KURASA

Thursday, May 17, 2012

MBOLEA VUNDE


1. Namna ya kutayarisha Mboji/Mbolea Vunde/Mbolea Hai
Mboji ni sehemu ya viumbe (mabaki ya mimea na wanyama (matamahuruku)) ambayo imeozeshwa kwa muda mrefu ili kusazwa na viumbe vidogo vidogo. Sehemu za vitu kama majani, matunda na mabaki ya mboga hutengeneza mbolea ya mboji. Matokeo ya kusazwa huku ni tofauti kabisa na zile sehemu zilizowekwa. Mboji iliyoiva hubadilika rangi na kuwa ya hudhurungi, tifutifu na hunukia vizuri.
Mboji ni rahisi kutengeneza, gharama zake ni za chini sana na inafaa mno kuongezwa kwenye udongo ili kuinua mazao ya shamba.
Vipande vya vitu au sehemu ya viumbe mara nyingi huwa vimejazwa nyumbani au shambani bila mpangilio wowote. Hivi vinaweza kutumika kutengenezea mboji lakini itachukua muda mrefu kabla ya kuoza, na hivyo rotuba yake kupotea. Lakini kama muda ukitengwa ili kushugulikia mbolea matokeo yatakuwa mazuri na ya kufaa. Mabaki kutoka shambani na jikoni yanatumika katika kutengenezea mboji.
Mboji iliyotunzwa vyema huwa na rutuba nzuri kwa mimea inapotumiwa shambani. Mboji huchemka hata kiasi cha kuua magonjwa ya mimea na mbegu za magugu.
Majani makavu ya ndizi ni mazuri kwa kutunza vifaa vya mbolea na kuweka ukavu. Hali hii huwa huzuia kupotea kwa maji kabla ya kujenga lundo la mboji na wakati mbolea inapokuwa inaiva.


1.1 Vifaa visivyofaa kuwekwa kwenye mboji
 Sehemu za mimea ambazo zimenyunyiziwa dawa ya kuwaua wadudu (viuatilifu) na kwekwe juzijuzi (Pesticide/herbicides).  Vipande vya nyama kwa sababu vinavutia panya na wadudu wengine. Sehemu nyingi za Mboji ni sehemu ya viumbe (mabaki ya mimea na wanyama (matamahuruku)) ambayo imeozeshwa kwa muda mrefu ili kusazwa na viumbe vidogo vidogo. Sehemu za vitu kama majani, matunda na mabaki ya mboga hutengeneza mbolea ya mboji. Matokeo ya kusazwa huku ni tofauti kabisa na zile sehemu zilizowekwa. Mboji iliyoiva hubadilika rangi na kuwa ya hudhurungi, tifutifu na hunukia vizuri. Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea , Mboji ni rahisi kutengeneza, gharama zake ni za chini sana na inafaa mno kuongezwa kwenye udongo ili kuinua mazao ya shamba. Vipande vya vitu au sehemu ya viumbe mara nyingi huwa vimejazwa nyumbani au shambani bila mpangilio wowote. Hivi vinaweza kutumika kutengenezea mboji lakini itachukua muda mrefu kabla ya kuoza, na hivyo rotuba yake kupotea. Lakini kama muda ukitengwa ili kushugulikia mbolea matokeo yatakuwa mazuri na ya kufaa. Mabaki kutoka shambani na jikoni yanatumika katika kutengenezea mboji.  Mboji iliyotunzwa vyema huwa na rutuba nzuri kwa mimea inapotumiwa shambani. Mboji huchemka hata kiasi mimea na majani ambazo ziliambukizwa ugonjwa.  Vifaa vilivyo na ncha kali kama mwiba ambavyo vyaweza kujeruhi mikono na miguu. Magugu ambayo yanarudiarudia kila mwaka. Magugu kama hayo huuliwa kwa kuanikwa kwenye jua kali ili yakauke baadaye huchomwa ili yasienee na jivu lake huongezwa kwenye biwi, matunda na mabaki ya mboga hutengeneza mbolea ya mboji. Matokeo ya kusazwa huku ni tofauti kabisa na zile sehemu zilizowekwa. Mboji iliyoiva hubadilika rangi na kuwa ya hudhurungi, tifutifu na hunukia vizuri.

Mboji ni rahisi kutengeneza, gharama zake ni za chini sana na inafaa mno kuongezwa kwenye udongo ili kuinua mazao ya shamba.
Vipande vya vitu au sehemu ya viumbe mara nyingi huwa vimejazwa nyumbani au shambani bila mpangilio wowote. Hivi vinaweza kutumika kutengenezea mboji lakini itachukua muda mrefu kabla ya kuoza, na hivyo rotuba yake kupotea. Lakini kama muda ukitengwa ili kushugulikia mbolea matokeo yatakuwa mazuri na ya kufaa. Mabaki kutoka shambani na jikoni yanatumika katika kutengenezea mboji.
Mboji iliyotunzwa vyema huwa na rutuba nzuri kwa mimea inapotumiwa shambani. Mboji huchemka hata kiasi cha kuua magonjwa ya mimea na mbegu za magugu.
Majani makavu ya ndizi ni mazuri kwa kutunza vifaa vya mbolea na kuweka ukavu. Hali hii huwa huzuia kupotea kwa maji kabla ya kujenga lundo la mboji na wakati mbolea inapokuwa inaiva.


