KURASA

Thursday, July 25, 2013

ATHARI ZA MAFUTA YA UBUYU NA TFDA


 
Mamlaka ya chakula na dawa (TFDA) imesisitiza kwamba mafuta ya ubuyu yana athari kubwa za kiafya na ni hatari kwa sababu yana tindikali ya mafuta ijulikanayo kama Clycopropenoic, moya ya madhara ya mafuta ya ubuyu ni pamoja na kusababisha saratani. TDFA imesema pia kutumia unga wa ubuyu na majani yake hakuna athari zozote kiafya kwa hiyo watu wanaweza kuendelea kutumia bila matatizo yoyote.
Kitaalamu tindikali ya Clycopropenoic inaweza kuondolewa kwenye mafuta hayo iwapo tu yatachemshwa katika kiwango cha digrii 180 za sentigredi kwa masaa 8 au kwa teknolojia ya kuyagandisha (hydrogenation) ambapo katika njia hizo zote mbili hakuna hata moja ambayo inatumika hapa nchini.

Miaka ya karibuni kumekuwa na ongezeko kubwa la matumizi ya bidhaa za asili ikiwemo ya aloe vera, ubuyu na bidhaa zake, hii inatokana na matatizo ya kiafya kama kisukari, ugonjwa wa moyo, magonjwa ya ngozi, uzazi, nguvu za kiume na kuongeza kinga mwilini. kutokana na hili matumizi ya ubuyu, majani yake na mafuta yake yaliongezeka zana huku watu wakiamini kwamba ni dawa na kinga ya magonjwa mbali mbali.


Hili walilotuambia TDFA tusilipuuze ila taasisi nyingine za kiutafiti kama SUA na  NIMRI zifanye utafiti wa kutosha sio tu kwa mafuta ya ubuyu bali pia kwenye dawa nyingine na vitu vya asili ili kubaidi madhara yanayoweza kujitokeza kwa waTanzania iwapo watatumia.