KURASA

Saturday, October 10, 2009

KUKATA PEMBE NA KUZUIA PEMBE KUOTA

Mnyama asiye na pembe hasa ng’ombe hupunguza uwezekano wa wanyama kuumizana na hata kuwadhuru binadamu, wanyama wadogo kama miezi miwili hadi mitatu ni vizuri wakachomwa ili kuzuia pembe kuota (disbudding) lakini kama pembe zimetokeza hamna jinsi ila kuzikata kwa kutumia msumeno au waya maalum (phatetomy wire)

DISBUDDING IRONS


Zoezi la kuzuia pembe kuota hufanyika kwa kutumia vyuma maalum (disbudding iron) ambavyo hupashwa moto na kuwa vyekundu, ndama huandaliwa kwa kulazwa chini na kisha kupunguzwa manyoya sehemu itakayochomwa ambapo ni pale pembe zinakoota, unaweza kuitambua sehemu hii kwa kupapasa na utaona kama pembe ndogo ndani ya ngozi. Sehemu husika isafishwe kwa spirit au eusol kabla ya zoezi kuanza.



Mtaalamu wa mifugo ndiye atakaye fanya zoezi hili kwa kufuata kanuni za kitaalam, kabla ya kuanza zoezi ni muhimu mnyama kupigwa sindano ya ganzi, kisha sehemu husika huchomwa na chuma cha moto, na chuma kuzungushwa kila upande na mwisho kama anazibua ataondoa kile kipande kinachoota na kumalizia kwa kukausha sehemu iliyobaki kwa kutumia chuma kile kile, baada ya hapo dawa za kupulizia za vidonda, iodine tincture au dawa za kufukuza wadudu hupakwa sehemu husika na mnyama huachiwa huru.



Kuhusu ukataji wa pembe ambayo imeshaota, baada ya mnyama kufungwa na kulazwa chini huchomwa ganzi na ukataji huanza. Kama utatumia msumeno lazima damu nyingi itatoka, zuia damu hii kwa kuunguza sehemu ndogo ya pembe iliyobaki kwa kuichoma na disbudding iron au chuma chochote cha moto. Inashauriwa kutumia phatetomy wire kwa sababu wakati unakata pembe waya huu huunguza pembe na kufanya damu isitoke kabisa



Kuna baadhi ya aina za ngombe wa kisasa hazina pembe kabisa mfano Hereford na mbegu kama Friesian baadhi yao huwa hawana pembe, kwa mbegu za kienyeji kama zebu (SHZ)huwa na pembe fupi fupi