1.1 Vifaa visivyofaa kuwekwa kwenye mboji
 Sehemu za mimea ambazo zimenyunyiziwa dawa ya kuwaua wadudu (viuatilifu) na kwekwe juzijuzi (Pesticide/herbicides).  Vipande vya nyama kwa sababu vinavutia panya na wadudu wengine. Sehemu nyingi za Mboji ni sehemu ya viumbe (mabaki ya mimea na wanyama (matamahuruku)) ambayo imeozeshwa kwa muda mrefu ili kusazwa na viumbe vidogo vidogo. Sehemu za vitu kama majani, matunda na mabaki ya mboga hutengeneza mbolea ya mboji. Matokeo ya kusazwa huku ni tofauti kabisa na zile sehemu zilizowekwa. Mboji iliyoiva hubadilika rangi na kuwa ya hudhurungi, tifutifu na hunukia vizuri. Maelezo ya msingi kuhusu mboji/mbolea vunde/mbolea , Mboji ni rahisi kutengeneza, gharama zake ni za chini sana na inafaa mno kuongezwa kwenye udongo ili kuinua mazao ya shamba. Vipande vya vitu au sehemu ya viumbe mara nyingi huwa vimejazwa nyumbani au shambani bila mpangilio wowote. Hivi vinaweza kutumika kutengenezea mboji lakini itachukua muda mrefu kabla ya kuoza, na hivyo rotuba yake kupotea. Lakini kama muda ukitengwa ili kushugulikia mbolea matokeo yatakuwa mazuri na ya kufaa. Mabaki kutoka shambani na jikoni yanatumika katika kutengenezea mboji.  Mboji iliyotunzwa vyema huwa na rutuba nzuri kwa mimea inapotumiwa shambani. Mboji huchemka hata kiasi mimea na majani ambazo ziliambukizwa ugonjwa.  Vifaa vilivyo na ncha kali kama mwiba ambavyo vyaweza kujeruhi mikono na miguu.huwa vimejaa nyumbani au shambani bila mpangilio wowote. Hivi vinaweza kutumika kutengenezea mboji lakini itachukua muda mrefu kabla ya kuoza, na hivyo rotuba yake kupotea. Lakini kama muda ukitengwa ili kushugulikia mbolea matokeo yatakuwa mazuri na ya kufaa. Mabaki kutoka shambani na jikoni yanatumika katika kutengenezea mboji.
 Mboji iliyotunzwa vyema huwa na rutuba nzuri kwa mimea inapotumiwa shambani. Mboji huchemka hata kiasi mimea na majani ambazo ziliambukizwa ugonjwa.
 Vifaa vilivyo na ncha kali kama mwiba ambavyo vyaweza kujeruhi mikono na miguu.
 Magugu ambayo yanarudiarudia kila mwaka. Magugu kama hayo huuliwa kwa kuanikwa kwenye jua kali ili yakauke baadaye huchomwa ili yasienee na jivu lake laweza kuongezwa kwenye lundo la mbolea.
 Vitu visivyo kua na uhai kama plastiki na chuma. 


1.2 Mfano wa vitu vinavyoweza kutumiwa kutengenezea mboji nyumbani





2. Namna ya kutengeneza mboji ya mimea
Kusanya vitu na vifaa vinavyohitajika katika utengenezaji wa mboji ambayo ni;
 Majani mengi mabichi/kijani na makavu. Majani jamii ya mikunde ni mazuri sana kwani hutengeneza kirutubishi cha naitrojeni (N) kwa wingi.
 Mabua ya mahindi au vitawi vya miti
 Udongo wa kawaida wa juu
 Samadi, mbolea yoyote ya wanyama au mboji ya zamani
 Majivu au vumbi la mkaa
 Maji

2.1 Hatua
1) Chagua sehemu karibu na eneo ambalo mboji itaenda kutumika na ambapo kuna hifadhi ya kutosha kukinga dhidi ya upepo, jua na mvua.
2) Katakata majani yawe madogo madogo ili yaweze kuoza haraka. Tengeneza msingi kama mita sita (6) urefu na upana wake mita 2 kwa kutumia majani magumu kama matawi/vijiti. Hii itahakikisha maji yanatiririka na hewa ina zunguka vizuri. Hakikisha kuna nafasi ya kutosha kufanyia kazi kwenye biwi bila kulikanyaga.
3) Weka sentimita 10 ya majani ambayo hayaozi haraka kwa mfano mabua vya mahindi au mimea mibichi/kijani.
4) Weka sentimita 10 ya vifaa ambavyo huoza haraka kwa mfano maganda ya mboga na matunda.
5) Weka sentimita 2 ya samadi (mbolea-hai ya wanyama), mabaki ya mbolea ya zamani kama yaweza kupatikana.
6) Weka udongo wa juu sentimita 10 kutoka kwenye shamba ambalo hulimwa.
7) Majivu na mkojo vyaweza kunyunyuziwa juu ili kufanya biwi/lundo kuoza haraka. Kukatakata majani
8) Nyunyizia maji kwenye biwi mpaka lilowe.
9) Rudia mpangilio huu kuanzia namba nne (4) mpaka lundo lifike mita moja (1.m) hadi moja na nusu (1.5m) kwenda juu isipokuwa vijiti/matawi ya kwanza.

2.2 Zingatia
Biwi/lundo cha mboji kinatakiwa kifunukwe ili kupunguza/kuzuia mvuke ama mvua nyingi ambayo hubeba rotuba kutoka kwenye mbolea. Weka gunia, nyasi ama matawi ya ndizi yaliyokauka.



 Kila tabaka/kunjo/safu yafaa kupangwa kuanzia kwenye ukingo ili lundo la mbolea lisiporomoke.
 Namna nyigine ya kuzuia lundo kuporomoka ni kwa kuweka vipande vya mbao kando ya biwi. Wavu wa nyuzi za chuma utafanya biwi kukauka.



