KURASA

Thursday, May 21, 2009

MICHONGOMA

Sehemu nyingi za duniani ikiwemo nchi yetu Tanzania michongoma imekuwa ikitumika kwa miaka mingi kwa matumizi mbali mbali, matumizi ya michingoma yameanzia zaidi ya miaka 4000 – 6000 iliyopita na michongoma iliyopo ambayo ina umri mkubwa zaidi ni miaka 700 na inapatika nchini ujerumani kiwa na urefu zaidi ya nyumba ya kawaida
Michongoma hutokana na aina mbali mbali za mimea ambayo baadhi ni miti na mingine hukua kama vichaka, yote hii huwa na sifa ya kuwa na miiba na kuhimili ukame ingawa baadhi ya mimea na miti ambayo haina miba hutumika kama michongoma mfano mi krismas (cupresus lusitanica, thujia orientalis)

thujia orientalis


UPANDAJI
Upandaji hutegemeana na aina ya mmea wenyewe, baadhi hutumia vipandikizi, mingine hutumia mbegu na mingine kwa njia zote mbili, ile inayooteshwa kwa vipandikizi huweza kuoteshwa sehemu na ikimea huhamishiwa sehemu husika wakati ile inayooteshwa kwa mbegu mara nyingi huoteshwa sehemu husika moja kwa moja. Huwa haihitaji kumwagiliwa maji ila inapokuwa midogo, ikishakuwa nikubwa inauwezo wa kukua kwa kutegemea mvua tu labda kama kuna ukame

MATUMIZI

MIPAKA –

Mara nyingi hasa majumbani tumeina watu wakitumia michongoma kama mipaka, sehemu za pwani na sehemu zenye mvua chache hutumia zaidi ile yenye miiba, wakati sehemu za bara hasa zenye baridi hutumia ile isiyo na miiba kama mipaka.

UREMBO –
BOUGAINVILEA


MKRISMAS

Wakati mwingine michongoma hutumika kama urembo ikiwa kama mipaka au ikipandwa mmoja mmoja kama maua au miti ya urembo, miti kama mikrismas (cupresus lustanica) na (thujia orientalis) ambayo iko kama mikrismas ila majani yake yako bapa kama yamepigwa pasi. Inapatikana mikoa ya Kilimanjaro, Arusha, Manyara, Lushoto, Mbeya, Iringa, Songea n.k pia kuna inayojuliakana kama boganivilia

KUKINGA UPEPO

–Mara chache sana ambapo michongoma huachwa na kuwa mikubwa kama miti na kutumika kukinga upepo kwenye nyumba na mashamba, sehemu nyingine huwa tu imesahaulika kukatwa na kuwa mikubwa na kufanya kazi ya kukinga upepo.

ULINZI

Hii ndio kazi hasa ya michongoma na haya matumizi yake yalianzia huku, na miti inayotumiaka hapa ni ile yenye miiba zaidi, unaweza kukuta imepandwa kama mpaka na ulinzi au ulinzi peke yake ikiwa ndani ya mipaka. Hutumika kulinda makazi, mazao na mifugo kwenye mazizi, kuna baadhi ya mimea ambayo huwekwa kwenye mazizi na jamii za wafugaji ambazo huaminika kufukuza wanyama wakali kama simba na fisi wasishambulie mifugo.