KURASA

Friday, December 24, 2010

SALAMU TOKA KWA DADA NAYMA



Kaka Ben Salaam
Leo nimekula ugali nyama na mchicha. Jana nilienda shamba nikachuma mchicha wa shambani kwangu, na mahindi ya ugali wa shambani kwangu, baadhi ya siku huwa nakula kande jioni ya mahindi ya shambani kwangu huwa nakula ndizi za shambani kwangu nakula mayai ya mifugo yangu na mapapai makomamanga, mihogo na viazi kuku wa kienyeji mifugo yangu mapera na mastafeli.



Unajua nilianzaje kupenda kilimo? niliingiwa uchungu siku moja kwenda sokoni nikauziwa papai sh 1500/- du nikaamua kuanza kupanda site miti ya matunda hadi ikawa imezidi ndipo nikaamua kutafuta shamba kwa ajili ya mahitaji ya nyumbani kwangu nilifanikiwa hivyo matunda mengi siku hizi nakula natoa site nilikopanda miaka ya nyuma kuna ndizi aina kama sita, michungwa miwili mfenesi mmoja umeshaanza kuzaa muembe mmoja mkomamanga m-peach na m-apple ingawa hiyo m-apple sijala matunda bado mihogo kidogo. Huko shambani ndoko nimepatas uhuru wa kupanda kila ninachoona nakipenda ili niweze kula. Nusu ua shamba napanda mitiki kwa ajili ya kulinda shamba langu, Hahahahaha Back to Eden.

NAYMA