3. Wadudu wenye manufaa na mazingira yanayohitajika kwenye Biwi
3.1 Wadudu ambao husaidia kufanya biwi kuoza
Viumbe wengi wanaohusika na kazi hii ya kuoza ni wadogo hawaonekani kwa macho matupu. Ila viumbe hawa huhitaji maji, hewa na vipande/sehemu ya viumbe wengine ambazo kwao ni chakula. Viumbe hawa hula vipande hivyo na hutoa hewa ya carbon dioxide, maji na joto.
Kuna hatua tatu kubwa wakati biwi linapooza; hatua ya kupanda joto, hatua ya kupoa/kuwa baridi na hatua ya kukomaa.
Wakati ya hatua ya kupanda joto, joto hufikia kiwango cha juu sana katikati mwa biwi. Uzuri wa joto hili ni kwamba magonjwa yaliyokuwa kwenye viungo vya biwi na mbegu za magugu huchomwa hadi kufa. Hatua ya pili ya kuwa baridi; uyoga (fungi) huwa na faida nyingi kwa sababu kazi yake ni kuzisaga nyuzi ngumu ambazo zimo kwenye viungo vya mimea au majani.
Kwenye hatua ya tatu, ‘hatua ya kukomaa’ viumbe wakubwa kama mchwa na nyungunyungu husaidia kusaga na kuchanganya mbolea.
Hali ya anga ikiwa na joto jingi viumbe hawa hufanya kazi haraka kuliko wakati ambapo hali ya anga ni baridi. Aina ya viungo vilivyotumika kujenga/kukuza biwi na ukali/uchungu (pH) wa udongo pia huathiri kiwango cha mbolea kuoza.
3.2 Mazingira yanayohitajika kwenye biwi
Biwi huhitaji vitu vitatu: hewa, maji na joto.

Hewa
Viumbe wadogo kwenye biwi huhitaji hewa ili waweze kuishi. Hewa ya carbon dioxide (CO2) ambayo imetolewa na wadudu hawa huhitaji kutolewa nje. Ikiwa hewa safi itakosekana, viumbe wengine wasiohitajika huingia na kutoa harufu mbaya na pia kufanya mbolea isioze haraka.

Maji
Kazi ya viumbe wadogo huwa polepole ikiwa biwi ni kavu. Aidha ikiwa biwi litalowa maji basi viumbe wadogo watakufa na kufanya biwi kuwa na uchachu badala ya kutengeneza mbolea. Hivyo basi kukagua kiwango halisi cha maji huhitaji ujuzi fulani.
Joto
Biwi hutoa joto wakati linaoza. Lundo likiwa na joto jingi viumbe wadogo hutoka, kisha huweza kurudi pindi linapopoa.
4. Matunzo ya Biwi
Ili kupata mbolea nzuri, biwi linapojengwa yafaa lishughulikiwe kwa utaratibu. Biwi hilo litahitaji maji, kupinduliwa, joto na muda unaofaa wa kukomaa.

4.1 Maji
Wakati wa kiangazi biwi/lundo la mboji huhitaji kumwagiliwa maji kila wiki. Maji katika lundo la mbolea hupimwa kwa kuweka fungu dogo la nyasi na kulitoa baada ya dakika tano. Nyasi isipoonyesha majimaji au unyevu itabidi maji yamwagwe kwenye lundo hilo.
Kuna njia kadha za kuzuia mvuke kuinuka kutoka kwenye biwi, hali kadhalika kiwango cha maji yanayomwagiliwa:
 Funika lundo kwa majani ya ndizi ama nyasi.
 Funika lundo kwa udongo.
 Lundo lisigeuzwegeuzwe

Biwi likilowa maji itabidi kifunuliwe na kuachwa kikauke kwenye jua kabla ya kujengwa tena.

4.2 Kupindua/kugeuza
Katika muda wa wiki tatu (3) baada ya kujenga/kukuza biwi/lundo ukubwa wake utakuwa umepungua sana. Kupindua biwi uhakikishe ya kwamba majani yaliyo kando yameoza pia hewa safi imerejeshwa. Kupindua biwi huchanganya majani yaliyotengenezwa na kukijenga upya. Majani yalivyo kando huwekwa katikati, ikiwa kuna ukavu, maji mengi na majani/viungo vikavu huongezwa. Kupindua kunatikiwa kufanyike kila baada ya wiki tatu.
Hali ya joto na kiwango cha maji yafaa kupimwa siku chache baada ya kupinduliwa. Kupinduliwa kwa mara ya tatu kutahitajika ikiwa viungo havitakuwa vimeoza kikamilifu. 


Mbolea yaweza kutengenezwa bila kupinduliwa ila viungo vilivyo kando havitaoza. Mbegu za magugu na viungo na magonjwa ya mimea hayatakufa. Viungo vilivyobaki hutengwa na kutumiwa kwenye biwi lingine. Japokuwa kugeuza hakuna lazima, kunapendekezwa ili kupata mbolea nzuri.

4.3 Kiwango cha Joto
Kupima kiwango cha joto kwenye biwi kunahitaji kijiti kirefu kichomwe ndani ya lundo siku kumi (10) baada ya kujengwa. Kijiti yafaa kionyeshe joto la kutosha kinapoguswa kwa mkono, la sivyo kuoza bado hakujaanza kufanyika. Katika hali kama hii, maji ama hewa itahitajika kwenye biwi na biwi kuachwa kwa muda. Ikiwa biwi lina joto jingi, biwi linaoza basi viumbe hai wanaweza kufa. Katika hali hii, hewa na maji itabidi kuongezwa ili kufanya biwi lipoe. Kiasi cha joto yafaa kupimwa mara kwa mara kwa kutumia kijiti.



Chini ya 57C
Joto hili linaweza kuivisha mboji lakini haliwezi kuua mbegu za magugu na magonjwa.

57-71C
Joto muafaka kwaajili ya kuivisha mbojj na kuua mbegu za magugu na magonjwa. Katika kiwango hiki cha joto, mbegu zote na vijimelea vyote vya magonjwa vilivyoko kwenye mchanganyiko wa mboji hufa na hivyo kutokuwepo pale mboji inapokuwa imeiva.

Zaidi ya 71C
Joto hili ni kali sana na huweza kusababisha madhara mengineyo kama vile kuzalishwa kwa gesi zenye madhara pia wadudu wenye manufaa ambao husaidia mboji kuiva huweza kukimbia. 


Muhimu kuhakikishakuwa joto halizidi sana ili kuweza kuwa na mboji bora yenye virutubisho




KILIMO BORA CHA NYANYA



Nyanya ni aina ya mboga inayo zalishwa kwa wingi sana duniani. Kwa Tanzania, nyanya ni zao la kwanza katika mazao ya mboga linalo limwa na kuliwa kwa wingi ukilinganisha na mboga zingine. Nyanya hutumika karibu Katika kila mlo. Kulingana na umuhimu wa zao hili kama chakula na pia kama zao linalomwingizia kipato Mkulima, kuna haja ya kutoa mafunzo kuhusu mbinu bora za uzalishaji wake. Pia kuna umuhimu wa kufundisha wakulima kutoka sehemu zingine wasiolima zao hili ili nao waweze kuzalisha nyanya na hivyo kuongeza idadi ya aina za mboga katika maeneo yao.




