KURASA

Sunday, January 17, 2010

UGONJWA WA MIGUU NA MIDOMO - FOOT AND MOUTH DISEASE

KWATO ZA MNYAMA MWENYE FMD


Ugonjwa huu husababishwa na virusi jamii ya Aphtovirus vinavyoambukiza binadamu pia (Aphtae epizooticae) ambavyo vipo kwenye Makundi ya A, O, C, SAT1, SAT2, SAT3, Asia1, vinauwezo wa kuishi kwenye matezi na ndani ya mifupa (bone marrow) madhali PH isiwe chini ya 6 na vinauwezo wa kuendelea kuishi kwenye mwili wa mnyama aliyekufa au kwenye udongo kwa mwezi mzima madhali PH isizidi 6. Kama lilivyo jina lake ugonjwa huu hushambulia kwato na midomo (fizi)
Ugonjwa huua zaidi ndama kuliko wanyama wakubwa, hushambulia wanyama wenye kwato kama ng’ombe, mbuzi, kondoo, punda, farasi, nguruwe, nyati maji, na wanyama wengine wenye kwato wanyama jamii ya ngamia, llama na nyati pori, huwa hawasumbuliwi sana na ugonjwa huu

MIKONO YA MTU ALIYEAMBUKIZWA UGONJWA


KUSAMBAA
Ugonjwa hussambazwa kwa njia ya mate, machozi, kinyesi, viatu, vifaa vya kuhudumia wanyama, nyama, maziwa, magari na hata hewa hasa kwa ukanda wa pwani usizidi futi 300 kutoka usawa wa bahari, wanyama ambao wana vijidudu na hawaumwi (carriers) kama nyati pori pia husambaza ugonjwa huu.

DALILI KUU
Toka mnyama aambukizwe huchukua siku 2 -14 na dalili kuu ni uzalishaji wa maziwa kushuka, kusaga meno, joto hupanda, mnyama huchechemea na kurusha mateke, ukiangalia fizi na kati kati ya kwato utaona kama vipele ambavyo baadae hupasuka na kuwa vidonda, wanyama hutoa mimba na wanyama wadogo (ndama )hufa

DAWA
Ugonjwa huu hauna dawa, bali unaweza kutibu vidonda kwa kutumia dawa (antibiotic) kama ulipo hakuna dawa unaweza kutumia chumvi au magadi ukiyeyusha kwenye maji na kuosha kwenye fizi na kwato za mnyama

KINGA
Kuna chanjo za ugonjwa huu ambazo hupigwa , sindano ya pili hupigwa baada ya siku 30 na baada ya hapo ni kila baada ya miezi 6 ( waone maafisa ugani wa mifugo) unaweza kuwakinga wanyama wako kwa kuzuia mwingiliano na wanyama wengine na kabla ya kuleta mnyama mpya hakkisha amepata chanjo zote (sijui wangapi wanafanya hii) pia karantini zitumike mara mlipuko wa ugonjwa huu unapotokea, wanyama wenye ugonjwa wauwawe na kuchomwa moto (incineration)

MFANO WA KIBAO CHA KARANTINI


WANYAMA WENYE UGONJWA WAKICHOMWA MOTO