KURASA

Thursday, September 19, 2013

MBWA - KWA TAARIFA YAKO



 Kama unafuga mbwa na umemzoea basi kila mara unapokaa naye mchunguze namna macho yake yanavyo jaribu kuwasiliana na wewe kila mara, mara zote macho haya hofuatana na lugha ya mwili (body language)
 Anapokuwa na furaha, anahitaji kitu, kuna hatari, joto au baridi sana au hata anaumwa  ishara ya macho pia huonekana
 Kama umemzoea mbwa wako unaweza kuanza kuhisi kama kuna kitu hakiko sawa kwa kumuangalia kwenye macho, cha muhimu ni kujua akiwa kwenye hali ya kawaida macho yake yanakuwa kwenye hali gani au huwa anakuangalia vipi?

 Mbwa hunywa maji kwa kuukunja ulimi wake kwa nyuma na kuyachota kisha kuyaingiza mdomoni, tofauti na wengi wanavyojua kwamba huwa analamba maji
 Mbwa haonyeshwi upendo kwa kukumbatiwa, kama ulikuwa unafanya hivyo acha mara moja maana mbwa hutafsiri kukumbatiwa kawa kuonyesha utawala wako, mbwa anayetawala ndio hukumbatia wenzake kama ishara ya ukuu
 Mikanda ya mbwa ya shingoni iligunduliwa zama za ugiriki ya zamani, nia kuu ilikuwa kuwalinda mbwa dhidi ya mashambulizi ya wanyama wengine kama mbweha na fox