KURASA

Friday, September 27, 2013

NG'OMBE - KWA TAARIFA YAKO

 Ng'ombe mwenye afya kwa kawaida pua yake huwa na unyevu unyevu au kama vile inatoa jasho jembamba sana.Ukiona ng'ombe wako ana pua iliyokauka na haina unyevuunyevu basi ujue hiyo ni dalili kwamba kuna tatizo katika mwili wake, hii inaweza pia kuwa dalili ya maambukizi au magonjwa
 Pua ya ng'ombe inauwezo wa kunusa umbali wa kilometa 8 au maili 5, ndio maana wanaweza kukimbia machungoni au hata kuvunja banda na kufuata mazao mashambani sababu ya harufu, msimu wa membe tatizo la kutoroka ndio huwa kubwa hasa maembe yapaoanza kuiva
Kwa siku hutumia masaa 6 kula chakula na hutumia masaa 8 kucheua na na kutafuna tena na hunywa maji kiasi cha lita 12 mpaka 25 kutegemeana na ukubwa na hula kiasi cha kilo mpaka 45 kwa ng'ombe wakubwa
Ng'ombe mwenye kilo 1000 huweza kuzalisha kiasi cha tani 10 za mbolea kwa mwaka
Ng'ombe aina ya friesian (pichani juu)ambao ni kinara wa uzalishaji wa maziwa duniani wana rangi nyeupa na mabaka meusi ambapo haya mabaka meusi hayafanani kama zilivyo alama za vidole kwa binadamu. ng'ombe anauwezo wa kusikia sauti ndogo na kubwa zaidi ya binadamu

Mpwapwa breed ni mbegu ya ng;ombe iliyo patikana nchini Tanzania baada ya tafiti kadhaa za kitaalam