KURASA

Saturday, January 23, 2010

VODACOM NA WAATHIRIKA WA MAFURIKO



Katika kuthamini waliopatwa na maafa ya mafuriko pote nchini kampuni ya simu ya VODACOM imeanzisha kampeni inayojulikana kama RED ALERT itakayowawezesha wateja wake kuchangia kadri wawezavyo ili kuwasaidia waathirika wa mvua na mafuriko pote nchini

Kwa ufupi ni kwamba ukitaka kuchangia waliopatwa na maafa pote hapa nchini kama Kilosa, Same, Tanga na Dodoma basi tuma neno MAAFA kwenda namba 15599 na hapo utakatwa shilingi 250/= (PAMOJA NA KODI) kama mchango wako kwa waathirika wa mvua na mafuriko.

Serekali imefanya tathmini na kutangaza kwamba kiasi cha shilingi billioni 10 zinahitajika ili kuweza kuwasaidia wale walioathirika mpaka hali itakapo tengemaa, na kampeni hii ni kuanzia tarehe 24th January 2010 paka 30th January 2010 (wiki moja tu)

MTI MZEE ZAIDI DUNIANI

Mti mzee kuliko yote duniani ulio hai ni bristlecone pine (Pinus longaeva) unaoitwa Methuselah mti huu unapatikana marekani California katika mlima mweupe, mti huu ambao uko futi 11,000 juu ya usawa wa bahari una miaka 4838 na sio tu ni mti mzee zaidi bali ni kiumbe kizee zaidi duniani cha asili (non-cloned) kilicho hai
Kabla ya Methuselah haujagunduliwa kwamba ni mti mzee zaidi duniani Mwaka 1957 na Edmund Schulman iliaminika kwamba mti mkubwa aina ya Sequoias ndio mti wenye umri mkuwa zaidi ukiwa na miaka 2000

MITI AINA YA METHUSELAH HUKO CALIFORNIA KATIKA MLIMA MWEUPE


Mti mwingine aina ya Prometheus uligunduliaka baada ya mwanafunzi wa Mwaka wa mwisho chuoni 1964 ajulikanaye kama , Donald R. Currey alipokuwa akifanya majaribio ya kisayansi na kifaa chake cha kuchimbia viini vya miti miti kuvunjika ndani ya mti, aliomba ruhusa ya kuukata mti huo (iliauchunguze zaidi) kutoka idara ya misitu na alistaajabu alipokubaliwa (wenzetu hawakati miti hovyo hovyo bila sababu maalum) na baada ya kuukata mti huo ndipo walipogundua kwamba ni mti wenye umri mkubwa zaidi duniani ukiwa na zaidi ya miaka 5000.

MITI AINA YA METHUSELAH WENYE MIAKA 4838



Kwa hiyo Prometheus ndio mti mzee zaidi kugunduliwa lakini umekufa baada ya kukatwa na Methuselah ndio mti mzee zaidi duniani ulio hai mpaka sasa. Miti ya Methuselah iko mingi na yote ikiwa na umri zaidi ya miaka 4000 na ipo California katika mlima mweupe lakini mahali ulipo kutwa mti wa Prometheus pamefanywa siri kwani bado wanaendelea kulichunguza eneo hili wakiamini wataukuta mti mwingine wenye umri unaofanana na ule walioukata

KISIKI CHA MTI WA PROMETHEUS BAADA YA KUKATWA