MAHITAJI YA ZAO LA NYANYA
Nyanya hustawi vizuri kwenye maeneo ya joto, yasiyo na ukungu mwingi hasa wakati zao linatoa maua na matunda. Zao hili hupenda kipindi kirefu cha jua na joto ili kuongeza ukuaji wa matunda na kupunguza magonjwa ya aina ya ukungu/kuvu. Zao hili halipendi mvua nyingi ingawa linahitaji maji kwa wingi. Katika kipindi chenye mvua nyingi na jua kidogo nyanya hushindwa kutoa maua na matunda ya kutosha bali huweka majani mengi. Katika kipindi hiki pia, nyanya hushambuliwa sana na magonjwa ya ukungu. Nyanya hupendelea udongo unaopitisha maji kwa urahisi na wenye rutuba ya kutosha na hivyo hupenda samadi. Udongo uwe umetifuliwa vya kutosha kuruhusu mizizi kushika vema.


AINA ZA NYANYA
Kuna aina kuu mbili za nyanya kulingana na ukuaji wa mmea: yaani nyanya inayo refuka zenye kuhitaji egemezi (mfano Money maker) na aina ya pili ni nyanya fupi zenye kutoa matawi mengi mfano Roma na Cal J.


UKUAJI WA MICHE
Miche ya nyanya huzalishwa kwenye kitalu kwa kupanda mbegu. Mbegu za nyanya huota baada ya siku 5 hadi 10. Baada ya kukua kitaluni kwa muda wa wiki 4 hadi 5 toka kuota kwa mbegu, miche hupandwa shambani. Kabla ya kupandikiza shambani miche huandaliwa kwa kupunguza umwagiliaji maji kwa siku moja au mbili ili miche izoee hali ngumu kabla ya kuhamishiwa shambani. Hapo shambani miche hupandikizwa kwa kuzamishwa katika kina kirefu zaidi ya ilivyo kuwa kitaluni. Hii inasaidia miche kutoa mizizi ya pembeni mingi zaidi kwa ajili ya kufyonza maji pamoja na virutubisho aridhini. Baada ya kupandikiza mwagilia maji ya kutosha. Usimwagilie maji juu ya mche wa nyanya. Katika kipindi cha jua kali, tandaza nyasi kwenye tuta ili kupunguza upotevu wa maji na unaweza kuweka kivuli kwa kutumia majani ya miti au migomba. Kulingana na aina ya nyanya na rutuba ya udongo, nafasi ya kupandia ni sm 60 kati ya mstari hadi mstari na 45 hadi 60 nafasi ya mche hadi mche. Kama udongo hauna rutuba ya kutosha inapendekezwa kutumia nafasi kubwa ya kupanda.


UTUNZAJI
Nyanya fupi zisizo refuka kwenda juu, ni rahisi sana kutunza na hazihitaji huduma nyingi. Tatizo kubwa ni kuwa kwa kutambaa chini, katika kipindi cha mvua huwa karibu na magonjwa yatokanayo na udongo. Katika kipindi cha jua kali, matunda huungua kwani mmea huwa na majani machache tu yanayo kinga matunda yasipigwe na mionzi ya jua.


MBOLEA
Licha ya mbolea ya kupandia, unashauriwa kuongeza mbolea kipindi cha wiki mbili au tatu baada ya kupandikiza miche bustanini. Mbolea hii ya kukuzia iwekwe kuzunguka shina la mmea kwa umbali wa sentimeta 5 hadi saba kutoka kwenye shina. Kwa mbolea kama vile CAN, NPK, au SA tumia kifuniko kimoja cha soda kwa shina. Mbolea hii inaweza kuwekwa mara mbili kabla ya mvuno wa kwanza. Ili kurefusha kupindi cha uzaaji wa zao la nyanya (na hata mazao mengine yatoayo matunda kama vile nyanya chungu, biringanya, pilipili hoho, nk) inapaswa kuongezea mbolea katika kipindi cha uvunaji mfano baada ya kuvuna mara mbili unashauriwa kuongeza mbolea ya samadi na mbolea kama vile NPK. Hii inasaidia mmea kuendelea kutoa maua bila kuchoka. Kwa kawaida nyanya fupi jamii ya “Roma” huweza kuzaa na kuvunwa kwa kipindi cha wiki 6 hadi 8 tu. Lakini kama utakuwa unaongezea mbolea na kukazania matunzo ya bustani (hasa usafi wa bustani na Kumwagilia maji ya kutosha), nyanya zinaweza kuendelea kuzaa kwa muda mrefu zaidi. Hii ni tofauti
na mazoea ya wakulima wengi kuwa mara nyanya zianzapo kuzaa huduma za palizi na usafi wa shamba huachwa na kutilia maanani kazi ya kuvuna pekee. Hii inajitokeza zaidi kwenye aina ya nyanya fupi.
Kwa nyanya fupi ni vizuri kuhakikisha kuna matawi mengi iwezekanavyo ili kuweza kupata matunda mengi zaidi. Hivyo usipunguze matawi katika aina hii ya nyanya. Kwa nyanya ndefu zenye kuhitaji egemezi,tunashauriwa kukuza nyanya kwa tawi moja lisilo na vichipukizi pembeni au matawi mawili na kuacha mnyanya urefuke.
Kupunguza majani ni muhimu pia katika kupunguza maambukizo ya ukungu katika shina na pia kutoa nafasi ili
mwanga kupenya na kuruhusu mzunguko wa hewa. Majani yapunguzwe kipindi cha asubuhi kwa kutumia mkono na siyo kisu kwani kinaweza kueneza magonjwa kutoka mche hadi mche. Kwa nyanya ndefu, majani ya chini ya matunda huondolewa kadiri unavyo endelea kuvuna. Unashauriwa upunguze majani wakati wa asubuhi kwa kutumia mkono na pia usitoe zaidi ya majani matatu katika mmea kwa mara moja.


