KURASA

Friday, December 5, 2008

GOLD FISH

Hawa wapo aina nyingi sana duniani, lakini hapa kwetu Tanzania kuna aina ambazo ni maarufu zaidi aina hizo ni Gold, Black Moor, Bubbles eye,Oranda, Telescope eye Shibunkins, Red cap n.k


RED CAP




Ni samaki wagumu kiasi wanaoweza kuhimili mazingira ya wastani, wanahitaji joto la wastani mpaka baridi kiasi, kwa mazingira ya tanzania hawahitaji heater na wala wasiwekwe sehemu amabayo watapata mwanaga wa jua moja kwa moja (direct sunlight) labda kama uko sehemu zenye baridi sana

SHUBUNKINS


Hakikisha chombo cha kufugia kina nafasi ya kutosha, gold fish mkubwa nahitaji kiasi cha lita 25 za maji peke yake ili aweze kuishi maisha mazuri. kwa kaida samaki hawa huwa wanachafua sana maji kwa sababu ya tabia yao ya kula sana wakati wote (piggy), na inamchukua muda mfupi kukitoa chakula kwa njia ya kinyesi

BLACK MOOR


Chombo cha kufugia kinatakiwa kiwe na sehemu za kujificha samaki kiasi cha 50% - 70% ili samaki wajione wako salama. Hakikisha unapunguza maji 25% kila baada ya wiki na kuweka maji mapya, na kila baada ya wiki 4 unatoa maji yote, unasafisha chombo chako, mawe, filter pamoja na urembo uliopo ndani na kuweka maji mapya 100%

TELESCOPE EYES

Gold fish huwa wanakula mara mbili kwa siku, tumia chakula maalum ambacho kinauzwa madukani, vyakula kama uduvi, dagaa na ubongo vinaweza kulishwa kama wako kwenye bwawa tu kwa sababu huchafua sana vioo na maji. Gold fish huwa wanakula chochote kile (omnivorous)ila inabidi uwe makini usije ukawalisha zaidi (overfeeding) kwa sababu wanaweza kufa

GOLD



Hakikisha chombo kina mfumo wa kusafisha maji (filter) na mfumo wa uingizaji hewa (pump)ili kujua kipimo halisi cha ukubwa wa filter na pump itabidi usome mwongozo wa mtumiaji na mtengenezaji (user manual)

BUBBLES