KURASA

Sunday, August 15, 2010

KILIMO CHA MICHUNGWA NA MACHENZA

Ndugu Ali Kalufya alitaka kujua kwa kina ukuliama wa michungwa na jamii yake, aliuliza swali hili katika mtandao wa Dada Subi nami najaribu kumweleza haya...

Michungwa na Jamii yake hustawi zaidi ukanda wa pwani wenye joto kiasi, mvua nyingi na udongo wenye rutuba, kwa Tanzania mikoa kama Pwani, Dar es salaam, Tanga, Mtwara, Lindi, na Morogoro ni maarufu kwa kilimo hiki

MBEGU
Kwa kuanzia unakusanya mbegu za mlimao kutoka katika malimao yaliyokomaa na ikiwezekana yawe yameiva yakiwa mtini, kausha mbegu zake na kisha unaweza kutolea ganda la nje ili ziweze kuota vizuri.

KITALU
Mwaga mbegu zako kwenye kitali na uzifukie kwa udongo kiasi cha nusu sentimeta, mwagia maji kilasiku na baada ya wiki 3 - 6 mbegu zitaanza kuchipua,

MICHE YA MILIMAO TAYARI KWA KUUNGWA


baada miche kufikia kiasi cha sentimeta 3 - 5, miche ihamishiwe kwenye pakiti zenye udongo wenye mbolea ya kutosha na viwekwe kwenye kivuli kiasi

MICHE YA JAFFER BAADA YA KUUNGWA


KUUNGA MICHE
Miche ikifikia urefu wastani sentimeta 30 - 45 inawezwa kuungwa ikiwa unataka iwe michungwa au michenza, kazi hii inahitaji utaalamu kiasi na unaweza kuomba msaada kutoka kwa maafisa ugani wa Kilimo. Kwa michungwa kuna iana mbili kuu hapa Tanzania ambazo ni Jaffer na Valencia. Jaffer ni rahisi kuunga kwa sababu vikonyo vyake ni vikuwa na viko wazi kwenye miti,miti yake huwa mikubwa na inazaa sana, lakini huathirika sana jua likiwa kali na matun da mengi huanguka, pia machungwa yake hukua na kuiva haraka, soko likiwa baya mengi huishia shambani kwa kuanguka

MTI WA JAFFER


JINSI YA KUUNGA MICHE YA MILIMAO KUWA MICHUNGWA AU MACHENZA


Valencia ni miti ya wastani, vikonyo havipo wazi kwa hiyo huwapa kazi waungaji (hawaipendi) ina uzao wa wastani na inakabili ukame na matunda yake hayaivi haraka, msimu wa machungwa ukiwa katikati wewe ndio unaanza kuvuna na ukisha bado unakuwa na machungwa wakati bei iko juu

MTI WA VALENCIA



UPANDAJI
Baada ya uungaji kukubali unaweza kuandaa shamba lako kwa kuchimba mashimo, kuweka mbolea na kusubiri msimu wa mvua, miche ipandwe mara baada tu ya mvua za kwanza kunyesha, umbali wa kupanda ni mita 8 * 8 kwa jaffer na mita 5 * 8 kwa valencia

KUPALILIA
Miche isafishiwe si chini ya mara 2 - 4 kwa mwaka na miche ikifikisha miaka mitatu unaweza ukasafishia visahani na kufyeka sehemu nyingine

UZAO
Kuanzia miaka mitatu miche itaanza kutoa maua na kuzaa na huchanganya kuzaa baada ya miaka mitano, miche huendelela kuzaa hadi kufikia miaka 25 - 30 tangu kupandwa

WADUDU/MAGONJWA
Magonjwa makuu ni fangasi, miti kunyauka na nzi wa michungwa, dawa kwa ajili ya magonjwa yote haya zinapatikana madukani

CHUNGWA LILILOSHAMBULIWA NA NZI WA MICHUNGWA