KURASA

Friday, March 19, 2010

MBWA WAKIPANDANA KWA NINI HUNASIANA AU KUNATANA?



Nadhani karibia kila mtu ameshawahi kuona mbwa wakipandana, kama bado basi maelezo haya yatakusaidia siku ukiwaona, mara baada ya mbwa dume kumpanda jike utaona dume anageuka na kupeana mgongo na jike kila mmoja akiangalia upande wake wakati huo huo, uume ukiwa bado ndani ya uke, wanakuwa kama wanavutana na wakati mwingine wanaweza kutoa milio kama wanalalamika, unaweza kuhisi wanaumia na ukataka kuwatenganisha ACHA na wala usijaribu kufanya hivyo utawaumiza.

Kwa kawaida mbwa dume anapoanza kumpanda jike uume unakuwa haujasimama bali husaidiwa na kiuongo kijulikanacho kama baculum, hii ni tishu kama mfupa na iko ndani ya uume wa mbwa. Wakati mbwa dume anapotaka kumwaga manii ndani ya uke ndipo damu hujaa kwenye uume na hapo uume hutanuka (kudinda) kwa hiyo akimaliza kutoa manii uume hunasa ndani ya uke kwa sababu ya kule kutanuka.



Mbwa dume anapogeuka anazipa muda Mbegu za kiume ziweze kuingia vizuri kwenye uke na hivyo kusababisha ujauzito, ukitumia nguvu kuwaachanisha, mbali na kuumia pia jike hataweza kupata ujauzito. Hiki ni kitu cha asili kwa hiyo husaidia pia kuzuia madume mengine yasiingilie tendo hili na kulikatisha wakati Mbegu bado zinaogelea na kuyafuata mayai kwenye mji wa mimba, kwa kawaida hata kama mbwa madume walikuwa wanapigana kila mmoja akitaka kumpanda jike, mara baada ya Yule aliyefanikiwa kupanda na kugeuka wale wengine huacha vurugu zote.

MBWA WALIONASIANA BAADA YA KUPANDANA


Tendo hili huchukua kati ya dakika 20 – 30 na mbwa hufanikiwa kunasuka mara baada ya damu kupungua kwenye uume na uume kusinyaa na kupungua ukubwa. Kwa mbwa dume ambaye ni mara yake ya kwanza kupanda basin a hata yeye huchanganyikiwa atakapoona amenasa, anaweza hata kujaribu kujinasua au kupiga kelele, unachotakiwa ni kumshika shika shika mbwa wako kichani huku ukimuongelesha kwa upole, yaani jaribu kumpunguza presha ili atulie