UMWAGILIAJI
Nyanya ni zao linalohitaji maji mengi sana kwa ajili ya ukuaji wa mmea na matunda yake. Umwagiliaji uwe wa kulingana kwa kila siku iliyo pangwa. Usibadilishe ovyo kiasi cha maji na ratiba ya kumwagilia. Hii inasababisha kuoza kwa kitako cha nyanya. Pia ili kutunza maji katika udongo, inashauriwa kuweka matandazo katika mzunguko wa shina la nyanya au bustani yote. Nyanya inayo kua vizuri hutumia maji lita mbili kwa siku
katika kipindi cha jua kali. Hivyo katika umwagiliaji ni busara kuzingatia kiasi hiki cha maji katika kipindi kama hiki. Pia kama unatumia keni, mpira au bomba usimwagilie maji juu ya matawi ya nyanya kwani umwagiliaji wa namna hii utasababisha kuenea kwa magonjwa ya ukungu.


MATATIZO YA KILIMO CHA NYANYA
Matatizo yanayosumbua kilimo cha zao hili ni magonjwa na wadudu waharibifu. Hapa tutajifunza mbinu mbali mbali za kuzuia magonjwa na wadudu waharibifu.


WADUDU WAHARIBIFU

FUNZA WA NYANYA (Funza wa vitumba)
Huyu funza hushambulia mazao mengine kama vile pamba, mahindi, mtama, maharage n.k. Mdudu huyu hushambulia matunda ya nyanya kwa kutoboa na hivyo kuyafanya yapoteze soko kwasababu hayafai kuuzwa katika soko na pia yanaweza kuoza wakati wa usafirishaji. Ili kuthibiti piga dawa ya kuua wadudu kama vile thiodan, sevin ya unga, karate, selecron, n.k. Muarobaini hutumika pia katika kupunguza uharibifu wa mdudu huyu.


INZI WEUPE

Wadudu hawa huruka ruka kwenye shamba la nyanya na kukaa chini ya majani. Mdudu huyu hueneza magonjwa ya virusi kama vile “ukoma wa nyanya”. Usafi wa shamba na mazingira ya yake ni muhimu katika kupunguza kuzaana kwa wadudu hawa. Ili kuthibiti wadudu hawa kwenye bustani ya mboga na pia katika maficho yao, piga dawa kama vile karate, cypermethrin mara kwa mara. Panda mimea mingine (kama vile tumbaku) inayo vutia wadudu hawa kwenye maeneo ya bustani kisha piga dawa katika miche ya tumbaku ili kuwaangamiza kwa wingi.



MINYOO
Mdudu huyu hukaa kwenye udongo wenye unyevu wa kutosha. Huvamia mizizi ya nyanya na kuharibu mfumo wa usafirishaji maji na chakula kwenye nyanya iliyo athirika. Uking'oa mche wa nyanya utaona vifundo kwenye mizizi.
KUZUIA
Mbinu za kuthibiti ongezeko la wadudu hawa ni kuharibu hali ya udongo inayo mfanya aishi na kuzaana. Mbinu hizi ni: Kulima shamba kwa kutifua baada ya kuvuna nyanya ili udongo wa chini ukae juani na kukauka. Hii inasaidia kuangamiza wadudu hawa kwa joto na ukosefu wa maji. Choma moto na kuteketeza mabaki ya nyanya baada ya kuvuna. kuzungusha aina ya zao la nyanya au jamii ya nyanya na mazao mengine yasiyo vamiwa na adui huyu. Hii huwafanya minyoo wasipate hifadhi na chakula kutoka kwenye mimea wanayo tumia kuishi na kuzaliana. Hivyo idadi yao kupungua katika udongo. kabla ya kupanda zao weka samadi nyingi katika udongo kwenye eneo lililo athiriwa na wadudu hawa kwani hawapendi udongo wenye samadi nyingi. Panda manung'a nung'a (Tagetes spp) katika eneo lililoathirika na minyoo hawa, mimea hii hutoa sumu ya aina fulani ambayo huathiri ukuaji na kuzaliana kwa minyoo hawa.


MAGONJWA
Uchunguzi umeonyesha kuwa katika maeneo ya Kilombero na Gairo, nyanya na mazao mengine jamii ya nyanya ndiyo hushambuliwa sana na magonjwa kuliko mazao mengine ya mboga.


UKUNGU
Huu ni ugonjwa unaopenda hali ya unyevu mwingi hewani. Hivyo hujitokeza zaidi wakati wa masika. Pia sehemu zenye umande mwingi wakati wa usiku, ugonjwa huu hujitokeza hata wakati wa kiangazi.


DALILI ZAKE
Ugonjwa huu hushambulia shina, maua na matunda. Kuungua kwa majani kama vile yamechomwa na maji moto. Chini ya jani utaona unga unga mweupe. Matunda pia hushambuliwa na ugonjwa huu na hugeuka kuwa meusi na magumu.


