ya hapo damu ya  mnyama itachukuli na kupelekwa kwenye maabara ikisafirisha kwenye hali ya ubaridi (refrigeration)

DAWA
Ugonjwa wa PPR hauna dawa ila kwa wanyama watakaoweza kuhimili dawa za kuua bakteria (antibiotics) zitasaidia kuzuia mashambulizi ya juu dhidi ya bakteria

KINGA
Chanjo ya ugonjwa huu ipo, wasiliana na maafisa ugani wa mifugo katika eneo lako chanjo ni muhimu mara moja kwa mwaka kabla ya kuanza kwa mvua za masika, tenga wanyama wapya wiki tatu kabla ya kuwachanganya na wengine, tenga wanyama wagonjwa na wazima mara ugonjwa unapoibuka, osha mabanda yako kwa dawa zakuulia virusi kama virukill au tumia dawa za madoa kama JIK kiasi cha lita kwa lita 30 za maji kisha pulizia