KURASA

Monday, April 27, 2015

JINSI YA KUANDAA MBEGU ZA MITIKI

Hizi ni mbegu kutoka kwa wakala wa mbegu wa taifa (TTSA) wanaopatikana eneo la Kihonda Morogoro Mjini

Nilinunua jumla ya kilo 4 kwenye mifuko ya kilo mojamoja kwa kila mfuko
Nilifungua mifuko yangu na kuweka mbegu zote kwenye kiroba kimoja
Nikaweka mawe ndani ya kiroba ili kukipa uzito utakao nihakikishia mbegu kuzama zitakapo kuwa ndani ya maji
weka kwemye pipa na utie maji, kilo moja ya maji inahitaji kama lita 20 ambazo utabadilisha kila baada ya masaa 12 yaani asubuhi na jioni kwa muda wa siku 7 kisha utazitoa na kuzianika kwa siku moja kabla ya kuzipanda kwe ye kitalu