KUZUIA
Inabidi kuchanganya mbinu mbali mbali za kupambana na ugonjwa huu. Kwanza ni usafi wa shamba kwa jumla yaani hakikisha unaondoa magugu katika bustani. Tandaza nyasi juu ya matuta yaliyo pandwa nyanya. Ondoa majani yaliyo zeeka na yanayo onyesha dalili za ugonjwa huu. katika kupunguza majani, hakikisha sehemu za chini ya mmea ni wazi na kuna mzunguko mzuri wa hewa. Punguza majani katika mmea ili kupunguza umande na ukungu kwenye mmea. Baada ya kupunguza majani na machipukizi hakikisha unatupa mbali majani hayo na siyo kuyaacha kwenye tuta la bustani. Ondoa kabisa mmea ulio na dalili za ugonjwa huu Kupiga dawa katika kipindi cha mvua mara baada ya mvua kubwa. Fanya hivyo mara moja au mara mbili kwa wiki kutegemea na wingi au mfululizo wa mvua. Unapoona jua limetoka piga dawa ili ugonjwa usijitokeze tena. Baadhi ya madawa yanayofaa kukinga ugonjwa huu ni Dithane M45, Bravo, Benlate , Ridomil, Topsin n.k. Kumbuka kuwa kila
mwaka madawa yenye nguvu zaidi hutengenezwa, hivyo uliza watalaam walioko karibu nawe. Ingawa Blue Copper inauzwa kwa bei nafuu, nguvu yake in kidogo sana kuthibiti huu ugonjwa. Muarobaini pia unaweza kutumika kupunguza ugonjwa huu. Changanya unga unaotokana na mbegu za muarobaini kiasi cha nusu kilo ya unga katika lita 20 za maji.


UKOMA WA NYANYA
Huu ni ugonjwa wa virus unao enezwa na inzi mweupe. Inzi hawa hushambulia zaidi nyanya wakati wa kiangazi, hasa kipindi cha joto kali.

DALILI
Majani machanga hujikunja na baadaye majani yote. Kupungua kwa utoaji maua na matunda na hata yakitokea matunda huwa ni madogo. Mmea kudumaa na kutozaa kabisa.






KUZUIA
Mbinu madhubuti ni kupunguza kuenea kwa ugonjwa huu kwenye shamba kwa kudhibiti kuzaana na kuenea kwa mdudu (inzi mweupe) kama tulivyo ona katika kupambana na mdudu huyo, yaani: Kuondoa mimea michache iliyo shikwa na ugonjwa maana wadudu hawa wanachukua ugonjwa huu kutoka mimea hii. Kutumia mbegu zilizo hakikishwa kuwa zinaweza kuvumilia ugonjwa huu na kutoa mavuno mazuri. Usilime nyanya karibu na eneo lililo na mazao kama bamia,mipapai maana mimea hii huhifadhi inzi mweupe. Kuua inzi weupe wanaofyonza nyanya na kusambaza virusi kwa kutumia madawa. Tumia madawa kama vile Selecron, Decis, Karate n.k. Epuka kuchanganya zao la nyanya na mazao mengine yanayohifadhi hawa nzi kama vile mipapai na bamia. Ng'oa na kuchoma moto mimea yote iliyougua ugonjwa huu.


UGONJWA WA KUOZA SEHEMU YA SHINA INAYOGUSA UDONGO NA MMEMA KUNYAUKA KAMA UMEKOSA MAJI
Wadudu wanaosabisha ugonjwa huu hupatikana ardhini. Hakuna dawa ya kutibu ugonjwa huu baada ya dalili
kujitokeza. Kupiga madawa za viwandani ardhini kabla ya kupanda nyanya husaidia kupungu wadudu wa ugonjwa. Epuka kupanda nyanya au mazao jamii ya nyanya katika eneo moja kwa muda mrefu mfulilizo. Baadhi ya mazao yanayohusiana na nyanya ni bilinganya, pilipili, ngogwe, mnavu, n.k.
Ugonjwa wa miche michanga ya nyanya kuoza sehemu ya shina inayogusa udongo na kufa ghafla
Ugonjwa huu hushambulia miche kitaluni na husabishwa na wadudu waishio ardhini. Mara baada ya dalili, ugonjwa huu hauna dawa ila unaweza kukingwa kwa kutumia njia zifuatazo: Choma moto udongo wa kutengenezea kitalu kabla ya kupanda mbegu zako. Kutumia mboji husaidia kukinga miche dhidi ya ugonjwa huu. Epuka kumwagilia maji kupita kiasi na kutumia kuvuli kizito


MATUNDA YA NYANYA KUOZA KITAKO
Huu ni ugonjwa unaosababishwa na: Umwagiliaji wa nyanya bustanini usio na mpangilio maalumu. Mfano, kumwagilia mimea maji mengi kisha kuiacha bila maji kwa siku kadhaa. Upungufu wa virutubisho aina ya chokaa. Dalili zake ni matunda ya nyanya kuoza sehemu ya kitako na kuonyesha rangi nyeusi. Kuzuia ugonjwa huu, zingatia kuwa na utaratibu mzuri wa kumwagilia maji ambao haubadiliki ovyo kiratiba na kiasi cha maji
yanayowekwa. Rutubisha mimea kwa madini ya chokaa kwa kutumia mbolea aina ya CAN zenye madini haya.



UPUNGUFU WA WADINI YA FOSFPRASI















Tuesday, May 8, 2012

UUNGAJI WA MICHE YA MATUNDA


Kuchagua matunda ya mlimao kutoka kwenye mti mama
Chagua na kuvuna malimao yaliyoiva vizuri.Usitumie malimao yaliyooza.
Miche ya milimao ndiyo imekuwa ikitumika sana kama miche shina kwa ajili ya kuunganisha michungwa na miti ya matunda ya jamii yake kama vile michenza, midimu, madalanzi, mawashington nk. 
Aina nyingine ya mmea shina kwa ajili ya kuunganisha michungwa na miti ya matunda ya jamii yake ni Karizo na Volkameriana. Aina hizi bado ni ngeni kwa watu wengi.

Kukamua na kundaa mbegu za malimao.
Kata tunda kwa mzunguko bila kuingiza kisu hadi katikati ya tunda ili kuepuka kukata mbegu. • 
Kamua mbegu zote kutoka kwenye tunda na ziweke kwenye chombo kisafi.Safisha mbegu ili kutoa utelezi wote (utelezi unazuia uotaji mzuri wa mbegu). • 
Chagua nbegu zinazozama kwenye maji kwani mbegu zinazoelea juu ya maji hazioti. • 
Mbegu za malimao zipandwe mara tu baada ya kusafishwa kwani kwa kufanya hivyo mbegu zinaota vizuri zaidi kuliko mbegu zinazokaushwa kwanza kabla ya kupanda.

