KURASA

Monday, December 14, 2009

NDIGANA KALI - EAST COAST FEVER (ECF)

Huu ni ugonjwa wa ng’ombe, nyati na nyati wa India wakaao kwenye maji (water buffalo) ambao umeenea sana hapa nchini kwetu, msambazaji mkuu ni kupe (rephicephalus appendiculatus) na ng’ombe huanza kuugua siku 10 – 25 (wastani siku 14) toka kuambukizwa ugonjwa huu, protozoa aina ya theileria parva ndiye husababisha ugonjwa huu



DALILI KUU ZA NDIGANA KALI
-Joto kali hadi kufikia 42c kwa kawaida ng’ombe huwa na joto 38c
-Manyoya ya mgongoni husimama muda wote na huwa na rangi ya udongo (brown) kwa mbali
-Kuharisha
-Kutoa makamasi laini
-Matezi ya shingo kuvimba
-Kupe aina ya rephicephalus appendiculatus utawaona kwenye masikio ya mnyama (sio lazima)
-Mnyama hushindwa kula vizuri
-Pua (muzzle) huwa kavu bila unyevu unyevu



TIBA
Dawa aina ya BUTALEX ni maarufu sana hapa nchini kwa ajili ya kukabiliana na ugonjwa huu, ni muhimu dalili za mwanzo zinapoonekana kumtaarifu mtaalam wa mifugo na ikithibitika ni Ndigana kali tiba ianze mara moja ikiambatana na OTC 20% ili kushusha homa.

KINGA
Kinga kubwa ni kuogesha mifugo yako mara kwa mara, dawa ya ruzuku ijulikana yo kama PARANEX hupatikana katika maduka yote ya kilimo na mifugo. Dawa nyingine nazo zinafaa kuogeshea kwa kufuata masharti ya mtengenezaji.