KURASA

Thursday, September 23, 2010

DADA NAYMA ANAOMBA USHAURI ZAIDI

Hello Bro Bennet. Angalia miche yangu hatua iliyofikia bado sijaipeleka shambani,
naomba ushauri zaidi niliiotesha mwezi wa tano mwezi wa saba nikaiweka kwenye mifuko miche 300 tu.
nayma





Dada Nayma leo naomba nikuweke hadharani, wadau huyu dada nimekuwa nikimshauri kuanzia kuandaa mbegu, kitalu, kusia mbegu, umwagiliaji, kuhamisha mbegu kutoka kwenye kitalu hadi kwenye vipakti

Dada Nayma miche yako bado ni michanga kiasi, na kama unafuatilia utabiri wa mvua za msimu wa September mpaka November ni kwamba hakutakuwa na mvua za kutosha ila kwa mikoa ya kanda ya ziwa na zaidi Bukoba, nakushauri endelea kumwagilia miche yako ikue zaidi huku ukisubiri mvua za mwezi wa December mwishoni na January 2011, hapo itakuwa mikubwa ya kuweza kuhimili kama mvua zitakuwa chache

NB Hongera sana na anza kuandaa mbegu nyingine ili mwezi wa January uwe na miche mingi zaidi

KILA KAZI NA HATARI ZAKE

Leo nilikuwa nimekwenda kutibu mbwa 9 katika kampuni ya usafirishaji ijulikanayo kama Ruvuvu transport huko kurasini, mbwa hao walikuwa wanasumbuliwa na ugonjwa wa minyoo ya kwenye ngozi ujulikanao kama MANGE, ugonjwa huu husambazwa na viroboto wa mbwa


HAPA MBWA ANAANDALIWA



KUCHOMA SINDANO MBWA