Kuandaa tuta na kupanda mbegu za malimao
Andaa tuta lenye kimo cha sentimeta 20. Tumia udongo unaopitisha maji kwa urahisi ( udongo wa kichanga au mchanga wenyewe ni bora zaidi). Sawazisha vizuri sehemu ya juu ya tuta.

Kupanda mbegu za malimao:
Weka alama za mistari kwenye tuta kwa nafasi ya sentimeta kumi (10) mstari hadi msitari (alama hizo ziwe na kina cha sentimeta moja na nusu (1.5) hivi. Panda mbegu kwa kuzidondosha moja moja kwenye mstari kwa nafasi ya sentimeta moja (1). Fukia mbegu kwa kurudishia udongo wa pembeni ya mstari. Mbegu za limao zinaota siku ishirini na nane au zaidi toka siku ya kupandwa.


Kupandikiza miche shina ya milimao
Miche ya milimao ina pandikizwa ikiwa na majani mawili yaliyokomaa. Jaza udongo kwenye kiriba ukiacha nafasi ya sentimeta mbili juu kwa ajili ya kumwagilia maji. Ng'oa miche bila kuharibu mizizi. 
Pandikiza miche iliyo bora tu. Tumia kijiti au kifaa maalumu kuweka shimo katikati ya kiriba. • 
Weka mche kwenye shimo na shindilia udongo vizuri. 
Zingatia kwamba mmea unaweza kuathirika endapo udongo utafukiwa juu sana ya sehemu linalotenganisha mizizi na shina.

Kutunza miche shina ya mlimao
Ondoa matawi ya pembeni kila mara yanapojitokeza.Dhibiti wadudu na magonjwa kila vinapojitokeza. 
Miche wa mlimao inakuwa tayari kwa kuunganishwa inapofikia umri wa miezi sita (6) hadi miezi tisa (9) (hutegemea matunzo). Mche unakuwa kwenye hatua nzuri ya kuunganishwa unapofikia unene wa penseli.

NAMNA  YA UUNGANISHAJI MICHE JAMII YA MICHUNGWA
KWA KUTUMIA MKATO WA HERUFI T





KWA KUTUMIA KIPANDE




Kutunza miche iliounganishwa
Mwagilia maji mara kwa mara kuhakikisha kuna unyevu wa kutosha wakati wote.
Ondolea machipukizi chini ya sehemu iliyounganishwa ili chakula cha mmea kitumike kwenye sehemu ya juu
iliyounganishwa tu
Baada ya siku 14 hadi 21 mmea huwa tayari umesha ungana na mara nyingine vitawi kuchipua.
Kwa miche ya jamii ya michungwa huu ni wakati wa kufungua utepe/plastiki.
Kwa miche ya miembe baada ya kitawi kuchipua na kufikia majani manne yaliyokomaa ondoa utepe /plastiki kwa kuifungua polepole (utepe unaweza kufunguliwa mapema endapo utakuwa unaonekana kuuzuia mche kukua).
Tangu kubebesha hadi kupandikiza huchukua wastani wa miezi 3 hadi 6.
Ni vema kupandikiza mwanzo wa majira ya masika.
Mti uliobebeshwa unauwezo wa kutoa maua wakati wowote baada ya kuunga. Lakini si vema kuuruhusu uzae mapema kwani utadumaa.
Mti uruhusiwe kuzaa baada ya kupata ukubwa wa kutosha Kwa hali ya kawaida hii ni baada ya miaka mitatu.

Wadudu na magonjwa ya miche ya mitunda kitaluni
Wadudu na viumbe wengine jamii ya buibui, jamii ya minyoo wadogo wadogo na magonjwa vinavyoweza kuleta madhara kwa miche kwenye kitalu.

Wadudu waharibifu
i. Chawa mfuta
Hushambulia miche ya milimao, miembe na mchungwa kitaluni na bustanini.
Hufyonza utomvu kutoka sehemu changa za mmea na majani.
Wadudu hawa hutoa maji maji yenye sukari ambayo huvutia vimelea vya ukungu mweusi kutokea kwenye
majani na hivyo kuathiri shughuli za utengenezaji wa chakula cha mmea.

Kuzuia
Kuna wadudu wadogo wadogo wenye umbo la kobe wanaokula chawa mafuta. Jamii hii ya wadudu huonekana pia kwenye maboga.
Kama wadudu hawa wanaleta madhara unaweza kutumia dawa za kuulia wadudu kama vile Endosulfan (Thiodan), Diaziozon, Fenitrothion, Karate na Decis.
Pia tumia mbegu za mwarobaini zilizosagwa na kuchangaywa ndani ya maji pamoja na sabuni ya unga.
Matunda ya mti huu yameonyesha kupunguza kwa kiasi kikubwa wadudu wa aina hii.

ii. Viwavi wa majani ya mitunda jamii ya michungwa
Mama wa kiwavi huyu ni kiepeo mkubwa mwenye rangi nyeusi pamoja na mabaka meupe. Kipepeo jike hutaga
mayai kwenye majani na baada ya mayai kutotolewa viwavi hutokea. Huwa ni wadogo wenye rangi ya udongo ama kijani na alama nyeupe mgongoni. Viwavi hawa hutoa vitu kama pembe mbili kichwani za kutishia maadui na hutoa harufu mbali wanapobugudhiwa

Madhara
Viwavi hawa hula majani machanga kwenye miche. Huweza kusababisha miche kunyauka kwa kukosa majani hasa kwa miche midogo ya michungwa.

Kuzuia
Kagua miche mara kwa mara na kuwaondoa kwa mkono na kuwauwa au tumia dawa za kuulia wadudu kama vile Endosulfan, Diazonon na Fenitrothion.

iii. Viwavi waharibifu wa majani
Hawa ni viwavi wanao kula majani na kuweka alama zinazofanana na mifereji au mistari ndani ya jani. Jani lililo shambuliwa na mdudu huyu huonyesha michoro ya njia ndani ya jani alimo pita mdudu. Mama wa viwavi hawa ni nondo. Viwavi hawa ni wadogo na wembamba kiasi kuwa hula sehemu ya katikati ya jani na huacha
ngozi yenye rangi ya fedha. Jani linaonyesha alama kama michoro ya vinjia vingi alimo pita funza. ushambulia majani machanga na husababisha jani kujikunja na kuathiri kazi ya utengenezaji chakula cha mmea.

Kuzuia
Dawa - diazinon, fenitrothion, thionex, karate, decis, n.k.

iv. Mdudu anayefyonza majani machanga ya miembe.
Mdudu mkubwa ana rangi nyeusi kwenye mabawa na mwili wake una rangi nyekundu. Ana pembe ndefu kuzidi urefu wa mwili wake. Wadudu wakubwa na wadogo hushambulia mimea kwa kufyonza na hivyo kuingiza/kueneza sumu inayosababisha sehemu zilizofyonzwa kufa.

v. Wadudu wanaofyonza maji maji kwenye matawi na majani ya miche
Wadudu hawa hufunikwa na utando mweupe kama nta. Wadudu wakubwa na wadogo hufyonza chakula cha mmea kwenye mashina, matawi na majani ya miche na hata miti mikubwa ya matunda jamii ya michungwa. Wadudu hawa hufuatwa sana na sisimizi kwa vile wanatoa maji yenye sukari ambayo husababisha ukungu mweusi ambao hufanya matawi na majani kuonekana kama yamepakwa masizi.

Kuzuia
Zuia sisimizi ambao huwafuata wadudu hawa, kwani sisismizi huzuia maadui asili wa hawa wadudu wasiweze kuwashambulia.
Tumia dawa za aina ya – Diazinon au Endosulfan ili kuwaua.

vi) Panzi (Mburumundu)
Panzi hawa wanaweza kuleta madhara makubwa pindi wanapokuwa wengi katika kitalu. Kwani aina hii ya panzi hula majani ya miche na miti midogo iliyopandikizwa shambani hasa wakati wa kiangazi.
Kuzuia
Kuwatoa kwa mkono au fimbo na kuwauwa.
Nyunyizia Mafuta ya taa;
Dawa:- Fenitrothion

vii) Nyenyere
Ni vidudu vidogo jamii ya buibui.Viumbe hawa hushambulia majani ya miche na miti mikubwa
na matunda.Nyenyere hushambulia sana miche hasa wakati wa kiangazi na kipindi chenye joto kali

Kuzuia
Kama mshambulizi ni makubwa tumia dawa - Malathion, dicofol.

Minyoo wadogo wadogo
Minyoo hawa hushambulia mizizi ya miche na miti mikubwa ya mitunda jamii ya michungwa.
Ni vizuri kubadilisha mchanga/udongo au kikuzia mimea mara kwa mara kwenye kitalu cha kuoteshea miche.
Endapo si rahisi kufanya hivyo tumia dawa kama vile furadan au unga wa matunda ya mwarobaini kabla ya kuotesha tena miche sehemu hiyo hiyo.

Magonjwa ya Mitunda jamii ya michungwa shambani
i) Vidonda katika shina
Huletwa na aina fulani ya ukungu. Dalili za ugonjwa huu ni kutokea sehemu ya shina ambayo hubadilika rangi.
Huongezeka ukubwa na baadaye kutoa utomvu. Ugonjwa huu hutokea sana kwenye sehemu iliyo na udongo ambao hutuamisha maji.

ii) Ugonjwa wa kukauka miti
Husababishwa na virusi ambavyo husambazwa na chawa weusi. Ugonjwa huu hujionyesha kwa dalili zifuatazo:-
Kwa mitunda kama dalansi na ndimu sehemu ya shina, ganda hunyauka na ndani yake hutokea mipasuko pasuko. Kisha mmea hudhoofika pole pole na hutoa matunda madogo madogo. Majani ya mitunda hubadilika ghafla na kuwa njano. Dalili hizi hutokea kutegemea aina ya mche-shina na kikonyo vilivyotumika. Mche shina unaoweza kustahimili ugonjwa huu ni limao, mchungwa na michenza aina ya cleoptra.

iii) Ugonjwa wa kutobadilika rangi kwa machungwa
yanapokomaa
Ugonjwa huu hutokea hasa katika sehemu za miinuko ya kati na husambazwa na vidudu viitwavyo psyllids, na vile vile kwa kuchukua vikonyo vya kubebeshea kutoka kwenye miti inayoonyesha dalili za ugonjwa.
Ugonjwa huu sio tishio sehemu za joto za nyanda za chini. Dalili za ugonjwa huu ni kama zifuatavyo: Kwenye majani hutokea mabaka ya rangi ya njano dalili kama vile mti uliokosa madini ya Zinc. Vile vile hutokea machipukizi ya kusimama yasiyo ya kawaida, matunda huwa ya ukali na hayabadiliki rangi kuwa njano yanapoiva.

Kuzuia
Sehemu ambazo ugonjwa unaweza kutokea angalia wadudu kama chawa. Hakikisha wadudu hawa hawashambulii miche kwenye kitalu. Wakiwepo, majani huonyesha kujikunja kwa kuweka mafundo sehemu ya juu. Vile vile epuka kuchukua vikonyo kutoka kwenye miti yenye dalili za ugonjwa huu.

iv)Nzi weupe wa kwenye mimea jamii ya michungwa
Hawa ni wadudu ambao hukaa kwenye  majani ya mimiea wakizaliana na kufyonza virutubisho vya mmea, na hii husababisha mmea kudumaa na kutoa mazao duni





Kuzuia
Nja ya kiusalama zaidi ni kwa kupandisha shambani wadudu aina ya Cales noacki ambao huwala hawa nzi weupe na kuzuia kusambaa kwao




 Magonjwa ya matunda ya miembe shambani
Ukungu wa majani Husababishwa na ukungu ambao kwenye majani hutokea alama enye rangi ya kahawia na halafu jani hujikunja na baadaye kudondoka.

Kuzuia
Tumia dawa ya ukungu - kama vile Benomyl.
Pulizia maji ya yaliyo changanywa na unga wa mbegu za muarobaini